Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Novemba, 2017

Madhara ya Kufuata Matamanio

Assallaam Aleykum WarahmatulLaah Wabarakatuh Shukurani zote Anastahiki Allaah, Mola wa ulimwengu wote. Rehma na amani zimshukie Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam), ahli zake na Masahaba wake. Enyi Waislamu muogopeni Allaah kwa kadri Anavyopaswa kuogopewa. Allaah Amesema, “Enyi mlioamini ! Mcheni Mwenyezi Mungu kama ipasavyo kumcha ; wala msife ila nanyi ni Waislamu.”  (Aal 'Imraan 3:102) Ucha Mungu ni dalili ya Iymaan. Kwani kwa ucha Mungu ndipo mtu anaweza kudumu katika njia iliyonyooka (iliyo sawa) Jueni kuwa muongozo sahihi ni muongozo wa Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam), Ubaya wa mambo yote ni uzushi, na kila uzushi ni uovu, na kila ovu linampeleka mtu motoni. Enyi Waislamu! Allaah Amewaumba viume ili wamuabudu na wafungamane na Amri Zake na makatazo Yake. Allaah Anasema, "Nami Sikuwaumba majini na watu ila waniabudu Mimi."  (Adh-Dhaariyaat 51:56)   Allaah pia Anasema, "Enyi watu! Muabuduni Mola wenu Mlezi Aliye

Kumpaka Mtoto Mchanga Wanja Au Masizi Usoni Kwa Ajili Kumkinga Na Husda Inafaa ?

SWALI:   Assalam Aleykoum Warrahmatullah Wabarakatu. Suala langu la kumpaka mtoto mchanga wanja au masizi usoni ili iwe ni kinga kwa macho ya watu na husda ua kumvisha uzi mweusi ni kinga? na kama si kinga tumfanyie nini iwe kinga tumsomee ayatul kursi asubuhi na jioni au? Na kama nimefanya hivyo jee ni shirki? Naomba ufafanuzi haraka sana asanteni Mola akuzidishieni elmu na taqwa AMIN.   JIBU:   Sifa zote njema Anastahiki Allaah Aliyetukuka Mola Mlezi wa walimwengu wote, Swalah na salamu zimshukie kipenzi chetu Mtume Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) na Swahaba zake (Radhiya Allaahu ‘anhum) na watangu wema mpaka Siku ya Mwisho.   Shukrani zetu za dhati kwa swali lako kuhusu kumpaka mtoto mchanga wanja au masizi usoni kwa ajili ya kinga. Hakika ni kuwa wanja ni dawa ya macho pekee wala si kinga ya hasadi. Kufanya hivyo, yaani kumpaka mtoto wanja au masizi usoni haifai kishari’ah kwani huko kunaingia katika shirki kwa kuufanya wanja na hayo masizi yanaweza

Ikiwa Majini Ni Viumbe Dhaifu Vipi Wamuingie Binaadamu Bila Ya Kuweza Kupona?

SWALI   Assalam alaykum warahmatul-allah wabarakatu.   Nimesikia kuwa majini ni viumbe dhaifu kuliko binaadamu na tunawaogopa bure tu, sasa suala langu linakuja pale tunapoona baadhi ya watu wanaugua maradhi ya mashetani (kupanda jini kichwani) baadhi ya walimu na masheikh wetu wanasema hakuna maradhi ya aina hii na mimi huko nyuma nimepata ku sikia kwamba, maradhi hayo yapo na yanatibika. Na kwa kusema hayo ni kutokana na mwalimu wangu kunipa hadithi ya kisa cha Nabii Sulaiman Bin daoud alokuwa Rasuli na Mfalme kwa viumbe vyote kwa wakati huo kwamba alipata kuwauliza majini kuhusu wanavyomuingia binaadam na kumpoteza au kumpatia maradhi na dawa gani itumike wao hutoka na wakampatia majibu kwa kumpa baadhi ya aya za Quran au sura kwamba zikisomwa hizi sisi hutoka na kumuacha huyo mtu. Jee lipi lina ukweli kati ya haya kuhusu maradhi hayo, yapo au hayapo, na kisa hiki ni sahihi au si sahihi?   Wabillah Tawfiq.   JIBU Waleykum Salaam WarahmatulLaah Wabarakatuh AlhamduliLLaah Hi

Kipi kikudanganyacho ukamuasi Mola wako

  Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala)   ((يَا أَيُّهَا الْإِنسَانُ مَا غَرَّكَ بِرَبِّكَ الْكَرِيمِ)) "Ee mwana Aadam! Nini kilichokughuri kuhusu Rabb wako Mkarimu?" [Al-Infitwaar: 6] Utukufu gani wa Mwenye maneno haya yenye kushtua nyoyo na kusisimua mwili?Siku utakayoitwa "Ee Mwanaadamu maskini uliye dhaifu, kitu gani kikudanganyacho?"Nini kilichokughilibu hata ukamu'asi Allaah Mmoja (Pekee) Mwenye nguvu? (za mwisho)Nini kilichokudanganya hata ukavuka mipaka ya Mola wako?Nini kilichokudanganya hata ukapuuza Swalaah?Nini kilichokudanganya hata ukatenda maovu usiku na mchana?Nini kilichokudanganya hata ukapeleka macho yako kutazama yalio haramu?Nini kilichokudanganya hata ukawa humuogopi Mola wako kama unavyowaogopa viumbe vyengine?Nini kilichokudanganya hata ukawa huna khofu ya kukutana na Mola wako na kuhesabiwa?Je, ni dunia? Na Je? Hujui kama dunia ni nyumba ya kupita tu?Au ni shahawaat (matamanio)?  Hujui kama nayo ni ya kuondoka?Au ni Shaytwaan a

Miongoni Mwa 'Ulamaa Waliopinga Mawlid

1.      Shaykhul-Islaam Ibn Taymiyyah -  Iqtidhwaa As-Swiraatw Al-Mustaqiym  (2/619) na Majmu’ al-Fataawa  (1/312)     2.      Shaykh Taajud-Diyn ‘Umar bin ‘Aliy Al-Lakhmiy Al-Iskandariyy (Mwanachuoni wa Madh-hab ya Al-Malikiy Alexandria mwaka 734H) -  Al-Mawruwd fiy Kalaami ‘alaa ‘amal al-Mawlid .     3.      Shaykh Muhammad Bukhiyt al-Mutwiy’iy al-Hanafiyy (Mufti wa Diyaar Al-Miswriyyah)     4.      Shaykh ‘Aliy Mahfuwdhw – katika kitabu:  Al-Ibdaa’ fiy Midhwaari al-Ibtidaa’     5.      Shaykh Raashid Ridhwaa – Amenukuu katika Muswannafaati zake mfano: Al-Manaar (9/96), (2/74), (29/664-668), (17/111), (76), na Fataawa (Juz. 5, uk.  2112-2115), (Juz. 4, uk. 1242-1243)     6.      Shaykh Muhammad bin ‘Abdis-Salaam Khudhwar Ash-Shaqiyri – Katika kitabu chake:  As-Sunan wal-Mubtada’aati .     7.      Shaykhul-Islaam Al-Mujaddid Muhammad bin ‘Abdil-Wahhaab.     8.      Al-‘Allaamah Shaykh ‘Abdur-Rahmaan Aal Shaykh – Katika:  Ad-Durar As-Sanniyyah .     9.  

Mjadala Baina Ya Salafi Na Sufi Kuhusu Maulidi

  Sufi:                Hamwishi nyinyi Mawahabi kupinga Maulidi!   Salafi :             Mawahabi? Kwani unavyojua wewe nini maana ya Uwahabi?   Sufi:                 Si ndio dhehebu linalopinga Maulidi?   Salafi :            Maskini, ndio hivyo wengi hamjui maana yake mnapachika tu jina na wengineo mkidhani kuwa Wahabi ni dhehebu au kundi au kuna watu wanajiita hivyo? Tunafahamu nyinyi Masufi mnajiita Masufi na hamna ishkali katika hilo, Ibaadhi wanajiita Ibaadhi na hawana tatizo na hilo, Shia wanajiita Shia na wanaridhia hilo, lakini hakuna watu wanaojiita Wahabi wala hawaridhii hilo japo baadhi ya ‘Ulamaa wamesema kama kushikamana na Sunnah za Mtume Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) ni Uwahabi, basi hilo si tatizo. Lakini hakuna aliyetangulia katika Wanachuoni aliyejiita Wahabi. Basi hebu nikufahamishe hao waliotunga jina la Uwahabi, ni Masufi wenzako na Mashia na wakinasibisha jina hilo na mlinganiaji Mwanachuoni Muhammad bin Al-Wahhaaab ambaye amezali

Sababu 35 za Muislamu Asisherehekee Maulid

AlhamduliLLaah, Swalaah na salaam zimshukie Nabiy wetu Muhammad (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na Swahaba zake (Radhwiya Allaahu 'anhum) na waliowafuata kwa wema mpaka Siku ya Mwisho.   Zifuatazo ni baadhi ya hoja za wazi kutoka katika Qur-aan na Sunnah zinazopinga Maulidi, tukitumai kuwa zitamtosheleza Muislamu aikinaishe nafsi yake kuwa Maulidi ni jambo la uzushi katika Dini.    SABABU YA KWANZA:   Kumpenda Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):   Kwa sababu ya kumpenda Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) ni kumfuata Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam). Naye (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) tokea kuzaliwa kwake hadi kufariki kwake hakusherehekea siku yake ya kuzaliwa wala Maswahaba zake hawakumsherehekea. Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):     قُلْ إِن كُنتُمْ تُحِبُّونَ اللّهَ فَاتَّبِعُونِي يُحْبِبْكُمُ اللّهُ وَيَغْفِرْ لَكُمْ ذُنُوبَكُمْ وَاللّهُ غَفُورٌ رَّحِيمٌ Sema (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم)