Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Februari, 2018

Tathmini mwezi wa Ramadhani

Kila sifa njema inamstahikia Allaah Aliyetukuka Muumba wa ulimwengu na walimwengu wake, ambae Alituwafikisha kuukamilisha mwezi wa Ramadhaan kwa kufunga Swawm yake nyakati za mchana, kusimama visimamo nyakati za usiku, kuisoma Qur-aan iliyoteremsha ndani yake na kutekeleza kila tulilowafikishwa kulitekeleza kadiri ya uwezo wetu.   Swalah na Salamu zimfikie kipenzi cha Waumini Mtume Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) na Sahaba zake kiraam (Radhiya Allaahu 'anhum) na kila anaewafuata  kwa ihsaanmpaka Siku ya Mwisho. Masiku ya Ramadhaan yaliyotunukiwa kila aina ya neema na baraka ndio yamekwishapita mpito wa usiku na mchana, na ndio hivyo hivyo unavyopita umri wetu, leo tuko hai juu ya ardhi na kesho wafu ndani yake. Ndugu yangu katika iymaan, umemaliza Swawm ya Ramadhaan na yote yaliyoambatana na Ramadhaan, mambo ambayo utekelezaji wake ulitarajiwa uwe wenye  Ikhlaasw : kwamba hapakusudiwi katika utekelezaji wa hicho kinachotekelezwa chochote ki...

Hatari ya kueneza Hadithi Dhaifu

Assallaam Aleykum WarahmatulLaah Wabarakatuh Ndugu Waislamu , tunachukua fursa hii ya kutekeleza amri ya Allaah   سبحانه وتعالى   na Mtume Wake  صلى الله عليه وآله وسلم   katika Hadiyth Sahiyh ifuatayo :     عَنْ تَمِيمٍ الدَّارِيِّ أَنَّ النَّبِيَّ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ :((الدِّي...

Madhara ya kufuata Matamanio

Assallaam Aleykum WarahmatulLaah Wabarakatuh Shukurani zote Anastahiki Allaah, Mola wa ulimwengu wote. Rehma na amani zimshukie Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam), ahli zake na Masahaba wake. Enyi Waislamu muogopeni Allaah kwa kadri Anavyopaswa kuogopewa. Allaah Amesema, “Enyi mlioamini! Mcheni Mwenyezi Mungu kama ipasavyo kumcha; wala msife ila nanyi ni Waislamu.”  (Aal 'Imraan 3:102) Ucha Mungu ni dalili ya Iymaan. Kwani kwa ucha Mungu ndipo mtu anaweza kudumu katika njia iliyonyooka (iliyo sawa) Jueni kuwa muongozo sahihi ni muongozo wa Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam), Ubaya wa mambo yote ni uzushi, na kila uzushi ni uovu, na kila ovu linampeleka mtu motoni. Enyi Waislamu! Allaah Amewaumba viume ili wamuabudu na wafungamane na Amri Zake na makatazo Yake. Allaah Anasema, "Nami Sikuwaumba majini na watu ila waniabudu Mimi."  (Adh-Dhaariyaat 51:56)   Allaah pia Anasema, "Enyi watu! Muab...

Valentine Day (Siku ya Wapendao)

Assallaam Aleykum WarahmatulLaah Wabarakatuh BismiLLaah wa AlhamduliLLaah was-Swalaatu was Salaamu ‘alaa Muhammad wa ‘ alaa ‘ Aalihi wa Aswhaabihil Kiraam , wa Ba’ad ,   Naam AlhamdulilLaah Allaah سبحانه وتعالى Ametuchagulia Dini ya Kiislamu, Dini ya haki na Hatokubali dini yoyote nyingine. Anasema:    ((وَمَن يَبْتَغِ غَيْرَ الإِسْلاَمِ دِينًا فَلَن يُقْبَلَ مِنْهُ وَهُوَ فِي الآخِرَةِ مِنَ ...