Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Novemba, 2018

Kufuga Ndevu

Kuachilia ndevu ni wajibu kwa wanaume kwa dalili zifuatazo: 1- Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) ameamuru kuziachilia. Amri hii ni ya lazima, kwani hakuna kiashirio chochote kinachoigeuza na kuipeleka katika usunnah. Na kati ya amri hizo ni neno lake Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam):   خالفوا المشركين: وفروا اللحى، وأحفوا الشوارب ((Kuweni kinyume na washirikina; fugeni ndevu kwa wingi na punguzeni masharubu))  [Hadiyth Sahihi: Imetolewa na Al-Bukhaariy (5892) na Muslim (259)] Na neno lake (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam):   جزوا الشوارب، وأرخوا اللحى، خالفوا المجوس ((Kateni masharubu na ziachilieni ndevu; nendeni kinyume na wanaoabudu moto))  [Hadiyth Sahihi: Imetolewa na Muslim (260)] 2- Ni kwamba kuzinyoa ni sawa na kujifananisha na makafiri kama inavyoonekana katika Hadiyth mbili zilizotangulia. 3- Ni kwamba kuzinyoa ni sawa na kuubadilisha Uumbaji wa Mwenyezi Mungu na kumtii Shaytwaan

Adabu za Kisheria katika Dini

                                           Assallaam  Aleykum  WarahmatulLaah  Wabarakatuh Shari’ah ya Kiislamu imeasisi na kulingania ustaarabu mbali mbali wa jamii. Wakati huo huo, imetahadharisha kuwepo adhabu siku ya Qiyaamah pindipo mtu atakaposhindwa kushikamana na Shari’ah hizo. Imaam Muslim amepokea kwamba Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema:  ((Je munamjua nani muflisi?))  Walijibu:  ((Muflisi miongoni mwetu ni yule ambaye hana pesa wala mali.))  Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akasema:  ((Muflisi ndani ya ummah wangu ni yule anayekuja siku ya Qiyaamah akiwa na Swalah, Zakaah na Swawm, hata hivyo alikuwa akivunjia heshima, kusengenya, kutukana na kuwapiga wengine. Hivyo wenye kumdai wanalipwa kutokana na matendo yake mazuri. Iwapo mema yake yamemalizika, anaadhibiwa kwa matendo yao maovu hadi pale anapotupwa Motoni.)) 1. Adabu za Kula: a.     Anza kula kwa jina la Allaah (BismiLlaahir Rahmaanir Rahiym) na malizia kwa kumhimi

Tiba ya Talbiynah

Talbiynah  Inatuliza Moyo Na Kuondosha Baadhi Ya Huzuni Talbiynah  ni uji unaotokana na unga unaosagwa wa shayiri.     Talbiynah katika Sunnah ilikuwa ikitumiwa zaidi katika misiba kwa ajili ya kuondosha baadhi ya huzuni kwa dalili ya Hadiyth zifuatazo: عَنْ عَائِشَةَ رضى الله عنها أَنَّهَا كَانَتْ تَأْمُرُ بِالتَّلْبِينِ لِلْمَرِيضِ وَلِلْمَحْزُونِ عَلَى الْهَالِكِ، وَكَانَتْ تَقُولُ: إِنِّي سَمِعْتُ رَسُولَ اللَّهِ صلى الله عليه وسلم يَقُولُ: ((إِنَّ التَّلْبِينَةَ تُجِمُّ فُؤَادَ الْمَرِيضِ، وَتَذْهَبُ بِبَعْضِ الْحُزْنِ)) Imepokelewa kutoka kwa ‘Aaishah (Radhwiya Allaahu ‘anhaa) kwamba alikuwa akiamrisha  talbiynah  kwa ajili ya mgonjwa na mtu aliyefikwa na huzuni kwa ajili ya kufariki mtu wake. Akawa anasema: “Nimesikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: ((Hakika  talbiynah  inamtuliza moyo wa mgonjwa na kuufanya mchangamfu na inaondosha baadhi ya huzuni zake))  [Al-Bukhaariy,  Kitaab Atw-Twibb,  Baab At-Talbiynah Lil-