Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Madhara Ya Ghiybah (Kusengenya) Na An-Namiymah (Kufitinisha) -Sehemu ya 12

Madhara Ya An-Namiymah (Kufitinisha ) - Vipi Kutibu An-Namiymah?

 

Mafunzo yafuatayo yataweza Inshaa-Allaah kutibu maovu ya An-Namiymah ikiwa yatatekelezwa na inampasa kila mwenye tabia hii haraka ajifunze ili kujiepusha na maouvu haya yanayosababisha ufisadi na chuki baina ya ndugu Waislamu. Tutambue kuwa hii ni moja wapo ya jihadi ya nafsi kwa kujiepusha na maovu yanayoamrishwa na nafsi, ambayo ni jihadi  bora kabisa na itamuweka Muislamu katika Ridhaa Ya Mola wake Mtukufu. Amesema Mtume (Swalla-Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) kupitia usimulizi wa Fadhwaalah bin ‘Ubaydullaah (Radhiya Allaahu ‘anhu):

 

(( ألا أخبركم بالمؤمن؟ من أمنه الناس علىأموالهم وأنفسهم، والمسلم من سلم الناس من لسانه ويده، والمجاهد من جاهد نفسه في طاعة الله، والمهاجر من هجر الخطايا والذنوب))  أحمد والحاكم , قال الألباني  "إسناد صحيح" سلسلة الأحاديثالصحيحة

((Je, nikujulisheni kuhusu Muumini? Anayeaminiwa na watu juu ya mali zao na nafsi zao. Na Muislmu anayeweka amani kwa watu kwa ulimi wake na mkono wake. Na mfanyaji jihadi ni yule anayefanya jihadi ya nafsi yake katika kumtii Allaah, na mhamaji Hijrah ni anayehama makosa na madhambi)) [Ahmad,   Al Haakim  na amesema Al-Albaanyi katika Silisilatul-Ahaadiyth Asw-Swahiyhah:  “Hii isnaad Swahiyh]

 

 

Mwenye kufitinishwa

 

1-    Inapasa mwenye kuletewa fitna kutahadhari na mfitinishaji kwani mfitinishaji ni fasiki na fasiki anahitaji kukhofiwa hadi upatikane ushahidi kamaasemayo ni kweli. Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) (Subhaanahu wa Ta'ala):

 

 

((يَا أَيُّهَا الذِينَ آمَنُوا إِنْ جَاءَكُمْ فَاسِقٌ بِنَبَأٍ فَتَبَيَّنُوا أَنْ تُصِيبُوا قَوْمًا بِجَهَالَةٍ فَتُصْبِحُوا عَلَىمَا فَعَلْتُمْ نَادِمِينَ ))

 

((Enyi mlio amini! Akikujieni mpotovu na khabari yoyote, ichunguzeni, msije mkawasibu watu kwa kutojua, na mkawa tena wenye kujuta kwa mliyoyatenda)) [Al-Hujuraat: 6]

 

 

2-      Kutokuamini asemayo, uwe na dhana nzuri na nduguyo unayepatana naye, badala ya dhana mbaya kama Anavyosema Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) (Subhaanahu wa Ta'ala):

 

((يَا أَيُّهَا الذِينَ آمَنُوا اجْتَنِبُوا كَثِيرًا مِنَ الظَّنِّ إِنَّ بَعْضَ الظَّنِّ إِثْمٌ))

((Enyi mlioamini! Jiepusheni na dhana nyingi, kwani baadhi ya dhana ni dhambi))[Al-Hujuraat: 12]

 

3-      Usipendelee kuwa na urafiki na mfitinishaji na anapokuja  kukufitinsha ni vizuri kumpa nasaha, kumkataza asiwe anafanya hivyo hata kama ni kweli kamsikia mwenzako anakusengenya. Kufanya hivi, utakuwa umemfunza yeye kuepukana na tabia hiyo kwani akitambua kuwa wewe sio mtu wa kukubali kupokea ufitinishaji hatorudia tena kwako mara nyingine. Vile vile itakuwa ni kheri kwako kutokusikia tena ufitinishaji na utaepukana na kuwachukia marafiki na ndugu zako ambao una maelewano nao. Kwa ujumla utazuia ufisadi wa aina hii utendeke. Na lau kila mmoja atakuwa anafanya hivi basi bila shaka jamii nzima itaokoka na ufisadi huu wa kufitinisha.

 

Mwenye kufitinisha

 

1.      Ajishughulishe na kumdhukuru Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) kwa kila aina ya dhikr.

 

2.       Afikirie na akhofu adhabu za kufitinisha.

 

3.       Afikirie ubaya ulioje kuwafitinisha watu na kutia chuki katika nyoyo za watu, je, yeyemwenyewe atapendwa kufitinishwa na kipenzi chake?

 

4.       Asome mada zote za Ghiybah ziliomo humu Fisabillaah.com ili atambue hatari ya kutouhifadhi ulimi.

 

 

 

Mwisho wa mada ya An-Namiymah

 

Tunamuomba Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) Atuhifadhi na Atuepushe na maovu haya na kila aina ya movu mengine tubakie katika Ridhaa Yake. Aamiyn.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Hukumu ya kupeleka barua ya posa kwenye kitambaa cheupe

                      Hukumu ya kupeleka barua ya posa kwenye kitambaa cheupe  Hakika ni kuwa posa ilivyofanyika katika Uislamu kuanzia wakati wa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) inafahamika vilivyo. Posa inaweza kuja kutoka kwa mume na watu wake kwa jamaa za mke au mzazi wa mke kumtafutia binti yake mume. Ikiwa wazazi watakwenda kwa wazazi wa mke, baada ya kupeleka maneno, na wazazi wa mke watataka kupatiwa muda wa kufikiria, kufanya shuuraa, kuulizia, kutafiti na baadaye kukubali au kukataa. Ikiwa wamekubali baada ya kumshauri binti  yao  ni vyema mume mtarajiwa aende amuone atakaye kuwa mkewe ili apate kutulia na kuridhika kabla siku ya Nikaah. Binti huyo au wazazi wake wataweka kiwango cha mahari ambacho mume anatakiwa kutoa. Hii njia ya kuweka pesa kwenye kitambaa au bahasha haipo katika mafunzo ya Kiislam, na huenda ni njia ya kitamaduni fulani au itikadi f...

Maana ya Uadilifu

                                         MAANA  YA  UADILIFU  KATIKA  UISLAMU Assallaam  Aleykum  WarahmatulLaah  Wabarakatuh Alhamdu Lillaahi Rabil'aalamiyn) Allaahumma Swalli 'alaa Muhammad wa 'alaa aali Muhammad kamaa Swallayta 'alaa Ibraahiym wa 'alaa aali Ibraahiym wa Baarik 'alaa Muhammad wa 'alaa aali Muhammad kamaa Baarakta 'alaa Ibraahiym wa 'alaa aali Ibraahiym fil'aalamyna Innaka Hamiydun Majiyd. Ndugu zangu Waislam Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) Anasema katika Qur-aan. إِنَّ اللَّـهَ يَأْمُرُ بِالْعَدْلِ وَالْإِحْسَانِ وَإِيتَاءِ ذِي الْقُرْبَىٰ وَيَنْهَىٰ عَنِ الْفَحْشَاءِ وَالْمُنكَرِ وَالْبَغْيِ ۚيَعِظُكُمْ لَعَلَّكُمْ تَذَكَّرُونَ Hakika Allaah Anaamrishia uadilifu na ihsaan na kuwapa (mahitajio na msaada) jamaa wa karibu; na Anakataza machafu na munkari na ukandamizaji. Anakuwaidhini huenda mkapata kukumb...

Viungo vya Mwili vitashuhudia Matendo ya Mwanaadamu Siku ya Qiyaamah

Anasema Allaah  سبحانه وتعالى   ((الْيَوْمَ نَخْتِمُ عَلَى أَفْوَاهِهِمْ وَتُكَلِّمُنَا أَيْدِيهِمْ وَتَشْهَدُ أَرْجُلُهُمْ بِمَا كَانُوا يَكْسِبُونَ)) ((Leo Tunaviziba vinywa vyao, na iseme Nasi mikono  yao , na itoe ushahidi miguu  yao kwa waliyokuwa wakiyachuma))  [Yaasiyn :65 ] Siku ya Qiyaamah viungo vya miili vitakuwa ni vyenye kushuhudia matendo ya binaadamu aliyoyatenda hapa duniani: Mfano mikono itasema: "nimeiba".  Miguu itasema, "nimekwenda sehemu ya ma'asi". Macho yatasema, "nimetazama machafu".  Masikio yatasema, "nimesikiliza nyimbo, au umbea" na kadhalika. Na hivi ndivyo itakavyokuwa hali ya makafiri, wanafiki na wenye kumuasi Mola siku ya kufufuliwa,  watakapokanusha madhambi waliyoyatenda duniani na kuapa kwamba hawakuyafanya, Allaah  سبحانه وتعالى  Atawafunga midomo  yao na kuviamrisha viungo vizungumze:   عن أنس بن مالك قال: كنا عند النبي صلى ال...