Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Kujifunza elimu ya Kishari´ah ni nuru

            Kujifunza elimu ya Kishari´ah ni nuru




Kwa hali yoyote, kujifunza elimu ni jambo lisilokuwa na shaka kwamba ndio maisha na nuru iliyoamrishwa na Allaah (Jalla wa ´Alaa), ikaamrishwa na Mtume Wake (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na wakakokoteza kwayo. Amesema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Mwenye kushika njia akitafuta humo elimu, basi Allaah humsahilishia njia ya kuelekea Peponi. Hawakusanyiki watu katika nyumba miongoni mwa nyumba za Allaah, wakikisoma Kitabu cha Allaah na wakadarasishana baina yao, isipokuwa huteremka juu yao utulivu, rehema huwafunika, Malaika huwazunguka na Allaah huwataja kwa wale walioko pamoja Naye.”[1]
Amesema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Malaika hukunjua mbawa zao kwa mwenye kutafuta elimu hali ya kuridhia kile anachokifanya.”
Haya ni makokotezo juu ya kujifunza elimu na kuikimbilia ili dini ya mja iweze kunyooka, anufaike mwenyewe na pia awanufaishe wengine. Ni jambo lisilokuwa na shaka ya kwamba ikitoweka elimu na wakatoweka wanachuoni, basi Ummah utaangamia. Amesema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Hakika Allaah hatoiondoa elimu hii kwa kuinyakua kutoka kwenye vifua vya wanachuoni, lakini ataiondoa elimu kwa kufa kwa wanachuoni, mpaka pasibakie mwanachuoni yoyote ndipo watu watawachukua viongozi wajinga. Watawauliza maswali wafutu bila ya elimu. Matokeo yake watapotea na kuwapoteza wengine.”[2]
Kutoa fatwa pasi na elimu ni kupotea na kuwapoteza wengine. Ni lazima fatwa iwe juu ya elimu katika Qur-aan na Sunnah. Vinginevyo inakuwa ni upotevu na maangamivu. Haya hayawezi kupatikana isipokuwa kwa kusoma na mtu awe na hima ya kusoma kabla ya muda kupita midhali wanachuoni wapo. Utafika wakati ambapo hakuna mwanachuoni hata mmoja, hapo ndipo watu watawaelekea wajinga, wenye kujifanya ni wanachuoni na wasomaji ambapo watatoa fatwa pasi na elimu na matokeo yake wapotee wao na wapotoshe wengine.
[1] Ameipokea Muslim (2699).
[2] Ameipokea al-Bukhaariy (100) na Muslim (2673).



Rejea kitab  Sharh Nawaaqidh-il-Islaam, uk. 196-197

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Hukumu ya kupeleka barua ya posa kwenye kitambaa cheupe

                      Hukumu ya kupeleka barua ya posa kwenye kitambaa cheupe  Hakika ni kuwa posa ilivyofanyika katika Uislamu kuanzia wakati wa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) inafahamika vilivyo. Posa inaweza kuja kutoka kwa mume na watu wake kwa jamaa za mke au mzazi wa mke kumtafutia binti yake mume. Ikiwa wazazi watakwenda kwa wazazi wa mke, baada ya kupeleka maneno, na wazazi wa mke watataka kupatiwa muda wa kufikiria, kufanya shuuraa, kuulizia, kutafiti na baadaye kukubali au kukataa. Ikiwa wamekubali baada ya kumshauri binti  yao  ni vyema mume mtarajiwa aende amuone atakaye kuwa mkewe ili apate kutulia na kuridhika kabla siku ya Nikaah. Binti huyo au wazazi wake wataweka kiwango cha mahari ambacho mume anatakiwa kutoa. Hii njia ya kuweka pesa kwenye kitambaa au bahasha haipo katika mafunzo ya Kiislam, na huenda ni njia ya kitamaduni fulani au itikadi f...

Maana ya Uadilifu

                                         MAANA  YA  UADILIFU  KATIKA  UISLAMU Assallaam  Aleykum  WarahmatulLaah  Wabarakatuh Alhamdu Lillaahi Rabil'aalamiyn) Allaahumma Swalli 'alaa Muhammad wa 'alaa aali Muhammad kamaa Swallayta 'alaa Ibraahiym wa 'alaa aali Ibraahiym wa Baarik 'alaa Muhammad wa 'alaa aali Muhammad kamaa Baarakta 'alaa Ibraahiym wa 'alaa aali Ibraahiym fil'aalamyna Innaka Hamiydun Majiyd. Ndugu zangu Waislam Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) Anasema katika Qur-aan. إِنَّ اللَّـهَ يَأْمُرُ بِالْعَدْلِ وَالْإِحْسَانِ وَإِيتَاءِ ذِي الْقُرْبَىٰ وَيَنْهَىٰ عَنِ الْفَحْشَاءِ وَالْمُنكَرِ وَالْبَغْيِ ۚيَعِظُكُمْ لَعَلَّكُمْ تَذَكَّرُونَ Hakika Allaah Anaamrishia uadilifu na ihsaan na kuwapa (mahitajio na msaada) jamaa wa karibu; na Anakataza machafu na munkari na ukandamizaji. Anakuwaidhini huenda mkapata kukumb...

Viungo vya Mwili vitashuhudia Matendo ya Mwanaadamu Siku ya Qiyaamah

Anasema Allaah  سبحانه وتعالى   ((الْيَوْمَ نَخْتِمُ عَلَى أَفْوَاهِهِمْ وَتُكَلِّمُنَا أَيْدِيهِمْ وَتَشْهَدُ أَرْجُلُهُمْ بِمَا كَانُوا يَكْسِبُونَ)) ((Leo Tunaviziba vinywa vyao, na iseme Nasi mikono  yao , na itoe ushahidi miguu  yao kwa waliyokuwa wakiyachuma))  [Yaasiyn :65 ] Siku ya Qiyaamah viungo vya miili vitakuwa ni vyenye kushuhudia matendo ya binaadamu aliyoyatenda hapa duniani: Mfano mikono itasema: "nimeiba".  Miguu itasema, "nimekwenda sehemu ya ma'asi". Macho yatasema, "nimetazama machafu".  Masikio yatasema, "nimesikiliza nyimbo, au umbea" na kadhalika. Na hivi ndivyo itakavyokuwa hali ya makafiri, wanafiki na wenye kumuasi Mola siku ya kufufuliwa,  watakapokanusha madhambi waliyoyatenda duniani na kuapa kwamba hawakuyafanya, Allaah  سبحانه وتعالى  Atawafunga midomo  yao na kuviamrisha viungo vizungumze:   عن أنس بن مالك قال: كنا عند النبي صلى ال...