Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Desemba, 2018

Kuzidisha kheri

Assallaam Aleykum WarahmatulLaah Wabarakatuh Baada ya Allaah Kufaradhisha kufunga Ramadhaan, Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akawashaji´isha kuifuatisha Ramadhaan kwa kufunga siku zile za Shawwaal. Amefanya hivi ili ujira wao uweze kuwa mkubwa na ili waweze kulipwa kama aliyefunga mwaka mzima. Abu Ayyuub al-Answaariy (Radhiya Allaahu ´anhu) ameeleza kwamba Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema: “Anayefunga Ramadhaan na akaifuatisha kwa kufunga siku sita za Shawwaal, ni kama amefunga mwaka mzima.” Haafidhw al-Mundhiriy amesema: “ Ameipokea Muslim, Abu Daawuud, at-Tirmidhiy, an-Nasaa´iy, Ibn Maajah na at-Twabaraaniy amezidisha na kusema: “Nilisema: “Kila siku hulipwa kwa kumi.” Akasema: “Ndio.” Wamepokezi wake ni wapokezi sahihi. Mwaka hauwezi kuzidi siku 360. Siku sita za Shawwaal zikiwekwa katika Ramadhaan nzima na kila siku moja inalipwa kwa thawabu kumi (kwa kuwa tendo moja zuri linalipwa mara kumi) Waislamu wanazingatiwa kuwa wame

Msimu katika misimu ya Aakhirah

Assallaam  Aleykum  WarahmatulLaah  Wabarakatuh Kama jinsi Allaah Amevyofadhilisha baadhi ya watu juu ya wengine na baadhi ya sehemu juu ya zingine, kadhalika Amefadhilisha baadhi ya zama kuliko zingine. Miongoni mwa hayo Amefadhilisha mwezi wa Ramadhaan uliobarikiwa kuliko miezi mingine. Ameutofautisha na miezi mingine na Kuuchagua kuwa ni mwezi wa wajibu kwa watu kufunga:  ُ ار َ ت ََيْ َ و ُ َ َشاء ا ي َ م ُ لُق َك ََيْ ُّ ب َ ر َ و “Na Mola wako Anaumba Atakavyo, na Anachagua (Atakavyo).”28:68 Allaah Ameufadhilisha mwezi huu na Kuufanya kuwa ni msimu bora. Humo wanashindishana waja katika kumwabu Allaah ili waweze kufikia mafanikio na kujikurubisha kwa Allaah. Wanajikurubisha kwa Mola Wao kwa kufunga mchana na kusimama usiku na kusoma Kitabu Chake Kitukufu ambacho haitokifikia ubatili mbele yake na wala nyuma yake; ni uteremsho kutoka kwa Mwenye hikmah wa yote daima na Mwenye kustahiki kuhimidiwa. Wanajikurubisha kwa Allaah kupitia hicho na utiifu mwingine wote. L

Dunia ni nyumba ya majaribio na mtihani

Assallaam  Aleykum  WarahmatulLaah  Wabarakatuh Allaah Ameumba viumbe Wake ili wamwabudu Yeye Mmoja asiyekuwa na mshirika. Amesema katika Kitabu Chake Titukufu:  ُونِ د ُ ب ْ ع َ ي ِ َّل ل َِّ إ َ نس اْْلِ َ ن و َّ ُت ا ْْلِ ْ لَق َ ا خ َ م َ و “Na Sikuumba majini na wanadamu wa isipokuwa waniabudu.”51:56  Ametuma Mitume Wake watukufu ili wawaoneshe waja njia ya ´ibaadah:  َ و َ ه َّ ُوا الل د ُ ب ْ اع واَّل أَنِ ُ رس َّ ٍ َّمة ا ِِف ُك ِّل أُ َ ن ْ ث َ ع َ َ ْد ب لَق َ َت و اغُو َّ وا الط ُ ب ِ ن َ ت ْ اج “Na kwa yakini Tulituma katika kila ummah Rasuli (awaamrishe watu wake) kwamba: “Mwabuduni Allaah na jiepusheni na twaaghuwt (miungu ya uongo).”16:36 Amefanya maisha ya dunia kuwa ni sehemu ya majaribio yao na mtihani ili waoneshe ni nani katika wao alie na matendo mazuri:  ال َ َم ع ُ ن َ ْس أَح ْ ُّ ُكم أَي ْ ُكم َ لُو ْ ب َ ي ِ ل َ اة َ ي َ ا ْْل َ ْ َت و و َ الْم َ لَق َ ي خ ذِ َّ ال “Ambaye Ameumba mauti na uhai ili Akujaribuni ni nani kati yenu mwenye ‘ama

Duaa Sahihi ya Tashahhud

Swali tulifundishwa madrasa kusema ( athahiyathu, almubarakathu, aswalawathu, athwayibathu lillah....) je hivi ni makosa, maana maagizo yanasema ( athahiyatu lillah, waswalawathu, wathwayibathu..) Jibu Ulivyotaja mwanzo wa hizo du'aa za Tashahhud, zote mbili zimethibitika kuwa Amezisoma Mtume  صلى الله عليه وآله وسلم    kutokana na uthibitisho unaopatikana katika kitabu cha Swiffatus-Swalaatun-Nabiyy (Swifa za Swalah ya Mtume  صلى الله عليه وآله وسلم  ) kilichoandikwa na mtaalamu ma'arufu wa Ahlus-Sunnah Sh Albani (Allaah  سبحانه وتعالى Amrehemu) 1)          Tashahhud ya Ibn 'Abbas ambaye amesema,   ((Mtume  صلى الله عليه وآله وسلم alikuwa akitufundisha Tashahhud kama  alivyokuwa akitufundisha (surah za) Qur'aan.  Alikuwa akisema: Attahiyaatul-Mubaarakaatus-Swalawaatut-Twayyibaatu Lillah, Assalaam 'Alayka Ayyuhan-Nabiyyu WarahmatuLLahi Wabrakaatuh.  Assalaamu ' Alaynaa Wa  'Alaa 'Ibaadil-Llahis-Swaalihiyn.  Ash-h

Du'aa za Qunut ni Lazima zisomwe katika Swalah ya Alfajiri?

Swali swali langu ni kwamba dua hii ya Qunut ni lazima iombwe usiku baa ya kusali rakaa mbili au unaweza ukaomba wakati wowote? Pia naomba unipatie dua yenyewe kama  iko tofauti na ile isomwayo katika swala ya alfajir. Jibu BismiLLaah wa AlhamduliLLaah was-Swalaatu wa Salaamu ‘alaa Muhammad wa ‘alaa  aalihi wa Aswhaabihil Kiraam ,  wa  Ba’ad: Kwanza  tujue kwamba maana ya 'witr' (witiri) ni namba isiyoweza kugawanyika  kama  moja au tatu au tano na kadhalika.  Na Swalah ya Witr ambayo ni Sunnah iliyosisitizwa sana, huswaliwa usiku baada ya Swalah ya 'Ishaa hadi asubuhi kabla ya Alfajiri.  Hivyo hakuna Raka'ah mbili zinazoswaliwa usiku na kusomwa du'aa ya Qunuut kama ulivyosema, bali husomwa du'aa hiyo baada ya kuinuka kutoka kurukuu katika Raka'ah ya mwisho ya Swalah za Witr.  Unaweza kuswali Raka'a tatu au tano au saba au tisa au kumi na moja.  Utaswali Raka'a mbili mbili na kila baada ya Raka'a mbili utatoa sala

Kuomba Dua pamoja baada ya Swalah ya Fardh

SWALI assalam alaykum warahmatullah wabaraqatuh, katika misikiti mingi tunasoma dua kwa pamoja (imam au mtu mwengine anasoma na wengine tunaitikia) jee hii ni sunna,faradhi au bidaa na kama haifai tuombe vipi baada ya swala. JIBU Wa Aleykum  Sallaam  WarahmatulLaah  Wabarakatuh Naam kwanza kabisa Du'aa ni ‘ibaadah kama alivyosema Mtume Muhammad (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam):  عن النعمان بن بشير رضي الله عنه عن النبي صلى الله عليه وسلم ((   الدعاء هو العبادة  ((  ثم قرأ: (( وَقَالَ  رَبُّكُمُ  ادْعُونِي  أَسْتَجِبْ  لَكُمْ  إِنَّ  الَّذِينَ    يَسْتَكْبِرُونَ  عَنْ  عِبَادَتِي  سَيَدْخُلُونَ  جَهَنَّمَ  دَاخِرِينَ ))  رواه الترمذي Imetoka kwa An-Nu'maan bin Bashiyr (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Du'aa ni ‘ibaadah)) Kisha Akasoma: (( Na Rabb wenu Amesema: “Niombeni, Nitakuitikieni. Hakika wale wanaotakabari na kuniabudu wataingika Jahanam wadhalilike )) [Ghaa

Inafaa kumuombea Dua Mzazi ambaye si Muislamu?

SWALI: Je mtoto aweza kumuombea dua gani mzazi wake hali ya kuwa huyo mzazi si muislaam? JIBU:   Naam kwanza kabisa ikiwa  mzazi  huyo  yuko  hai  unaweza  ukamuombea  Du'aa  ili  Mwenyezi Mungu  amuongoze  na  aulainishe  moyo  wake  ili  aweze  kuingia  kwenye  Uislaam. Ama ikiwa  mzazi  huyo  ameshafariki  hali  yakuwa  hakusilimu  na  kafa  kwenye  ukafiri  hapo  tena  haifai  kumuombea  Du'aa na  wala  kumuombea  (Maghufira) msamaha  kwasabubu  ameshakuwa  ni  mtu  wa  motoni  milele  na  ndio  ahadi  ya  Mwenyezi Mungu Amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu قَالَ اللهُ تَعَالَى ﴿ اسْتَغْفِرْ لَهُمْ أَوْ لَا تَسْتَغْفِرْ لَهُمْ إِن تَسْتَغْفِرْ لَهُمْ سَبْعِينَ مَرَّةً فَلَن يَغْفِرَ اللَّهُ لَهُمْ ۚ ذَٰلِكَ بِأَنَّهُمْ كَفَرُوا بِاللَّهِ وَرَسُولِهِ ۗ وَاللَّهُ لَا يَهْدِي الْقَوْمَ الْفَاسِقِينَ ﴾ Waombee msamaha au usiwaombee. Hata ukiwaombea msamaha mara sabiini, Mwenyezi Mungu hatawasamehe. Hayo ni kwa sababu ya kuwa wao wamemkataa Mwenyez

kuondosha chakula kilichobaki kati ya meno kabla ya kutawadha?

Swali:  Ni wajibu kwa mtu kuondosha chakula kilichobaki kati ya meno kabla ya kutawadha? Jibu:  Kilicho dhahiri kwangu ni kwamba sio wajibu kukiondosha kabla ya kutawadha. Lakini hapana shaka kuwa kusafisha meno ndio kamilifu, safi zaidi na mtu anaepuka maradhi ya meno.  Kwa sababu uchafu huu ukibaki unaweza kusababisha harufu na kuleta magonjwa kwenye meno na fizi. Mtu anatakiwa anapomaliza kula atumie mjiti kwenye meno yake ili kile chakula kilichobaki kwenye meno kiondoke. Vilevile atumie  Siwaak.  Kwa kuwa chakula kinabadilisha harufu ya kinywa. Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema kuhusu  Siwaak: “Unasafisha kinywa na unamridhisha Mola.” Hii ni dalili inayofahamisha kuwa kila pale ambapo kinywa kinahitajia kusafishwa basi kunasafishwa kwa  Siwaak.  Ndio maana wanachuoni wakasema kuwa imekokotezwa zaidi kutumia  Siwaak  wakati inapobadilika harufu ya kinywa kwa sababu ya kunywa au kwa sababu nyingine. Marejeo :  Majmuu´-ul-Fataawaa

Nyaki za kutumia Mswaki

Swali:  Ni lini imekokotezwa zaidi kutumia  Siwaak ? Ni ipi hukumu ya kutumia  Siwaak  wakati wa Khutbah? Jibu:  Imekokotezwa zaidi kutumia  Siwaak  wakati mtu anapoamka kutoka usingizini, mara ya kwanza mtu anapotaka kuingia nyumbani, wakati wa kutawadha katika kusukutua na mtu anaposimama kwa ajili ya kuswali. Ni sawa kwa yule mwenye kusubiri swalah kutumia  Siwaak.  Lakini asitumie  Siwaak  wakati wa Khutbah. Kwani kufanya hivo kunamshughulisha. Isipokuwa ikiwa kama atakuwa na miayo. Katika hali hii atumie  Siwaak  ili kufukuza usingizi. Marejeo :  Majmuu´-ul-Fataawaa (11/115)

Kutumia sabuni wakati wa Wudhuu

Swali:  Ni ipi hukumu ya kuosha mikono na uso kwa sabuni wakati wa kutawadha? Jibu:  Kuosha mikono na uso kwa sabuni wakati wa kutawadha sio jambo lililowekwa katika Shari´ah. Bali ni kupetuka mpaka na kupindukia. Imethibiti ya kwamba Mtume Muhammad(Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema: “Wameangamia wale wenye kuvuka mipaka. Wameangamia wale wenye kuvuka mipaka.” Alisema hivo mara tatu. Lau tuseme kuwa kwenye mikono ya mtu kuna uchafu usiotoka isipokuwa kwa kutumia sabuni au kitu kingine kinachosafisha, katika hali hiyo hakuna ubaya. Ama ikiwa ndio mazowea ya mtu basi kutumia sabuni kutazingatiwa kuwa ni kuvuka mipaka na Bid´ah. Mtu asifanye hivo. Marejeo :  Majmuu´-ul-Fataawaa (11/151)

Hukumu ya Wudhuu kwa mwaamke aliyepaka kucha rangi

Swali:  Ni ipi hukumu ya wudhuu´ kwa yule ambaye kwenye kucha zake amepaka rangi ya kucha? Jibu:  Rangi ya kucha ni kitu anachopaka mwanamke juu ya kucha na ni kitu kilicho na ukoko.  Kwahiyo haijuzu kwa mwanamke kuitumia kipindi ambapo anaswali kwa kuwa inazuia maji kufika kwenye ngozi wakati wa kutawadha.  Kila kitu kinachozuia maji kufika kwenye ngozi haijuzu kwa mwenye kutawadha kukitumia. Kwa kuwa Allaah amesema: فَاغْسِلُوا وُجُوهَكُمْ وَأَيْدِيَكُمْ “Hivyo basi osheni nyuso zenu na mikono yenu mpaka kwenye visugudi.” (05:06) Mwanamke huyu ambaye amepaka juu ya kucha zake rangi ya kucha yanazuia maji kufika kwenye ngozi.  Kwa hivyo hawezi kusadikishwa ya kwamba ameosha mikono. Katika hali hiyo anakuwa ameacha kiungo cha faradhi wakati wa kutawadha au wakati wa kuoga. Kuhusu wale wasioswali, kama mfano wa mwanamke mwenye hedhi, hakuna neno kuitumia. Isipokuwa ikiwa kama rangi hii ni katika mambo maalum ya makafiri. Katika hali hiyo itak

Hukumu ya Kuacha mabega wazi kwa mwanamke

Swali:  Ni ipi hukumu ya mwanamke kuswali na huku ameweka ´Abaa´ah yake juu ya mabega yake? Imenifikia kutoka kwako kwamba katika hali hii swalah yake inabatilika kwa kuwa imefanana na vazi la mwanaume. Jibu:  Allaah ndiye Mwenye kutakwa msaada. Mwanamke huyu imepokelewa vilevile kinyume chake katika yale yaliyoenezwa na wanawake kwamba sisi tunasema kwamba ni sawa kwa mwanamke kuvaa ´Abaa´ah juu ya mabega hata kama hilo litafanywa sokoni na madukani. Yote mawili ni makosa. Sisi tunasema mwanamke kuweka ´Abaa´ah juu ya mabega yake wakati wa swalah hakuna neno. Kwa sababu hili ni jambo lililozoeleka kwa wanawake. Si jambo maalum kwa wanaume peke yao mpaka tuseme kuwa huku ni kujifananisha na wanaume. Kuhusu mwanamke kuweka ´Abaa´ah yake juu ya mabega masokoni na mbele za watu asifanye hivo. Kwa sababu kule kuweka kwake ´Abaa´ah yake juu ya mabega kunapelekea kufichukua fomu ya mabega yake na shingo yake na kuonyesha kama shingo yake ni ndefu au ni fupi, jambo ambalo