Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Viungo vya Mwili vitashuhudia Matendo ya Mwanaadamu Siku ya Qiyaamah

Anasema Allaah سبحانه وتعالى

 ((الْيَوْمَ نَخْتِمُ عَلَى أَفْوَاهِهِمْ وَتُكَلِّمُنَا أَيْدِيهِمْ وَتَشْهَدُ أَرْجُلُهُمْ بِمَا كَانُوا يَكْسِبُونَ))
((Leo Tunaviziba vinywa vyao, na iseme Nasi mikono yao, na itoe ushahidi miguu yao kwa waliyokuwa wakiyachuma)) [Yaasiyn:65
]

Siku ya Qiyaamah viungo vya miili vitakuwa ni vyenye kushuhudia matendo ya binaadamu aliyoyatenda hapa duniani: Mfano mikono itasema: "nimeiba".  Miguu itasema, "nimekwenda sehemu ya ma'asi". Macho yatasema, "nimetazama machafu".  Masikio yatasema, "nimesikiliza nyimbo, au umbea" na kadhalika.
Na hivi ndivyo itakavyokuwa hali ya makafiri, wanafiki na wenye kumuasi Mola siku ya kufufuliwa,  watakapokanusha madhambi waliyoyatenda duniani na kuapa kwamba hawakuyafanya, Allaah سبحانه وتعالى Atawafunga midomo yao
na kuviamrisha viungo vizungumze:
 عن أنس بن مالك قال: كنا عند النبي صلى الله عليه وسلم، فضحك حتى بدت نواجذه، ثم قال:  (( أتدرون مم أضحك؟)) قلنا: الله ورسوله أعلم. قال: ((من مجادلة العبد ربه يوم القيامة، يقول: رب : ألم تجرني من الظلم؟ فيقول: بلى. فيقول: لا أجيز علي إلا شاهدًا من نفسي.   فيقول كَفَى بِنَفْسِكَ الْيَوْمَ عَلَيْكَ  ، وبالكرام الكاتبين  شهودا. فيختم على فيه، ويُقال لأركانه: انطقي. فتنطق بعمله، ثم يخلى بينه وبين الكلام، فيقول: بُعدًا لَكُنَّ وسُحقًا، فعنكنَّ كنتُ أناضل))  مسلم والنسائي،.
Imetoka kwa Anas Bin Maalik ambaye alisema, "Tulikuwa na Mtume صلى الله عليه وآله وسلم akacheka mpaka magego yake yakaonekana, kisha akauliza: ((Je? Mnajua kwa nini nacheka?)). Tukasema: Allaah na Mjumbe wake Wanajua.  Akasema: ((([Nacheka] kwa sababu ya majadiliano wa mja na Mola wake Siku ya Qiyaamah, atasema, Ewe Mola wangu, hutonihifadhi na dhulma? (Allaah) Atasema: Bila shaka. Atasema:  Sitokubali  shahidi yeyote dhidi yangu isipokuwa  mwenyewe. (Allaah) Atasema:  Nafsi yako inakutosha leo kukuhisabu. Na watukufu wenye kuandika watakuwa mashahidi dhidi yako.  Kisha mdomo wake utazibwa na vitaambiwa viungo vyake: Sema! (Viungo) vitasema aliyoyafanya. Kisha ataachiwa aseme na atasema (kuviambia viungo vyake): Angamieni, kwani ilikuwa kwa ajili yenu nikigombania ))  [Muslim 4.2280 na An-Nasai  katika Al-Kubrah 6:508
]
Hadiyth nyingine:
 عن أبو موسى الأشعري، رضي الله عنه-: ((يُدعى المؤمن للحساب يوم القيامة، فَيَعْرضُ عليه رَبُّه عملَه فيما بينه وبينه، فيعترف فيقول: نعم أيْ رب، عملتُ عملتُ عملت. قال: فيغفر الله له ذنوبه، ويستره منها. قال: فما على الأرض خَليقة ترى من تلك الذنوب شيئًا، وتبدو حسناته، فَوَدَّ أن الناس كلهم يرونها، ويُدعى الكافر والمنافق للحساب، فَيَعرضُ رَبُّه عليه عمله، فيجحد وفيقول: أي رب، وعزتك لقد كتب علي هذا الملك ما لم أعمل. فيقول له الملك: أما عملت كذا، في يوم كذا، في مكان كذا؟ فيقول: لا وعزتك أيْ رب ما عملتُه. فإذا فعل ذلك خُتِم على فيه((. قال أبو موسى الأشعري: فإني أحسب أول ما ينطق منه الفخذ اليمنى، ثم تلا    الْيَوْمَ نَخْتِمُ عَلَى أَفْوَاهِهِمْ وَتُكَلِّمُنَا أَيْدِيهِمْ وَتَشْهَدُ أَرْجُلُهُمْ بِمَا كَانُوا يَكْسِبُونَ
Imetoka kwa Abu Musa Al-Ash'ariyyiرضي الله عنه kwamba: ((Mu'uumini ataitwa kuhesabiwa siku ya Qiyaamah, na Mola wake atamuonyesha amali zake,  baina yake na Mola wake Atakubali na kukiri kwa kusema: Ndio Mola, nimefanya hayo.  Kisha Allaah Atamsamehe madhambi yake na Kuyaficha wala hakuna kiumbe katika ardhi atakayeona  madhambi hayo, lakini vitendo vyake vyema vitaonekana na Atataka watu wote wavione. Kisha Kafiri na Munaafiq ataletwa hesabuni na Mola wake atamuonyesha vitendo na atakanusha kwa kusema: Ewe Mola, kwa Utukufu Wako, Malaika huyu ameandika vitendo ambavyo sikuvifanya. Malaika atasema kumwambia: Hukufanya kadha na kadha, siku kadha na kadha? Atasema: Kwa Utukufu wako sikufanya.  Atakaposema hivi, Allaah Atamziba mdomo wake)). Abu Musa Al-Ash'ariyyi رضي الله عنه kasema: nafikiri kiungo cha kwanza kuzungumza kitakuwa ni paja la kulia.  Kisha akasoma:
   ((الْيَوْمَ نَخْتِمُ عَلَى أَفْوَاهِهِمْ وَتُكَلِّمُنَا أَيْدِيهِمْ وَتَشْهَدُ أَرْجُلُهُمْ بِمَا كَانُوا يَكْسِبُونَ))
((Leo tunaviziba vinywa vyao, na iseme nasi mikono yao, na itoe ushahidi miguu yao kwa waliyo kuwa wakiyachuma)) [Imaam Ahmad]

Hivyo ndivyo viungo vya mwili vitakavyomchongea mtu muovu siku ya Qiyaama kwa vitendo viovu vyote alivyovitenda. Na ushahidi mwingine Ametutolea Allaah سبحانه وتعالى  katika aya hizi pia:
 ((وَيَوْمَ يُحْشَرُ أَعْدَاء اللَّهِ إِلَى النَّارِ فَهُمْ يُوزَعُونَ))
)) حَتَّى إِذَا مَا جَاؤُوهَا شَهِدَ عَلَيْهِمْ سَمْعُهُمْ وَأَبْصَارُهُمْ وَجُلُودُهُمْ بِمَا كَانُوا يَعْمَلُونَ))
 ((وَقَالُوا لِجُلُودِهِمْ لِمَ شَهِدتُّمْ عَلَيْنَا قَالُوا أَنطَقَنَا اللَّهُ الَّذِي أَنطَقَ كُلَّ شَيْءٍ وَهُوَ خَلَقَكُمْ أَوَّلَ مَرَّةٍ وَإِلَيْهِ تُرْجَعُونَ))
 ((وَمَا كُنتُمْ تَسْتَتِرُونَ أَنْ يَشْهَدَ عَلَيْكُمْ سَمْعُكُمْ وَلَا أَبْصَارُكُمْ وَلَا جُلُودُكُمْ وَلَكِن ظَنَنتُمْ أَنَّ اللَّهَ لَا يَعْلَمُ كَثِيرًا مِّمَّا تَعْمَلُونَ))
((Na siku watakapokusanywa maadui wa Allaah  kwenye Moto, nao wakigawanywa kwa makundi))
((Hata watakapoufikia Moto yatawashuhudia masikio yao, na macho yao na ngozi zao kwa waliyokuwa wakiyatenda))
((Na wao wataziambia ngozi zao: Kwa nini mmetushuhudilia? Nazo zitasema: Ametutamkisha Allaah  Ambaye Ametamkisha kila kitu! Na Yeye ndiye Aliyekuumbeni mara ya kwanza, na Kwake Yeye tu mtarejeshwa))
((Na hamkuwa wenye kujificha hata masikio yenu, na macho yenu, na ngozi zenu, zisikushuhudilieni. Lakini mlidhani kwamba Allaah Hayajui mengi katika mliyo kuwa mkiyatenda))[  Fus-swilat: 19-22]
Kwa hivyo inampasa Mwanaadamu ajichunge na maovu na atambue kuwa viungo alivyoumbwa navyo katika mwili wake ni kwa ajili ya matumizi yenye kumridhisha Mola wake, na sio kwa ajili ya ma'asi, kwani kila kiungo kitakuja kuulizwa:
 ((إِنَّ السَّمْعَ وَالْبَصَرَ وَالْفُؤَادَ كُلُّ أُولئِكَ كَانَ عَنْهُ مَسْؤُولا))

((Hakika masikio, na macho, na moyo - hivyo vyote vitaulizwa)) [Al-Israa: 36]


Maana, mtu ataulizwa siku ya Qiyaama kuhusu hivyo viungo (alivyovitumia) na viungo vitaulizwa kuhusu yeye (Mtu) na ataulizwa kavitumia vipi. [Tafsiyr Ibn Kathiyr]

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Mume kunyonya maziwa ya mkewe inafaa...?

Swali Mume kunyonya maziwa (matiti) ya mkewe inafaa...? Jibu Hakuna Uharamu wa Mume  kunyonya matiti ya mke wake.  Allaah(Subhaana wa Taala) Anasema kwamba:  ((نِسَآؤُكُمْ حَرْثٌ لَّكُمْ فَأْتُواْ حَرْثَكُمْ أَنَّى شِئْتُمْ وَقَدِّمُواْ لأَنفُسِكُمْ وَاتَّقُواْ اللّهَ وَاعْلَمُواْ أَنَّكُم مُّلاَقُوهُ وَبَشِّرِ الْمُؤْمِنِينَ)) ((Wake zenu ni kama konde zenu. Basi ziendeeni konde zenu mpendavyo. Lakini jitangulizieni kheri nafsi zenu, na mcheni Allaah , na jueni kuwa hakika nyinyi mtakutana Naye. Na wape bishara njema Waumini)) [2:223] Kwahiyo mwanamke anayo ruhusa ya kumchezea mkewe sehemu yoyote ya mwili wake pamoja na kunyonya maziwa ya mkewe isipokuwa tu Kufanya naye jimai kwa sehemu ya nyuma (liwati). Aayah hii:  “ Wake zenu ni konde kwenu. Basi ziendeeni konde zenu (panapotoka kizazi) vyovyote mpendavyo. “   imeteremka kuhusu Mayahudi waliokuwa wakisema kuwa mwanaume akimuingilia mke wake kupitia upande wa nyuma basi anazaliwa mtoto akiwa ana makengeza. Ndipo i

Kusikiliza Nasheed na Kaswida zenye Muziki na Vinanda

Swali Inafaa Kusikiliza Nasheed na Kaswida zenye  Muziki na Vinanda Jibu  Shukrani zetu za dhati kwa swali lako kuhusu hukumu ya muziki inayotiwa katika Nashiyd na Qaswiydah. Muziki na utumiaji wa ala za muziki ni haramu katika Dini yetu hii, Uislamu. Zifuatazo ni dalili kuhusu hilo:   Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “ Kutakuwa watu katika Ummah wangu watakao halalisha uzinzi, uvaaji wa Hariri, pombe (unywaji) na ma’aazif (ala za muziki) ” (al-Bukhaariy).   Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “ Mwisho wa zama (dunia) kutakuwa na maporomoko ya ardhi, mawe kutoka mbinguni na kugeuza kwa wanyama, wakati ambapo ala za muziki na waimbaji wanawake watakapoenea na pombe kuruhusiwa ” (atw-Twabaraniy).   Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “ Watu katika ummah wangu watakunywa pombe, kuiita kwa jina jingine. Watatiwa furaha kwa uchezaji wa ala za muziki na uimbaji wa wanawake (watakao

Hukumu ya Mke kutoka nyumbani bila Ruksa ya mumewe

Naam shukrani kwa swali lako kuhusu mkeo kutoka bila ya ruhusa yako kwenda katika mishuari zake. Matatizo haya hutokea mara nyingi kwa mke kutokuwa na ufahamu na ujuzi wa Dini ya Kiislamu. Au mara nyingine huwa kweli ana elimu lakini hushindwa kufuata kimatendo kwa sababu moja au nyingine. Au huenda akawa na elimu, lakini akakosa Dini. Kwa ajili hiyo Imaam al-Bukhaariy, ana mlango katika  Swahiyh  yake wenye kichwa cha habari, “ Elimu Kabla Ya ‘Amali ”. Hata hivyo, huenda mtu akawa na elimu lakini akawa hana ‘amali kwa sababu ya kutokuwa na ikhlaasw.   Ni juu ya mke kumtii mumewe katika mambo yasiyo ya maasi, kwani hakuna utiifu katika maasiya. Ikiwa mume hakutoa ruhusa mbali na kuwa yu mbali na mkewe ni wajibu wa mke kutii amri hiyo. Hata hivyo, haifai kwa mume kuweka vikwazo vya kupita kiasi,  kama kumzuia kwenda kwa wazazi wake na mahali ambapo anaweza kupata elimu ya Kidini. Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala) Anasema: “ Wakikutiini, basi msiwatafutie njia ” (an-Nisaa’ [4]: 34). Hii