Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Machi, 2018

Uzushi Wa Kuomba Maghfirah Katika Mwezi Wa Rajab

SWALI:   Assalam aleikum warahma tullahi wabarakatu  Kutoka katika hadith Qudsi Allah amesema, Mtu yeyote atakaye sema: Astagh'firullah dhul jalali wal- ikramu min jamii dhunubi wal-aatham" mara 1000 katika mwezi wa Rajab basi sitomuadhibu mtu huyo katika kaburi wala siku ya kiama  watumie Waislam wengine.     JIBU:   AlhamduliLLaah - Himidi Anastahiki Allaah (Subhaanahu wa Ta’aala) Rabb wa walimwengu, Swalaah na salamu zimshukie Nabiy Muhammad (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na Swahaba zake (Radhwiya Allaahu 'anhum) na waliowafuata kwa wema mpaka Siku ya Mwisho.   Hakuna dalili ya fadhila hizo. Baada ya utafiti tumetambua kwamba uzushi wa du’aa na adhkaar kama hizo zimejaa katika vitabu na mitandao ya Kishia.   Uzushi huo unasambazwa katika mitandao ya jamiii na la kusikitisha ni kuona jinsi Waislamu wanavyoharakisha kuwatumia watu bila ya kufanya utafiti, kwa kutekeleza amri ya mzushi huyo katika hilo swali hapo juu kuwa ‘watumie Waislam wengi

Amali Za Kutenda Na Mambo Ya Kujiepusha Nayo Katika Miezi Mitukufu

AlhamduliLLaah. Inapasa tumshukuru Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) Kutupa umri hadi kutufikisha katika mwezi mwengine mtukufu.  Ni fursa nyingine ya kutenda mema tuchume thawabu nyingi. Mema ambayo hatuna budi kuyatenda kwa ajili ya kujenga Aakhirah yetu kabla haijafika siku ya kuaga kwetu dunia.   Utukufu wa miezi hiyo mitukufu imetajwa katika Qur-aan na Sunnah: Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):     إِنَّ عِدَّةَ الشُّهُورِ عِندَ اللَّـهِ اثْنَا عَشَرَ شَهْرًا فِي كِتَابِ اللَّـهِ يَوْمَ خَلَقَ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضَ مِنْهَا أَرْبَعَةٌ حُرُمٌ ۚ ذَٰلِكَ الدِّينُ الْقَيِّمُ ۚ فَلَا تَظْلِمُوا فِيهِنَّ أَنفُسَكُمْ ۚ وَقَاتِلُوا الْمُشْرِكِينَ كَافَّةً كَمَا يُقَاتِلُونَكُمْ كَافَّةً ۚ وَاعْلَمُوا أَنَّ اللَّـهَ مَعَ الْمُتَّقِينَ﴿٣٦﴾ Hakika idadi ya miezi mbele ya Allaah ni kumi na mbili katika hukmu ya makadirio ya Allaah , ( tangu ) siku Aliyoumba mbingu na ardhi . Kati ya hiyo , ( iko miezi ) minne mitukufu . Hivyo ndiyo Dini iliyo nyoofu . Bas

Mwezi Wa Rajab na Fadhila Zake

  بسم الله الرحمن الرحيم     Tunamshukuru Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) kwa kutupa umri wa kufika katika mwezi mtukufu wa Rajab, na Atujaalie uzima na afya tukutane tena na kipenzi chetu kitukufu Ramadh waan.  Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa):     نَّ عِدَّةَ الشُّهُورِ عِندَ اللَّـهِ اثْنَا عَشَرَ شَهْرًا فِي كِتَابِ اللَّـهِ يَوْمَ خَلَقَ السَّمَاوَاتِ وَالْأَرْضَ مِنْهَا أَرْبَعَةٌ حُرُمٌ ۚ ذَٰلِكَ الدِّينُ الْقَيِّمُ ۚ فَلَا تَظْلِمُوا فِيهِنَّ أَنفُسَكُمْ ۚ وَقَاتِلُوا الْمُشْرِكِينَ كَافَّةً كَمَا يُقَاتِلُونَكُمْ كَافَّةً ۚ وَاعْلَمُوا أَنَّ اللَّـهَ مَعَ الْمُتَّقِينَ﴿٣٦﴾ Hakika idadi ya miezi mbele ya Allaah ni kumi na mbili katika hukmu ya makadirio ya Allaah, (tangu) siku Aliyoumba mbingu na ardhi. Kati ya hiyo iko minne mitukufu. Hivyo ndiyo Dini iliyo nyoofu. Basi msijidhulumu humo nafsi zenu, na piganeni vita na washirikina wote kama wao wanavyokupigeni vita nyote. Na jueni kwamba Allaah Yu Pamoja na wenye taqwa.    [At-Tawbah: 36]     Na R