Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Neema za Pepo tuliyoahidiwa

                                                           Neema za Pepo Tuliyoahidiwa



Maelezo ya Neema za Pepo tuliyoahidiwa na Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) yametajwa mno katika Qur-aan na Hadiyth, Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala):

إنَّ لِلْمُتَّقِينَ مَفَازًا حَدَائِقَ وَأَعْنَابًا.  وَكَوَاعِبَ أَتْرَابًا. وَكَأْسًا دِهَاقًا. لَّا يَسْمَعُونَ فِيهَا لَغْوًا وَلَا كِذَّابًا جَزَاء مِّن رَّبِّكَ عَطَاء حِسَابًا. 

((Hakika wenye taqwa [wamchao Allaah] wanastahiki kufuzu. Mabustani na mizabibu. Na wake waliolingana nao. Na bilauri zilizojaa. Hawatosikia humo upuuzi wala uongo. Malipo kutoka kwa Mola wako kipawa cha kutosha)) [An-Nabaa: 31-36]


Anasema tena (Subhaanahu wa Ta'ala) katika Suratul-Waaqiah

 وَالسَّابِقُونَ السَّابِقُونَ.  أُوْلَئِكَ الْمُقَرَّبُونَ.  فِي جَنَّاتِ النَّعِيمِ.  ثُلَّةٌ مِّنَ الْأَوَّلِينَ.  وَقَلِيلٌ مِّنَ الْآخِرِينَ. عَلَى سُرُرٍ مَّوْضُونَةٍ. مُتَّكِئِينَ عَلَيْهَا مُتَقَابِلِينَ. يَطُوفُ عَلَيْهِمْ وِلْدَانٌ مُّخَلَّدُونَ.  بِأَكْوَابٍ وَأَبَارِيقَ وَكَأْسٍ مِّن مَّعِينٍ.  لَا يُصَدَّعُونَ عَنْهَا وَلَا يُنزِفُونَ. وَفَاكِهَةٍ مِّمَّا يَتَخَيَّرُونَ.  وَلَحْمِ طَيْرٍ مِّمَّا يَشْتَهُونَ. وَحُورٌ عِينٌ.  كَأَمْثَالِ اللُّؤْلُؤِ الْمَكْنُونِ.  جَزَاء بِمَا كَانُوا يَعْمَلُونَ.

((Na wa mbele watakuwa mbele. Hao ndio watakaokaribishwa. Katika Bustani zenye neema. Fungu kubwa katika wa mwanzo. Na wachache katika wa mwisho. Watakuwa juu ya viti vya fakhari vilivyotonewa. Wakiviegemea wakielekeana. Wakitumikiwa na wavulana wa ujana wa milele. Kwa vikombe na mabirika na bilauri za vinywaji kutoka chemchem safi. Hawataumwa kichwa kwa vinywaji hivyo wala hawatoleweshwa. Na matunda wayapendayo.Na nyama za ndege kama wanavyo tamani. Na Mahuurul-’Ayn.  Walio kama mfano wa lulu ziliohifadhiwa. Ni malipo kwa waliyokuwa wakiyatenda)) [Al-Waaqi’ah: 10-24]

Surah hiyo tukufu inaendelea kutaja Neema za Pepo

((لَا يَسْمَعُونَ فِيهَا لَغْوًا وَلَا تَأْثِيمًا. إِلَّا قِيلًا سَلَامًا سَلَامًا. وَأَصْحَابُ الْيَمِينِ مَا أَصْحَابُ الْيَمِينِ. فِي سِدْرٍ مَّخْضُودٍ.  وَطَلْحٍ مَّنضُود. وَظِلٍّ مَّمْدُودٍ. وَمَاء مَّسْكُوبٍ. وَفَاكِهَةٍ كَثِيرَةٍ.  لَّا مَقْطُوعَةٍ وَلَا مَمْنُوعَةٍ. وَفُرُشٍ مَّرْفُوعَةٍ. إِنَّا أَنشَأْنَاهُنَّ إِنشَاء. فَجَعَلْنَاهُنَّ أَبْكَارًاعُرُبًا أَتْرَابًا. لِّأَصْحَابِ الْيَمِينِ. ثُلَّةٌ مِّنَ الْأَوَّلِينَ. وَثُلَّةٌ مِّنَ الْآخِرِينَ))

((Humo hawatasikia porojo wala maneno ya dhambi. Isipokuwa maneno ya Salama, Salama. Na wale wa mkono wa kulia, ni yepi yatakuwa ya wa kuliani?  Katika mikunazi isiyo na miba.  Na migomba iliyopangiliwa. Na kivuli kilichotanda. Na maji yanayomiminika.  Na matunda mengi. Hayatindikii wala hayakatazwi. Na matandiko yaliyonyanyuliwa. Hakika Sisi Tutawaumba [Mahuurul-‘Ayn] upya. Na tutawafanya vijana. Wanapendana na waume zao, hirimu moja. Kwa ajili ya watu wa kuliani. Fungu kubwa katika wa mwanzo. Na fungu kubwa katika wa mwisho)) [Al-Waaqi’ah: 25-40]

Wa kwanza kuingia Peponi ni Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kama alivyosema:

 (( آتي الجنةَ فأستفتحُ - أي فأستأذن - فيقولُ الخازنُ : من أنتَ ؟ فأقول : أنا محمد !! فيقول :بِكَ أُمرت ألا أفتحَ لأحدٍ قبلكَ (( أخرجه الإمام مسلم في صحيحه 

((Nitafika [katika mlango wa] Pepo nitaomba idhini ya kuingia, atasema milinzi: Nani wewe? Nitasema: Mimi ni Muhammad. Atasema: Kwako nimeamrishwa wala sikuamrishwa nimfungulie mtu mwingine kabla yako)) [Muslim]


Tutazame baadhi ya Hadiyth chache miongoni mwa nyingi  zinazosimulia neema za Pepo:

Daraja yake:
 
عن أبي سعيد الخدري عن النبي صلى الله عليه و سلم قال: ((إن في الجنة مئة درجة، ولو أن العالمين اجتمعوا في إحداهن وسعتهم)) رواه أحمد بن حنبل في مسنده

Kutoka kwa Abi Sa'iyd al-Khudriy (Radhiya Allaahu 'anhu) kwamba Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Hakika katika Pepo kuna daraja mia. Na lau kama walimwengu wangelikusanyika katika mojawapo wangeenea) [Ahmad bin Hanbal katika Musnad yake]

عن أبي هريرة عن النبي صلى الله عليه و سلم قال: ((إن في الجنة مئة درجة أعدها الله للمجاهدين في سبيله، بين كل درجتين كما بين السماء و الأرض، فإذا سألتم الله فاسألوه الفردوس...إلخ)) رواه البخاري

Kutoka kwa Abu Hurayrah (Radhiya Allaahu 'anhu) kwamba Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Katika Pepo kuna daraja mia ambazo Ameziahidi Allaah kwa wanaopigana Jihaad kwa ajili Yake, baina ya kila daraja mbili kama (masafa ya) baina mbingu na ardhi, kwa hivyo, mnapomuomba Allaah Mumuombe (pepo ya) Al-Firdaws))[al-Bukhaariy]


Hakuna uchafu humo

  قال رسول الله صلى الله عليه وسلم : (( إن أول زمرة يدخلون الجنة على صورة القمر ليلة البدر ، ثم الذين يلونهم على أشد كوكب دري في السماء إضاءة ، لا يبولون ولا يتغوطون ، ولا يتفلون ولا يمتخطون ، أمشاطهم الذهب ، ورشحهم المسك ، ومجامرهم الألوة - الألنجوج ، عود الطيب - وأزواجهم الحور العين ، على خلق رجل واحد ، على صورة أبيهم آدم ، ستون ذراعا في السماء((البخاري

Amesema Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): ((Kundi la mwanzo watakaongia Peponi watakuwa kama mwezi unapokuwa kamili. Kisha watafuatia ambao watakuwa kama nyota zinazong’ara mbinguni. Hawatakojoa, wala hawatofanya haja kubwa, wala  hawatotema mate, wala hawatopenga kamasi,  vitana vyao vya dhahabu na jasho lao litanukia kama  misk,  vyetezo vyao watatumia udi wa mawardi, wake zao watakuwa ni  Huurul-‘Ayn wenye macho makubwa. Watu watakuwa katika umbo la aina ya mtu mmoja, la baba yao Aadam [wakiwa] nchi sitini kwa urefu)) [Al-Bukhaariy]   


Mito yake

عَنْ حَكِيم بْن مُعَاوِيَة عَنْ أَبِيهِ قَالَ سَمِعْت رَسُول اللَّه صَلَّى اللَّه عَلَيْهِ وَسَلَّمَ يَقُول: (( فِي الْجَنَّة بَحْر اللَّبَن وَبَحْر الْمَاء وَبَحْر الْعَسَل وَبَحْر الْخَمْر ثُمَّ تَشَقَّقُ الْأَنْهَار مِنْهَا بَعْد)) وَرَوَاهُ التِّرْمِذِيّ

Imetoka kwa Hakiym bin Mu'aawiyah kutoka kwa baba yake ambaye amesema: Nimemsikia Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema: ((Katika Pepo, kuna bahari ya maziwa, na bahari ya maji, na bahari ya asali na bahari ya ulevi [wenye ladha]) kisha mito itafunguka humo)) [At-Tirmidhiy]

Baada ya kutambua sifa chache hizo Pepo yenye Neema, tunatumai kwamba tutajitahdi kufanya mema mengi ili tujaaliwe kuingia Peponi ambako maisha yake ni ya kudumu milele kwa furaha na amani.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Mume kunyonya maziwa ya mkewe inafaa...?

Swali Mume kunyonya maziwa (matiti) ya mkewe inafaa...? Jibu Hakuna Uharamu wa Mume  kunyonya matiti ya mke wake.  Allaah(Subhaana wa Taala) Anasema kwamba:  ((نِسَآؤُكُمْ حَرْثٌ لَّكُمْ فَأْتُواْ حَرْثَكُمْ أَنَّى شِئْتُمْ وَقَدِّمُواْ لأَنفُسِكُمْ وَاتَّقُواْ اللّهَ وَاعْلَمُواْ أَنَّكُم مُّلاَقُوهُ وَبَشِّرِ الْمُؤْمِنِينَ)) ((Wake zenu ni kama konde zenu. Basi ziendeeni konde zenu mpendavyo. Lakini jitangulizieni kheri nafsi zenu, na mcheni Allaah , na jueni kuwa hakika nyinyi mtakutana Naye. Na wape bishara njema Waumini)) [2:223] Kwahiyo mwanamke anayo ruhusa ya kumchezea mkewe sehemu yoyote ya mwili wake pamoja na kunyonya maziwa ya mkewe isipokuwa tu Kufanya naye jimai kwa sehemu ya nyuma (liwati). Aayah hii:  “ Wake zenu ni konde kwenu. Basi ziendeeni konde zenu (panapotoka kizazi) vyovyote mpendavyo. “   imeteremka kuhusu Mayahudi waliokuwa wakisema kuwa mwanaume akimuingilia mke wake kupitia upande wa nyuma basi anazaliwa mtoto akiwa ana makengeza. Ndipo i

Kusikiliza Nasheed na Kaswida zenye Muziki na Vinanda

Swali Inafaa Kusikiliza Nasheed na Kaswida zenye  Muziki na Vinanda Jibu  Shukrani zetu za dhati kwa swali lako kuhusu hukumu ya muziki inayotiwa katika Nashiyd na Qaswiydah. Muziki na utumiaji wa ala za muziki ni haramu katika Dini yetu hii, Uislamu. Zifuatazo ni dalili kuhusu hilo:   Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “ Kutakuwa watu katika Ummah wangu watakao halalisha uzinzi, uvaaji wa Hariri, pombe (unywaji) na ma’aazif (ala za muziki) ” (al-Bukhaariy).   Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “ Mwisho wa zama (dunia) kutakuwa na maporomoko ya ardhi, mawe kutoka mbinguni na kugeuza kwa wanyama, wakati ambapo ala za muziki na waimbaji wanawake watakapoenea na pombe kuruhusiwa ” (atw-Twabaraniy).   Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “ Watu katika ummah wangu watakunywa pombe, kuiita kwa jina jingine. Watatiwa furaha kwa uchezaji wa ala za muziki na uimbaji wa wanawake (watakao

Hukumu ya Mke kutoka nyumbani bila Ruksa ya mumewe

Naam shukrani kwa swali lako kuhusu mkeo kutoka bila ya ruhusa yako kwenda katika mishuari zake. Matatizo haya hutokea mara nyingi kwa mke kutokuwa na ufahamu na ujuzi wa Dini ya Kiislamu. Au mara nyingine huwa kweli ana elimu lakini hushindwa kufuata kimatendo kwa sababu moja au nyingine. Au huenda akawa na elimu, lakini akakosa Dini. Kwa ajili hiyo Imaam al-Bukhaariy, ana mlango katika  Swahiyh  yake wenye kichwa cha habari, “ Elimu Kabla Ya ‘Amali ”. Hata hivyo, huenda mtu akawa na elimu lakini akawa hana ‘amali kwa sababu ya kutokuwa na ikhlaasw.   Ni juu ya mke kumtii mumewe katika mambo yasiyo ya maasi, kwani hakuna utiifu katika maasiya. Ikiwa mume hakutoa ruhusa mbali na kuwa yu mbali na mkewe ni wajibu wa mke kutii amri hiyo. Hata hivyo, haifai kwa mume kuweka vikwazo vya kupita kiasi,  kama kumzuia kwenda kwa wazazi wake na mahali ambapo anaweza kupata elimu ya Kidini. Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala) Anasema: “ Wakikutiini, basi msiwatafutie njia ” (an-Nisaa’ [4]: 34). Hii