Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Fadhila za Kutoa

Assallaam Aleykum WarahmatulLaah Wabarakatuh

125- Asmaa´ bint Abiy Bakr (Radhiya Allaahu ´anhaa) amesema:


“Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) alisema kunambia: “Toa au chinja. Usihesabu Allaah akaanza kuhesabu Anavyokupa na usizuie Allaah akaanza kuzuia kutoka kwako.”[1]

126- Jaabir (Radhiya Allaahu ´anh) amesema:

“Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) hakupatapo kuombwa kitu kamwe akasema: “Hapana”.[2]

127- Abu Sa´iyd al-Khudriy (Radhiya Allaahu ´anh) amesema:

“Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema: “Ambaye yuko na kipando cha ziada basi ampe ambaye hana kipando na ambaye yuko na chakula cha ziada ampe ambaye hana chakula.” Alifanya tukaona kuwa hakuna yeyote katika sisi ambaye yuko na haki zaidi ya kile chenye kutosheleza.”[3]

128- Anas (Radhiya Allaahu ´anh) amesema:

“Kuna mbedui alikuja kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akamuomba kitu ambapo Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akaamrisha apewe kondoo 40.000. Mtu yule akarejea kwa watu wake na kuwaambia: “Enyi watu wangu! Ingieni katika Uislamu! Muhammad akatoa kiasi cha kwamba mtu hakhofii ufakiri tena kamwe.”[4]

129- Ibn ´Umar (Radhiya Allaahu ´anh) amesema:

“Sijawahi kuona mtu baada ya Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) ambaye ni mkarimu sana kama Mu´aawiyah.”

130- ´Urwah amesema:

“Mu´aawiyah alituma 100.000 kwa ´Aaishah. ´Aaishah hawakuwahi kusimama isipokuwa alizigawa zote. Mfanya kazi wake akaingia na kusema: “Ungeliweka dirhamu mia moja tukapata kununua nyama.” Akamwambia: “Ungenikumbusha tokea mwanzo.”

131- Mu´aawiyah alipokuwa akikutana na al-Hasan alikuwa anamwambia: “Karibu, ee mtoto wa Mtume wa Allaah” na anaamrisha apewe dirhamu 300.000. Na pindi anapokutana na Ibn-uz-Zubayr alikuwa akimwambia: “Karibu, ee binamu yake na Mtume wa Allaah” na anaamrisha apewe 100.000.

132- Hammaad bin Abiy Sulaymaan alikuwa kila siku katika Ramadhaan akifungua swawm na watu khamsini. Siku ya ´Iyd anawanunulia nguo na kila mmoja anampa 100.

133- Kuna mwanamke alikuja kwa Hassan bin Abiy Sinaan kuomba. Akamtazama na kusema: “Ee kijana! Mpe dirhamu 400.” Kukasemwa: “Ee Abu ´Abdillaah! Hivi kweli unampa dirhamu 400 mwombaji?” Akasema: “Nilivyoona alivomzuri ninachelea wanaume wengine wasije kufitinishwa naye. Ndio maana nikamtajirisha. Huenda akawepo mwanaume ambaye atapendelea kumuoa.”

134- Kuna mtu alimuomba Sa´iyd bin al-´Aasw ambapo akasema: “Ee kijana! Mpe dirhamu 500.” Mtu yule akaanza kulia. Akamuuliza: “Ni kipi kinachokuliza?” Akasema: “Ni kwa sababu ardhi huwala watu kama nyinyi.”

135- Twa´mah al-Ja´fariy amesema:

“´Imraan bin Muusa alikuwa akinitumia dinari 1000 na 2000 na akisema: “Zigawa kwa ndugu zako na usiwaambie kuwa zimetoka kwangu.”

136- Inasemekana kuwa pindi Qays bin ´Ubaadah alipopatwa na maradhi watu wachache watu ndio walimtembelea. Alipouliza sababu akaambiwa: “Wanakuonea haya kwa sababu unawadai pesa.” Akasema: “Hakuna kheri yoyote kwa pesa ambayo inanizuia mimi na ndugu zangu. Waambie kuwa madeni yote yemfutika.” Jioni kizingiti kikavunjika kwa sababu ya watu wengi waliokuja kumtembelea.

137- Bakr bin ´Abdillaah amesema:

“Ninapenda zaidi pesa ambayo inanifungamanisha na ndugu zangu. Na ninachukia zaidi pesa ambayo inaniacha nyuma.”

138- ´Aliy bin Abiy Twaalib (Radhiya Allaahu ´anh) amesema:

“Muislamu bora ni yule mwenye kuunga [uhusiano], akasaidia na akanufaisha.”

139- ash-Sha´biy amesema:

“Ninampenda zaidi mtu ambaye anamuhurumia masikini, anamsaidia muhitajia, anamwangalia yatima na kumchanya msafiri kuliko mwenye kufanya ´ibaadah katika Ka´bah kwa miaka arobaini. Watu bora ni wale wenye wenye manufaa.”

[1] al-Bukhaariy (1433) na Muslim (1029).

[2] Muslim (4/1805).

[3] Muslim (12/33).

[4] Muslim (15/72)

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Hukumu ya kupeleka barua ya posa kwenye kitambaa cheupe

                      Hukumu ya kupeleka barua ya posa kwenye kitambaa cheupe  Hakika ni kuwa posa ilivyofanyika katika Uislamu kuanzia wakati wa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) inafahamika vilivyo. Posa inaweza kuja kutoka kwa mume na watu wake kwa jamaa za mke au mzazi wa mke kumtafutia binti yake mume. Ikiwa wazazi watakwenda kwa wazazi wa mke, baada ya kupeleka maneno, na wazazi wa mke watataka kupatiwa muda wa kufikiria, kufanya shuuraa, kuulizia, kutafiti na baadaye kukubali au kukataa. Ikiwa wamekubali baada ya kumshauri binti  yao  ni vyema mume mtarajiwa aende amuone atakaye kuwa mkewe ili apate kutulia na kuridhika kabla siku ya Nikaah. Binti huyo au wazazi wake wataweka kiwango cha mahari ambacho mume anatakiwa kutoa. Hii njia ya kuweka pesa kwenye kitambaa au bahasha haipo katika mafunzo ya Kiislam, na huenda ni njia ya kitamaduni fulani au itikadi f...

Maana ya Uadilifu

                                         MAANA  YA  UADILIFU  KATIKA  UISLAMU Assallaam  Aleykum  WarahmatulLaah  Wabarakatuh Alhamdu Lillaahi Rabil'aalamiyn) Allaahumma Swalli 'alaa Muhammad wa 'alaa aali Muhammad kamaa Swallayta 'alaa Ibraahiym wa 'alaa aali Ibraahiym wa Baarik 'alaa Muhammad wa 'alaa aali Muhammad kamaa Baarakta 'alaa Ibraahiym wa 'alaa aali Ibraahiym fil'aalamyna Innaka Hamiydun Majiyd. Ndugu zangu Waislam Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) Anasema katika Qur-aan. إِنَّ اللَّـهَ يَأْمُرُ بِالْعَدْلِ وَالْإِحْسَانِ وَإِيتَاءِ ذِي الْقُرْبَىٰ وَيَنْهَىٰ عَنِ الْفَحْشَاءِ وَالْمُنكَرِ وَالْبَغْيِ ۚيَعِظُكُمْ لَعَلَّكُمْ تَذَكَّرُونَ Hakika Allaah Anaamrishia uadilifu na ihsaan na kuwapa (mahitajio na msaada) jamaa wa karibu; na Anakataza machafu na munkari na ukandamizaji. Anakuwaidhini huenda mkapata kukumb...

Viungo vya Mwili vitashuhudia Matendo ya Mwanaadamu Siku ya Qiyaamah

Anasema Allaah  سبحانه وتعالى   ((الْيَوْمَ نَخْتِمُ عَلَى أَفْوَاهِهِمْ وَتُكَلِّمُنَا أَيْدِيهِمْ وَتَشْهَدُ أَرْجُلُهُمْ بِمَا كَانُوا يَكْسِبُونَ)) ((Leo Tunaviziba vinywa vyao, na iseme Nasi mikono  yao , na itoe ushahidi miguu  yao kwa waliyokuwa wakiyachuma))  [Yaasiyn :65 ] Siku ya Qiyaamah viungo vya miili vitakuwa ni vyenye kushuhudia matendo ya binaadamu aliyoyatenda hapa duniani: Mfano mikono itasema: "nimeiba".  Miguu itasema, "nimekwenda sehemu ya ma'asi". Macho yatasema, "nimetazama machafu".  Masikio yatasema, "nimesikiliza nyimbo, au umbea" na kadhalika. Na hivi ndivyo itakavyokuwa hali ya makafiri, wanafiki na wenye kumuasi Mola siku ya kufufuliwa,  watakapokanusha madhambi waliyoyatenda duniani na kuapa kwamba hawakuyafanya, Allaah  سبحانه وتعالى  Atawafunga midomo  yao na kuviamrisha viungo vizungumze:   عن أنس بن مالك قال: كنا عند النبي صلى ال...