Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Mwanamke Mwenye Hedhi Afanye Nini Masiku ya Mwisho Kupata Laylatul-Qadr?

SWALI

Nilikuwa nawaza mwanamke mwenye hedhi afanye nini usiku wa Laylatul-Qadr ili aweze kupata thawabu zaidi kwa kujishughulisha na ibada? Na kama inafaa, ibada ya aina gani inaruhusiwa afanye usiku huo?


JIBU


Naam,Mwanamke mwenye hedhi anaweza kufanya vitendo vyote vya ibada isipokuwa kuswali, kufunga, kuzunguka Ka'bah na kukaa I'tikaaf Msiktini.

Imesimuliwa kwamba Mtume  صلى الله عليه وآله وسلم  alikuwa akikesha usiku katika siku kumi za mwisho za Ramadhaan.

(Al-Bukhaariy 2401) na (Muslim 1174) wamesimulia kwamba Mama wa Waumini 'Aaishah رضي الله عنهاamesema ((Zinapoingia siku kumi za mwisho katika Ramadhaan, Mtume صلى الله عليه وآله وسلم hujiepusha na wake zake, na hukesha usiku na kuwaamsha 'aila (familia) yake))

Kukesha usiku haina maana kwamba ni kwa kuswali pekee, bali ni kwa kila aina ya vitendo vya ibada, na hivi ndivyo walivyofasiri 'Ulamaa.

Al-Haafidh kasema: "Kukesha usiku ina maana kwamba kufanya aina za vitendo vya ibada"

An-Nawawy kasema:  "Kukesha usiku kwa kusimama kuswali na kadhalika",  akasema katika 'Awn al-Ma'abuud' kwamba ni kuswali, kufanya dhikr na kusoma Qur-aan.

Kuswali kwa kusimama ni kitendo bora kabisa Muislamu anaweza kufanya usiku wa Laylatul-Qadr kutokana na kauli ya Mtume صلى الله عليه وآله وسلم :((Yeyote atakayesimama  kuswali  usiku wa Laylatul-Qadr kwa imani na kutaraji malipo atafutiwa madhambi yake ya nyuma)) Al-Bukhaariy 1901 na Muslim 760

Kwa sababu mwanamke mwenye hedhi haruhusiwi kuswali, ila anaweza kukesha usiku kwa kufanya aina ya vitendo vya 'Ibaadah zingine mbalimbali kama vile:

1) Kusoma Qur-aan

2) Kumdhukuru Allaah  kama kusema Subhaan-Allaah, La ilaaha illa Allaah, al-Hamdu Lillaah, anaweza kurudia kusema Subhaana-Allaah wal-Hamdu Lillaah, wa laa ilaaha illa Allaah, wa Allaahu Akbar na vile vile Subhaana Allaah wa bihamdihi, Subhaana Allaahul-‘Adhiym.

3) Istighfaar kwa kurudia kusema "Astaghfiru-Allaah"

4) Kuomba Du'aa.  Anaweza kumuomba Allaah anayohitaji ya duniani na Akhera kwani Du'aa ni kitendo bora kabisa cha 'Ibaadah. Mtume صلى الله عليه وآله وسلم amesema ((Du'aa ni 'Ibaadah))  At-Tirmidhiy, 2895; na imesemwa kuwa ni  Swahiyh na Al-Albaaniy katika Swahiyh At-Tirmidhiy, 2370

Mwanamke mwenye hedhi anaweza kufanya vitendo vyote hivi usiku wa Laylatul-Qadr. 

 Na Allaah Anajua zaidi

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Hukumu ya kupeleka barua ya posa kwenye kitambaa cheupe

                      Hukumu ya kupeleka barua ya posa kwenye kitambaa cheupe  Hakika ni kuwa posa ilivyofanyika katika Uislamu kuanzia wakati wa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) inafahamika vilivyo. Posa inaweza kuja kutoka kwa mume na watu wake kwa jamaa za mke au mzazi wa mke kumtafutia binti yake mume. Ikiwa wazazi watakwenda kwa wazazi wa mke, baada ya kupeleka maneno, na wazazi wa mke watataka kupatiwa muda wa kufikiria, kufanya shuuraa, kuulizia, kutafiti na baadaye kukubali au kukataa. Ikiwa wamekubali baada ya kumshauri binti  yao  ni vyema mume mtarajiwa aende amuone atakaye kuwa mkewe ili apate kutulia na kuridhika kabla siku ya Nikaah. Binti huyo au wazazi wake wataweka kiwango cha mahari ambacho mume anatakiwa kutoa. Hii njia ya kuweka pesa kwenye kitambaa au bahasha haipo katika mafunzo ya Kiislam, na huenda ni njia ya kitamaduni fulani au itikadi f...

Maana ya Uadilifu

                                         MAANA  YA  UADILIFU  KATIKA  UISLAMU Assallaam  Aleykum  WarahmatulLaah  Wabarakatuh Alhamdu Lillaahi Rabil'aalamiyn) Allaahumma Swalli 'alaa Muhammad wa 'alaa aali Muhammad kamaa Swallayta 'alaa Ibraahiym wa 'alaa aali Ibraahiym wa Baarik 'alaa Muhammad wa 'alaa aali Muhammad kamaa Baarakta 'alaa Ibraahiym wa 'alaa aali Ibraahiym fil'aalamyna Innaka Hamiydun Majiyd. Ndugu zangu Waislam Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) Anasema katika Qur-aan. إِنَّ اللَّـهَ يَأْمُرُ بِالْعَدْلِ وَالْإِحْسَانِ وَإِيتَاءِ ذِي الْقُرْبَىٰ وَيَنْهَىٰ عَنِ الْفَحْشَاءِ وَالْمُنكَرِ وَالْبَغْيِ ۚيَعِظُكُمْ لَعَلَّكُمْ تَذَكَّرُونَ Hakika Allaah Anaamrishia uadilifu na ihsaan na kuwapa (mahitajio na msaada) jamaa wa karibu; na Anakataza machafu na munkari na ukandamizaji. Anakuwaidhini huenda mkapata kukumb...

Viungo vya Mwili vitashuhudia Matendo ya Mwanaadamu Siku ya Qiyaamah

Anasema Allaah  سبحانه وتعالى   ((الْيَوْمَ نَخْتِمُ عَلَى أَفْوَاهِهِمْ وَتُكَلِّمُنَا أَيْدِيهِمْ وَتَشْهَدُ أَرْجُلُهُمْ بِمَا كَانُوا يَكْسِبُونَ)) ((Leo Tunaviziba vinywa vyao, na iseme Nasi mikono  yao , na itoe ushahidi miguu  yao kwa waliyokuwa wakiyachuma))  [Yaasiyn :65 ] Siku ya Qiyaamah viungo vya miili vitakuwa ni vyenye kushuhudia matendo ya binaadamu aliyoyatenda hapa duniani: Mfano mikono itasema: "nimeiba".  Miguu itasema, "nimekwenda sehemu ya ma'asi". Macho yatasema, "nimetazama machafu".  Masikio yatasema, "nimesikiliza nyimbo, au umbea" na kadhalika. Na hivi ndivyo itakavyokuwa hali ya makafiri, wanafiki na wenye kumuasi Mola siku ya kufufuliwa,  watakapokanusha madhambi waliyoyatenda duniani na kuapa kwamba hawakuyafanya, Allaah  سبحانه وتعالى  Atawafunga midomo  yao na kuviamrisha viungo vizungumze:   عن أنس بن مالك قال: كنا عند النبي صلى ال...