Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Agosti, 2017

Madhara Ya Ghiybah (Kusengenya) Na An-Namiymah (Kufitinisha) -Sehemu ya 12

Madhara Ya An-Namiymah (Kufitinisha ) - Vipi Kutibu An-Namiymah?   Mafunzo yafuatayo yataweza Inshaa-Allaah kutibu maovu ya An-Namiymah ikiwa yatatekelezwa na inampasa kila mwenye tabia hii haraka ajifunze ili kujiepusha na maouvu haya yanayosababisha ufisadi na chuki baina ya ndugu Waislamu. Tutambue kuwa hii ni moja wapo ya jihadi ya nafsi kwa kujiepusha na maovu yanayoamrishwa na nafsi, ambayo ni jihadi  bora kabisa na itamuweka Muislamu katika Ridhaa Ya Mola wake Mtukufu. Amesema Mtume (Swalla-Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) kupitia usimulizi wa Fadhwaalah bin ‘Ubaydullaah (Radhiya Allaahu ‘anhu):   (( ألا أخبركم بالمؤمن؟ من أمنه الناس علىأموالهم وأنفسهم، والمسلم من سلم الناس من لسانه ويده، والمجاهد من جاهد نفسه في طاعة الله، والمهاجر من هجر الخطايا والذنوب))  أحمد والحاكم , قال الألباني  "إسناد صحيح" سلسلة الأحاديثالصحيحة ((Je, nikujulisheni kuhusu Muumini? Anayeaminiwa na watu juu ya mali zao na nafsi zao. Na Muislmu anayeweka amani kwa watu kwa ulimi wake na

Madhara Ya Ghiybah (Kusengenya) Na An-Namiymah (Kufitinisha)

Madhara Ya An- Namiymah ( Kufitinisha ) - Sababu za Kufitinisha , Sifa Za Mfitinishaji -Sehemu ya 11     Kufitinisha baina ya watu ni jambo ovu linalochukiza mbele ya Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) Ambaye Ametuamrisha tuepukane nalo kamaAnavyosema:   ((وَتَعَاوَنُواْ عَلَى الْبرِّ وَالتَّقْوَى وَلاَ تَعَاوَنُواْ عَلَى الإِثْمِ وَالْعُدْوَانِ))   ((Na saidianeni katika wema na ucha Mungu. Wala msisaidiane katika dhambi na uadui)) [Al-Maaidah :2]     Vile vile Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala):     ((وَلَا تَبْغِ الْفَسَادَ فِي الْأَرْضِ إِنَّ اللَّهَ لَا يُحِبُّ الْمُفْسِدِينَ))   ((Wala usitafute kufanya ufisadi katika ardhi. Hakika Allaah Hawapendi mafisadi)) [Al-Qaswas: 77]   Sababu zinazomfanya mtu afitinishe :   1.       Ujinga wa kutokujua makatazo yake katika Qur-aan na hatari yake na adhabu zake kutoka kwa Mola Muumba.   2.      Nafsi kuwa na chuki na uhasidi wa kuona ndugu wawili wanapendana na kushirikiana katika mambo yao. Amesema Mtume

Madhara Ya Ghiybah (Kusengenya) Na An-Namiymah (Kufitinisha) -Sehemu ya 10

Madhara Ya An-Namiymah ( Kufitinisha ) - Maana , Hukumu Na Adhabu Zake     Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala):     ((وَلاَ تُطِعْ كُلَّ حَلاَّفٍ مَّهِينٍ)) ((هَمَّازٍ مَّشَّاء بِنَمِيمٍ))  ((مَنَّاعٍ لِّلْخَيْرِ مُعْتَدٍ أَثِيمٍ))     ((Wala usimtii kila mwingi wa kuapa wa kudharauliwa)) ((Mtapitapi, apitaye akifitini)) ((Mwenye kuzuia kheri, dhaalimu, mwingi wa madhambi)) [Al-Qalam: 10-12]         Maana ya An-Namiymah   Ni kufitinisha, kwa maana kuchongeza kwa kuhamisha au kupeleka maneno baina ya watu ili kusababisha wachukiane.   Mfano kumwambia mwenzio: "Fulani kasema kuhusu wewe kadhaa na kadhaa". Au, "Fulani anakuchukia wala hakupendi". Kufitini huku kunaweza kuwa ni kwa kutamka maneno, au kwa kuandika au hata kwa kuonyesha ishara. Kufitinisha kwa kumsingizia mtu au hata kama huyo mtu alisema kweli  usemi huo haijuzi kufitinisha.   Mtu kama huyu mwenye kufitinisha ni mwenye nyuso mbili anamkabili kila mmoja kwa uso mzuri kumbe h

Madhara Ya Ghiybah (Kusengenya) Na An-Namiymah (Kufitinisha) -Sehemu ya 9

Madhara Ya Ghiybah - Hali Zinazoruhusu Ghiybah       Tumebainishiwa katika Shari’ah yetu ya Kiislamu kuwa ziko hali zinazojuzu Ghiybah kwa sababu ya maslaha yanayopatikana. Nazo ni kama ifuatavyo:     1-Kupinga dhulma ya Qaadhi au Kiongozi au kuzuia dhulma isitendeke     Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala):   ((لاَّ يُحِبُّ اللّهُ الْجَهْرَ بِالسُّوَءِ مِنَ الْقَوْلِ إِلاَّ مَن ظُلِمَ)) ((Allaah Hapendi uovu uenezwe kwa maneno ila kwa mwenye kudhulumiwa))[An-Nisaa: 148].         2-Katika kushitaki anapodhulumiwa mtu haki yake :     Kutoa aibu ya mtu inapohitajika mfano kushtaki kwa mhusika (mkuu atakayeweza kutatua matatizo) kuwa 'fulani kanidhulumu kadhaa na kadhaa, au kanifanyia kadhaa na kadhaa, au fulani hanipi haki yangu kadhaa na kadhaa". Hii ni kutokana na dalili ya Hadiyth ifuatayo:     عن عائشة رضي الله عنها  :  أن هنداً زوجة أبي سفيان قالت : يارسول الله إن أبا سفيان رجل شحيح وليس   يعطيني ما يكفيني وولدي إلا ما أخذت منه ، وهو

Madhara Ya Ghiybah (Kusengenya) Na An-Namiymah (Kufitinisha) -Sehemu ya 8

Madhara Ya Ghiybah - Kafara ( Fidia ) Ya Ghiybah     Ghiybah ni madhambi ambayo yanayomharibia mtu amali zake njema na kujazwa dhambi za yule anayemsengenya na hatimaye kumuangamiza motoni. Hivyo inampasa Muislamu mwenye tabia ovu ambayo ni hatari kwake, haraka afanye kafara ya maovu hayo. Kafara yenyewe ni kama ifuatavyo:     Kutubu   Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala):       ((يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا تُوبُوا إِلَى اللَّهِ تَوْبَةً نَّصُوحًا))     ((Enyi mlioamini! Tubuni kwa Allaah toba iliyo ya kweli!)) [At-Tahriym: 8]     Tawbatun-Nasuuah (Tawbah ya kweli) ni ile mtu anayokamilisha shuruti zake nazo ni:     1.        Kuacha kitendo kiovu hicho. 2.        Kujuta 3.        Kuazimia kutokurudia tena maovu 4.       Ikiwa inahusu haki ya binaadamu basi lazima kwanza kurudisha haki hiyo.   Vipi ujihalalishe na Ghiybah   Kama ilivyo sharti ya nne kuwa kwa vile Ghiybah inahusu haki ya binaadamu basi lazima kwanza urudishe haki ya uliyemsengenya

Madhara Ya Ghiybah (Kusengenya) Na An-Namiymah (Kufitinisha) -,Sehemu ya 7

Madhara Ya Ghiybah - Vipi Kujiokoa Na Kuokoa Jamii Kutokana na Ghiybah Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala): ((وَإِذَا رَأَيْتَ الَّذِينَ يَخُوضُونَ فِي آيَاتِنَا فَأَعْرِضْ   عَنْهُمْ حَتَّى يَخُوضُواْ فِي حَدِيثٍ غَيْرِهِ وَإِمَّا يُنسِيَنَّكَ   الشَّيْطَانُ فَلاَ تَقْعُدْ بَعْدَ الذِّكْرَى مَعَ الْقَوْمِ   الظَّالِمِينَ))     ((Na unapowaona wanaoziingilia Aayah zetu, basi jitenge nao mpaka waingilie mazungumzo mengine. Na kamaShaytwaan akikusahaulisha, basi baada ya kutanabahi usikae pamoja na watu madhaalimu)) [Al-An'aam: 68] Hiyo ni moja ya njia ya kujiokoa na maovu haya ya Ghiybah, nayo ni kujiepusha na wanaopendelea kuzungumza yasiyo na maana na yanayomkosesha mtu radhi za Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala). Njia nyingine nyingi tunazitaja chini ya Makala hii na inayofuatia.   Njia Za Kujiokoa Na   Kuwaokoa Wenzako Na   Ghiybah : 1.     Kuwa na Taqwa na umkhofu Mola Wako na kusoma Aayah na Hadiyth zenye maonyo na adhabu za Ghiybah.   2.     Fikiria

Madhara Ya Ghiybah (Kusengenya) Na An-Namiymah (Kufitinisha) -Sehemu ya 6

Madhara Ya Ghiybah - Sababu Za Kutendeka Uovu Wa Ghiybah   1-Kuambatana na marafiki waovu        Moja ya sababu inayosababisha kutenda maasi ya Ghiyba ni kuambatana na marafiki waovu wasiomkhofu Mola wao kwani rafiki muovu humuathiri mwenziwe kwa yale anayoyatenda. Mfano mzuri ametupigia  Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)   عن أبي موسى الأشعري رضي الله عنه أن النبي صلى الله عليه وسلم قال: (( إنما مثل الجليس الصالح و جليس السوء كحامل   المسك ونافخ الكير، فحامل المسك إما أن يحذيك وإما أن تبتاع منه، وإما أن   تجد منه ريحاً طيبة، ونافخ الكير إما أن يحرق ثيابك وإما أن تجد منه ريحاً خبيثة))  متفق عليه     Abu Muusa Al-Ash'ariyy (Radhiya Allaahu 'anhu) amesimulia: Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Mfano wa jaliys [mtu unayeambatana naye] mwema na jaliys mbaya ni kamamfano wa mbebaji miski na mfua chuma (anayevuvia kipulizo). Mbebaji miski ima atakupa au utanunua kutoka kwake au utapata harufu nzuri kwake. Na mfua c

Madhara Ya Ghiybah (Kusengenya) Na An-Namiymah (Kufitinisha)

Madhara Ya Ghiybah - Kuharamisihwa Kwake Na Na Adhabu Zake Katika Sunnah   Baada ya kujikumbusha makatazo na adhabu za Ghiybah katika Qur-aan, tukaona jinsi gani maovu haya yalivyokemewa na Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala), tunaendelea kutaja makatazo yake na adhabu zake katika Sunnah:     عن أبي بكرة رضي الله عنه أن رسول الله صلى الله عليه وسلم قال في خطبته   يوم النحر بمنى في حجة الوداع: (( إن دمائكم، واموالكم وأعراضكم حرام   عليكم كحرمة يومكم هذا، في شهركم هذا، في بلدكم هذا، ألا بلغت ))  متفق عليه   Kutoka kwa Abu Bakrah (Radhiya Allaahu 'anhu) amesimulia  kuwa Mtume (Swalla Allahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alisema katika khutba yake ya siku ya An-Nahr [siku ya kuchinja – yaani siku ya 'Iydul-Adhwhaa] huko Minaa katika Hajjatulwadaa' [Hijjah ya kuaga] ((Hakika damu zenu, mali zenu na heshima zenu ni haramu kwenu kama uharamu (wa kutenda dhambi) siku yenu hii katika mji wenu huu. Je nimefikisha?))[Al-Bukhaariy na Muslim] Hadiyth hii inatuonyesha ji

Madhara Ya Ghiybah (Kusengenya) Na An-Namiymah (Kufitinisha) -Sehemu ya 4

Madhara Ya Ghiybah - Kuharamishwa Kwake Na Adhabu Zake Katika Quraan   Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala): ((وَلاَ تَقْفُ مَا لَيْسَ لَكَ بِهِ عِلْمٌ إِنَّ السَّمْعَ وَالْبَصَرَ وَالْفُؤَادَ كُلُّ أُولئِكَ كَانَ عَنْهُ مَسْؤُولاً))   (( Wala usifuate   ( ukipita ukisema au kuyafanya ) usiyo na ilimu ( ujuzi ) nayo . Hakika masikio , na macho, na moyo   hivyo vyote vitaulizwa ))  [ Al-Israa : 36]      Na Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala):   (( وَلاَ يَغْتَب بَّعْضُكُم بَعْضًا أَيُحِبُّ أَحَدُكُمْ أَن يَأْكُلَ لَحْمَ أَخِيهِ مَيْتًا فَكَرِهْتُمُوهُ وَاتَّقُوا اللَّهَ إِنَّ اللَّهَ تَوَّابٌ رَّحِيمٌ)) (( Wala msisengenyane nyinyi kwa nyinyi . Je ! Yupo katika nyinyi anayependa kuila nyama ya nduguye aliyekufa ? Mnalichukiahilo ! Na mcheni Allaah . Hakika Allaah ni Mwenye kupokea toba , Mwenye kurehemu ))  [ Al-Hujuraat :   12] Ibn 'Abbaas (Radhiya Allaahu 'anhuma) amesema: Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) Ameharamisha

Madhara Ya Ghiybah (Kusengenya) Na An-Namiymah (Kufitinisha) -Sehemu ya 4

Madhara Ya Ghiybah - Kuharamishwa Kwake Na Adhabu Zake Katika Quraan   Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala): ((وَلاَ تَقْفُ مَا لَيْسَ لَكَ بِهِ عِلْمٌ إِنَّ السَّمْعَ وَالْبَصَرَ وَالْفُؤَادَ كُلُّ أُولئِكَ كَانَ عَنْهُ مَسْؤُولاً))   (( Wala usifuate   ( ukipita ukisema au kuyafanya ) usiyo na ilimu ( ujuzi ) nayo . Hakika masikio , na macho, na moyo   hivyo vyote vitaulizwa ))  [ Al-Israa : 36]      Na Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala):   (( وَلاَ يَغْتَب بَّعْضُكُم بَعْضًا أَيُحِبُّ أَحَدُكُمْ أَن يَأْكُلَ لَحْمَ أَخِيهِ مَيْتًا فَكَرِهْتُمُوهُ وَاتَّقُوا اللَّهَ إِنَّ اللَّهَ تَوَّابٌ رَّحِيمٌ)) (( Wala msisengenyane nyinyi kwa nyinyi . Je ! Yupo katika nyinyi anayependa kuila nyama ya nduguye aliyekufa ? Mnalichukiahilo ! Na mcheni Allaah . Hakika Allaah ni Mwenye kupokea toba , Mwenye kurehemu ))  [ Al-Hujuraat :   12] Ibn 'Abbaas (Radhiya Allaahu 'anhuma) amesema: Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) Ameharamisha

Madhara Ya Ghiybah (Kusengenya) Na An-Namiymah (Kufitinisha) -Sehemu ya 3

Madhara Ya Ghiybah - Maana Ya Ghiybah , Tofauti Baina Ya Ghiybah , Buhtaan Na Ifk   Maana ya Ghiybah:   Kilugha:  Kila kilichokuwa hakipo mbele yako. Na imeitwa Ghiybah kwa kutokuweko anayetajwa wakati anapotajwa na wengine.    Kishari’ah: Kumsengenya mtu asiyekuwepo kwa mambo ambayo atachukia kuyasikia. Na maana yake ametujulisha Mtume (Swalla Allahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alipowauliza Maswahaba:   ((   أتدرون ما الغيبة؟))   قالوا: الله ورسوله أعلم؛ قال:(( ذكرك أخاك بما   يكره  ...))   ((Je mnajua maana ya  Ghiybah ? [Kusengenya])) Wakasema: Allaah na Mjumbe Wake wanajua. Akasema: ((Kumsema ndugu yako anayoyachukia …..)) [Al-Bukhaariy]   Imaam An-Nawawiy amesema kuhusu Ghiybah: "Kumsema mtu nyuma yake kwa yale anayoyachukia"   Akaendelea kusema: "Kumsema mtu kwa anayoyachukia ikiwa yanayohusu mwili wake, au dini yake, au dunia yake, au nafsi yake, au umbile lake au tabia yake, au mali yake, au wazazi wake, au mtoto wake, au mke wake, au mt