Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Kipi kikudanganyacho ukamuasi Mola wako


 

Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala)  

((يَا أَيُّهَا الْإِنسَانُ مَا غَرَّكَ بِرَبِّكَ الْكَرِيمِ))

"Ee mwana Aadam! Nini kilichokughuri kuhusu Rabb wako Mkarimu?" [Al-Infitwaar: 6]

Utukufu gani wa Mwenye maneno haya yenye kushtua nyoyo na kusisimua mwili?Siku utakayoitwa "Ee Mwanaadamu maskini uliye dhaifu, kitu gani kikudanganyacho?"Nini kilichokughilibu hata ukamu'asi Allaah Mmoja (Pekee) Mwenye nguvu? (za mwisho)Nini kilichokudanganya hata ukavuka mipaka ya Mola wako?Nini kilichokudanganya hata ukapuuza Swalaah?Nini kilichokudanganya hata ukatenda maovu usiku na mchana?Nini kilichokudanganya hata ukapeleka macho yako kutazama yalio haramu?Nini kilichokudanganya hata ukawa humuogopi Mola wako kama unavyowaogopa viumbe vyengine?Nini kilichokudanganya hata ukawa huna khofu ya kukutana na Mola wako na kuhesabiwa?Je, ni dunia? Na Je? Hujui kama dunia ni nyumba ya kupita tu?Au ni shahawaat (matamanio)?  Hujui kama nayo ni ya kuondoka?Au ni Shaytwaan aliyekuhadaa? Kwani hujui kama yeye kwako ni adui mkubwa?Basi ni kipi kilichokudanganya? Jibu! Jibu! Ndugu Muislamu, leo kabla ya kesho kufika! Kwani hujijui kama utafika kesho kama alivyosema Mshairi: 

 

تزود من التقوى فإنك لا تدري  

Zidisha taqwa  kwani hujui

 

إذا جن عليك ليل هل تعيش إلى الفجر

Usiku utakapokufunika, je, utaishi hadi Alfajiri?

 

 

فكم من صحيح مات بغير علة                  

Kwani wangapi waliokuwa na siha zao wamekufa bila ya maradhi

 

وكم من سقيم عاش حينا من الدهري

Na wangapi walio wagonjwa wameishi miaka?

 

 

وكم من صغار يرتجى طولة عمرهم 

Na Wangapi miongoni mwa wadogo wametumainiwa maisha marefu

 

وقد دخلت أجسادهم ظلمة القبر

Na miili yao imekwishaingia katika kiza cha kaburi

 

فكم من فتى يمسي ويصبح ضاحكا

Na vijana wangapi wameamka huku wanacheka

وقد نسجت أكفانه وهو لايدري

Kumbe huku sanda yao inashonwa/inaandaliwa naye hajui

 

 

وكم من عروس زينوها لزوجها

Na bi harusi wangapi  amepambwa kwa ajili ya mume wake

وقد قبضت أرواحهم ليلة القدر

Na roho zao zimechukuliwa usiku wa Laylatul-Qadri?

 

وكم من ساكن عند الصباح بقصره

Na wangapi asubuhi walikuwa katika maqasri yao wakikaa

 

وعند المساء قد كان من ساكن القبر

Na jioni yakawa makazi yao ni kaburi?

 

فكن مخلصا وأعمل الخير دائما

Kuwa mwenye ikhlaas na utende mema daima

لعلك تحظى بالمثوبة والأجر

Huenda ukawafikishwa kupata thawabu na jazaa

 

 

وداوم على تقوى الإله فإنها أمان 

Na dumisha Taqwa ya Mola Wa Pekee kwani ni hifadhi

 

من الأهوال في موقف الحشر

Itakayokulinda na hali katika siku ya kukufuliwa

 

 

لا إله إلا الله ...

Laa Ilaah Illa Allaah

 

Ee ndugu Muislamu imekuingia khofu ya kurudi kwa Mola wako na kuacha kuendelea kudanganyika?

 

Kumbuka madhambi yako na amka usiku ujikaribishe kwa Mola Mtukufu Mwenye kusamehe madhambi na Mwenye Rahmah na urudie hii Aayah mara kwa mara ili ingie katika moyo wako.  

((يَا أَيُّهَا الْإِنسَانُ مَا غَرَّكَ بِرَبِّكَ الْكَرِيمِ))

"Ee mwana Aadam! Nini kilichokughuri kuhusu Rabb wako Mkarimu?" [Al-Infitwaar: 6]

 

Ndugu Muislamu, tafakari matukio yaliyotajwa katika hii Surah Tukufu yatakayotokea siku ambayo hutoweza kujisaidia wala kusaidiwa!

 

 

بِسْمِ اللَّـهِ الرَّحْمَـٰنِ الرَّحِيمِ

 

 

إِذَا السَّمَاءُ انفَطَرَتْ ﴿١﴾

1. Mbingu zitakapopasuka.

 

وَإِذَا الْكَوَاكِبُ انتَثَرَتْ ﴿٢﴾

2. Na sayari zitakapoanguka na kutawanyika.

 

وَإِذَا الْبِحَارُ فُجِّرَتْ ﴿٣﴾

3. Na bahari zitakapolipuka.

 

وَإِذَا الْقُبُورُ بُعْثِرَتْ ﴿٤﴾

4. Na makaburi yatakapopinduliwa chini juu na kufichuliwa.

 

عَلِمَتْ نَفْسٌ مَّا قَدَّمَتْ وَأَخَّرَتْ﴿٥﴾

5. Nafsi itajua yale iliyoyakadimisha na iliyoyaakhirisha.

 

يَا أَيُّهَا الْإِنسَانُ مَا غَرَّكَ بِرَبِّكَ الْكَرِيمِ ﴿٦﴾

6. Ee mwana Aadam! Nini kilichokughuri kuhusu Rabb wako Mkarimu?

 

الَّذِي خَلَقَكَ فَسَوَّاكَ فَعَدَلَكَ ﴿٧﴾

7. Ambaye Amekuumba Akakusawazisha (umbo sura, viungo) na Akakupima na kukulinganisha sawa.

 

فِي أَيِّ صُورَةٍ مَّا شَاءَ رَكَّبَكَ﴿٨﴾

8. Katika sura Aliyotaka Akakutengeneza.

[Al-Infitwaar: 1-8]

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Hukumu ya kupeleka barua ya posa kwenye kitambaa cheupe

                      Hukumu ya kupeleka barua ya posa kwenye kitambaa cheupe  Hakika ni kuwa posa ilivyofanyika katika Uislamu kuanzia wakati wa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) inafahamika vilivyo. Posa inaweza kuja kutoka kwa mume na watu wake kwa jamaa za mke au mzazi wa mke kumtafutia binti yake mume. Ikiwa wazazi watakwenda kwa wazazi wa mke, baada ya kupeleka maneno, na wazazi wa mke watataka kupatiwa muda wa kufikiria, kufanya shuuraa, kuulizia, kutafiti na baadaye kukubali au kukataa. Ikiwa wamekubali baada ya kumshauri binti  yao  ni vyema mume mtarajiwa aende amuone atakaye kuwa mkewe ili apate kutulia na kuridhika kabla siku ya Nikaah. Binti huyo au wazazi wake wataweka kiwango cha mahari ambacho mume anatakiwa kutoa. Hii njia ya kuweka pesa kwenye kitambaa au bahasha haipo katika mafunzo ya Kiislam, na huenda ni njia ya kitamaduni fulani au itikadi f...

Maana ya Uadilifu

                                         MAANA  YA  UADILIFU  KATIKA  UISLAMU Assallaam  Aleykum  WarahmatulLaah  Wabarakatuh Alhamdu Lillaahi Rabil'aalamiyn) Allaahumma Swalli 'alaa Muhammad wa 'alaa aali Muhammad kamaa Swallayta 'alaa Ibraahiym wa 'alaa aali Ibraahiym wa Baarik 'alaa Muhammad wa 'alaa aali Muhammad kamaa Baarakta 'alaa Ibraahiym wa 'alaa aali Ibraahiym fil'aalamyna Innaka Hamiydun Majiyd. Ndugu zangu Waislam Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) Anasema katika Qur-aan. إِنَّ اللَّـهَ يَأْمُرُ بِالْعَدْلِ وَالْإِحْسَانِ وَإِيتَاءِ ذِي الْقُرْبَىٰ وَيَنْهَىٰ عَنِ الْفَحْشَاءِ وَالْمُنكَرِ وَالْبَغْيِ ۚيَعِظُكُمْ لَعَلَّكُمْ تَذَكَّرُونَ Hakika Allaah Anaamrishia uadilifu na ihsaan na kuwapa (mahitajio na msaada) jamaa wa karibu; na Anakataza machafu na munkari na ukandamizaji. Anakuwaidhini huenda mkapata kukumb...

Viungo vya Mwili vitashuhudia Matendo ya Mwanaadamu Siku ya Qiyaamah

Anasema Allaah  سبحانه وتعالى   ((الْيَوْمَ نَخْتِمُ عَلَى أَفْوَاهِهِمْ وَتُكَلِّمُنَا أَيْدِيهِمْ وَتَشْهَدُ أَرْجُلُهُمْ بِمَا كَانُوا يَكْسِبُونَ)) ((Leo Tunaviziba vinywa vyao, na iseme Nasi mikono  yao , na itoe ushahidi miguu  yao kwa waliyokuwa wakiyachuma))  [Yaasiyn :65 ] Siku ya Qiyaamah viungo vya miili vitakuwa ni vyenye kushuhudia matendo ya binaadamu aliyoyatenda hapa duniani: Mfano mikono itasema: "nimeiba".  Miguu itasema, "nimekwenda sehemu ya ma'asi". Macho yatasema, "nimetazama machafu".  Masikio yatasema, "nimesikiliza nyimbo, au umbea" na kadhalika. Na hivi ndivyo itakavyokuwa hali ya makafiri, wanafiki na wenye kumuasi Mola siku ya kufufuliwa,  watakapokanusha madhambi waliyoyatenda duniani na kuapa kwamba hawakuyafanya, Allaah  سبحانه وتعالى  Atawafunga midomo  yao na kuviamrisha viungo vizungumze:   عن أنس بن مالك قال: كنا عند النبي صلى ال...