Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Machapisho

Neema za Pepo tuliyoahidiwa

                                                            Neema za Pepo Tuliyoahidiwa Maelezo ya Neema za Pepo tuliyoahidiwa na Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) yametajwa mno katika Qur-aan na Hadiyth, Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala): إنَّ لِلْمُتَّقِينَ مَفَازًا .   حَدَائِقَ وَأَعْنَابًا.  وَكَوَاعِبَ أَتْرَابًا. وَكَأْسًا دِهَاقًا. لَّا يَسْمَعُونَ فِيهَا لَغْوًا وَلَا كِذَّابًا جَزَاء مِّن رَّبِّكَ عَطَاء حِسَابًا.  ((Hakika wenye taqwa [wamchao Allaah] wanastahiki kufuzu. Mabustani na mizabibu. Na wake waliolingana nao. Na bilauri zilizojaa. Hawatosikia humo upuuzi wala uongo. Malipo kutoka kwa Mola wako kipawa cha kutosha))  [An-Nabaa: 31-36] Anasema tena (Subhaanahu wa Ta'ala) katika Suratul-Waaqiah  وَالسَّابِقُونَ السَّابِقُونَ.  أُوْلَئِكَ الْمُقَرَّبُونَ.  فِي جَنَّاتِ النَّعِيمِ.  ثُلَّةٌ مِّنَ الْأَوَّلِينَ.  وَقَلِيلٌ مِّنَ الْآخِرِينَ. عَلَى سُرُرٍ مَّوْضُونَةٍ. مُتَّكِئِينَ عَلَيْهَا مُتَقَابِلِينَ
Machapisho ya hivi karibuni

Viungo vya Mwili vitashuhudia Matendo ya Mwanaadamu Siku ya Qiyaamah

Anasema Allaah  سبحانه وتعالى   ((الْيَوْمَ نَخْتِمُ عَلَى أَفْوَاهِهِمْ وَتُكَلِّمُنَا أَيْدِيهِمْ وَتَشْهَدُ أَرْجُلُهُمْ بِمَا كَانُوا يَكْسِبُونَ)) ((Leo Tunaviziba vinywa vyao, na iseme Nasi mikono  yao , na itoe ushahidi miguu  yao kwa waliyokuwa wakiyachuma))  [Yaasiyn :65 ] Siku ya Qiyaamah viungo vya miili vitakuwa ni vyenye kushuhudia matendo ya binaadamu aliyoyatenda hapa duniani: Mfano mikono itasema: "nimeiba".  Miguu itasema, "nimekwenda sehemu ya ma'asi". Macho yatasema, "nimetazama machafu".  Masikio yatasema, "nimesikiliza nyimbo, au umbea" na kadhalika. Na hivi ndivyo itakavyokuwa hali ya makafiri, wanafiki na wenye kumuasi Mola siku ya kufufuliwa,  watakapokanusha madhambi waliyoyatenda duniani na kuapa kwamba hawakuyafanya, Allaah  سبحانه وتعالى  Atawafunga midomo  yao na kuviamrisha viungo vizungumze:   عن أنس بن مالك قال: كنا عند النبي صلى الله عليه وسلم، ف

'Amali Inayotaqabaliwa

Kabla ya kuchukua hata hatua moja, Ewe kaka yangu na dada yangu uliye Muislamu, ni muhimu kwako kuijua njia ambayo maokozi yako yatapokuwa. Usijichokeshe kwa kutekeleza mambo mengi (ambayo ndani yake hamna Ikhlaas).  Kwani inaweza kuwa ya kwamba mtu atatenda matendo mengi, lakini hafaidiki na chochote isipokuwa kupata machofu kutokana na matendo hayo hapa duniani na kupata adhabu katika Akhera.  Haya yanatolewa mfano  katika   kauli ya Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam): “Inawezekana mtu anayefunga asipate chochote katika funga yake isipokuwa njaa na yule anayesimama usiku kuswali asipate chochote isipokuwa machofu”   Imesimuliwa na Ibn Maajah kutoka kwa Abu Hurayrah na Shaykh Al-Albaaniy kasema kwamba ni sahihi katika Swahiyh al-Jaami’, no.3482. [Na tunajikinga na Allaah kutokana na kuwa miongoni mwa watu kama hawa].  Allaah Aliyetukuka Anasema: Na Tutayaendea yale waliyoyatenda katika ‘amali Tuzifanye mavumbi yaliyotawanywa.  (Suratul al- Furqaan