Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Mei, 2019

Ni Sunnah kuswali Rak´ah mbili baada ya ´Aswr

Ni Sunnah kuswali Rak´ah mbili baada ya ´Aswr Alikuwa (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) haachi Rak´ah mbili kabla ya Fajr na Rak´ah mbili baada ya ´Aswr. Ameipokea Ibn Abiy Shaybah katika ”al-Muswannaf” (2/352): ´Affaan ametuhadithia: Abu ´Awaanah ametuhadithia: Ibraahiym bin Muhammad bin al-Muntashir ametuhadithia, kutoka kwa baba yangu ambaye alikuwa akiswali Rak´ah mbili baada ya ´Aswr. Wakati alipoulizwa akasema: ”Nisingeziswali isipokuwa ni kwa sababu nilimuona Masruuq akiziswali, pamoja na kwamba alikuwa ni mtu mwaminifu. Lakini nikamuuliza ´Aaishah kuhusu jambo hilo ambapo akasema: ”Alikuwa (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) haachi Rak´ah mbili kabla ya Fajr na Rak´ah mbili baada ya ´Aswr.” Miongoni mwa makosa yaliyoenea katika vitabu vya Fiqh ni pale wanapokataza Rak´ah mbili hizi bali na kutozitaja miongoni mwa jumla ya Sunnah za Rawaatib, pamoja na kwamba zimethibiti kuwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alikuwa akidumu kwazo kama ambavyo alikuwa akidumu kusw

Siku Kumi Za Mwisho Za Ramadhwaan

عَÙ†ْ عَائِØ´َØ©َ رَضِÙŠَ اللَّÙ‡ُ عَÙ†ْÙ‡َا Ù‚َالَتْ : "Ùƒَانَ رَسُولُ اللَّÙ‡ِ صَÙ„َّÙ‰ اللَّÙ‡ُ عَÙ„َÙŠْÙ‡ِ ÙˆَسَÙ„َّÙ…َ Ø¥ِØ°َا دَØ®َÙ„َ الْعَØ´ْرُ Ø£َØ­ْÙŠَا اللَّÙŠْÙ„َ ÙˆَØ£َÙŠْÙ‚َظَ Ø£َÙ‡ْÙ„َÙ‡ُ Ùˆَجَدَّ ÙˆَØ´َدَّ الْÙ…ِئْزَرَ"  Ø±ÙˆØ§Ù‡ البخاري (2024) ومسلم (1174) Imepokelewa kutoka kwa ‘Aaishah (Radhwiya Allaahu 'anhaa) kwamba: “Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa pindi zilipoinga kumi za mwisho, akikesha usiku na akiamsha ahli zake na akijitahidi na kukaza shuka yake."  [Al-Bukhaariy, Muslim]         Hadiyth hii ni  uthibitisho kuwa siku kumi za mwisho za Ramadhwaan zina fadhila mahsusi na adhimu kuliko siku nyenginezo ambazo Muislamu inampasa aongeze utiifu na kutekeleza ‘ibaadah kama kuswali, kumdhukuru Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) na kusoma Qur-aan. ‘Aaishah (Radhwiya Allaahu ‘anhaa) amtuelezea hali ya Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) inavyokuwa kama ni mfano bora kabisa kwa sifa nne zifuatazo: 1-Nabiy (Swalla Alla

Swalah ya Uzushi katika Kumi la Mwisho Wa Ramadhaan

SWALI Assalam allaykum warahmatullahi Kwanza napenda kuwapongeza wote wanaoshiriki katika kazi hii ya kuelimisha umma wa kiislam hasa kwa sisi ambao tuko kwenye nchi hizi za kimagharibi . Ahsanteni sana na allah atawajaza majazo mema leo duniani na kesho akhera. Suali langu ni hili tokea kukaribia kumi la mwisho la mwezi huu mtukufu wa ramadhan nimekuwa napokea email kutoka watu mbali mbali zinazoelezea kuhusu sala ya laylatul Qadri ambayo husaliwa  kwa rakaa zaidi ya kumi na moja pamoja sura zake maalum  kwa kila siku (yaani kila siku na sura zake maalum) kwa mfano kuna siku usome sura zinazoanza na haa mim na nyenginezo pia ikiwemo salatul tasbihi. hivyo naomba nasaha zenu watu wa alhidaaya kwani tumo ndani utata mkubwa waislam. Assalam alaykum warahmatullhi Barua yenyewe ni hii: ASSALAM ALAYKUM, NDUGU ZANGU WAISLAM NAWAOMBA TUFANYE BIDII NA JITIHADA NA KUHAKIKISHA KILA MMOJA WETU ANATEKELEZA SALA HII PINDI HALI IKIMRUHUSU, INSHAALLAH. TAREHE 21 USIKU - MWEZI WA RAMADHANI

Je,Inafaa Kufanya Adhkaar Nyumbani Kumi La Mwisho Ramadhwaan Ikiwa Siruhusiki Kwenda Msikitini?

SWALI Mimi huwa nakaa macho na kusoma kuran na kuswali tahjud, kuomba dua, kumtaja Allah kwa adkhaar katita kumi la mwisho wa mwezi wa ramadhani nikiwa nyumbani je ninafanya makosa? Nimesoma kwenye alhidaaya kuwa itikafu haikaliwi nyumbani je nifanye nini nami nataka kupata dhawabu zake na msikiti wetu hawaruhusiwi wanawake kukesha. JIBU Naam kwa Hakika ni kuwa adhkaar unaweza kuleta mahali popote na wakati wowote ule isipokuwa chooni lakini I‘tikaaf haifanywi isipokuwa katika Msikiti.  Jambo linalotakiwa kutoka kwenu ni kuweza kuzungumza na Imaam kuhusu kuruhusiwa kwa wanawake kufanya I’tikaaf kama walivyofanya Maswahaba wa kike (Radhwiya Allaahu ‘anhunna) wakati wa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) wakiwemo wakeze. Ikiwa wameshindwa kuwapa ruhusa nyinyi hamna haja kuhuzunika kwani ‘amali zote hutazamwa na kutegemea Niyyah.  Niyyah yako au yenu ikiwa nzuri basi mtapata thawabu kamili japokuwa hamkukaa I’tikaaf hiyo ndani ya Msi

Mwanamke Mwenye Hedhi Afanye Nini Masiku ya Mwisho Kupata Laylatul-Qadr?

SWALI Nilikuwa nawaza mwanamke mwenye hedhi afanye nini usiku wa Laylatul-Qadr ili aweze kupata thawabu zaidi kwa kujishughulisha na ibada? Na kama inafaa, ibada ya aina gani inaruhusiwa afanye usiku huo? JIBU Naam,Mwanamke mwenye hedhi anaweza kufanya vitendo vyote vya   ibada isipokuwa kuswali, kufunga, kuzunguka Ka'bah na kukaa I'tikaaf Msiktini. Imesimuliwa kwamba Mtume   صلى الله عليه وآله وسلم   alikuwa akikesha usiku   katika siku kumi za mwisho za Ramadhaan. (Al-Bukhaariy 2401) na (Muslim 1174) wamesimulia kwamba Mama wa Waumini 'Aaishah  رضي الله عنها amesema  ((Zinapoingia siku kumi za mwisho katika Ramadhaan, Mtume  صلى الله عليه وآله وسلم  hujiepusha na wake zake, na hukesha usiku na kuwaamsha 'aila (familia) yake)) Kukesha usiku haina maana kwamba ni kwa kuswali pekee, bali ni kwa kila aina ya vitendo vya ibada, na hivi ndivyo walivyofasiri 'Ulamaa. Al-Haafidh kasema: "Kukesha usiku ina maana kwamba kufanya aina za

Ramadhwaan Inaaga Chukua Fursa Masiku Yaliyobakia Kutenda Mazuri

Enyi waja wa Allaah! Hakika mwezi wa Ramadhwaan unaaga na hakuna kilichokabakia isipokuwa masiku machache. Basi aliyetenda mazuri katika mwezi aendelee kufanya na ambaye amekasiri, ajitahidi kumaliza mwezi kwa vizuri, kwani hakika matendo yanahesabika mwishoni mwake. Kwa hiyo  chukua fursa kwa (masiku) yaliyobakika ya mwezi, na uage mwezi kwa mazuri kabisa na amani. 

Usiku wa Laylatul-Qadr Hubadilika Kila Mwaka

Imaam Ibn Baaz (Rahimahu Allaah): Layaltul-Qadr hubadilika katika masiku ya kumi na si kwamba kuna siku maalumu katika nyusiku hizo. Huenda ikawa ni usiku wa 21 au 23 au 25 au 27 ambazo ni aghlabu zinategemewa na huenda pia ikwa usiku wa 29, au hata pia unaweza kuangukia masiku ya shafawiy (20, 22, 24, 26, 28). Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa akihusisha nyusiku hizi kwa kuongezea na kujitahidi (katika ‘ibaadah) ambazo hakuwa hakizitekeleza katika masiku ya 20 ya mwanzo (ya Ramadhwaan) na Maswahaba zake (Radhwiya Allaahu ‘anhum) na Salaf walikuwa nao wakihuisha nyusku hizi na kujitahidi mno katika aina mbali mbali za ‘amali njema.” [ Al-Ikhtiyaraat Al-Fiqhiyyah,  uk. 243]

Sharh Thawabu Za Kumfuturisha Mwenye Swawm

Kuhusu Hadiyth Ya Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): ((Atakayemfuturisha Aliye Na Swawm Atapata Thawabu Kama Zake Bila Ya Mwenye Swawm Kupungukiwa Na Kitu)). Wamekhitilafiana ‘Ulamaa katika maana ya  “Atakayemfuturisha mwenye swawm.”  Ikasemwa: Lilokusudiwa kumfuturisha ni chochote kidogo anochofuturu japo kama ni tende.  Na wengine wakasema: Imekusudiwa amfuturishe kwa kumshibisha kwa sababu ndio itakayomsaidia mwenye swawm usiku wake wote na huenda ikamtosheleza na sahuwr (daku). Lakini iliyo dhahiri katika Hadiyth ni kwamba mtu akimfuturisha mwenye swawm japo kwa tende moja basi atapata thawabu sawa na thawabu zake.  Kwa hiyo basi inampasa mtu atilie himma kufuturisha wenye swawm kwa kadiri ya uwezo wao khasa kwa vile wenye swawm wanahitaji kusaidiwa kutokana na umasikini wao na kuhitaji kwao kwa vile hawapati wenye kuwaandalia futari na kama hayo. [Imaam Ibn 'Uthaymiyn –  Sharh Riyaadhw Asw-Swaalihiyn ]

Kuichelewesha Zakaatul-Fitwr

SWALI Nilikuwa katika safari na nikasahau kutoa Zakaatul-Fitwr. Nikuwa nasafiri usiku wa 27 Ramadhwaan na hatukutoa Zakaatul-Fitwr hadi leo. JIBU Ikiwa mtu amechelewesha Zakaatul-Fitwr japokuwa alikumbukua kuitoa, basi atakuwa ni mtenda dhambi na itampasa atubie kwa Allaah na kuilipa kwa sababu ni kitendo cha ibada ambacho kinabakia kuwajibika japokuwa muda wa kutoa umepita kama mfano wa Swalaah. Lakini kama muulizaji huyu alivyotaja kuwa alisahau kuilipa kwa wakati wake, hivyo hakuna dhambi juu yake lakini lazima ailipe. Kusema kuwa hakuna dhambi juu yake ni maana kwa ujumla kutokana na dalili inayoonyesha kuwa hakuna dhambi kwa mtu anayesahau lakini bado atakuwa amewajibika kuilipa kutokana na sababu zilizotolewa juu. Wa biLLaahi At-Tawfiyq wa Swalla Allaahu ‘alaa Nabiyyina Muhammad wa aalihi wa Swahbihi wa sallam. [Fataawaa Al-Lajnah Ad-Daaimah  (2867)]

Kuwalipia Zakaatul-Fitwr Wafanyakazi

SWALI Tuna kiwanda na shamba ambamo kuna wafanyakazi wanaolipwa mishahara. Je tuwalipe Zakaatul-Fitwr au wajilipe wenyewe? JIBU Wafanyakazi ambao wanalipwa mishahara kwa kibarua chao katika kiwanda au shamba wanapaswa kujilipia wenyewe Zakaatul-Fitwr kwa sababu hukmu ya asili ni kwamba imewajibika kwako. (Hivyo hupasi wewe kuwalipia) Wa biLLaahi At-Tawfiyq wa Swalla Allaahu ‘alaa Nabiyyina Muhammad wa aalihi wa Swahbihi wa sallam. [Fataawaa Al-Lajnah Ad-Daaimah (9/372)]

Inaruhusiwa Kumpa Zakaatul-Fitwr Mama Wakubwa Na Wadogo?

 SWALI Je, inafaa kutoa Zakaatul-Fitwr kwa mama mkubwa na mama mdogo   ambaye ameachwa, hana watoto wa kiume bali ana watoto wa kike ambao wameolewa na anamiliki 500 mita mraba ya ardhi.  Hana chanzo cha kipato. Je inaruhusiwa kumpa Zakaah hii au wapewe maskini wengine? JIBU Sifa Zote Ni Za Allaah Kwanza: ‘Ulamaa wamekhitilafiana kuhusu watu wa kuwapa Zakaatul-Fitwr. Rai ya wengi wao ni kwamba wapewe aina nane ya watu ambao wametajwa kupewa (katika Suwrah At-Tawbah Aayah ya 60). Rai ya wengineo ni kwamba wapewe wote waliomo katika aina nane ya watu na wengineo wameona kwamba itolewe kwa masikini na wenye kuhitaji pekee. Inasema katika al-Mawsu’ah al-Fiqhiyyah (23/344): “Mafuqahaa wamekhitilafiana kuhusu nani apewe Zakaatul-Fitwr na kuna rai tatu: 1- Rai ya wengi wao ni kwamba inaruhusiwa kuigawa baina ya aina nane ya watu ambao Zakaah ya mali inapasa kuwapa. – Rai ya Maalik. 2- Rai ya Imaam Ahmad ambayo imependekezwa na Ibn Taymiyyah kwamba wapewe

Je,Ni Kweli Swawm Inanin'ginia Baina ya Mbingu na Ardhi hadi Mtu atoe Zakaatul-Fitwr?

SWALI Je, Hadiyth inayosema kuwa Swawm ya Ramadhaan inaning'inia baina ya mbinu na ardhi na haipandishwi juu hadi ilipwe Zakaatul-Fitwr ni Sahihi?  JIBU Naam kwanza kabisa Hadiyth hiyo ni dhaifu. Katika Al-Jaami' as-Swaghiyr, as-Suyuwtwiy ameihusisha kwa Ibn Shaahiyn katika Targhiyb yake: "Imesimuliwa katika Adhw-Dhwiyaa' kutoka kwa Jariyr bin 'Abdillaah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)  amesema: Mwezi wa Ramadhaan unaning'inia baina ya mbingu na ardhi na (Swawm) haipelekwi juu kwa Allaah isipokuwa kwa (kutolewa) Zakaatul-Fitwr" Imechambuliwa kuwa ni dhaifu na as-Suyuwtwiy. Al-Manaawiy ameeleza sababu yake katika Faydhw Al-Qadiyr ambako amesema: "Imesimuliwa na Ibn Al-Jawziy katika Al-Waahiyaat na kasema: Sio Swahiyh, isnaad yake inajumuisha Muhammad bin 'Ubayd al-Baswriy ambaye ni majhuwl (asiyejulikana). Imechambuliwa pia kuwa ni dhaifu na Imaam al-Albaan