Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Oktoba, 2017

Kisa cha Ummu Haraam Bint Milhaan (Radhwiya Allaahu 'Anhum)

Kisa cha Ummu Haraam Bint Milhaan ( Radhwiya Allaahu 'Anhum )   Na Ustadh Arabi Ibn Saidi   Haraam bin Milhaan na Sulaym bin Milhaan pamoja na dada zao Ummu Haraam bint Milhaan na Ummu Sulaym bint Milhaan (Radhwiya Allaahu 'anhum) ni ndugu wanne waliosilimu wote kwa pamoja tena siku moja mara baada ya Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kuwasili mji wa Madyinah.   Ndugu hawa walikuwa wakipendana sana na walikuwa wakimpenda sana Allaah na wakimpenda Rasuli Wake Muhammad (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam), na wote kwa pamoja walikuwa na shauku kubwa ya kufa kifo cha shaahid kwa ajili ya kupata ushindi wa kuingizwa katika Pepo ya Mola wao Subhaanahu wa Ta'aalaa.  Rasuli (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa akiwapenda sana watu wa nyumba hii, na imepokelewa kuwa mara nyingi alikuwa akiwatembelea wakati wa mchana, akila na kuswali kwao swala za Sunnah. Ndugu wa kike walipewa majina ya kubandika (kun-yah), wakaitw

Hukumu ya kuwa na marafiki (Boyfrienda na GirlFriend)

SWALI Assalam alaikum warahmatullahi wabarakatuh, nataka kuuliza kama kuwa na boy frend inaitikiwa katika dini ya islam,na nataka niwe na dalili ayat ama hadith.      wahadha assalam alaikum,kazi ndjema JIBU   Sifa zote njema Anastahiki Allaah Aliyetukuka Mola wa walimwengu wote, Swalah na salamu zimshukie kipenzi chetu Mtume Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) na Swahaba zake (Radhiya Allaahu ‘anhum) na watangu wema mpaka Siku ya Mwisho.   Tunamshukuru dada yetu kuuliza Swali muhimu kama hili ambalo linahitajika kujibiwa na kuelimisha ndugu zetu makatazo hayo ambayo sasa imekuwa kama ni jambo la kawaida katika jamii zetu na hali sio kutokana na mafunzo ya dini yetu.   Ayaah na dalili za kukataza jambo hili zipo nyingi zikiwa zinazoashiria makatazo moja kwa moja (directly) na nyinginezo zenye uhusiano na makatazo haya. Kuwa na boyfriend bila shaka kutasababisha yatendeke maasi baina ya mwanamke na mwanamume kwani shaytwaan huwa pamoja nao akiwachochea kuingi

Wanaume na wanawake kusalimiana kwa kupeana mikono

SWALI Mashekhe wetu wa Alhidaaya tunaomba mtupe maelezo kuhusu makatazo ya wanawake kusalimia wanaume kwa kutoa mikono maana nnavyojua haifai lakini nilipomkataza mwenzangu amenijibu: “Wapi imeandikwa katika Quran”. Asanteni.   JIBU Sifa zote njema Anastahiki Allaah Aliyetukuka Mola Mlezi wa walimwengu wote, Swalah na salamu zimshukie kipenzi chetu Mtume Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) na Swahaba zake (Radhiya Allaahu ‘anhum) na watangu wema mpaka Siku ya Mwisho Kwanza kutokana na mwenye kusema “Wapi imeandikwa katika Quran” atambue kwamba  sheria zetu za Kiislamu hazitokani na Qur-aan pekee, bali pia zinatokana na Sunnah pia ikiwa hazimo katika Qur-aan. Na hata mara nyingine utakuta kwamba sheria nyingine zimo katika Sunnah pekee na hazipatikani katika Qur-aan. Mifano mingi sana imo kuhusu mas-ala haya na Insha Allaah tutakapojaaliwa tutatayarisha makala inayoonyesha umuhimu au cheo cha Sunnah kulingana na Qur-aan. Kisha mtu mwenye kukanusha Sunnah akaamini

Dua Gani ya kurudisha Bikra

SWALI   Nimesoma nakala yenu, nimevutiwa sana na ushauri wenu. lakini kama ilivyo kwa wanaume zipo dawa za kienyeji za kuongeza uume ambazo hazina madhara. sasa naomba kuuliza hakuna dawa  za kienyeji za kuweza kurudisha bikira ambazo  hazina madhara? Tafadhali naomba unijibu kwenye email  yangu. asanteni   sana     JIBU   Sifa zote njema Anastahiki Allaah Aliyetukuka Mola wa walimwengu wote, Swalah na salamu zimshukie kipenzi chetu Mtume Muhammad (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na Swahaba zake (Radhiya Allaahu 'anhum) na watangu wema mpaka Siku ya Mwisho.     Shukrani zetu za dhati kwa dada yetu muuliza swali. Tunataka kuuliza kwa nini mwanamke wa Kiislamu anataka kurudisha ubikira? Hii ni njia ya udanganyifu inayotumiwa na wasichana wanaoolewa hasa kwa siku hizi katika mwambao wa Tanzania na Kenya. Kwa nini wanafanya hivyo? Bila shaka wengi wao wanafanya hivyo ili kuwadanganya ma-bwana harusi kwa ule usiku wa mwanzo kuwa wao bado ni watwahirifu na wame

Amana katika Uislamu

AMANA KATIKA UISLAMU Assallaam Aleykum WarahmatulLaah Wabarakatuh   Baada ya kumhimidi na kumshukuru Allaah Aliyetukuka Ambaye Ametuneemesha na fursa hii ya kukutana ili kunasihiana na kukumbushana. Swalah na salamu zimfikiye hashimu, Muhammad (Swalla Allaahu ‘Alayhi wa aalihi wa sallam), Maswahaba zake, ahli zake na Waumini wote mpaka Siku ya Qiyaamah.   Maudhui yetu ya leo ni muhimu sana katika zama zetu za leo na matatizo mengi tunakumbana nayo kwa sababu ya kukosekana. Hiyo ni maudhui ya amana.   Huenda mmoja wetu akauliza: Amana ina maana gani katika Dini yetu ya kweli? Suala hilo limejibiwa na Imaam al-Qurtwubiy (Allaah Amrehemu) pale aliposema: Amana inajumlisha shughuli zote za Kidini. Amana ndio faradhi ambazo kwayo Allaah Aliyetukuka Amewapatia waja Wake. Na wametofautiana katika tafsili, hivyo kukawa na kauli nyingi. Baadhi yake ni:   Pakasemwa: Hiyo ni kuweka amana ya mali na nyengineyo.   Na pakasemwa: Katika kila faradhi, na iliyo nzito ni amana ya mali.   N

Mazishi za Kiislamu

Mazishi Ya Kiislamu   Na Ustadh Arabi Ibn Saidi - Firdaus Islamic Foundation بسم الله الرحمن الرحيم Kwa hakika kila sifa njema ni Zake Allaah, tunamtukuza Yeye, na tunamtaka msaada Yeye na tunamuomba msamaha Yeye. Tunajilinda kwa Allaah kutokana na maovu ya nafsi zetu na udhaifu wa vitendo vyetu. Aliyeongozwa na Allaah hakuna wa kumpoteza na aliyepotezwa na Allaah hakuna wa kumuongoza. Nashuhudia kuwa hapana apasaye kuabudiwa kwa haki ila Allaah na nashuhudia kuwa Muhammad ni mja Wake na Mtume Wake. يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا اتَّقُوا اللَّـهَ حَقَّ تُقَاتِهِ وَلا تَمُوتُنَّ إِلا وَأَنتُم مُّسْلِمُونَ “Enyi walioamini! Mcheni Allaah kama apasavyo kuogopwa na wala msife isipokuwa nyinyi (mmeshakuwa) ni Waislamu.” (Qur-aan 3: 102)   يَا أَيُّهَا النَّاسُ اتَّقُوا رَبَّكُمُ الَّذِي خَلَقَكُم مِّن نَّفْسٍ وَاحِدَةٍ وَخَلَقَ مِنْهَا زَوْجَهَا وَبَثَّ مِنْهُمَا رِجَالا كَثِيرًا وَنِسَاءً ۚ وَاتَّقُوا اللَّـهَ الَّذِي تَسَاءَلُونَ بِهِ وَالأرْحَامَ ۚ إِنَّ اللَّـهَ كَانَ عَلَيْكُم