Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Madhara Ya Ghiybah (Kusengenya) Na An-Namiymah (Kufitinisha)

Madhara Ya Ghiybah - Kuharamisihwa Kwake Na Na Adhabu Zake Katika Sunnah

 

Baada ya kujikumbusha makatazo na adhabu za Ghiybah katika Qur-aan, tukaona jinsi gani maovu haya yalivyokemewa na Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala), tunaendelea kutaja makatazo yake na adhabu zake katika Sunnah:
 

 عن أبي بكرة رضي الله عنه أن رسول الله صلى الله عليه وسلم قال في خطبته يوم النحر بمنى في حجة الوداع: (( إن دمائكم، واموالكم وأعراضكم حرام عليكم كحرمة يومكم هذا، في شهركم هذا، في بلدكم هذا، ألا بلغت )) متفقعليه
 

Kutoka kwa Abu Bakrah (Radhiya Allaahu 'anhu) amesimulia  kuwa Mtume (Swalla Allahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alisema katika khutba yake ya siku ya An-Nahr [siku ya kuchinja – yaani siku ya 'Iydul-Adhwhaa] huko Minaa katika Hajjatulwadaa' [Hijjah ya kuaga] ((Hakika damu zenu, mali zenu na heshima zenu ni haramu kwenu kama uharamu (wa kutenda dhambi) siku yenu hii katika mji wenu huu. Je nimefikisha?))[Al-Bukhaariy na Muslim]

Hadiyth hii inatuonyesha jinsi gani makatazo hayo yaliyotajwa, yakiwemo ya kuvunjiana heshima yalivyokuwa mazito kwamba ni sawa na kutenda dhambi mji mtukufu na siku tukufu hiyo ya Yawmun-Nahr (siku ya kuchinja). Bila ya shaka kila mmoja wetu atapima umuhimu huu wa kuhifadhi heshima za wenzetu kwa kutowasengenya na kutoa aibu zao kwa wengine.
 

Ikiwa hata mtu ana sifa ambayo unaitaja nyuma yake huwa in maana ni kumsengenya kama alivyosema Mtume (Swalla Allahu 'alayhi wa aalihi wa sallam), seuze iwe ni kumsengenya mtu kwa  aibu asiyokuwa nayo au kumtolea aibu zake, au kumzulia kwa mabaya asiyokuwa nayo?
 

عن عائشة رضي الله عنها قالت: قلت للنبي صلى الله عليه وسلم حسبك من صفيه كذا وكذا. وقال بعض الرواة: تعني قصيرة، فقال: (( لقد قلت كلمة لو مزجت بماء البحر لمزجته )) قالت: وحكيت له إنسانا  فقال: (( ما احب أني حكيت إنسانا وان لي كذا وكذا )) رواه أبو داود   والترمذي   وقال: حديث حسن صحيح.

 

Mama wa Waumini 'Aaishah (Radhiya Allaahu 'anha) amesimulia: "Nilimwambia Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): "Achana na Swafiyyah; yuko kadhaa na kadhaa"  yaani ni mfupi – Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akasema: ((Hakika umetamka neno ambalo lau lingalichanganywa na maji ya bahari yangelibadilika)) (kutokana na uvundo wa neno hilo). 'Aaishah alisema: "Siku moja nilimuigiza mtu mbele yake Mtume (Swalla Allahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akaniambia: ((Mimi sipendi kumuiga mtu na ilhali mimi nina kadhaa na kadhaa)) [Abu Daawuud na At-Tirmidhiy na amesema Hadiyth hii ni Hasan Sahiyh] 
 

Dini yetu ya Kiislam imesisitiza sanakutunziana heshima na kuhifadhiana mabaya yetu.

 

 عن عبد اللَّه بن عَمْرو بن الْعاص رضي اللَّهعنهما عن النَّبِيِّ صَلّى اللهُ عَلَيْهِ وسَلَّم قال :  ((الْمُسْلِمُ مَنْ سَلِمَ الْمُسْلِمُونَ مِنْ لِسانِهِ ويَدِهِ ، والْمُهَاجِرُ مَنْ هَجَرَ ما نَهَى اللَّه عَنْهُ)) متفق عليه

 

Kutoka kwa 'Abdullaahi bin 'Amru bin Al-'Aasw (Radhiya Allaahu 'anhuma) ambaye amesema: Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Muislam ni yule wanaosalimika Waislam kwa ulimi wake na mkono wake, na Muhaajir (mwenye kuhama) ni yule anayehama yale Aliyoyakataza Allaah )) [Al-Bukhaariy na Muslim]

 

Umuhimu wa kuhifadhi ulimi ili usimuingize mtu motoni:

 

عن معاذِ بن جبلٍ رضي الله عنه قال: قلت: يا رسول الله، أخْبِرني بِعَمَلٍ يُدْخِلُني الجنَةَ ويُبَاعِدُني عَنِ النارِ. قال: ((لَقَدْ سألْتَ عَنْ عَظيمٍ، وإنَهُ لَيَسيرٌ عَلى من يَسَّرَهُ اللهُ تعالى عَلَيْهِ : تَعْبُدُ اللهَ لا تُشْرِكُ بِهِ شَيئاً، وتُقيمُ الصَّلاةَ  ،وتُؤتي الزكاةَ، وتصومُ رمضانَ، وتَحُجُّ البيتَ))

 

.ثم قال: (( ألا أَدُلُّكَ على أبْوَابِ الخيرِ؟: الصَّومُ جُنَّةٌ، والصَّدقةُ تُطْفِىءُ الخَطِيئةَ كما يُطْفىءُ الماءُ النارَ، وصَلاةَ الرَّجُلِ في جَوْفِ الَّليْلِ، ثم تلا: ((تَتَجَافَى جُنُوبُهُمْ عَنْ الْمَضَاجِعِ)) - حتى بلغ – ((يَعْمَلُونَ))  السجدة: 16-17 .

ثم قال:  ((ألا أُخْبِرُكَ بِرَأسِ الأمْرِ وَعَمودِهِ وَذِرْوَةِ سَنَامِهِ؟)) قلتُ: بَلىَ يا رسول الله. قال:  (( رَأْسُ الأمْرِ الإسلامُ، وعَمُودُهُ الصَّلاةُ، وَذِرْوَةُ سَنَامِهِ الجِهادُ )).ثم قال: ((ألا أخْبِرُكَ بِمِلاكَ ذَلِكَ  كلِّهِ ؟)) فَقُلْتُ بَلَى يا رَسول الله، فأخَذَ بِلِسانِهِ وقال:  ((كُفَّ عَلَيْكَ هذا)) . قلت: يا نبيَّ الله، وإنَّا لمؤاخَذُونَ بِما نَتَكَلَّمُ بِه؟)) فقال: (( ثَكِلَتْكَ أمُّكَ يَا مُعَاذُ,  وَهَلْ يَكُبُّ الناسَ في النارِ على وُجُوهِهِمْ ))  أو قال: ((على مناخِرِهِم - إلاَّ حَصَائدُ  ألسِنَتهم)) رَوَاهُ التِّرْمِذِيُّ   وَقَالَ: حَدِيثٌ حَسَنٌ صَحِيحٌ. 

 

Kutoka kwa  Mu'aadh bin Jabal (Radhiya Allaahu 'anhu) amesema: Nilisema: Ewe Mjumbe wa Allaah! Niambie kitendo ambacho kitanipeleka peponi na kitaniokoa na moto. Akasema: ((Umeniuliza jambo kubwa lakini ni rahisi kwa yule ambaye Mola Amemsahilishia.  Muabudu Allaah wala usimshirikishe na chochote, Swali, toa Zakaah, funga Ramadhaan, nenda kuhiji (Makka). Kisha akasema: ((Je? Nikuonyeshe  milango ya kheriSwawm ni ngao, Sadaka inazima dhambi kama vile maji yanavyozima moto, na kuswali katikati ya usiku: Kisha akasoma  ((Mbavu zao zinaachana na vitanda….)) hadi ilipomalizikia Aayah ((…wanayoyatenda))[As-Sajdah 32 : 16 na 17]  

 

Tena akasema:  ((Je, nikwambie kilele chahilo jambo; nguzo yake na sehemu yake ya juu kabisa?)) Nikasema: Ndio ewe Mjumbe wa AllaahAkasema: ((Kilele chake ni Uislam, nguzo yake ni Swalah na sehemu yake ya juu kabisa ni Jihaad))  Kisha akasema: ((Je, nikwambie muhimili wa yote haya?)) NikasemaNdio ewe Mjumbe  wa Allaah. Akaukamata ulimi wake na akasema; ((Uzuie huu)) Nikasema: Ewe Mjumbe wa Allaahyale tunayoyasema tutahukumiwa  kwayo? Akasema:  ((Mama yako akuhurumie ewe Mu'aadhKuna kitu zaidi kinachowaangusha watu kifudifudi motoni kama si mavuno ya ndimi zao?))[Imesimuliwa na At-Tirmidhiy na ni Hadiyth Hasan]

 

Baadhi ya hizo adhabu za Akhera alikwishaziona Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alipokwenda Israa wal Mi'raaj na katuelezea katika Hadiyth ifuatayo:

 

عن أنس قال: قال رسول الله صلى الله عليه وسلم (( لما عرج بي مررت بقوم لهم أظفار من نحاس يخمشون وجوههم وصدورهم، فقلت: من هؤلاء يا جبريل؟)) قال: هؤلاء الذين يأكلون لحوم الناس ويقعون في أعراضهم"

 

Kutoka kwa Anas (Radhiya Allaahu ‘anhu) kwamba Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Nilipopandishwa mbinguni (Siku ya Israa na Mi’raaj) nilipita kwa watu ambao walikuwa wana kucha za shaba nyeupe wakijichana nyuso zao na vifua vyao. Nikauliza: Nani hawa ewe Jibriyl? Akasema: Hawa ni watu ambao wamekula nyama za binaadamu na kuwavunjia heshima zao)) [Abu Daawud]

Inaendelea

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Hukumu ya kupeleka barua ya posa kwenye kitambaa cheupe

                      Hukumu ya kupeleka barua ya posa kwenye kitambaa cheupe  Hakika ni kuwa posa ilivyofanyika katika Uislamu kuanzia wakati wa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) inafahamika vilivyo. Posa inaweza kuja kutoka kwa mume na watu wake kwa jamaa za mke au mzazi wa mke kumtafutia binti yake mume. Ikiwa wazazi watakwenda kwa wazazi wa mke, baada ya kupeleka maneno, na wazazi wa mke watataka kupatiwa muda wa kufikiria, kufanya shuuraa, kuulizia, kutafiti na baadaye kukubali au kukataa. Ikiwa wamekubali baada ya kumshauri binti  yao  ni vyema mume mtarajiwa aende amuone atakaye kuwa mkewe ili apate kutulia na kuridhika kabla siku ya Nikaah. Binti huyo au wazazi wake wataweka kiwango cha mahari ambacho mume anatakiwa kutoa. Hii njia ya kuweka pesa kwenye kitambaa au bahasha haipo katika mafunzo ya Kiislam, na huenda ni njia ya kitamaduni fulani au itikadi f...

Maana ya Uadilifu

                                         MAANA  YA  UADILIFU  KATIKA  UISLAMU Assallaam  Aleykum  WarahmatulLaah  Wabarakatuh Alhamdu Lillaahi Rabil'aalamiyn) Allaahumma Swalli 'alaa Muhammad wa 'alaa aali Muhammad kamaa Swallayta 'alaa Ibraahiym wa 'alaa aali Ibraahiym wa Baarik 'alaa Muhammad wa 'alaa aali Muhammad kamaa Baarakta 'alaa Ibraahiym wa 'alaa aali Ibraahiym fil'aalamyna Innaka Hamiydun Majiyd. Ndugu zangu Waislam Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) Anasema katika Qur-aan. إِنَّ اللَّـهَ يَأْمُرُ بِالْعَدْلِ وَالْإِحْسَانِ وَإِيتَاءِ ذِي الْقُرْبَىٰ وَيَنْهَىٰ عَنِ الْفَحْشَاءِ وَالْمُنكَرِ وَالْبَغْيِ ۚيَعِظُكُمْ لَعَلَّكُمْ تَذَكَّرُونَ Hakika Allaah Anaamrishia uadilifu na ihsaan na kuwapa (mahitajio na msaada) jamaa wa karibu; na Anakataza machafu na munkari na ukandamizaji. Anakuwaidhini huenda mkapata kukumb...

Viungo vya Mwili vitashuhudia Matendo ya Mwanaadamu Siku ya Qiyaamah

Anasema Allaah  سبحانه وتعالى   ((الْيَوْمَ نَخْتِمُ عَلَى أَفْوَاهِهِمْ وَتُكَلِّمُنَا أَيْدِيهِمْ وَتَشْهَدُ أَرْجُلُهُمْ بِمَا كَانُوا يَكْسِبُونَ)) ((Leo Tunaviziba vinywa vyao, na iseme Nasi mikono  yao , na itoe ushahidi miguu  yao kwa waliyokuwa wakiyachuma))  [Yaasiyn :65 ] Siku ya Qiyaamah viungo vya miili vitakuwa ni vyenye kushuhudia matendo ya binaadamu aliyoyatenda hapa duniani: Mfano mikono itasema: "nimeiba".  Miguu itasema, "nimekwenda sehemu ya ma'asi". Macho yatasema, "nimetazama machafu".  Masikio yatasema, "nimesikiliza nyimbo, au umbea" na kadhalika. Na hivi ndivyo itakavyokuwa hali ya makafiri, wanafiki na wenye kumuasi Mola siku ya kufufuliwa,  watakapokanusha madhambi waliyoyatenda duniani na kuapa kwamba hawakuyafanya, Allaah  سبحانه وتعالى  Atawafunga midomo  yao na kuviamrisha viungo vizungumze:   عن أنس بن مالك قال: كنا عند النبي صلى ال...