Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Machi, 2019

Kufupisha kumswalia Mtume Muhammad (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kwa Mfumo wowote Haijuzu

   Kufupisha kumswalia Mtume Muhammad (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kwa Mfumo wowote Haijuzu Imaam Ibn Baaz (Rahimahu Allaah) amejibu kuhusu swali la hukmu ya kufupisha kumswalia Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): “Kama ilivyoamrishwa kumswalia Mtume Muhammad (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kwenye Swalaah katika Tashahhud, na imeamrishwa katika kutoa khutbah na kuomba Du’aa na kuomba maghfirah, na baada ya Adhaan, na wakati wa kuingia na kutoka Msikitini, na wakati wa kumtaja katika hali nyinginezo, hivyo basi ni muhimu zaidi kufanya hivyo katika kumtaja jina lake katika kitabu, barua, makala n.k.  Kwa hiyo, imeamrishwa kuandika Swalaah na Salaam kwa ukamilifu ili kutimiza amri ya Allaah ('Azza wa Jalla)  Aliyotuamrisha na ili msomaji apate kukumbuka kutaja kumswalia Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)  anapoisoma. Hivyo tusiandike Swalaah na Salaam kwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aa

Hukmu ya kuishi na Mke asiyeswali

SWALI Ni ipi hukmu ya mke asiyeswali, kwa kutambua kuwa nimeshambainishia adhabu anayopata mwenye kuacha kuswali, kuna baadhi ya nyakati anaswali na wakati mwengine anaacha. Kwa mfano anaswali Adhuhuri na anaacha (Swalaah) zote za Faradhi zilizobaki? JIBU Hukmu yake ni Kafiri. Na haijuzu kuendelea kubaki naye katika hifadhi yako. Inapasa kuwa naye mbali, isipokuwa kama atatubu tawbah ya kweli, la sivyo, ni waajib kuwa naye mbali (kuachana naye). Kwa sababu kuacha Swalaah ni ukafiri mkubwa. Anasema Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam): “Baina ya mtu na baina ya ushirikina na ukafiri ni kuacha Swalaah.”  [Muslim] Na anasema (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam): “Agano (Kinachotutofautisha) baina yetu (Waumini) na baina yao (Washirikina, Makafiri na Wanafiki) ni Swalaah, anayeiacha (Swalaah) amekufuru.”   [At-Tirmidhiy, Ibn Maajah na An-Nasaaiy] Hii ndio kauli sahihi katika kauli za Wanachuoni; kwamba kuiacha (Swalaah) ni ukafi

Maana ya Duaa ya ufunguzi wa Swalaah

                          Maana ya Duaa Ya ufunguzi wa Swalaah  " Wa Ta’ala Jadduka" SWALI Nini maana ya kauli yetu katika du’aa ya ufunguzi wa Swalaah:    وَتَعـالى جَـدُّكَ    Wwa Ta’ala Jadduka   Na Umetukuka Ujalali Wako JIBU     Maana yake ni:  Ukubwa, Uadhama, Ujalali kama Anavyosema Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) katika Suwratul Jinn kuhusu majini: وَأَنَّهُ تَعَالَىٰ جَدُّ رَبِّنَا مَا اتَّخَذَ صَاحِبَةً وَلَا وَلَدًا ﴿٣﴾   “Na kwamba hakika umetukuka kabisa Ujalali wa Rabb wetu, Hakujifanyia mke wala mwana .” [Al-Jinn: 3]     [Majmuw’ Al-Fataawaa 11/74] Du’aa hiyo ya ufunguzi wa Swalaah kikamilifu ni: سُبْـحانَكَ اللّهُـمَّ وَبِحَمْـدِكَ وَتَبارَكَ اسْمُـكَ وَتَعـالى جَـدُّكَ وَلا إِلهَ غَيْرُك Subhaanaka-LLaahumma wabihamdika watabaarakas-Smuka wa Ta’aalaaa Jadduka walaa ilaaha Ghayruka Utakasifu ni Wako Ee Allaah, na Himdi ni Zako, na Limebarikika Jina Lako, na Umetukuka Ujalali Wako, na hapana muabudiwa wa haki,

Kuzishikilia Sunnah kwa Magego

                                              Kuzishikilia Sunnah kwa Magego  عن أبي نَجِيح الْعِرْبَاضُ  بن سارية (رضي الله عنه) قال: وَعَظَنَا رَسُولُ اللَّهِ (صلى الله عليه و آله وسلم) مَوْعِظَةً بَلِيغَةً وَجِلَتْ مِنْهَا الْقُلُوبُ  وَذَرَفَتْ مِنْهَا الْعُيُونُ. فَقُلْنَا:  يَا رَسُولَ اللَّهِ كَأَنَّها مَوْعِظَةُ مُوَدِّعٍ فأوْصِنا. فَقَالَ: ((أُوصِيكُمْ بِتَقْوَى اللَّهِ وَالسَّمْعِ وَالطَّاعَةِ وَإِنْ تأَمَّرَ عَلَيْكُم عَبْدٌ حَبَشِيّ  ،  وَأَنَّهُ مَنْ يَعِشْ مِنْكُمْ فَسَيَرَى اخْتِلاَفًا كَثِيرًا  ،  فَعَلَيْكُمْ بِسُنَّتِي وَسُنَّةِ الْخُلَفَاءِ الرَّاشِدِينَ الْمَهْدِيِّينَ  ،  عَضُّوا عَلَيْهَا بِالنَّوَاجِذِ وَإِيَّاكُمْ وَمُحْدَثَاتِ الأُمُورِ فَإِنَّ كُلَّ بِدْعَةٌ ضَلاَلَةٌ))  رواه أبو داوود والترمذي وقال حديث حسن صحيح Imepokelewa kutoka kwa Abuu Najiyh Al-‘Irbaadhw bin Saariyah ( رضي الله عنه ) amesema: Rasuli wa Allaah ( صلى الله عليه وآله وسلم ) alitupa mawaidha mazito (yenye maana kubwa), nyoyo zikaogopa na macho yakabubujikwa machozi. Tukasema: Ee R

Misingi ya Fiqh'i

▶MISINGI YA FIQHI◀ Assallaam Aleykum Warahmatullah Wabarakatuh Ndugu zangu katika Imaani. 🖌Naam ndugu zangu katika Imani,Baada ya kueleza katika Darsa iliyopita Maana ya FIQH ki Lugha na Maana ya Wanachuoni wa Fani hii vile vile kutaja MISINGI YA FIQ-HI,muda huu tunaendelea katika kueleza Maana ya Kila Msingi katika Misingi ya Elimu hii ya FIQH. 1⃣QUR-AN ➡Qur-an Tukufu ni kitabu kilichokusanya maneno matukufu ya Mwenyezi Mungu alichoshushiwa Mtume wa mwisho, Nabii Muhammad kupitia kwa Malaika Jibril ili kiwe ni sheria na muongozo kwa wanadamu wote. 2⃣HADITH(SUNNAH) ➡Hadith ni tafsiri sahihi na ufafanuzi kamili wa Qur-ani Tukufu uliotolewa na Bwana Mtume Muhammad (Swalla Allaahu Aleyhi wa Sallaam)kwa njia ya vitendo, maneno na "IQRAARI". 🖌"IQRAARI" ni kitendo cha Bwana Mtume kumuona mtu akitenda jambo fulani, kisha Mtume asitoe maelekezo yoyote ya kukemea au kukataza. Ukimya huu wa Mtume hutafsirika kuwa jambo lile linafaa kwani Mtume hawezi kulinyamazia jam

Kusafiri bila Mahram kwa ajili ya kwenda kumtembelea mzazi

Swali Mwanamke huyu anauliza kama inajuzu kwake kusafiri bila Mahram kwa ajili ya kwenda kumtembelea mama yake anayeishi katika mji wa kikafiri kwa kuzingatia ya kwamba mama yake hana mtu mwengine huko? Jibu Haijuzu kwake kusafiri pasi na kuwa na Mahram. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema: “Si halali kwa mwanamke anayemuamini Allaah na siku ya Mwisho kusafiri isipokuwa awe pamoja naye Mahram.” Rejea Kitab  Sharh Ighaathat-il-Lahfaan (68)   Na  Allaah  anajua  zaidi

Mwanamke anaweza kusafiri na mwanamke mwenzake?

Swali Mwanamke anaposafiri hali ya kuwa pamoja naye yuko na mwanamke mmoja tu. Katika hali hii, Mahram anakuwa si wajibu kwake? Jibu Hapana Haijuzu.  Uwajibu bado uko pale pale. Kwa kuwa Mtume Muhammad(Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) anasema: “Si Halali kwa mwanamke anayemwamini Allaah na siku ya Mwisho, kusafiri isipokuwa awe pamoja naye Mahram.” Na makusudio ya Mahram, ni yule ambaye imeharamishwa kwake kumuoa. Na makusudio hapa anaingia mume vile vile. Na  Allaah  anajua  zaidi

Je, inajuzu kwa mwanamke kufanya kazi katika idara za serikali kwa hoja hana ambaye atampa matumizi?

Swali Je, inajuzu kwa mwanamke kufanya kazi katika idara za serikali kwa hoja hana ambaye atampa matumizi? Jibu Katika hali kama hii, haijuzu. Kwa kuwa atachanganyika na mudiri, raisi na atachukua ujira kutoka kwake.  Hili halijuzu. Mwanamke anazingatiwa kuwa ni fitina.  Na Mtume Muhammad(Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) anasema: “Mwanamke ni ´Awrah (uchi), Pindi anapotoka nje, matumaini ya Shaytwaan huongezeka.” وَإِذَا سَأَلْتُمُوهُنَّ مَتَاعًا فَاسْأَلُوهُنَّ مِن وَرَاءِ حِجَابٍ “Na mnapowauliza (wake zake) haja, waulizeni nyuma ya pazia.” (33:53) Hata kama Aayah hii inawahusu wake za Mtume Muhammad(Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam).  Hata hivyo, inawagusa wanawake wote, kama alivyosema Shaykh ash-Shinqiytwiy (Rahimahu Allaah). Mimi ninawanasihi kina dada, bali nasema kuwa haijuzu kufanya kazi katika idara kama hizi ambazo zina mchanganyiko na fitina. Hali kadhalika Hospitali za mchanganyiko, tunawanasihi kujiweka mbali na haya. Na 

Mwanamke kufanyakazi ya duka

Swali Inajuzu kwa mwanamke kufanya kazi kama keshia kwenye duka ikiwa amelazimika kufanya hivo? Jibu Hapana, haijuzu kwake kufanya hivo. Anatakiwa kufanya kazi tu ambazo zinahusiana na wanawake.  Hatakiwi kufanya kazi ambazo zina wanaume na wanawake. Rejea Kitab  Sharh Ighâthat-il-Lahfân (69)  

Mwanamke kufanyakazi katika mgahawa mchanganyiko

Swali Je, inafaa kwa mwanamke wa Kiislamu anayeishi nje ya nchi hii kufanya kazi kwenye mgahawa ulio na mchanganyiko kati ya wanaume na wanawake? Jibu Hapana HAIJUZU .  Ikiwa kuna kitengo kilichowekwa maalum kwa wanawake tu basi hakuna neno. Mwanamke Asiwahudumie wanaume. Rejea Kitab  Sharh Ighaathat-il-Lahfaan (68)  

Mwanamke aliacha swawm idadi nyingi na sasa anataka kulipa

Swali Mwanamke huyu anasema kuwa mpaka sasa hajalipa deni lake la Ramadhaan kwa miaka mingi. Ni lipi linalomlazimu hivi sasa? Jibu Ni lazima kwake kulipa kile kilichompita. Akisema kuwa hajui ni idadi ngapi zilizompita, tunamwambia afanye lililo salama na akadirie halafu baada ya hapo alipe kile kilichompita.  Hana juu yake kulisha chakula au kutoa swadaqah kwa mujibu wa maoni yenye nguvu. Kinachomlazimu ni yeye kulipa zile siku ambazo zilizompita. Rejea Kitab  al-Liqaa' ash-Shahriy (25)

Kinachowalazimu wanaochelewesha kulipa siku zao za Ramadhaan

Swali Mwanamke akila siku moja ya Ramadhaan na akachelewa kuilipa mpaka akaingiliwa na Ramadhaan nyingine – ni kipi kinachomlazimu hivi sasa? Jibu Ikiwa alichelewesha kulipa kwa sababu ya udhuru mpaka akaingiliwa na Ramadhaan ya pili hakuna kinachomlazimu isipokuwa kulipa baada ya kumaliza hiyo Ramadhaan ya pili.  Ama ikiwa alichelewesha pasi na udhuru basi analazimika kufanya mambo mawili: 1- Kulipa. Ni lazima kwake kulipa baada ya Ramadhaan aliyomo. 2- Kulisha masikini kwa kila siku moja. Hii ni kafara kwa kule kuchelewesha. Rejea Kitab  Sharh Thalaathat-il-Usuwl (07)

Ameacha kufunga miaka 10 kwa sababu ya mimba na kunyonyesha

Swali Kuna mwanamke aliacha kufunga Ramadhaan kwa muda wa miaka kumi kwa sababu ya mimba na kunyonyesha kwa sababu ya kuchelea afya na mtoto wake. Baada ya hapo akatubia. Je, tawbah inatosha au kuna kitu kingine kinachomlazimu? Jibu Ndio. Tawbah inatosha kwa sharti alipe yale masiku anayodaiwa. Akilipa masiku anayodaiwa itatosha.  Halazimiki kulisha kwa mujibu wa maoni yaliyo na nguvu miongoni mwa maoni mbalimbali ya wanachuoni. Wako wanachuoni wanaosema mtu akila na akachelewesha kulipa mpaka akaingiliwa na Ramadhaan ya pili bila udhuru wowote basi ni wajibu kwake kulipa na kulisha.  Lakini maoni sahihi ni kwamba halazimiki kulisha na kwamba kufunga kunamtosha. Rejea Kitab A l-Liqaa' ash-Shahriy (44)  

Ni ipi hukumu ya wudhuu´ wa mwanamke aliyepaka rangi ya kucha?

Swali Ni ipi hukumu ya wudhuu´ kwa yule ambaye kwenye kucha zake amepaka rangi ya kucha? Jibu Rangi ya kucha ni kitu anachopaka mwanamke juu ya kucha na ni kitu kilicho na ukoko. Haijuzu kwa mwanamke kuitumia kipindi ambapo anaswali kwa kuwa inazuia maji kufika kwenye ngozi wakati wa kutawadha. Kila kitu kinachozuia maji kufika kwenye ngozi haijuzu kwa mwenye kutawadha kukitumia. Kwa kuwa Allaah amesema: فَاغْسِلُوا وُجُوهَكُمْ وَأَيْدِيَكُمْ “Hivyo basi osheni nyuso zenu na mikono yenu mpaka kwenye visugudi.” (05:06) Mwanamke huyu ambaye amepaka juu ya kucha zake rangi ya kucha yanazuia maji kufika kwenye ngozi. Kwa hivyo hawezi kusadikishwa ya kwamba ameosha mikono. Katika hali hiyo anakuwa ameacha kiungo cha faradhi wakati wa kutawadha au wakati wa kuoga. Kuhusu wale wasioswali, kama mfano wa mwanamke mwenye hedhi, hakuna neno kuitumia. Isipokuwa ikiwa kama rangi hii ni katika mambo maalum ya makafiri. Katika hali hiyo itakuwa haijuzu kwa kuwa itakuwa ni kuji

Kujifunza elimu ya Kishari´ah ni nuru

            Kujifunza elimu ya Kishari´ah ni nuru Kwa hali yoyote, kujifunza elimu ni jambo lisilokuwa na shaka kwamba ndio maisha na nuru iliyoamrishwa na Allaah (Jalla wa ´Alaa), ikaamrishwa na Mtume Wake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na wakakokoteza kwayo. Amesema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam): “Mwenye kushika njia akitafuta humo elimu, basi Allaah humsahilishia njia ya kuelekea Peponi. Hawakusanyiki watu katika nyumba miongoni mwa nyumba za Allaah, wakikisoma Kitabu cha Allaah na wakadarasishana baina yao, isipokuwa huteremka juu yao utulivu, rehema huwafunika, Malaika huwazunguka na Allaah huwataja kwa wale walioko pamoja Naye.”[1] Amesema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam): “Malaika hukunjua mbawa zao kwa mwenye kutafuta elimu hali ya kuridhia kile anachokifanya.” Haya ni makokotezo juu ya kujifunza elimu na kuikimbilia ili dini ya mja iweze kunyooka, anufaike mwenyewe na pia awanufaishe wengine. Ni jambo lisilokuwa na shaka ya kwamba ikitoweka elimu