Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Je,Ni Kweli Swawm Inanin'ginia Baina ya Mbingu na Ardhi hadi Mtu atoe Zakaatul-Fitwr?

SWALI


Je, Hadiyth inayosema kuwa Swawm ya Ramadhaan inaning'inia baina ya mbinu na ardhi na haipandishwi juu hadi ilipwe Zakaatul-Fitwr ni Sahihi? 



JIBU


Naam kwanza kabisa Hadiyth hiyo ni dhaifu.

Katika Al-Jaami' as-Swaghiyr, as-Suyuwtwiy ameihusisha kwa Ibn Shaahiyn katika Targhiyb yake: "Imesimuliwa katika Adhw-Dhwiyaa' kutoka kwa Jariyr bin 'Abdillaah (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)  amesema: Mwezi wa Ramadhaan unaning'inia baina ya mbingu na ardhi na (Swawm) haipelekwi juu kwa Allaah isipokuwa kwa (kutolewa) Zakaatul-Fitwr"

Imechambuliwa kuwa ni dhaifu na as-Suyuwtwiy. Al-Manaawiy ameeleza sababu yake katika Faydhw Al-Qadiyr ambako amesema: "Imesimuliwa na Ibn Al-Jawziy katika Al-Waahiyaat na kasema: Sio Swahiyh, isnaad yake inajumuisha Muhammad bin 'Ubayd al-Baswriy ambaye ni majhuwl (asiyejulikana).

Imechambuliwa pia kuwa ni dhaifu na Imaam al-Albaaniy katika as-Silsilatul-Ahaadiyth ad-Dhwa'iyfah (43). Kasema: "Hata kama ingekuwa ni Hadiyth Swahiyh, basi maana iliyodhihiri ni kukubaliwa kwa Swawm ya Ramadhwaan inategemea baada ya kulipa Zakaatul-Fitwr tu, na ikiwa mtu hakulipa, basi Swawm  yake haitokubaliwa. Lakini simjui Mwanachuoni yeyote aliyesema hivyo na Hadiyth sio Swahiyh" [mwisho wa kunukuu]

Kwa vile Hadiyth sio Swahiyh, hakuna atakayeweza kusema kwamba Swawm ya Ramadhwaan inakubalika tu baada ya kutoa Zakaatul-Fitwr kwa saabu hakuna atakayejua hivyo isipokuwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam).

Imethibitika katika Sunan Abi Daawuwd kwamba Ibn 'Abbaas (Radhwiya Allaahu 'anhumaa) amesema: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)  amefaridhisha Zakaatul-Fitwr kuwalisha masikini kama ni kutakasa swiyaam za aliyefunga kutokana na maneno ya upuuzi na kauli chafu" [Imepewa daraja ya Hasan na Shaykh al-Albaaniy katika Swahiyh Sunan Abi Daawuwd] 

Hadiyth hii inaelezea hikma ya Zakaatul-Fitwr ambayo kufidia kasoro yoyote iliyotokea katika Swawm. Haisemi kuwa Swawm haitokubaliwa ila tu baada ya kutoa Zakaatul-Fitwr.

Na Allaah Anajua zaidi

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Hukumu ya kupeleka barua ya posa kwenye kitambaa cheupe

                      Hukumu ya kupeleka barua ya posa kwenye kitambaa cheupe  Hakika ni kuwa posa ilivyofanyika katika Uislamu kuanzia wakati wa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) inafahamika vilivyo. Posa inaweza kuja kutoka kwa mume na watu wake kwa jamaa za mke au mzazi wa mke kumtafutia binti yake mume. Ikiwa wazazi watakwenda kwa wazazi wa mke, baada ya kupeleka maneno, na wazazi wa mke watataka kupatiwa muda wa kufikiria, kufanya shuuraa, kuulizia, kutafiti na baadaye kukubali au kukataa. Ikiwa wamekubali baada ya kumshauri binti  yao  ni vyema mume mtarajiwa aende amuone atakaye kuwa mkewe ili apate kutulia na kuridhika kabla siku ya Nikaah. Binti huyo au wazazi wake wataweka kiwango cha mahari ambacho mume anatakiwa kutoa. Hii njia ya kuweka pesa kwenye kitambaa au bahasha haipo katika mafunzo ya Kiislam, na huenda ni njia ya kitamaduni fulani au itikadi f...

Maana ya Uadilifu

                                         MAANA  YA  UADILIFU  KATIKA  UISLAMU Assallaam  Aleykum  WarahmatulLaah  Wabarakatuh Alhamdu Lillaahi Rabil'aalamiyn) Allaahumma Swalli 'alaa Muhammad wa 'alaa aali Muhammad kamaa Swallayta 'alaa Ibraahiym wa 'alaa aali Ibraahiym wa Baarik 'alaa Muhammad wa 'alaa aali Muhammad kamaa Baarakta 'alaa Ibraahiym wa 'alaa aali Ibraahiym fil'aalamyna Innaka Hamiydun Majiyd. Ndugu zangu Waislam Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) Anasema katika Qur-aan. إِنَّ اللَّـهَ يَأْمُرُ بِالْعَدْلِ وَالْإِحْسَانِ وَإِيتَاءِ ذِي الْقُرْبَىٰ وَيَنْهَىٰ عَنِ الْفَحْشَاءِ وَالْمُنكَرِ وَالْبَغْيِ ۚيَعِظُكُمْ لَعَلَّكُمْ تَذَكَّرُونَ Hakika Allaah Anaamrishia uadilifu na ihsaan na kuwapa (mahitajio na msaada) jamaa wa karibu; na Anakataza machafu na munkari na ukandamizaji. Anakuwaidhini huenda mkapata kukumb...

Viungo vya Mwili vitashuhudia Matendo ya Mwanaadamu Siku ya Qiyaamah

Anasema Allaah  سبحانه وتعالى   ((الْيَوْمَ نَخْتِمُ عَلَى أَفْوَاهِهِمْ وَتُكَلِّمُنَا أَيْدِيهِمْ وَتَشْهَدُ أَرْجُلُهُمْ بِمَا كَانُوا يَكْسِبُونَ)) ((Leo Tunaviziba vinywa vyao, na iseme Nasi mikono  yao , na itoe ushahidi miguu  yao kwa waliyokuwa wakiyachuma))  [Yaasiyn :65 ] Siku ya Qiyaamah viungo vya miili vitakuwa ni vyenye kushuhudia matendo ya binaadamu aliyoyatenda hapa duniani: Mfano mikono itasema: "nimeiba".  Miguu itasema, "nimekwenda sehemu ya ma'asi". Macho yatasema, "nimetazama machafu".  Masikio yatasema, "nimesikiliza nyimbo, au umbea" na kadhalika. Na hivi ndivyo itakavyokuwa hali ya makafiri, wanafiki na wenye kumuasi Mola siku ya kufufuliwa,  watakapokanusha madhambi waliyoyatenda duniani na kuapa kwamba hawakuyafanya, Allaah  سبحانه وتعالى  Atawafunga midomo  yao na kuviamrisha viungo vizungumze:   عن أنس بن مالك قال: كنا عند النبي صلى ال...