Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Januari, 2019

Sadaqah inafaa kumtolea mama yangu aliyefariki?

*Swali* Jirani yangu aliniuliza kuhusu mama yangu aliye fariki kama nimemtolea sadaka baada ya kufa mimi nikamjibu sikutoa sadaka yoyote, isipokua mimi nijuavyo kama ana deni inabidi nimlipie ikiwa deni hilo ni kwa binaadamu au kwa Mwenyezi Mungu na kama aliweka nadhiri kwa Mwenyezi Mungu ya kufunga inabidi pia nimlipie kwa kufunga. Na zaidi na muombea dua yeye akanijibu haifai mtu akifiwa na mama yake inabidi amtolee sadaka ampelekee majuzuu na misahafu madrasa au msikitini sasa sijui uthibitisho wa hili. *Jibu* ✅Maiti ananufaika kwa yote yaliyopitishwa na sheria ya Kiislamu ima katika Kitabu cha Allaah (Subhaanahu wa Ta‘ala) na kwa uongofu wa Mtume Muhammad(Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam). ➡Imepokewa na Abu Hurayrah (Radhiya Allaahu ‘anhu) kuwa Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Anapokufa mwanaadamu basi amali zake zote hukatika isipokuwa kwa mambo matatu: Sadaka ya kuendelea, au elimu yenye manufaa au mtoto mwema anayemuombea” ↪Imepokelewa

Mume afanye nini ikiwa mkewe hataki kuswali?

*Swali* Mume achukue hatua gani ikiwa mke hataki kuswali? *Jibu* ✅Mara nyingi kama vile wanawake wanashindwa kufuata maagizo ya kuchagua mume wa sawa Kidini ndivyo wanaume wanavyofanya makosa hayo hayo. ➡Mume wa Kiislamu anatakiwa amchague mke mwenye Dini na Imani, maadili na tabia nzuri. ✅Kukosa kufuata maagizo hayo ya Mtume Muhammad(Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) ndio kunatokea matatizo kama hayo. ➡Hata hivyo, kosa lishatokea na inabidi tupate suluhisho kwa suala hilo nyeti. ➡Kulingana na maelezo yako ni kuwa mkeo inaonyesha bado ana Uislamu na Imani, hivyo anataka msukumo wa kuweza kutekeleza wajibu huo bila ya tatizo. ➡Jambo ambalo unatakiwa mwanzo kabisa kufanya ni kumnasihi mkeo kwa njia nzuri, kwani Allaah (Subhaana wa Taala) Anatuambia⤵ “Waite waelekee kwenye Njia ya Mola wako Mlezi kwa hikima na mawaidha mema, na ujadiliane nao kwa namna iliyo bora” ↪Rejea Qur'an 16: 125. ➡Inatakiwa utumie mbinu tofauti za kuweza kumvutia katika kuswali bila ya yeye

Hukmu ya Mke Asiyeswali

SWALI   Ni ipi hukmu ya mke asiyeswali, kwa kutambua kuwa nimeshambainishia adhabu anayopata mwenye kuacha kuswali, kuna baadhi ya nyakati anaswali na wakati mwengine anaacha. Kwa mfano anaswali Adhuhuri na anaacha (Swalaah) zote za Faradhi zilizobaki?     JIBU   Hukmu yake ni Kafiri. Na haijuzu kuendelea kubaki naye katika hifadhi yako. Inapasa kuwa naye mbali, isipokuwa kama atatubu tawbah ya kweli, la sivyo, ni waajib kuwa naye mbali (kuachana naye). Kwa sababu kuacha Swalaah ni ukafiri mkubwa.   Anasema Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam): “Baina ya mtu na baina ya ushirikina na ukafiri ni kuacha Swalaah.”  [Muslim]   Na anasema (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam): “Agano (Kinachotutofautisha) baina yetu (Waumini) na baina yao (Washirikina, Makafiri na Wanafiki) ni Swalaah, anayeiacha (Swalaah) amekufuru.”  [At-Tirmidhiy, Ibn Maajah na An-Nasaaiy]   Hii ndio kauli sahihi katika kauli za Wanachuoni; kwamba kuiacha (Swalaah) ni ukafiri mkubwa.

Hukumu ya Mke kutoka nyumbani bila Ruksa ya mumewe

Naam shukrani kwa swali lako kuhusu mkeo kutoka bila ya ruhusa yako kwenda katika mishuari zake. Matatizo haya hutokea mara nyingi kwa mke kutokuwa na ufahamu na ujuzi wa Dini ya Kiislamu. Au mara nyingine huwa kweli ana elimu lakini hushindwa kufuata kimatendo kwa sababu moja au nyingine. Au huenda akawa na elimu, lakini akakosa Dini. Kwa ajili hiyo Imaam al-Bukhaariy, ana mlango katika  Swahiyh  yake wenye kichwa cha habari, “ Elimu Kabla Ya ‘Amali ”. Hata hivyo, huenda mtu akawa na elimu lakini akawa hana ‘amali kwa sababu ya kutokuwa na ikhlaasw.   Ni juu ya mke kumtii mumewe katika mambo yasiyo ya maasi, kwani hakuna utiifu katika maasiya. Ikiwa mume hakutoa ruhusa mbali na kuwa yu mbali na mkewe ni wajibu wa mke kutii amri hiyo. Hata hivyo, haifai kwa mume kuweka vikwazo vya kupita kiasi,  kama kumzuia kwenda kwa wazazi wake na mahali ambapo anaweza kupata elimu ya Kidini. Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala) Anasema: “ Wakikutiini, basi msiwatafutie njia ” (an-Nisaa’ [4]: 34). Hii

Hukmu ya mke kutoroka kwa Mumewe sababu ya mume kuongeza mke wa pili

Naam ➡Hakika ni kuwa ni vigumu kutoa hukumu ya moja kwa moja kwani tumesikia kesi au kujitetea kwa upande mmoja. Hatujasikia yaliyomfanya mke atoroke. Hata hivyo, katika hali yoyote ile mke kisheria hafai kutoka kwa mumewe kwa sababu yoyote ila iwe kwa ajili ya kisheria ambayo amemnasihi mumewe mpaka akachoka. ➡Suala la mke kutoka mara moja ni ikiwa mume ameritadi kutoka katika Uislamu au maasiya makubwa dhahiri shahiri. ➡Mara nyingi wake kwa wivu ulio nje ya sheria hupandwa na hasira wakafanya mambo kama hayo kisha wakajuta baadaye. Wakati huo huenda majuto kama hayo yakawa hayana faida yoyote ile. ➡Kwa kuwa suala hilo lishatendeka wewe usiwe na hasira bali fuata njia za kisheria kumpata na kumrudisha mkeo. Njia ya rahisi ni kwako kwenda kwa wazazi wake na kutoa taarifa hiyo. ➡Mbali na kuwa wazazi wake huenda wakawa pamoja na binti yao. Hiyo ni kwa kuwa mke wa mtu akaja kwa wazazi na wazazi nao wakamuacha bila kumshurutisha kurudi. ➡Hata hivyo, tukichukulia dhana nzuri ni kuwa h

He, Uislamu umegawanyika makundi?

*Swali* Jee Uislam umegawanyikaaa? Una makundii? *Majibu* ✅Naam ni kweli kwamba Uislamu umegawanyika katika Makundi tofauti tofauti. ➡Kwa kifupi tu kwa kukupa mwangaza kidogo, utayajua yale makundi yaliyo potofu kwa kuona na kujua itikadi zao. ➡Mfano mzuri leo utaona wanaodai kuna mtume baada ya Mtume wa haki na wa mwisho Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam), utawaona pia wale wanaowakufurisha Maswahaba (Radhiya Allaahu ‘anhum) na kuwatukana wake za Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam), pia utawaona wengine wanaokufurisha Waislam na kuwatoa katika Dini kwa sababu wanaamini kuonekana Allaah Qiyaamah, na wanakufurisha Waislamu kwa sababu ya kufanya baadhi ya maasi, na pia utawaona wengine wanakataa Hadiyth za Mtume na kudai kuwa wao wanafuata Qur-aan pekee, na pia utawakuta wengine wanakwenda kuwaomba watu waliokufa makaburini ili wawasaidie haja zao, na wengi wengine wasio na idadi. ➡Tutalijua kundi lililookoka na ambalo halipo katika hayo makundi

Hadiyth Kuhusu "Ewe 'Aliy Fanya Mambo Matano Kabla Ya Kulala" Ni Sahihi?

SWALI Kwanza natoa shukrani zangu kwa wahusika wote wa al-hidaaya. Mimi maswali ni matano-   1. Ukiwa uatsoma suratul ikhlas mara tatu utakua umesoma quran nzima?               2. Ukiwa utasoma suratul fatiha mara nne utakuakama umetoa dirham elfu nne?   3. Ikiwa utasema laa ilaha illa Allah wahdahula sharika lahu mulku wa lahu lhamdu yuhyi wayumi wahuwa ala kulli shaiin qadiir. mara kumi basi utakua umezuru al-kaaba?                            4- Ukiwa utasema lahaula wala quwata illa billahi al alliyyu aladhim. mara kumi utakua umehifazi pahala pako peponi?     5- Ikiwa utasema: astaghafirullah adhiim alladhii la illaha illah huwa hayyu al-quyuum wa atubu alaihi. Mara kumi basi nitakua nimewaridhia niliohasimiana nao?  Nitashukuru al-hidaaya kama mtanijibu maswala yangu haya. inshallah. yote haya nikutaka uhakika kutoka kwenu.   JIBU Sifa zote njema Anastahiki Allaah Aliyetukuka Mola Mlezi wa walimwengu wote, Swalah na salamu zimshukie kipenzi chetu Mtume Muhammad (Swalla A

Hukmu ya Kusheherekea kumbukumbu ya Kifo

swali Je,inafaa kusheherekea Death Anniversary..? na ipi Hukmu ya Kusheherekea kumbukumbu ya Kifo ( Anniversary) Jibu Kwanza ni dhambi katika Uislamu kuweka kumbukumbu ya kifo inayojulikana kama ni ‘death anniversary’. Hili ni jambo la kuiga makafiri ambalo Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)  amekemea. Kwa hiyo kulitenda ni miongoni mwa madhambi makubwa unapaswa ujiepushe nalo kabisa. Uislamu ni Dini yenye kutuongoza katika mfumo mzima wa maisha hapa duniani. Kwa ajili hiyo, lolote tufanyalo ni lazima liambatane na Shariy’ah ya Uislamu. Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) aliwakuta watu wa Madiynah wakisherehekea siku kuu zao. Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akawaambia kuwa wao wamebadilishiwa hizo sikukuu zao kwa siku mbili kuu zilizo bora kabisa, nazo ‘Iyd al-Fitwr na Al-Adhw-haa. Ama sherehe ya anniversary hata ya Nabiy mwenyewe (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) haipo katika siku za s

Watu ambao Allaah hatowatizama wala Kuongea nao siku ya Qiyamah - sehemu ya 3

                            Watu ambao Allaah hatowatizama wala Kuongea nao siku ya Qiyamah                                                                     Hadiyth ya Tatu ن   أبي   هريرة   قال :  قال   رسول   الله   صلى   الله عليه   وسلم   (( ثَلَاثٌ لَا يُكَلِّمُهُمُ اللَّهُ يَوْمَ الْقِيَامَةِ ، وَلَا يَنْظُرُ إِلَيْهِمْ ، وَلَا يُزَكِّيهِمْ وَلَهُمْ عَذَابٌ أَلِيمٌ : رَجُلٌ عَلَى فَضْلِ مَاءٍ   بِالْفَلَاةِ   يَمْنَعُهُ مِنَ   ابْنِ السَّبِيلِ   ، وَرَجُلٌ بَايَعَ رَجُلًا بِسِلْعَةٍ بَعْدَ الْعَصْرِ فَحَلَفَ لَهُ بِاللَّهِ لَأَخَذَهَا بِكَذَا وَكَذَا فَصَدَّقَهُ وَهُوَ عَلَى غَيْرِ ذَلِكَ ، وَرَجُلٌ بَايَعَ إِمَامًا لَا يُبَايِعُهُ إِلَّا لِدُنْيَا فَإِنْ أَعْطَاهُ مِنْهَا وَفَى ، وَإِنْ لَمْ يُعْطِهِ مِنْهَا لَمْ يَفِ )) . Imepokelewa toka kwa Abuu Hurayrah akisema: “Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa Sallam) amesema: ((Watatu (wa aina tatu) Allaah Hatozungumza nao Siku ya Qiyaamah, wala Hatowaangalia, wala Hatowatakasa, na watapata adhabu iumizayo.

Watu ambao Allaah hatowatizama wala Kuongea nao siku ya Qiyamah - sehemu ya 2

                             Watu ambao Allaah hatowatizama wala Kuongea nao siku ya Qiyamah                                                                     Hadiyth ya Pili               Mwenye Kuburuza Nguo yake (Isbaal), Msimbuliaji,               na Mchuuzi wa Bidhaa yake kwa kiapo cha Uongo عن   أبي   ذر،   عن   النبي   صلى   الله   عليه   وسلم قال :  (( ثلاثةٌ   لا   يكلمهم   الله   يوم   القيامة،   ولا ينظر   إليهم،   ولا   يزكيهم،   ولهم   عذابٌ   أليمٌ)) ، قال :  فقرأها   رسول   الله   ثلاث   مرارٍ،   قال   أبو ذر :  خابوا   وخسروا،   من   هم   يا   رسول   الله؟ قال :  المسبل   إزاره،   والمنان،   والمُنَفِّقُ   سلعته بالحلف   الكاذب))   رواه   مسلم . Imepokelewa toka kwa Abuu Dharr (Radhwiya Allaahu 'anhu) toka kwa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)   akisema: ((Watatu (wa aina tatu) Allaah Hatozungumza nao Siku ya Qiyaamah, wala Hatowaangalia, wala Hatowatakasa, na watapata adhabu iumizayo)). Akasema: Rasuli akayasema hayo