Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Septemba, 2017

Aqiydah Iwe Mwanzo

Assallaam Aleykum WarahmatulLaah Wabarakatuh   Jambo la kwanza, kubwa, na la msingi katika kulingania watu kumtii Allaah, na kwa nini ‘Aqiydah iwe mwanzo.   ‘Aqiydah ni lazima ije mwanzo kwa sababu, kinachozusha mgawanyiko na maangamizi katika ulimwengu wa Kiislamu ni kukosekana ‘Aqiydah iliyo sahihi.     Kwa Nini ‘Aqiydah Liwe Ni Jambo La Mwanzo ?   Hakika ‘Aqiydah lazima ije mwanzo kwa sababu ni msingi wa Da’wah ya Mitume wote kama Allaah Alivotuma ujumbe Wake kupitia kwa Mitume Wake. Kama Anavyosema Allaah kwa kupitia kwa ulimi wa kila Mtume Aliyemtuma kwa watu wake: “Enyi watu! Muabuduni Allaah, hamna mungu isipokuwa Yeye” (Surat Huud 11: 84)   ‘Aqiydah lazima ije mwanzo kwa ajili ya kuepukana na kizuizi cha kubakia motoni (Jahannam) milele na kujiepusha na adhabu hiyo. Hamujasikia maneno ya Allaah Aliyetukuka: “Hakika Allaah hasamehe kushirikishwa, na husamehe yaliyo duni ya hilo kwa Amtakaye. Na anayemshirikisha Allaah basi hakika amezua dhambi kubwa” (Suratun

Kufunga Jumamosi Inapoangukia Siku Ya 'Arafah Au 'Aashuraa

SWALI LA KWANZA   Assalamu Alaykum Warahmatullahi Wabarakatu. Shukran kwa kazi zenu munazofanya kuelimisha umma. Tumeelezewa kwamba haifai mtu kufunga saum ya sita katika siku ya jumamosi, je hii ni sawa. Je ikiwa nafunga saum ya 13, 14 & 15 ikiangukia jumamosi nifunge au vipi? Shukran   SWALI LA PILI Eti kufungua Jumamosi haifai hata ikiwa ni siku ya Arafa au Ashoora?   Majibu   Waleykum Salaam WarahmatulLaah Wabarakatuh Sifa zote njema Anastahiki Allaah(Subhaanahu wa Ta'ala) Aliyetukuka Mola wa walimwengu wote, Swalah na salamu zimshukie kipenzi chetu Mtume Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihiwa sallam) na Swahaba zake (Radhwiya Allaahu ‘anhum) na watangu wema mpaka Siku ya Mwisho.   Tunawashukuru ndugu zetu waliouliza maswali hayo ambayo kwa nyakati za karibuni limeleta utata sana baina ya Wenye elimu, Wanafunzi na pia Waislamu wa kawaida.   Utata huu umesababishwa na kufahamika Hadiyth hii kuwa ni ya makatazo katu, nayo inasema: Kutoka kwa 'Abdull

Uzushi Unaodaiwa Kuhusu Mambo Yaliyotokea Siku Ya 'Aashuraa Tarehe 10

*Swali*   Asalam aleikum Nataka kujua kutoka kwenu Alhidaaya kuhusu haya mambo kuwa yametokea siku ya tarehe 10 Muharam, je ni kweli? Na upo ushahidi  wake? Mambo yenyewe ni  haya 1-Nabi Adam aliumbwa siku hii 2- Allah alipokea toba ya nabi Adam 3- Nabi Ibrahim alipewa daraja ya kuwa ni khalil wa Allah. 4-Nabi Ayub aliponeshwa 6- Nabi Musa aliokolewa na Firauni 5 Jahazi ya Nabi Nuuh ilitua katika ardhi kavu 7-Nabi Suleman alipewa ufalme 8-Nabi Yaqub alionana na Yusuf baada ya miaka 40 9-Nabi Yunus alitolewa katika tumbo la nyangumi baharini. 10-Nabi Idrees alipandishwa mbinguni 11-Nabi Isa alipandishwa mbinguni 12-Siku ya kiyama kitatokea tarehe 10 Muharam 13-Bahari na mbingu zilumbwa 14-Mtu akioga siku hii hatoumwa tena. 15-Huu ni mwezi wa huzuni, hivyo mtu asiowe au kuolewa wala asiwe na furaha ya lolote. 16-Kupikwa chakula maalum katika siku hii ya Ashuraa. 17- Kuomboleza kifo cha Imam Husein siku ya leo na kujipiga mwili pamoja na kujikatakata Nitashukuru kupa

Hukumu ya Kuapa kwa Asiyekuwa Allaah(Subhaana wa Taala)

Assallaam Aleykum WarahmatulLaah Wabarakatuh Naam,Ndugu zangu katika Imaani,kwanza kabisa #Haijuzu Muislamu kuapa isipokuwa kwa Jina la Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) kwa sababu kuapia kwa yeyote au chochote ni kumshirikisha Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa). ✅Inavyopasa kuapa ni ima kusema: “Wa-Allaahi”, au “BiLLaahi” au “Ta-Allaahi” kama ilivyothibiti katika Qur-aan. ✔Na Mtume Muhammad(Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amekataza kuapia chochote isipokuwa kwa Jina la Allaah akasema⤵  مَنْ حَلَفَ بِغَيْرِ اللَّهِ فَقَدْ كَفَرَ أَوْ أَشْرَكَ ((Atakayeapa pasi na Allaah, atakuwa amekufuru na amemshirikisha Allaah)  ↪Imepokelewa na Imaam Abu Daawuwd, At-Tirmidhiy, Ibn Hibbaan, Al-Haakim na wengineo na ameipa daraja ya Swahiyh Al-Albaaniy   ⏩Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Pekee Ndiye Mwenye haki kuapia Atakacho kwani Yeye ni Muumba wa kila kitu. ⏩Ndio maana Anaapia katika Qur-aan vitu vingi; Wa-Tiyni waz-Zaytuni, Wal-‘Aswr, Wadh-Dhwuhaa, Wash-Shamsi, Wal-Layl

Kisa cha Al-Husayn Bin 'Aliy (Radhiya Allaahu 'anhu)

Assallaam Aleykum WarahmatulLaah Wabarakatuh Naam, Ndugu zangu Katika Imaani Leo ninawaletea kisa cha Imaam Hussein kama ifuatavyo⤵   Jina lake ni Al-Husayn bin 'Aliy bin Abi Twaalib bin 'Abdil-Muttwalib bin Haashim bin Manaaf bin Qusay kutoka katika kabila la Ki-Quraysh tumbo la Bani Haashim, na umaarufu wake ni; 'Abu 'Abdullaah' na maana yake ni Baba yake 'Abdullaah.   Al-Husayn  ( Radhwiya Allaahu 'anhu )  ni mjukuu wa Mtume wa Allaah  ( Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam )  na kipenzi chake, mtoto wa pili wa 'Aliy bin AbiTwaalib  ( Radhwiya Allaahu 'anhu ) na mama yake ni Bibi Fatimah binti wa Mtume wa Allaah  ( Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam ) .   Ndugu zake ni wengi, lakini mashuhuri katika hao ni kaka yake Al-Hasan bin 'Aliy  ( Radhwiya Allaahu 'anhuma )  Khalifa wa tano wa Waislamu.   Amesema Ja'afar Asw-Swaadiq ( Radhwiya Allaahu 'anhu ): "Baina ya Al-Husayn na Al