Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Mei, 2018

Hukumu ya Kusema ‘''Swadaqa Allaahu Al-‘Adhwiym''’ baada ya Kusoma Qur-aan

Assallaam Aleykum WarahmatulLaah Wabarakatuh (Watu wengi katika jamii wana mazoea baada ya kumaliza kusoma Qur-aan, kusema ‘Swadaqa Allaahu Al-‘Adhwiym’. Wengi wakiwa wameathirika kwa mazoea ima ya kusikia kwenye radio au ya kuona video mbalimbali au Misikitini kutoka kwa wasomaji Qur-aan mbalimbali walio mashuhuri.   Ada hiyo, haina dalili yoyote katika shariy’ah. Bali ni kinyume na ilivyothibiti kutoka kwa Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) na waja wema waliotangulia).   Baada ya kumaliza kusoma Qur-aan usiseme ‘Swadaqa Allaahu Al-‘Adhwiym’, lakini sema:   سُبْحَانَكَ اللَّهُمَّ وَبِحَمْدِكَ، أشهد أن لاَ إِلَهَ إِلاَّ أَنْتَ، أَسْتَغْفِرُكَ وَأَتُوبُ إِلَيْك “ Subhaanaka Allaahumma wa Bihamdika , Ash-hadu Allaa ilaaha illa Anta, Astaghfiruka wa Atuwbu ilayka .”   Ni jambo la ki-Sunnah ambalo wanaghafilika nalo watu wengi baada ya kumaliza kusoma Qur-aan.   Ushahidi juu ya hilo ni Hadiyth kutoka kwa mama wa Waumini ‘Aaishah (Radhwiya Allaahu ‘anh

Kumwakilisha Mtu Kwenye Ndoa

    SWALI:   assalaamu alaykum je, nini hukumu ya kuwakilishana katika kuoa, yaani kuoa kwa niaba ya ndugu yako; ikiwa inafaa, je ni zipi taratibu zake?     JIBU:   AlhamduliLLaah Himidi Anastahiki Allaah (Subhaanahu wa Ta’aala) Rabb wa walimwengu, Swalaah na salamu zimshukie Nabiy Muhammad (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na Swahaba zake (Radhwiya Allaahu 'anhum) na waliowafuata kwa wema mpaka Siku ya Mwisho.     Wa 'Alaykumus Salaam wa RahmatuLLaahi wa Barakaatuh   Kukiwa na dharura ya kukosekana kwako kwenye kufunga ndoa, unaweza kutoa idhini yako ima kwa maandishi au kwa njia ya simu inayothibitisha ni wewe na Walii (baba wa mke au babu au kaka) akawepo na mashahidi wawili na mahari.   Tambua kuwa lazima awepo Walii wa mwanamke unayetaka kumuoa, kukosekana Walii kunaifanya ndoa isiwe sahihi; yaani batili.   Rasuli (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Hakuna ndoa bila Walii.”  [Ibn Maajah, At-Tirmidhiy, Abuu Daawuwd na Al

Makosa Yafanywayo Na Wenye Kufunga Katika Mwezi Wa Ramadhwaan

   Yafuatayo ni makosa ambayo yameonekana yakitendeka katika mwezi wa Ramadhwaan ima wanapokuwa Waislamu katika Swawm au baada ya kufuturu na katika Swalah za Qiyaamul-Layl. Hivyo inapasa tuyazingatie na kujiepusha nayo ili tubakie katika usalama wa Swawm zetu, Swalah zetu na mengine yote yanayohusu mwezi huu mtukufu:     1. Kutia niyyah kwa kutamka:   Baadhi wanaamini kuwa niyyah usipoitamka basi haijawa niyyah. Na pia huwafunza watoto kutamka maneno ya kutia niyyah, au kuwaamrisha wasikose kwenda kunuizwa Msikitini na mashekhe. Itambulike kuwa niyyah mahali pake ni moyoni na kutamka ni uzushi.      2. Kufunga bila kuswali:   Baadhi ya watu wanafunga bila ya kuswali au kutimiza Swalah ipasavyo. Watu kama hawa Swawm zao hazifai kwani Swalah ni nguzo ya Dini ya Kiislamu.     3. Kudhani kwamba Swalah ya Taraawiyh inaanzwa siku ya kwanza ya Ramadhwaan: Hali inaanza usiku ule unaoandama mwezi. Sunnah ni Waislamu waanze kuswali usiku huo na si baada ya kufunga siku ya kwanza

Hadiyth zisizosihi (Dhaiyfu) kuhusu Ramadhwaan <3>

Miongoni mwa hizo Hadiyth ni : اللهم بارك لنا في رجب وشعبان وبلغنا رمضان وقد ضعّفه  الألباني   في "ضعيف الجامع الصغير   “Ewe Mola Tubarikie katika –mwezi wa- Rajab na –mwezi wa- Sha’abaan na Tubalighishe –mwezi wa- Ramadhwaan.” Ni Hadiyth   Dhwa’iyf  ameitaja Shaykh Al-Albaaniy kwenye kitabu cha  Dhwa’iyf Al-Jaami’ Asw-Swaghiyr .   شعبان شهري، ورمضان شهر الله، وشعبان المطهر، ورمضان المكفر ضعّفه  الألباني   في  السلسلة الضعيفة.   “Sha’abaan ni mwezi wangu , na Ramadhwaan ni mwezi wa Allaah , na Sha’abaan   inatwahirisha , na Ramadhwaan inafuta ( madhambi )” Ameitaja Shaykh Al-Albaaniy kuwa ni dhaifu kwenye   Silsilat Al-Ahaadiyth Adhw-Dhwa’iyfah .   "  رجب شهر الله، وشعبان شهري، ورمضان شهر أمتي" ضعيف ، نص الشيخ  الألباني  على تضعيفه في السلسلة الضعيفة “Rajab ni mwezi wa Allaah, na Sha’abaan ni mwezi wangu, na Ramadhwaan ni mwezi wa ummah wangu” Hadiyth  Dhwa’iyf , ameitaja Shaykh Al-Albaaniy kwenye  Silsilat Al-Ahaadiyth A