Swali
Mume kunyonya maziwa (matiti) ya mkewe inafaa...?
Jibu
Hakuna Uharamu wa Mume kunyonya matiti ya mke wake.
Allaah(Subhaana wa Taala) Anasema kwamba:
((نِسَآؤُكُمْ حَرْثٌ لَّكُمْ فَأْتُواْ حَرْثَكُمْ أَنَّى شِئْتُمْ وَقَدِّمُواْ لأَنفُسِكُمْ وَاتَّقُواْ اللّهَ وَاعْلَمُواْ أَنَّكُم مُّلاَقُوهُ وَبَشِّرِ الْمُؤْمِنِينَ))
((Wake zenu ni kama konde zenu. Basi ziendeeni konde zenu mpendavyo. Lakini jitangulizieni kheri nafsi zenu, na mcheni Allaah , na jueni kuwa hakika nyinyi mtakutana Naye. Na wape bishara njema Waumini)) [2:223]
Kwahiyo mwanamke anayo ruhusa ya kumchezea mkewe sehemu yoyote ya mwili wake pamoja na kunyonya maziwa ya mkewe isipokuwa tu Kufanya naye jimai kwa sehemu ya nyuma (liwati).
Kwahiyo Mume inajuzu kwake kunyonya matiti ya mke wake.Na pia Mume hawi haramu kwake (kwa mkewe) hata kama atameza maziwa yake ya kifua.
Kwa maelezo zaidi Rejea Kitab Al-Lajnah ad-Daai´mah. al-Fataawaa al-Qayyimah lil-Usrah al-Muslimah, uk 118-119.
Na Allaah anajua zaidi
Mume kunyonya maziwa (matiti) ya mkewe inafaa...?
Jibu
Hakuna Uharamu wa Mume kunyonya matiti ya mke wake.
Allaah(Subhaana wa Taala) Anasema kwamba:
((نِسَآؤُكُمْ حَرْثٌ لَّكُمْ فَأْتُواْ حَرْثَكُمْ أَنَّى شِئْتُمْ وَقَدِّمُواْ لأَنفُسِكُمْ وَاتَّقُواْ اللّهَ وَاعْلَمُواْ أَنَّكُم مُّلاَقُوهُ وَبَشِّرِ الْمُؤْمِنِينَ))
((Wake zenu ni kama konde zenu. Basi ziendeeni konde zenu mpendavyo. Lakini jitangulizieni kheri nafsi zenu, na mcheni Allaah , na jueni kuwa hakika nyinyi mtakutana Naye. Na wape bishara njema Waumini)) [2:223]
Kwahiyo mwanamke anayo ruhusa ya kumchezea mkewe sehemu yoyote ya mwili wake pamoja na kunyonya maziwa ya mkewe isipokuwa tu Kufanya naye jimai kwa sehemu ya nyuma (liwati).
Aayah hii: “Wake zenu ni konde kwenu. Basi ziendeeni konde zenu (panapotoka kizazi) vyovyote mpendavyo.“ imeteremka kuhusu Mayahudi waliokuwa wakisema kuwa mwanaume akimuingilia mke wake kupitia upande wa nyuma basi anazaliwa mtoto akiwa ana makengeza. Ndipo ikateremka hii Aayah [Al-Bukhaariy, Muslim kutoka kwa Jaabir (رضي الله عنه)].
Pia, Ibn ‘Abbaas (رضي الله عنهما) alisema kuwa kauli hiyo; “Wanawake zenu ni konde kwenu“ iliteremshwa kuhusu baadhi ya watu wa Answaar ambao walikuja kwa Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) wakamuuliza (kuhusu kumuingilia mwanamke kutokea upande wa nyuma) akawajibu: “Muingilie vyovyote upendavyo madhali ni ukeni.”[Ahmad]
Hadiyth kama ilivyothibiti :
عَنْ جَابِرِ بْنِ عَبْدِ اللَّهِ، أَنَّ يَهُودَ، كَانَتْ تَقُولُ إِذَا أُتِيَتِ الْمَرْأَةُ مِنْ دُبُرِهَا فِي قُبُلِهَا ثُمَّ حَمَلَتْ كَانَ وَلَدُهَا أَحْوَلَ . قَالَ فَأُنْزِلَتْ: ((نِسَاؤُكُمْ حَرْثٌ لَكُمْ فَأْتُوا حَرْثَكُمْ أَنَّى شِئْتُمْ))
Imepokelewa kutoka kwa Jaabir bin ‘Abdillaah kwamba Mayahudi walikuwa wanasema pale mke anapoingiliwa mbele katika sehemu za siri, lakini akiwa amegeuka nyuma, na pindi anaposhika mimba husema kuwa mtoto atazaliwa kengeza. Hapo ikateremshwa Aayah:“Wake zenu ni konde kwenu. Basi ziendeeni konde zenu (panapotoka kizazi) vyovyote mpendavyo.“ [Muslim Kitaab An-Nikaah]
Kwahiyo Mume inajuzu kwake kunyonya matiti ya mke wake.Na pia Mume hawi haramu kwake (kwa mkewe) hata kama atameza maziwa yake ya kifua.
Kwa maelezo zaidi Rejea Kitab Al-Lajnah ad-Daai´mah. al-Fataawaa al-Qayyimah lil-Usrah al-Muslimah, uk 118-119.
Na Allaah anajua zaidi
Maoni