Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Mawlid Kufanywa Wakati Msichana Anavunja Ungo Na Kusherehekea Jambo Hilo Na Mafunzo Kwa Biharusi


SWALI

 

Asalaam Aeikum Ndugu zangu katika Uislam

Kwanza napenda kuchukua nafasi hii, kumshukuru Mwenyezi Mungu Subhaana waala Taala, kwa kunijaalia uzima na afya njema na uwezo wa kuweza kufahamu mtandao huu wa Alhidaaya. Katika siku ya leo napenda kuuliza maswali yafautayo ambayo yamekuwa yakinitatiza kichwani mwangu.

 

Kuna tabia katika baaaadhi ya jamii hapa kufanya sherehe, pengine husoma hata maulidi kwa mabinti zao baaada ya kuvunja ungo (kubalehe) Katika sherehe hizo pamoja na mambo mengine binti hufundishwa jinsi ya kuishi na mume pindi anapoolewa. Je mafunzo haya ni sahihi katika uislamu. Na kama si sahihi ni vipi binti wa kiislamu akikuwa hufunzwa

 

JIBU

 

AlhamduliLLaah Himidi Anastahiki Allaah (Subhaanahu wa Ta’aala) Rabb wa walimwengu, Swalaah na salamu zimshukie Nabiy Muhammad (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na Swahaba zake (Radhwiya Allaahu 'anhum) na waliowafuata kwa wema mpaka Siku ya Mwisho.

 

 

Hakuna katika shariY’ah ya Kiislamu sherehe yoyote inayofanywa baada ya msichana kubaleghe. Inatakiwa watoto, wasichana na wavulana waanze kufundishwa na wazazi wao kuanzia wanapofika miaka saba namna ya kufanya ‘Ibaadah kama Swaalah na kufunga. Hilo ni agizo la Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) pale aliposema:

“Waamrisheni watoto wenu kuswali wakiwa na miaka saba na watenganisheni katika malazi wakiwa na miaka kumi …” [Abuu Daawuwd].

 

Uislamu unatutaka sisi tuanze mapema kuwafundisha wasichana mambo mengi zaidi kwani wao wana tofauti kubwa na wenziwao wavulana kama kujisitiri, kujihifadhi kwa kuvaa hifadha wanapoanza kutoka damu ya hedhi na kujihifadhi.

 

Hakuna sherehe mbali na mafunzo kwa wasichana. Kisha kuna mafunzo ya kukaa na mume watakapoolewa kwa njia nzuri ya Kiislamu. Mambo hayo wanaweza kuyapata katika Madrasah kwani Uislamu unatuongoza katika kila jambo. Vilevile wanaweza kupata mafunzo hayo katika vitabu vya Kiislamu vinavyoeleza suala hilo. Na bila shaka wa kufundisha hayo kwa njia nzuri na muafaka zaidi ni mama mzazi au mlezi ili binti ainukie katika malezi ya Kiislamu na kuishi vizuri na mume wake Kiislamu pindi anapoolewa.  

Na Allaah anajua zaidi

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Hukumu ya kupeleka barua ya posa kwenye kitambaa cheupe

                      Hukumu ya kupeleka barua ya posa kwenye kitambaa cheupe  Hakika ni kuwa posa ilivyofanyika katika Uislamu kuanzia wakati wa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) inafahamika vilivyo. Posa inaweza kuja kutoka kwa mume na watu wake kwa jamaa za mke au mzazi wa mke kumtafutia binti yake mume. Ikiwa wazazi watakwenda kwa wazazi wa mke, baada ya kupeleka maneno, na wazazi wa mke watataka kupatiwa muda wa kufikiria, kufanya shuuraa, kuulizia, kutafiti na baadaye kukubali au kukataa. Ikiwa wamekubali baada ya kumshauri binti  yao  ni vyema mume mtarajiwa aende amuone atakaye kuwa mkewe ili apate kutulia na kuridhika kabla siku ya Nikaah. Binti huyo au wazazi wake wataweka kiwango cha mahari ambacho mume anatakiwa kutoa. Hii njia ya kuweka pesa kwenye kitambaa au bahasha haipo katika mafunzo ya Kiislam, na huenda ni njia ya kitamaduni fulani au itikadi f...

Maana ya Uadilifu

                                         MAANA  YA  UADILIFU  KATIKA  UISLAMU Assallaam  Aleykum  WarahmatulLaah  Wabarakatuh Alhamdu Lillaahi Rabil'aalamiyn) Allaahumma Swalli 'alaa Muhammad wa 'alaa aali Muhammad kamaa Swallayta 'alaa Ibraahiym wa 'alaa aali Ibraahiym wa Baarik 'alaa Muhammad wa 'alaa aali Muhammad kamaa Baarakta 'alaa Ibraahiym wa 'alaa aali Ibraahiym fil'aalamyna Innaka Hamiydun Majiyd. Ndugu zangu Waislam Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) Anasema katika Qur-aan. إِنَّ اللَّـهَ يَأْمُرُ بِالْعَدْلِ وَالْإِحْسَانِ وَإِيتَاءِ ذِي الْقُرْبَىٰ وَيَنْهَىٰ عَنِ الْفَحْشَاءِ وَالْمُنكَرِ وَالْبَغْيِ ۚيَعِظُكُمْ لَعَلَّكُمْ تَذَكَّرُونَ Hakika Allaah Anaamrishia uadilifu na ihsaan na kuwapa (mahitajio na msaada) jamaa wa karibu; na Anakataza machafu na munkari na ukandamizaji. Anakuwaidhini huenda mkapata kukumb...

Viungo vya Mwili vitashuhudia Matendo ya Mwanaadamu Siku ya Qiyaamah

Anasema Allaah  سبحانه وتعالى   ((الْيَوْمَ نَخْتِمُ عَلَى أَفْوَاهِهِمْ وَتُكَلِّمُنَا أَيْدِيهِمْ وَتَشْهَدُ أَرْجُلُهُمْ بِمَا كَانُوا يَكْسِبُونَ)) ((Leo Tunaviziba vinywa vyao, na iseme Nasi mikono  yao , na itoe ushahidi miguu  yao kwa waliyokuwa wakiyachuma))  [Yaasiyn :65 ] Siku ya Qiyaamah viungo vya miili vitakuwa ni vyenye kushuhudia matendo ya binaadamu aliyoyatenda hapa duniani: Mfano mikono itasema: "nimeiba".  Miguu itasema, "nimekwenda sehemu ya ma'asi". Macho yatasema, "nimetazama machafu".  Masikio yatasema, "nimesikiliza nyimbo, au umbea" na kadhalika. Na hivi ndivyo itakavyokuwa hali ya makafiri, wanafiki na wenye kumuasi Mola siku ya kufufuliwa,  watakapokanusha madhambi waliyoyatenda duniani na kuapa kwamba hawakuyafanya, Allaah  سبحانه وتعالى  Atawafunga midomo  yao na kuviamrisha viungo vizungumze:   عن أنس بن مالك قال: كنا عند النبي صلى ال...