Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Hukmu ya Kusheherekea kumbukumbu ya Kifo

swali

Je,inafaa kusheherekea Death Anniversary..? na ipi Hukmu ya Kusheherekea kumbukumbu ya Kifo (Anniversary)

Jibu


Kwanza ni dhambi katika Uislamu kuweka kumbukumbu ya kifo inayojulikana kama ni ‘death anniversary’. Hili ni jambo la kuiga makafiri ambalo Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)  amekemea. Kwa hiyo kulitenda ni miongoni mwa madhambi makubwa unapaswa ujiepushe nalo kabisa.

Uislamu ni Dini yenye kutuongoza katika mfumo mzima wa maisha hapa duniani. Kwa ajili hiyo, lolote tufanyalo ni lazima liambatane na Shariy’ah ya Uislamu.

Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) aliwakuta watu wa Madiynah wakisherehekea siku kuu zao. Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) akawaambia kuwa wao wamebadilishiwa hizo sikukuu zao kwa siku mbili kuu zilizo bora kabisa, nazo ‘Iyd al-Fitwr na Al-Adhw-haa.

Ama sherehe ya anniversary hata ya Nabiy mwenyewe (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) haipo katika siku za sherehe.

Ama hizi anniversaries  ambazo tunasherehekea ni katika ada na desturi za makafiri na mushrikina. Na kwa hilo Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amekataza katika Hadiyth:

 عن إبن عمر ((من تشبه بقوم فهو منهم)) ابن حبان - صحيح
Kutoka kwa Ibn 'Umar ((Mwenye kujifananisha na watu naye ni kama wao)) [Ibn Hibbaan ikiwa swahiyh]     

Na zimezuka anniversaries nyenginezo mbali na ya ndoa ambayo ndio iliyoanzishwa mwanzo na makafiri. Kumezuka  mpaka anniversary za kifo. 

Shariy’ah ya Kiislamu kuhusu mtu anapoweka nadhiri kwa ajili ya jambo lisilofaa basi anatakiwa asitekeleze hiyo nadhiri bali ajiepushe na hilo jambo. Dalili ni Hadiyth ifuatayo ya Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam):

عَنْ أبي طريفٍ عَدِيَّ بْنَ حَاتِمٍ  الطَّائي (رضي الله عنه) قال: سَمِعْتُ رسول اللَّهِ (صلى الله عليه و آله وسلم) يَقُولُ: ((مَنْ حَلَفَ عَلَى يَمِينٍ ثُمَّ رَأَى أَتْقَى لِلَّهِ مِنْهَا فَلْيَأْتِ التَّقْوَى))  رواه مسلم  
Imepokelewa kutoka kwa Abu Twariyf ‘Adiyy bin Haatim (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: Nimesikia Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akisema:
((Atakayeapa yamini [kufanya jambo] kisha akaona linalomridhisha zaidi Allaah kuliko aliloliapia, basi amche Allaah kwa kufanya linalomridhisha Allaah)) [Muslim]

Na  Allaah  anajua  zaidi

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Hukumu ya kupeleka barua ya posa kwenye kitambaa cheupe

                      Hukumu ya kupeleka barua ya posa kwenye kitambaa cheupe  Hakika ni kuwa posa ilivyofanyika katika Uislamu kuanzia wakati wa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) inafahamika vilivyo. Posa inaweza kuja kutoka kwa mume na watu wake kwa jamaa za mke au mzazi wa mke kumtafutia binti yake mume. Ikiwa wazazi watakwenda kwa wazazi wa mke, baada ya kupeleka maneno, na wazazi wa mke watataka kupatiwa muda wa kufikiria, kufanya shuuraa, kuulizia, kutafiti na baadaye kukubali au kukataa. Ikiwa wamekubali baada ya kumshauri binti  yao  ni vyema mume mtarajiwa aende amuone atakaye kuwa mkewe ili apate kutulia na kuridhika kabla siku ya Nikaah. Binti huyo au wazazi wake wataweka kiwango cha mahari ambacho mume anatakiwa kutoa. Hii njia ya kuweka pesa kwenye kitambaa au bahasha haipo katika mafunzo ya Kiislam, na huenda ni njia ya kitamaduni fulani au itikadi f...

Maana ya Uadilifu

                                         MAANA  YA  UADILIFU  KATIKA  UISLAMU Assallaam  Aleykum  WarahmatulLaah  Wabarakatuh Alhamdu Lillaahi Rabil'aalamiyn) Allaahumma Swalli 'alaa Muhammad wa 'alaa aali Muhammad kamaa Swallayta 'alaa Ibraahiym wa 'alaa aali Ibraahiym wa Baarik 'alaa Muhammad wa 'alaa aali Muhammad kamaa Baarakta 'alaa Ibraahiym wa 'alaa aali Ibraahiym fil'aalamyna Innaka Hamiydun Majiyd. Ndugu zangu Waislam Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) Anasema katika Qur-aan. إِنَّ اللَّـهَ يَأْمُرُ بِالْعَدْلِ وَالْإِحْسَانِ وَإِيتَاءِ ذِي الْقُرْبَىٰ وَيَنْهَىٰ عَنِ الْفَحْشَاءِ وَالْمُنكَرِ وَالْبَغْيِ ۚيَعِظُكُمْ لَعَلَّكُمْ تَذَكَّرُونَ Hakika Allaah Anaamrishia uadilifu na ihsaan na kuwapa (mahitajio na msaada) jamaa wa karibu; na Anakataza machafu na munkari na ukandamizaji. Anakuwaidhini huenda mkapata kukumb...

Viungo vya Mwili vitashuhudia Matendo ya Mwanaadamu Siku ya Qiyaamah

Anasema Allaah  سبحانه وتعالى   ((الْيَوْمَ نَخْتِمُ عَلَى أَفْوَاهِهِمْ وَتُكَلِّمُنَا أَيْدِيهِمْ وَتَشْهَدُ أَرْجُلُهُمْ بِمَا كَانُوا يَكْسِبُونَ)) ((Leo Tunaviziba vinywa vyao, na iseme Nasi mikono  yao , na itoe ushahidi miguu  yao kwa waliyokuwa wakiyachuma))  [Yaasiyn :65 ] Siku ya Qiyaamah viungo vya miili vitakuwa ni vyenye kushuhudia matendo ya binaadamu aliyoyatenda hapa duniani: Mfano mikono itasema: "nimeiba".  Miguu itasema, "nimekwenda sehemu ya ma'asi". Macho yatasema, "nimetazama machafu".  Masikio yatasema, "nimesikiliza nyimbo, au umbea" na kadhalika. Na hivi ndivyo itakavyokuwa hali ya makafiri, wanafiki na wenye kumuasi Mola siku ya kufufuliwa,  watakapokanusha madhambi waliyoyatenda duniani na kuapa kwamba hawakuyafanya, Allaah  سبحانه وتعالى  Atawafunga midomo  yao na kuviamrisha viungo vizungumze:   عن أنس بن مالك قال: كنا عند النبي صلى ال...