Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Juni, 2019

Sababu zinazokubalika mwanamke kutoa Mimba/Ujauzito

SWALI Sababu gani ya kisheria inayopelekea mwanamke kutoa mimba na asipate madhambi...? MAJIBU Kutoa mimba ikiwa ni kabla ya kupuliziwa roho au baada ya kupuliziwa roho kisheria ni haraam. Wakati unaokubalika kutoa mimba ni pale tu itakapokuwa kuna dharura za kisheria ndipo panaweza kukubalika tena kwa masharti yake. Dharura hizo, ni kama kumehakikishika kuwa kuna uwezekana wa mama kufariki kwa kuwa na kiumbe hicho, au kuendelea kwake kuwa na mimba hiyo kutamletea mauti. Na isitoshe kukubalika huko, bali kumetakiwa uthibitisho huo utolewe na daktari mwenye kuaminika kabisa. Na muhimu kwanza atafutwe daktari Muislamu mwenye kuaminika, ikishindikana, basi daktari yeyote ambaye ni muaminifu sana. Ama kuitoa mimba tu kwa sababu ya kutotaka mtoto, au kukhofia riziki yake, au malezi yake, au kuchelea gharama za maisha kama kumsomesha, kumvisha, au kumlisha n.k. hayo yote hayaruhusiwi kisheria kwani Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) Anasema: “Wala msiwaue wana wenu kwa kuogopa umasikin

Surah Ngapi Zilizoteremshwa Madiynah Na Ipi Ya Kwanza

SWALI Ni surah ngapi zizotemremshwa madina, na ni ipi ya kwanza?  MAJIBU Shukrani zetu za dhati kwa ndugu yetu muulizaji swali. Wanachuoni wametofautiana kuhusu suala la Suwrah zilizoteremka Madiynah na zile za Makkah. Tofauti hiyo inakuja kwa Suwrah mbili (yaani Ar-Rahmaan [Suwrah ya 55) na Al-Insaan au Ad-Dahr [Suwrah ya 76]). Wengine wanasema mojawapo au zote mbili zimeteremshwa Makkah na wengine wanasema Madiynah. Hivyo, kwa tofauti hiyo wengine wanasema Suwrah zilizoteremshwa Madiynah ni 28, wengine 27 na wengine tena 26. ama Suwrah ya kwanza kuteremshwa Madiynah ni Al-Baqarah, ambayo kwa mpangilio wa Qur-aan ni Surah ya pili. Na Allaah Anajua zaidi

Tafsiyr ya Aayah “Na Arshi Yake Ikawa Katika Maji”

SWALI Naomba maelezo na mafundisho kutoka katika aya "wakaana arshuhuu ala-lmaai"  MAJIBU Shukrani zetu za dhati kwa swali lako kuhusu Arshi ya Allaah Aliyetukuka. Aayah hiyo inapatikana katika Surah Huud (11). Aayah yenyewe inasema hivi: وَهُوَ الَّذِي خَلَق السَّمَاوَاتِ وَالأَرْضَ فِي سِتَّةِ أَيَّامٍ   وَكَانَ عَرْشُهُ عَلَى الْمَاء  لِيَبْلُوَكُمْ أَيُّكُمْ أَحْسَنُ   عَمَلاً وَلَئِن قُلْتَ إِنَّكُم مَّبْعُوثُونَ مِن بَعْدِ الْمَوْتِ   لَيَقُولَنَّ الَّذِينَ كَفَرُواْ إِنْ هَذَا إِلاَّ سِحْرٌ مُّبِين Maana ya Aayah hiyo ni: “Na Yeye Ndiye Aliyeumba mbingu na ardhi katika siku sita;  na ikawa ‘Arshi Yake juu ya maji ; (kakuumbeni) ili Akujaribuni nani kati yenu mwenye ‘amali nzuri zaidi. Na kama ukisema: “Nyinyi mtafufuliwa baada ya mauti”; bila shaka watasema wale waliokufuru: “Hakika haya si chochote isipokuwa ni sihiri bayana." [11: 7]. Hebu tutazame hii ibara imefasiriwa vipi na Wanachuoni wetu wa tafsiyr. Ibn Kathiyr naye ame

Aina za Laana na Wepi waliolaaniwa na Allaah?

Swali NANI HASWA ANASTAHIKI KUAMBIWA LAANA ZA ALLAAH ZIWE JUU YAKO. JE NI MAKAFIR AU MURTADINA AU WANAAFIQ? JE KUNA LAANA YA MTU MMOJA MMOJA UA WENGI WENGI? JIBU Shukrani zetu za dhati kwa swali lako kuhusu mas-ala ya laana. Laana si kitu kumpata mtu yeyote yule na hasa akiwa ni Muislamu. Laana kutoka kwa Allaah au Mtume Wake inampata mwenye kuacha amri na yule aliyekengeuka na maagizo  yao . Allaah Aliyetukuka na Mtume Muhammad (Swalla Allaahu 'Alayhi wa aalihi wa sallam) wametutajia watu waliteremshiwa laana hizo. Hebu tutazame baadhi ya mifano: a)              Allaah Aliyetukuka Anasema: " Hakika Allaah Amewalaani makafiri na Amewaandalia Moto mkali " (33: 64). b)             Allaah Aliyetukuka Anasema: " Kama wanafiki na wale wenye maradhi nyoyoni mwao na watangazao uovu mjini, hawataacha upotofu, kwa yakini Tutakusalitisha juu  yao , kisha hawatakaa humo karibu yako ila muda kidogo tu. Maluuni (wamelaaniwa) hao popote waoneka

Kumtaliki mke ambaye mmekataa kufunika uso

Swali Ipi hukumu kwa mwanamke kuonesha uso wake? Mwanamke ambaye hasikii maneno ya mume wake na anafunua uso wake, je inajuzu kumtaliki? Jibu Ndio. Kufuniko uso ni wajibu.  Ni wajibu kwa mwanamke kufuniko uso wake kwa kuwandio ´Awrah kubwa kwenye mwili wake. Maono hutazama usoni mwa wanawake. Na wala hajulikani mwanamke mzuri kutokana na mbaya isipokuwa ni kwa (kutazama) uso wake. Uso ni fitina kubwa.  Ni wajibu kwa dada wa Kiislamu kufunika uso wake kutokana na wanaume ambao sio Mahaarim zake. Na wala asijali ushawishi wa washawishi leo hii ambao wanatatiza suala la mwanamke kufuniko uso wake. Hakika Dini yake ndio imemlazimisha hilo. Na kumcha Allaah na kumtii Allaah na Mtume Wake ndio ambao wamemlazimisha. Asijali upuuzi ambao unaenezwa hivi leo. Kufuniko uso kuna tofauti, kuna kadhaa na kadhaa. Wanachotaka ni mwanamke kuonesha uzuri wake au akae na wanaume naye ni mwenye kuonesha uzuri wa uso wake, wanja wake na vipodozi vya usoni mwake na kuka

Haijuzu imamu kuwaambia maamuma hivi kabla ya swalah

Baadhi ya maimamu wanasema: “Allaah haitazami safu iliyopinda.” Hii sio Hadiyth. Haijuzu kuwaambia watu maneno haya. Kwa kuwa ni kitu hakikuthibiti kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na wala hakina msingi. Msemo: “Allaah hatazami… “ ni katika sifa za Allaah. Kwa ajili hiyo haijuzu kulithibitisha isipokuwa kwa dalili. Inatosheleza kusema yale yaliyosemwa na Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam). Tukiona mtu amesogea mbele kidogo au amebaki nyuma kidogo tuseme: “Waja wa Allaah! Mtazisawazisha safu zenu au Allaah atatofautisha kati ya nyuso zenu.” Bi maana nyoyo zenu. Kuhusu kusema: “Allaah haitazami safu iliyopinda.” hata kama yanasemwa na baadhi ya maimamu, lakini hata hivyo ni jambo lisilokuwa na msingi na wala haijuzu kulisema watu wakaja kuitakidi kuwa ni Hadiyth kutoka kwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ilihali hayatoki kwa Mtume wa Allaah. Rejea Kitaab  al-Liqaa' ash-Shahriy (16)

Achana na mume asiyeswali kabisa

Swali Mimi nimeolewa na mwanaume mwenye kuacha swalah mwezi mzima, miezi miwili na haswali mpaka ijumaa. Siku moja nilikataa kulala nae na kukawa kumetokea baina yetu ugomvi ambapo akanitaliki talaka mbili. Nimechanganyikiwa na nachelea tunachokifanya mimi na yeye ni haramu. Naomba unielekeze na uelekeze wanaume sampuli hii pamoja na kuwa baba yangu hayajui yote yaliyopitika. Jibu Mwanaume ambaye haswali kabisa, si ijumaa wala swalah zengine, ni kafiri. Katika hali hii si halali kwa mwanamke kubaki nae sekunde hata moja. Allaah (Tabaarak wa Ta´ala) amesema: فَإِنْ عَلِمْتُمُوهُنَّ مُؤْمِنَاتٍ فَلَا تَرْجِعُوهُنَّ إِلَى الْكُفَّارِ ۖ لَا هُنَّ حِلٌّ لَّهُمْ وَلَا هُمْ يَحِلُّونَ لَهُنَّ “Mkiwatambua kuwa ni waumini, basi msiwarejeshe kwa makafiri; wao si wake halali kwao na wala wao waume hawahalaliki kwao.” (60:10) Kuhusu mwanaume ambaye wakati fulani anaswali na wakati mwingine haswali naonelea kuwa sio kafiri. Lakini hata hivyo ni mtenda dhambi kubwa.

Haijuzu kwa mke kubaki na mume kafiri asiyeswali

Swali Tatizo langu ni kuhusiana na mume wangu, ni mwanaume ambaye ana mapungufu katika Dini yake, haswali. Na pindi ninapomwita kuswali anakasirika na ananifanyia istihzai. Na anaendelea kuacha Swalah kwa hoja kuwa baba yake alikuwa haswali, hii ndio sababu na yeye haswali. Niliendelea na hali ya kumkumbusha na siku moja akanambia: “Ukiendelea kwa hali hii, mlango uko wazi”, hapo ndio nilifika namuomba Talaka. Na mara ya pili ilikuwa takriban sababu hiyo hiyo. Akanambia: “Usiniongeleshi mpaka siku ya Qiyaamah”. Ipi rai yako kwa mtu huyu na kwa maneno yake aliyosema kwa minasaba miwili, wa kwanza na wa pili? Je, huchukuliwa ni Talaka au nini? Na je, inajuzu kwangu kubaki nae katika hali hii? Jibu Mwanaume huyu haijuzu kubaki nae. Maadamu anaacha Swalah kama ulivyosema, kwa hilo anakuwa kafiri. Ikiwa baba yake naye haswali, kaiga kwake. Na wala haijuzu kumuiga kafiri asiyeswali, anatukana Dini, au anafanya kitu miongoni mwa vitu vinavyovunja Uislamu wa mtu au maasi

kuvumilia maudhi ya wanawake wanapokuwa wajawazito

Swali:  Mimi nilioa na tahamaki mke wangu akaniomba talaka kwa hoja kwamba hakuishi maisha ya starehe vile alivyotarajia. Mimi ni kijana na mwanafunzi vilevile ambaye hali yangu ni ya kawaida. Kuniomba kwake talaka kulikuwa ni pasi na haki na mimi sikuwa na nia ya kumtaliki kwa kuwa alikuwa ni mjamzito. Je, akiniomba talaka ni haki kwangu kurudishiwa mahari? Isitoshe mahari yenyewe ilikuwa ni misaada kutoka kwa watu. Je, ikiwa atanipa mahari hayo nina haki ya kuzitumia au nitatakiwa kuzirudisha kule nilikozichukua pamoja na kuwa mimi ni mwenye madeni tele yasiyojua yeyote isipokuwa Allaah pekee. Jibu:  Katika hali hii mwanaume akiweza kuwa na subira na asimjibu ndio bora zaidi. Hili ni kwa sababu mbili: Ya kwanza : Baadhi ya wanawake wanapokuwa na mimba wanawachukia waume zao. Wanawachukia waume zao hata kama ameishi naye miaka mingi. Kwa hivyo awe na subira juu yake mpaka yataisha. Huenda akarudi katika hali yake ya kawaida na yakamuondoka yaliyomkereta moyoni mwake.

Kaandika talaka kisha kaichana, je imepita?

Swali:  Mimi nimemuoa mwanamke ambaye anaasi amri zangu na wala hanitii kwa kitu. Na daima anatoka nyumbani bila ya idhini yangu nakwenda kufanya baadhi ya kazi ambazo zimenifanya kunighadhibisha na kufikiria kumtaliki. Ikawa nimeandika karatasi ambapo nimeandika kuwa “nimekutaliki Talaka mbili” na nikamtaja kwa jina lake na la baba yake. Wakati huo nilikuwa nyumbani peke yangu na sikuwa na yeyote. Lakini baada ya hapo nikawa nimeichana hiyo karatasi na wala hakuna yeyote aliyejua kilichokipitika wala yeye. Na wakati huo ili-kuwa ni kabla ya miezi mitano. Talaka imepita au hapana? Jibu:  Ndio, zimepita Talaka mbili. Ukimtaliki kwa kuandika au kwa kumtakia, Talaka inakuwa imepita hata kama hukushuhudisha. Lakini umebaki na Talaka moja, ikiwa ulikuwa hujamtaliki kabla ya hapo umebaki na Talaka moja. Unaweza kumrejea, na unaweza kumchumbia tena ikiwa kishatoka ndani ya eda. Muhimu ni kuwa kumebakia Talaka moja, ikiwa ulikuwa hujamtaliki kabla ya Talaka hii uliyoandika. Muuliza

Talaka za Bid´ah

Swali Tumejua kupitia barnamiji hii ya kwamba haipiti Talaka kwa mwenye hedhi na mwenye mimba. Je, ni kuwa haipiti kabisa au inapita baada ya Twahara? Jibu Talaka ya mwenye hedhi haipiti kutokana na kauli sahihi (yenye nguvu) ya wanachuoni, tofauti na kauli ya jamhuri. Jamhuri ya wanachuoni wanaona kuwa inapita. Hali kadhalika kwa mwenye nifasi.  Lakini kauli ya sahihi katika kauli za wanachuoni, na ndio waliokuwa wakifutu baadhi ya Taabi´iyn na Ibn ´Umar (Radhiya Allaahu ´anhumaa) na akaichagua Shayk-ul-Islaam bin Taymiyyah, mwanafunzi wake Ibn al-Qayyim na kundi katika wanachuoni, kuwa Talaka hii haipiti. Kwa kuwa inakwenda kinyume na Shari´ah ya Allaah, kwa kuwa Allaah Kawekea Shari´ah kumtaliki mwanamke katika hali ya Twahara ya nifasi, hedhi na katika Twahara ambayo mume wake hakumjamii.  Hii ndio Talaka ya Kishari´ah. Akimtaliki katika hedhi, nifasi au Twahara ambayo amemjamii, Talaka hii ni Bid´ah na wala haipiti kutokana na kauli ya sahihi ya

Mashahidi katika talaka

                      Mashahidi katika talaka Allaah (Subhaana wa Ta´ala) amesema kwamba: فَإِذَا بَلَغْنَ أَجَلَهُنَّ فَأَمْسِكُوهُنَّ بِمَعْرُوفٍ أَوْ فَارِقُوهُنَّ بِمَعْرُوفٍ وَأَشْهِدُوا ذَوَيْ عَدْلٍ مِّنكُمْ وَأَقِيمُوا الشَّهَادَةَ لِلَّـهِ “atakapokaribia kufikia muda wao, basi wazuieni kwa wema au farikianeni nao kwa wema na mshuhudishe mashahidi wawili wenye uadilifu katika nyinyi na simamisheni ushahidi kwa ajili ya Allaah. “65:02 Ameamrisha kuwepo mashahidi wakati mume atapomrejea mke. Ummah umeafikiana juu ya kwamba mashahidi wanatakiwa kuwepo. Wako waliosema kwamba maamrisho ni kwa njia ya uwajibu na wengine wamesema maamrisho ni kwa njia ya mapendekezo tu. Baadhi ya watu wamedhani kuwa ushahidi ni kwa ajili ya talaka na kwamba talaka haipiti isipokuwa mpaka kuwepo mashahidi. Haya yanakwenda kinyume na maafikiano, Qur-aan na Sunnah. Hakuna yeyote katika wanachuoni wanaotambulika aliyesema hivo. Mara ya kwanza talaka iliruhusiwa kwa kuwepo mashahidi