Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Mchumba anachelewa kupeleka posa nyumbani

*Swali*

Asalam alaykum, shekh :mm nna mchumba angu  lkn anakua mgumu kuja kuleta posa nymbani, jee? nimsomee dua gani ili aweze Kuja haraka maana ni cku nyingi tena naomba unisaidie unifahamishe ustadh.

*Majibu*

Wa Aleykum Sallaam WarahmatulLaah Wabarakatuh

BismiLLaah wa AlhamduliLLaah was-Swalaatu wa Salaamu ‘alaa Muhammad wa ‘alaa  aalihi wa Aswhaabihil Kiraam, wa Ba’ad.

*Maana ya Uchumba Kisheria*

✅Uchumba katika Uislamu ni pale *mwanamme anayetaka kuoa au jamaa zake au mtu yeyote aliyemwakilisha anapokwenda kwa wazazi wa msichana/Bint/Mwanamke* kuposa/kupeleka Barua na kukubaliwa.

*✅Huo ndio unaitwa uchumba*

➡Ama kinyume na hivyo unakuwa ni urafiki baina ya mvulana na msichana. *Na hili katika Uislamu limekatazwa kwani ni Haramu*

✅Na hili limekatazwa kishari’ah.

➡Na hapo katika Swali lako umesema kwamba una Mchumba wako Lakini anakuwa mgumu *kuleta posa nyumbani* ina maana kuwa Huyo mwanaume *Kisheria si Mchumba wako kwasababu bado hajapeleka barua ya Posa nyumbani kwenu*

➡Katika Uislamu Hakuna *Boyfriend wala Girlfriend* na hii ni *Haramu*

➡Ayaah na dalili za kukataza jambo hili zipo nyingi zikiwa zinazoashiria makatazo moja kwa moja (directly) na nyinginezo zenye uhusiano na makatazo haya.

➡Kuwa na boyfriend bila shaka kutasababisha yatendeke maasi baina ya mwanamke na mwanamume kwani shaytwaan huwa pamoja nao akiwachochea kuingia katika kumuasi Mola wao⤵

عن عمر رضي الله عنه عن النبي صلى الله عليه وسلم : ((ما خلا رجل بامرأة إلا كان الشيطان ثالثهما)) الترمذي

Kutoka kwa 'Umar (Radhiya Allaahu 'anhu) kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam): ((Hachanganyiki mwanamume na mwanamke ila shaytwaan huwa ni watatu wao))
↪Imepokelewa na Imaam At-Tirmidhiy

✅Ndio maana pia Mtume Muhammad ((Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) ameonya kukaa faraagha mwanamke na mwanamume⤵

قال صلىالله عليه سلم : ((لا يخلوّنّ أحدكم بامرأةإلا مع ذى محرم)) متفق عليه

Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: ((Hawi faraagha mmoja wenu pamoja na mwanamke ila awepo Mahram wake))
↪Imepokelewa na Imaam Al-Bukhaariy Na Muslim

➡Matokeo yake ni shaytwaan kuwafikisha kuingia katika maasi ya zinaa na ndio maana sheria ya Kiislamu haikuruhusu jambo hilo au kufunga uchumba inavyojulikana engagement. Bali inatakiwa kufunga ndoa moja kwa moja baada ya kuwafikiana pande zote.

➡Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala)⤵

((وَالْمُحْصَنَاتُ مِنَ الْمُؤْمِنَاتِ وَالْمُحْصَنَاتُ مِنَ الَّذِينَأُوتُواْ الْكِتَابَ مِن قَبْلِكُمْ إِذَا آتَيْتُمُوهُنَّ أُجُورَهُنَّمُحْصِنِينَ غَيْرَ مُسَافِحِينَ وَلاَ مُتَّخِذِي أَخْدَانٍ وَمَنيَكْفُرْ بِالإِيمَانِ فَقَدْ حَبِطَ عَمَلُهُ وَهُوَ فِي الآخِرَةِ مِنَالْخَاسِرِين))

((Na pia wanawake wema miongoni mwa Waumini, na wanawake wema miongoni mwa waliopewa Kitabu kabla yenu, mtakapowapa mahari yao, mkafunga nao ndoa, bila ya kufanya uasharati wala kuwaweka kinyumba. Na anayekataa kuamini bila shaka amali yake imepotea, naye katika Akhera atakuwa miongoni mwa wenye khasara))
↪Surat Al-Maaidah Aya ya 5


✅Hizo ni mila za kikafiri ambazo zinapasa tuepukano nazo na ambazo Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) Ametuonya⤵

((وَلَن تَرْضَى عَنكَ الْيَهُودُ وَلاَ النَّصَارَى حَتَّى تَتَّبِعَ مِلَّتَهُم))
((Mayahudi hawawi radhi nawe, wala Wakristo, mpaka ufuate mila yao))
↪Surat Al-Baqarah Aya ya 120

✅Ewe Msichana wa Kiislamu unapokabiliwa na mvulana kutaka kufanya urafiki ujiepushe kabisa bali umshauri kwanza awasiliane na wazazi wako na baada ya kumjua kuwa ni mtu mwenye dini na tabia nzuri basi wazazi wasichelewa kukuozesha nawe uridhike kwani hivyo ndivyo ipasavyo na tulivyopewa mafunzo kutoka kwa Mtume Muhammad(Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam⤵

((إِذَا خَطَبَ إِلَيْكُمْمَنْ تَرْضَوْنَ دِينَهُ وَخُلُقَهُ فَزَوِّجُوهُ إِلَّا تَفْعَلُوا تَكُنْ فِتْنَةٌفِي الْأَرْضِ وَفَسَادٌ عَرِيضٌ))   رواهالترمذي   وقال الألباني : حسن

((Atakapoposa kwenu yule mtakaeridhika na dini yake, na tabia yake, basi muozesheni, kwani kutokufanya hivyo itakuwa fitna katika ardhi (duniani) na ufisadi mpana (mkubwa) ))
↪Imepokelewa na Imaam At-Tirmidhiy kasimulia na Shaykh Albaaniy amesema ni Hadiyth Hasan.

*Ewe Mwanamke akitokea Mwanaume anayetaka kukuoa kabla hujamkubalia kwenda kupeleka Barua ua Posa nyumbani kwenu Tafadhali Swali Swalah ya Istikhaarah*

✅Istikhaarah maana yake ni kuomba uchaguzi au aumuzi katika jambo.

➡Na Swalah ya Istikhaarah hakika ni zawadi kubwa tuliyopewa sisi Umma wa Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم, kwani ina faida kubwa sana kwetu kwani hatuamui jambo letu tunaloliomba katika Swalah hii, ila baada ya kumuomba Allaah سبحانه وتعالى Atuamulie Yeye hilo jambo kama lina kheri na sisi Atufanikishe nalo na kama ni la shari Atuepushe nalo.

➡Yeye Pekee Allaah سبحانه وتعالى Ndiye mwenye kujua ya ghayb (yasiyoonekana) yaani yatakayotokea siku za mbele yaliyokuwa yameshandikwa katika Lawhun Mahfuudhw.

*Na Dua ya Kuomba katika Swalah ya Istikhaarah ilivyokuja katika Du'aa kuwa tunasema⤵*

اللّهُـمَّ إِنِّـي أَسْتَخيـرُكَ بِعِاْـمِك، وَأسْتَقْـدِرُكَ بِقُـدْرَتِـك، وَأَسْـألُـكَ مِنْ فَضْـلِكَ العَظـيم، فَإِنَّـكَ تَقْـدِرُ وَلا أَقْـدِر، وَتَـعْلَـمُ وَلا أَعْلَـم، وَأَنْـتَ عَلاّمُ الغُـيوب، اللّهُـمَّ إِنْ كُنْـتَ تَعْـلَمُ أَنَّ هـذا الأمْـرَ  (وَيُسَـمِّي  حاجته)  خَـيْرٌ لي في دينـي وَمَعـاشي وَعاقِـبَةِ أَمْـري، ( عَاجِلِهِ و آجِلِه)   فَاقْـدُرْهُ لي وَيَسِّـرْهُ لي ثـمَّ بارِكْ لي فيـه، وَإِنْ كُنْـتَ تَعْـلَمُ أَنَّ هـذا الأمْـرَ شَـرٌ  لي في دينـي وَمَعـاشي وَعاقِـبَةِ أَمْـري، ( عَاجِلِهِ و آجِلِه) فَاصْرِفْـهُ عَنّيِ  وَاصْرِفْني عَنْـهُ وَاقْـدُرْ ليَ الخَـيْرَ  حَيْـثُ كانَ ثُـمَّ أَرْضِـني بِِـه .

*"Allahumma inniy astakhiyruka bi’ilmika, wa astaqdiruka biqudratika wa as-aluka min fadhwlikal-‘adhwiym, fainnaka Taqdiru wa laa aqdir, wa Ta’alamu wa laa a’alamu wa Anta ‘Allaamul-ghuyuub. Allahumma in Kunta Ta’alamu anna haadhal-amra (Utaje jambo lako) Khayrul-liy fiy diyniy wa ma’aashiy, wa ‘aaqibati amriy, ‘aajilihi wa aajilihi Faqdir-hu-liy wa Yassirhu-liy, thumma Baarik-liy fiyh. Wain Kunta Ta’alamu anna haadhal-amra sharrul-liy fiy diyniy wa ma’aashiy wa ‘aaqibati amriy ‘aajilihi wa aajilihi, Faswrif-hu ‘anniy Waswrifniy ‘anhu Waqdir-liyal-khayra haythu kaana Thummar-dhwiniy bih"*

“Ewe Allah,  hakika mimi nakutaka ushauri (muelekezo) kwa ujuzi Wako, na nakuomba Uniwezeshe kwa uwezo Wako, na nakuomba fadhila Zako kubwa, hakika Wewe Unaweza, nami siwezi, nawe Unajua nami sijui, nawe ni Mjuzi wa yale yaliyofichikana.   Ewe Allah, iwapo jambo hili kutokana na ujuzi Wako (utalitaja jambo lako) lina kheri na mimi katika dini yangu na maisha yangu na mwisho wa jambo langu (karibu na mbali) basi nakuomba Uniwezeshe nilipate, na Unifanyie wepesi, kisha Unibariki, na iwapo unajua kwamba jambo hili ni shari kangu katika dini yangu na maisha yangu na mwisho wa jambo langu (karibu na mbali) basi Liepushe na mimi na Niepushe nalo, na  Nipangie  jambo jengine lenye  kheri nami popote lilipo, kisha Niridhishe kwalo”

✅Kwa hiyo inampasa Muislamu awe anaitumia sana Swalah hii kwa kila jambo lake, likiwa ni dogo au kubwa kwani juu ya kupata faida ya kwamba unamuachia Allaah سبحانه وتعالى  Mwenye Ujuzi Mwenye Hikma kutuamulia, pia unapata thawabu za kuswali Raka'ah mbili.

✅Lakini haifai kuswali Swalah hii kwa ajili ya mambo maovu au anapotaka mtu kutimiza fardhi.

➡Mfano mwizi haimpasi kuiswali Swalah hii ili atake uamuzi kama akaibe au la maana kuna baadhi ya Waumini hawachelewi kuniuliza maswali . Au mwanamke asiiswali Swalah hii ikiwa yuko katika wasiwasi wa shaytwaani unaotaka kumpelekea kufanya zinaa na kadhalika.

⏩Vile vile asiswali mtu Swalah hii katika kutimiza mambo ya kheri kama mfano kutimiza fardhi ya kutoa Zakah au Sadaka na kadhalika wakati shaytwaan atakapokutia wasiwasi kukuzuia kutenda amali hizo njema.

✅Swalah hii inaweza kutumika katika mambo yanayofaa mfano unataka kwenda safari, au umeomba kazi katika shirika fulani, au unataka kuoa au mwanamke amekuja kuposwa na kadhalika.

Na Allaah anajua zaidi

Imeandaliwa na *Manhaj Salafy Mtwara*

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Hukumu ya kupeleka barua ya posa kwenye kitambaa cheupe

                      Hukumu ya kupeleka barua ya posa kwenye kitambaa cheupe  Hakika ni kuwa posa ilivyofanyika katika Uislamu kuanzia wakati wa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) inafahamika vilivyo. Posa inaweza kuja kutoka kwa mume na watu wake kwa jamaa za mke au mzazi wa mke kumtafutia binti yake mume. Ikiwa wazazi watakwenda kwa wazazi wa mke, baada ya kupeleka maneno, na wazazi wa mke watataka kupatiwa muda wa kufikiria, kufanya shuuraa, kuulizia, kutafiti na baadaye kukubali au kukataa. Ikiwa wamekubali baada ya kumshauri binti  yao  ni vyema mume mtarajiwa aende amuone atakaye kuwa mkewe ili apate kutulia na kuridhika kabla siku ya Nikaah. Binti huyo au wazazi wake wataweka kiwango cha mahari ambacho mume anatakiwa kutoa. Hii njia ya kuweka pesa kwenye kitambaa au bahasha haipo katika mafunzo ya Kiislam, na huenda ni njia ya kitamaduni fulani au itikadi f...

Maana ya Uadilifu

                                         MAANA  YA  UADILIFU  KATIKA  UISLAMU Assallaam  Aleykum  WarahmatulLaah  Wabarakatuh Alhamdu Lillaahi Rabil'aalamiyn) Allaahumma Swalli 'alaa Muhammad wa 'alaa aali Muhammad kamaa Swallayta 'alaa Ibraahiym wa 'alaa aali Ibraahiym wa Baarik 'alaa Muhammad wa 'alaa aali Muhammad kamaa Baarakta 'alaa Ibraahiym wa 'alaa aali Ibraahiym fil'aalamyna Innaka Hamiydun Majiyd. Ndugu zangu Waislam Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) Anasema katika Qur-aan. إِنَّ اللَّـهَ يَأْمُرُ بِالْعَدْلِ وَالْإِحْسَانِ وَإِيتَاءِ ذِي الْقُرْبَىٰ وَيَنْهَىٰ عَنِ الْفَحْشَاءِ وَالْمُنكَرِ وَالْبَغْيِ ۚيَعِظُكُمْ لَعَلَّكُمْ تَذَكَّرُونَ Hakika Allaah Anaamrishia uadilifu na ihsaan na kuwapa (mahitajio na msaada) jamaa wa karibu; na Anakataza machafu na munkari na ukandamizaji. Anakuwaidhini huenda mkapata kukumb...

Viungo vya Mwili vitashuhudia Matendo ya Mwanaadamu Siku ya Qiyaamah

Anasema Allaah  سبحانه وتعالى   ((الْيَوْمَ نَخْتِمُ عَلَى أَفْوَاهِهِمْ وَتُكَلِّمُنَا أَيْدِيهِمْ وَتَشْهَدُ أَرْجُلُهُمْ بِمَا كَانُوا يَكْسِبُونَ)) ((Leo Tunaviziba vinywa vyao, na iseme Nasi mikono  yao , na itoe ushahidi miguu  yao kwa waliyokuwa wakiyachuma))  [Yaasiyn :65 ] Siku ya Qiyaamah viungo vya miili vitakuwa ni vyenye kushuhudia matendo ya binaadamu aliyoyatenda hapa duniani: Mfano mikono itasema: "nimeiba".  Miguu itasema, "nimekwenda sehemu ya ma'asi". Macho yatasema, "nimetazama machafu".  Masikio yatasema, "nimesikiliza nyimbo, au umbea" na kadhalika. Na hivi ndivyo itakavyokuwa hali ya makafiri, wanafiki na wenye kumuasi Mola siku ya kufufuliwa,  watakapokanusha madhambi waliyoyatenda duniani na kuapa kwamba hawakuyafanya, Allaah  سبحانه وتعالى  Atawafunga midomo  yao na kuviamrisha viungo vizungumze:   عن أنس بن مالك قال: كنا عند النبي صلى ال...