Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Madhara Ya Ghiybah (Kusengenya) Na An-Namiymah (Kufitinisha) -Sehemu ya 10

Madhara Ya An-Namiymah (Kufitinisha) - Maana, Hukumu Na Adhabu Zake

 

 

Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala):

 

 

((وَلاَ تُطِعْ كُلَّ حَلاَّفٍ مَّهِينٍ)) ((هَمَّازٍ مَّشَّاء بِنَمِيمٍ))  ((مَنَّاعٍ لِّلْخَيْرِ مُعْتَدٍ أَثِيمٍ))  

 

((Wala usimtii kila mwingi wa kuapa wa kudharauliwa)) ((Mtapitapi, apitaye akifitini)) ((Mwenye kuzuia kheri, dhaalimu, mwingi wa madhambi)) [Al-Qalam: 10-12]

 

 

 

 

Maana ya An-Namiymah

 

Ni kufitinisha, kwa maana kuchongeza kwa kuhamisha au kupeleka maneno baina ya watu ili kusababisha wachukiane.

 

Mfano kumwambia mwenzio: "Fulani kasema kuhusu wewe kadhaa na kadhaa". Au, "Fulani anakuchukia wala hakupendi". Kufitini huku kunaweza kuwa ni kwa kutamka maneno, au kwa kuandika au hata kwa kuonyesha ishara. Kufitinisha kwa kumsingizia mtu au hata kama huyo mtu alisema kweli  usemi huo haijuzi kufitinisha.

 

Mtu kama huyu mwenye kufitinisha ni mwenye nyuso mbili anamkabili kila mmoja kwa uso mzuri kumbe hampendelei kheri, ni kama kinyonga anayebadilika rangi kwa hali anayojipendelea nafsi yake. Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) ametuonya watu kama hawa kwa kusema:

 

 عن أبي هريرة ((إن شر الناس ذو الوجهين الذي يأتي هؤلاء بوجه وهؤلاء بوجه))  البخاري  

Kutoka kwa Abu Hurayrah: ((Hakika watu waovu kabisa ni wenye nyuso mbili ambao wanawaendea kundi la watu kwa uso mmoja na kundi la watu wengine kwa uso mwingine)) [Al-Bukhaariy]

 

 

Mtu huyu ni tofauti na Muislamu mkweli mwenye uso mmoja katika hali zote baina ya ndugu zake au rafiki zake, naye ana ulimi mmoja wa ukweli, hasemi ila yanaomridhisha Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala):

 

 

Hukmu ya An-Namiymah

 

Ni haraam kama ilivyobainishwa katika Qur-aan na Sunnah na miongoni mwa madhambi makubwa.

 

Athari ya An-Namiymah

 

Mtafaruku baina ya watu, kuondosha furaha katika nyoyo na badala yake maudhi, kujenga uadui, kuchukiana, kukatiana au kuzuiliana rizki, na huenda ikasabisha hata kuuana.

 

 عن ابن مسعود رضي الله عنه أن النبي "صلى الله عليه وسلم "قال  : ((ألا أنبئكم ما العضه؟ هي النميمة القالة بين الناس))  رواه مسلم

 

Kutoka kwa Ibn Mas'uud (Radhiya Allaahu 'anhu) ambaye amesimulia kwamba: Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Je, nikujulisheni nini Al-'Adhwhu? Ni kuchongeza baina ya watu)) [Muslim]

 

Adhabu zake

 

Kuharamishwa Pepo:

 

 

 عن حذيفة رضي الله عنه قال: قال رسول الله صلى الله عليه وسلم: ((لا يَدْخُلُ الجَنَّةَ نَمَّامٌ)) رواه البخاري ومسلم

 

Kutoka kwa Hudhayfah (Radhiya Allaahu 'anhu) ambaye amesema: Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Mchongezi hataingia Peponi))[Al-Bukhaariy na Muslim]

 

 

 

Adhabu Kaburini

 

  عن ابن عباس رضي الله عنهما أن رسول الله صلى الله عليه وسلم مر بقبرين فقال ((إنهما يعذبان, وما يعذبان في كبير,  بلى إنه كبير: أما أحدهما كان يمشي بالنميمة و أما ألأخر فكان لا يستتر من بوله)) متفق عليه

 

Kutoka kwa Ibn 'Abbaas  (Radhiya Allaahu 'anhuma) ambaye amesimulia kwamba: Mtume (Swalla Allahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) aliyapitia makaburi mawili na akasema: ((Hakika hawa wanaadhibiwa. Wala hawaadhibiwi kwa sababu ya jambo kubwa. Ndio ni  jambo kubwa! Mmoja wao alikuwa akipita kuchongeza na mwingine alikuwa hajikingi na mkojo [anapokojoa]))[Al-Bukhaariy na Muslim]

Inaendelea

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Hukumu ya kupeleka barua ya posa kwenye kitambaa cheupe

                      Hukumu ya kupeleka barua ya posa kwenye kitambaa cheupe  Hakika ni kuwa posa ilivyofanyika katika Uislamu kuanzia wakati wa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) inafahamika vilivyo. Posa inaweza kuja kutoka kwa mume na watu wake kwa jamaa za mke au mzazi wa mke kumtafutia binti yake mume. Ikiwa wazazi watakwenda kwa wazazi wa mke, baada ya kupeleka maneno, na wazazi wa mke watataka kupatiwa muda wa kufikiria, kufanya shuuraa, kuulizia, kutafiti na baadaye kukubali au kukataa. Ikiwa wamekubali baada ya kumshauri binti  yao  ni vyema mume mtarajiwa aende amuone atakaye kuwa mkewe ili apate kutulia na kuridhika kabla siku ya Nikaah. Binti huyo au wazazi wake wataweka kiwango cha mahari ambacho mume anatakiwa kutoa. Hii njia ya kuweka pesa kwenye kitambaa au bahasha haipo katika mafunzo ya Kiislam, na huenda ni njia ya kitamaduni fulani au itikadi f...

Maana ya Uadilifu

                                         MAANA  YA  UADILIFU  KATIKA  UISLAMU Assallaam  Aleykum  WarahmatulLaah  Wabarakatuh Alhamdu Lillaahi Rabil'aalamiyn) Allaahumma Swalli 'alaa Muhammad wa 'alaa aali Muhammad kamaa Swallayta 'alaa Ibraahiym wa 'alaa aali Ibraahiym wa Baarik 'alaa Muhammad wa 'alaa aali Muhammad kamaa Baarakta 'alaa Ibraahiym wa 'alaa aali Ibraahiym fil'aalamyna Innaka Hamiydun Majiyd. Ndugu zangu Waislam Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) Anasema katika Qur-aan. إِنَّ اللَّـهَ يَأْمُرُ بِالْعَدْلِ وَالْإِحْسَانِ وَإِيتَاءِ ذِي الْقُرْبَىٰ وَيَنْهَىٰ عَنِ الْفَحْشَاءِ وَالْمُنكَرِ وَالْبَغْيِ ۚيَعِظُكُمْ لَعَلَّكُمْ تَذَكَّرُونَ Hakika Allaah Anaamrishia uadilifu na ihsaan na kuwapa (mahitajio na msaada) jamaa wa karibu; na Anakataza machafu na munkari na ukandamizaji. Anakuwaidhini huenda mkapata kukumb...

Viungo vya Mwili vitashuhudia Matendo ya Mwanaadamu Siku ya Qiyaamah

Anasema Allaah  سبحانه وتعالى   ((الْيَوْمَ نَخْتِمُ عَلَى أَفْوَاهِهِمْ وَتُكَلِّمُنَا أَيْدِيهِمْ وَتَشْهَدُ أَرْجُلُهُمْ بِمَا كَانُوا يَكْسِبُونَ)) ((Leo Tunaviziba vinywa vyao, na iseme Nasi mikono  yao , na itoe ushahidi miguu  yao kwa waliyokuwa wakiyachuma))  [Yaasiyn :65 ] Siku ya Qiyaamah viungo vya miili vitakuwa ni vyenye kushuhudia matendo ya binaadamu aliyoyatenda hapa duniani: Mfano mikono itasema: "nimeiba".  Miguu itasema, "nimekwenda sehemu ya ma'asi". Macho yatasema, "nimetazama machafu".  Masikio yatasema, "nimesikiliza nyimbo, au umbea" na kadhalika. Na hivi ndivyo itakavyokuwa hali ya makafiri, wanafiki na wenye kumuasi Mola siku ya kufufuliwa,  watakapokanusha madhambi waliyoyatenda duniani na kuapa kwamba hawakuyafanya, Allaah  سبحانه وتعالى  Atawafunga midomo  yao na kuviamrisha viungo vizungumze:   عن أنس بن مالك قال: كنا عند النبي صلى ال...