Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Dunia ni nyumba ya majaribio na mtihani

Assallaam  Aleykum  WarahmatulLaah  Wabarakatuh


Allaah Ameumba viumbe Wake ili wamwabudu Yeye Mmoja asiyekuwa na mshirika.

Amesema katika Kitabu Chake Titukufu:

 ُونِ د ُ ب ْ ع َ ي ِ َّل ل َِّ إ َ نس اْْلِ َ ن و َّ ُت ا ْْلِ ْ لَق َ ا خ َ م َ و

“Na Sikuumba majini na wanadamu wa isipokuwa waniabudu.”51:56

 Ametuma Mitume Wake watukufu ili wawaoneshe waja njia ya ´ibaadah:

 َ و َ ه َّ ُوا الل د ُ ب ْ اع واَّل أَنِ ُ رس َّ ٍ َّمة ا ِِف ُك ِّل أُ َ ن ْ ث َ ع َ َ ْد ب لَق َ َت و اغُو َّ وا الط ُ ب ِ ن َ ت ْ اج

“Na kwa yakini Tulituma katika kila ummah Rasuli (awaamrishe watu wake) kwamba: “Mwabuduni Allaah na jiepusheni na twaaghuwt (miungu ya uongo).”16:36

Amefanya maisha ya dunia kuwa ni sehemu ya majaribio yao na mtihani ili waoneshe ni nani katika wao alie na matendo mazuri:

 ال َ َم ع ُ ن َ ْس أَح ْ ُّ ُكم أَي ْ ُكم َ لُو ْ ب َ ي ِ ل َ اة َ ي َ ا ْْل َ ْ َت و و َ الْم َ لَق َ ي خ ذِ َّ ال

“Ambaye Ameumba mauti na uhai ili Akujaribuni ni nani kati yenu mwenye ‘amali nzuri zaidi.”67:02

Kisha Akasema:

 ُو َف الْغ ُ ِزيز َ الْع َ و ُ ه َ و ُ ر

“Naye ni Al- ‘Aziyzul-Ghafuwr (Mwenye enzi ya nguvu Asiyeshindika daima - Mwingi wa kusamehe).”67:02


Amesema hivi ili kuonesha kuwa Anawalipa hawa wanaopewa mtihani wanaotenda matendo mema. Malipo haya yametokamana na Jina Lake alGhafuur (Mwingi wa kusamehe).

Upande mwingine Ameonesha pia kuwa wale wasiotenda matendo mazuri wanastahiki kuadhibiwa kutokana na Jina Lake al-´Aziyz (Mwenye enzi ya nguvu asiyeshindika daima). Hili linaenda sambamba na Kauli Yake:

 ُ يم ِ ُب اْْلَل َذا َ الْع َ و ُ َذاِِب ه َ ن ع أَ َّ َ و

“Na kwamba Adhabu Yangu, ndiyo adhabu iumizayo.”15:50


Kwahiyo Ndugu zangu katika Imaani, Tumche Allaah na Tufanye Mema

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Hukumu ya kupeleka barua ya posa kwenye kitambaa cheupe

                      Hukumu ya kupeleka barua ya posa kwenye kitambaa cheupe  Hakika ni kuwa posa ilivyofanyika katika Uislamu kuanzia wakati wa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) inafahamika vilivyo. Posa inaweza kuja kutoka kwa mume na watu wake kwa jamaa za mke au mzazi wa mke kumtafutia binti yake mume. Ikiwa wazazi watakwenda kwa wazazi wa mke, baada ya kupeleka maneno, na wazazi wa mke watataka kupatiwa muda wa kufikiria, kufanya shuuraa, kuulizia, kutafiti na baadaye kukubali au kukataa. Ikiwa wamekubali baada ya kumshauri binti  yao  ni vyema mume mtarajiwa aende amuone atakaye kuwa mkewe ili apate kutulia na kuridhika kabla siku ya Nikaah. Binti huyo au wazazi wake wataweka kiwango cha mahari ambacho mume anatakiwa kutoa. Hii njia ya kuweka pesa kwenye kitambaa au bahasha haipo katika mafunzo ya Kiislam, na huenda ni njia ya kitamaduni fulani au itikadi f...

Maana ya Uadilifu

                                         MAANA  YA  UADILIFU  KATIKA  UISLAMU Assallaam  Aleykum  WarahmatulLaah  Wabarakatuh Alhamdu Lillaahi Rabil'aalamiyn) Allaahumma Swalli 'alaa Muhammad wa 'alaa aali Muhammad kamaa Swallayta 'alaa Ibraahiym wa 'alaa aali Ibraahiym wa Baarik 'alaa Muhammad wa 'alaa aali Muhammad kamaa Baarakta 'alaa Ibraahiym wa 'alaa aali Ibraahiym fil'aalamyna Innaka Hamiydun Majiyd. Ndugu zangu Waislam Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) Anasema katika Qur-aan. إِنَّ اللَّـهَ يَأْمُرُ بِالْعَدْلِ وَالْإِحْسَانِ وَإِيتَاءِ ذِي الْقُرْبَىٰ وَيَنْهَىٰ عَنِ الْفَحْشَاءِ وَالْمُنكَرِ وَالْبَغْيِ ۚيَعِظُكُمْ لَعَلَّكُمْ تَذَكَّرُونَ Hakika Allaah Anaamrishia uadilifu na ihsaan na kuwapa (mahitajio na msaada) jamaa wa karibu; na Anakataza machafu na munkari na ukandamizaji. Anakuwaidhini huenda mkapata kukumb...

Viungo vya Mwili vitashuhudia Matendo ya Mwanaadamu Siku ya Qiyaamah

Anasema Allaah  سبحانه وتعالى   ((الْيَوْمَ نَخْتِمُ عَلَى أَفْوَاهِهِمْ وَتُكَلِّمُنَا أَيْدِيهِمْ وَتَشْهَدُ أَرْجُلُهُمْ بِمَا كَانُوا يَكْسِبُونَ)) ((Leo Tunaviziba vinywa vyao, na iseme Nasi mikono  yao , na itoe ushahidi miguu  yao kwa waliyokuwa wakiyachuma))  [Yaasiyn :65 ] Siku ya Qiyaamah viungo vya miili vitakuwa ni vyenye kushuhudia matendo ya binaadamu aliyoyatenda hapa duniani: Mfano mikono itasema: "nimeiba".  Miguu itasema, "nimekwenda sehemu ya ma'asi". Macho yatasema, "nimetazama machafu".  Masikio yatasema, "nimesikiliza nyimbo, au umbea" na kadhalika. Na hivi ndivyo itakavyokuwa hali ya makafiri, wanafiki na wenye kumuasi Mola siku ya kufufuliwa,  watakapokanusha madhambi waliyoyatenda duniani na kuapa kwamba hawakuyafanya, Allaah  سبحانه وتعالى  Atawafunga midomo  yao na kuviamrisha viungo vizungumze:   عن أنس بن مالك قال: كنا عند النبي صلى ال...