Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Septemba, 2018

Mchumba anachelewa kupeleka posa nyumbani

*Swali* Asalam alaykum, shekh :mm nna mchumba angu  lkn anakua mgumu kuja kuleta posa nymbani, jee? nimsomee dua gani ili aweze Kuja haraka maana ni cku nyingi tena naomba unisaidie unifahamishe ustadh. *Majibu* Wa Aleykum Sallaam WarahmatulLaah Wabarakatuh BismiLLaah wa AlhamduliLLaah was-Swalaatu wa Salaamu ‘alaa Muhammad wa ‘alaa  aalihi wa Aswhaabihil Kiraam, wa Ba’ad. *Maana ya Uchumba Kisheria* ✅Uchumba katika Uislamu ni pale *mwanamme anayetaka kuoa au jamaa zake au mtu yeyote aliyemwakilisha anapokwenda kwa wazazi wa msichana/Bint/Mwanamke* kuposa/kupeleka Barua na kukubaliwa. *✅Huo ndio unaitwa uchumba* ➡Ama kinyume na hivyo unakuwa ni urafiki baina ya mvulana na msichana. *Na hili katika Uislamu limekatazwa kwani ni Haramu* ✅Na hili limekatazwa kishari’ah. ➡Na hapo katika Swali lako umesema kwamba una Mchumba wako Lakini anakuwa mgumu *kuleta posa nyumbani* ina maana kuwa Huyo mwanaume *Kisheria si Mchumba wako kwasababu bado hajapeleka barua ya Posa nyumbani kwenu*

Mchumba anachelewa kupeleka posa nyumbani

*Swali* Asalam alaykum, shekh :mm nna mchumba angu  lkn anakua mgumu kuja kuleta posa nymbani, jee? nimsomee dua gani ili aweze Kuja haraka maana ni cku nyingi tena naomba unisaidie unifahamishe ustadh. *Majibu* Wa Aleykum Sallaam WarahmatulLaah Wabarakatuh BismiLLaah wa AlhamduliLLaah was-Swalaatu wa Salaamu ‘alaa Muhammad wa ‘alaa  aalihi wa Aswhaabihil Kiraam, wa Ba’ad. *Maana ya Uchumba Kisheria* ✅Uchumba katika Uislamu ni pale *mwanamme anayetaka kuoa au jamaa zake au mtu yeyote aliyemwakilisha anapokwenda kwa wazazi wa msichana/Bint/Mwanamke* kuposa/kupeleka Barua na kukubaliwa. *✅Huo ndio unaitwa uchumba* ➡Ama kinyume na hivyo unakuwa ni urafiki baina ya mvulana na msichana. *Na hili katika Uislamu limekatazwa kwani ni Haramu* ✅Na hili limekatazwa kishari’ah. ➡Na hapo katika Swali lako umesema kwamba una Mchumba wako Lakini anakuwa mgumu *kuleta posa nyumbani* ina maana kuwa Huyo mwanaume *Kisheria si Mchumba wako kwasababu bado hajapeleka barua ya Posa nyumbani kwenu*

Tashahhud inayofaa

*Katika Tashahhud inafaa Kusema “Assalaamu ‘Alaan Nabbiy” Badala ya Kusema “Assalaamu ‘Alayka Ayyuhan Nabbiy”..?* ✅Naam,  Inaonekana kulingana na swali lako hukumuelewa vizuri huyo ndugu aliyekuambiwa hayo kwani katika Tashahhud hakuna kusema *Swallu 'alan Nabiy*. Hakuna riwaya hata ya kutungwa ambayo inatueleza hilo. ➡Hata hivyo, inaonyesha kuwa katika kuandika au kusikia ima ulisikia au uliandika makosa badala ya Assalaamu 'alan Nabiy ukasikia au ukaandika Swallu 'alan Nabiy. ➡Hili tamko ambalo umeliandika mara nyingi hutumiwa na baadhi ya watu katika mihadhara na mawaidha wakitaka kuwarudisha watu katika kusikiliza mawaidha kwa kusema Swallu 'alan Nabiy, ingawa haya ni mambo yasiyothibiti na yasiyo na dalili. Kwa hiyo, tutajaribu kukuelezea kwa mujibu wa haya marekebisho ambayo tumeyafanya ili kuwe na faida kwa wasomi wa tovuti hii yenu. ✅Uislamu  kama ulivyo umewekewa vitu sahali na vyepesi kwa maslahi yetu sisi binadamu. Jambo hili humfanya kila mwanadamu anaye

Masiyh Dajjal

Assallaaam Aleykum WarahmatulLaah Wabarakatuh Maana ya neno Masiyh (Masiya):   Kuna zaidi ya maoni hamsini ya kiwanazuoni yenye maana ya Masiyh. Wanasema kwamba neno hili linatumika sehemu zote kwa Aliyemkweli [Masiyh wa Kweli, yaani (Yesu)] na mpotoshaji aliye muongo [dhidi ya ‘Kristo’ ama Dajjaal]. Masiyh ndiye Mkweli, ‘Iysaa bin Maryam (Yesu mwana wa Mariyamu), Masiyh wa uongofu, aliyewaponya wale waliozaliwa vipofu ama viguru, na kuwafanya wafu kuwa hai kwa uwezo wa Allaah. Masiyh wa kuigiza (al-Masiyh ad-Dajjaal) ni muongo anayewaongoza watu kwenye uovu, Masiyh wa upotovu atawadanganya watu kwa namna alizojaaliwa, kama vile kuteremsha mvua, kuihuisha ardhi na kuifanya kuchipua mimea, na ‘miujiza’ mengineyo. Kwa hivyo, Allaah Amewaumba Masiyh wawili, ambao mmoja wao ni tofauti kwa mwengine. Wanazuoni wanasema kwamba sababu ya kwanini Dajjaal akaitwa Masiyh ni kwasababu moja kati ya macho yake ni  mamsuuh  (kimaana ni ‘lililo futika’; lililo tandazika au lililo kwaruzika, yaan

Swalah ya Sharuuq au Swalah ya Dhuhaa?

*Swalah ya Shuruuq ni sawa na Swalah ya Dhwuhaa* ✅Naam, Swalaatush-Shuruuq au Swalaatul-Ishraaq (Swalah baada ya kuchomoza jua). ➡Kutokana na fadhila zake kwamba⤵ ((عن أنس عن النبي صلى الله عليه وسلم ، أنه قال : من صلى الفجر في جماعة ثم قعد يذكر الله   حتى تطلع الشمس ثم صلى ركعتين كانت له كأجر حجة وعمرة تامة تامة تامة)) أخرج الترمذي  صححه الألباني “Imetoka kwa Anas kwamba Mtume ((Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema, Atakayeswali Alfajiri katika Jama'ah kisha akakaa anamkumbuka Allaah mpaka likachomoza jua kisha akaswali Raka'ah mbili, atapata ujira kama ujira wa kwenda Hajj na 'Umrah ulio kamili kamili kamili.” ↪Imetolewa na At-Tirmidhiy na kaisahihisha Al-Albaaniy ➡Inavyopaswa ni kukaa baada Swalah ya Alfajiri hadi jua litoke na upite wakati wa makruuh (unaochukiza kuswali) yaani wakati pale jua linapochomoza hasa, usubiri kama takriban dakika kumi na tano hadi ishirini hivi ndio uswali rakaa mbili. ⏩Ndio maana ikaitwa *Swalaatush-Shuruuq*, lakin

Fanya Ibadah kwa Wakati

*Fanya Ibadah kwa Wakati, Usipuuze* ✅Allaah (Subhaana wa Talaa) katika Surat An-Nisaa Aya ya 103 Anasema kwamba⤵ فَإِذَا قَضَيْتُمُ الصَّلَاةَ فَاذْكُرُوا اللَّـهَ قِيَامًا وَقُعُودًا وَعَلَىٰ جُنُوبِكُمْ ۚ فَإِذَا اطْمَأْنَنتُمْ فَأَقِيمُوا الصَّلَاةَ ۚ إِنَّ الصَّلَاةَ كَانَتْ عَلَى الْمُؤْمِنِينَ كِتَابًا مَّوْقُوتًا Mtakapomaliza Swalaah, mdhukuruni Allaah msimamapo, na mkaapo na mnapolala ubavuni mwenu Mtakapopata utulivu, simamisheni Swalaah (kama desturi), hakika Swalaah kwa Waumini ni fardhi iliyowekwa nyakati maalumu. ➡Maamrisho ya kutimiza Swalaah kwa wakati wake, na makemeo ya kuipuuza yamesisitizwa katika Qur-aan ana Sunnah na miongoni mwa Hadiyth za Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) ni⤵ ✅‘Abdullaah bin Mas'uwd  (رضي الله عنه)  amehadithia kwamba: Nilimuuliza Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم): Ni ‘amali gani inayopendeza kwa Allaah? Akajibu: “Ni kuswali kwa wakati wake.” Nikamuuliza tena: Kisha ni ‘amali gani? Akajibu: “Ni kuwafanyia ihsani wazazi

Maana ya Tawhiyd na Aina za Tawhiyd

بِسْمِ الله الرَّحْمنِ الرَّحِيم الْحمْدُ لِلَّه وَالصَّلاةُ وَالسِّلامُ عَلى خَاتم الأنْبِيَاء وَالْمُرْسَلِين، الْمَبْعُوثُ رَحْمَةً لِلْعَالَمِين، مُحَمَّد وَعَلى آلِه وَأصْحابِه أجْمَعِين وَمَنْ تَبِعَهُمْ بِإِحْسَانٍ إِلَى يَوْمِ الدِّينِ. Himdi Anastahiki Allaah, Swalaah na salaam zimfike Nabiy na Rasuli wa mwisho, aliyetumwa awe rahmah kwa walimwengu, Muhammad, pamoja na ahli zake na Maswahaba zake wote, na wanaowafuata kwa ihsaan mpaka Siku ya Malipo.   Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) Anasema: فَاعْلَمْ أَنَّهُ لَا إِلَـٰهَ إِلَّا اللَّـهُ  Basi jua kwamba: laa ilaaha illa Allaah (hapana muabudiwa wa haki ila Allaah)   [Muhammad: 19]     Maana ya Tawhiyd kama alivyosema ‘Allaamah ‘Abdir-Rahmaan Naaswir As-Sa’dy katika Al-Qawlus-Sadiyd Fiy Maqaaswidit-Tawhiyd - Sharh Kitaab At-Tawhiyd: “Tambua kwamba maana ya Tawhiyd haina mipaka. Ni maarifa na kukiri kumpwekesha Ar-Rabb (Mola) kwa Sifa za ukamilifu, na kuthibitisha kwamba Anapwekeshwa katika Sifa Zake Adhimu na Tukufu