Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Mume afanye nini ikiwa mkewe hataki kuswali?

*Swali*

Mume achukue hatua gani ikiwa mke hataki kuswali?

*Jibu*

✅Mara nyingi kama vile wanawake wanashindwa kufuata maagizo ya kuchagua mume wa sawa Kidini ndivyo wanaume wanavyofanya makosa hayo hayo.

➡Mume wa Kiislamu anatakiwa amchague mke mwenye Dini na Imani, maadili na tabia nzuri.

✅Kukosa kufuata maagizo hayo ya Mtume Muhammad(Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) ndio kunatokea matatizo kama hayo.

➡Hata hivyo, kosa lishatokea na inabidi tupate suluhisho kwa suala hilo nyeti.

➡Kulingana na maelezo yako ni kuwa mkeo inaonyesha bado ana Uislamu na Imani, hivyo anataka msukumo wa kuweza kutekeleza wajibu huo bila ya tatizo.

➡Jambo ambalo unatakiwa mwanzo kabisa kufanya ni kumnasihi mkeo kwa njia nzuri, kwani Allaah (Subhaana wa Taala) Anatuambia⤵

“Waite waelekee kwenye Njia ya Mola wako Mlezi kwa hikima na mawaidha mema, na ujadiliane nao kwa namna iliyo bora”
↪Rejea Qur'an 16: 125.

➡Inatakiwa utumie mbinu tofauti za kuweza kumvutia katika kuswali bila ya yeye kuwa na kinyongo juu ya suala hilo.

➡Mpatie vipeperushi kuhusu umuhimu wa Swalah na madhara ya kuacha, vitabu, kanda, kaseti na njia nyingine.

✅Ikiwa imeshindikana hilo, itabidi sasa uingize mkono wa wazazi wenu kama inavyotaka sheria.

➡Allaah (Subhaana wa Taala) Anasema kwamba⤵

“Na ambao mnachelea kutoka katika utiifu wanasihini, muwahame katika malazi na wapigeni. Wakikutiini msiwatafutie njia ya kuwaudhi bure. Hakika Allaah ndiye Aliye juu na Mkuu. Na mkichelea kutakuwapo mfarakano baina ya mke na mume basi pelekeni muamuzi kutokana na jamaa za mume, na muamuzi kutokana na jamaa za mke. Wakitaka mapatano Allaah Atawawezesha. Hakika Allaah ni Mjuzi Mwenye khabari”
↪Rejea Qur'an 34 – 35.

➡Hivyo Mume inatakiwa ufuate mfumo ufuatao⤵

1⃣Kuwanasihi katika ya haki na ukweli.

2⃣Mhame(Jitenge naye katika Kitanda) katika malazi.

3⃣Mpige mkeo kipigo ambacho hakitamuumiza bali cha kumtisha wala usimpige uso.

4⃣Kuwe na suluhisho kwa kutumia waamuzi kutoka upande wa mke na mume ili waamue hilo.

✅Ikiwa hakukupatikana suluhisho lolote na wala mkeo hakubadilika basi itabidi umuache.

➡Na ikiwa itatokea hilo itabidi usirudie kosa tena unapotaka kuoa mwingine. Hata hivyo, tunaamini kuwa haitofikia hapo, In Shaa Allaah

Na Allaah Anajua zaidi

Imeandaliwa na *Imaam Masjid Tawbah*

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Hukumu ya kupeleka barua ya posa kwenye kitambaa cheupe

                      Hukumu ya kupeleka barua ya posa kwenye kitambaa cheupe  Hakika ni kuwa posa ilivyofanyika katika Uislamu kuanzia wakati wa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) inafahamika vilivyo. Posa inaweza kuja kutoka kwa mume na watu wake kwa jamaa za mke au mzazi wa mke kumtafutia binti yake mume. Ikiwa wazazi watakwenda kwa wazazi wa mke, baada ya kupeleka maneno, na wazazi wa mke watataka kupatiwa muda wa kufikiria, kufanya shuuraa, kuulizia, kutafiti na baadaye kukubali au kukataa. Ikiwa wamekubali baada ya kumshauri binti  yao  ni vyema mume mtarajiwa aende amuone atakaye kuwa mkewe ili apate kutulia na kuridhika kabla siku ya Nikaah. Binti huyo au wazazi wake wataweka kiwango cha mahari ambacho mume anatakiwa kutoa. Hii njia ya kuweka pesa kwenye kitambaa au bahasha haipo katika mafunzo ya Kiislam, na huenda ni njia ya kitamaduni fulani au itikadi f...

Maana ya Uadilifu

                                         MAANA  YA  UADILIFU  KATIKA  UISLAMU Assallaam  Aleykum  WarahmatulLaah  Wabarakatuh Alhamdu Lillaahi Rabil'aalamiyn) Allaahumma Swalli 'alaa Muhammad wa 'alaa aali Muhammad kamaa Swallayta 'alaa Ibraahiym wa 'alaa aali Ibraahiym wa Baarik 'alaa Muhammad wa 'alaa aali Muhammad kamaa Baarakta 'alaa Ibraahiym wa 'alaa aali Ibraahiym fil'aalamyna Innaka Hamiydun Majiyd. Ndugu zangu Waislam Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) Anasema katika Qur-aan. إِنَّ اللَّـهَ يَأْمُرُ بِالْعَدْلِ وَالْإِحْسَانِ وَإِيتَاءِ ذِي الْقُرْبَىٰ وَيَنْهَىٰ عَنِ الْفَحْشَاءِ وَالْمُنكَرِ وَالْبَغْيِ ۚيَعِظُكُمْ لَعَلَّكُمْ تَذَكَّرُونَ Hakika Allaah Anaamrishia uadilifu na ihsaan na kuwapa (mahitajio na msaada) jamaa wa karibu; na Anakataza machafu na munkari na ukandamizaji. Anakuwaidhini huenda mkapata kukumb...

Viungo vya Mwili vitashuhudia Matendo ya Mwanaadamu Siku ya Qiyaamah

Anasema Allaah  سبحانه وتعالى   ((الْيَوْمَ نَخْتِمُ عَلَى أَفْوَاهِهِمْ وَتُكَلِّمُنَا أَيْدِيهِمْ وَتَشْهَدُ أَرْجُلُهُمْ بِمَا كَانُوا يَكْسِبُونَ)) ((Leo Tunaviziba vinywa vyao, na iseme Nasi mikono  yao , na itoe ushahidi miguu  yao kwa waliyokuwa wakiyachuma))  [Yaasiyn :65 ] Siku ya Qiyaamah viungo vya miili vitakuwa ni vyenye kushuhudia matendo ya binaadamu aliyoyatenda hapa duniani: Mfano mikono itasema: "nimeiba".  Miguu itasema, "nimekwenda sehemu ya ma'asi". Macho yatasema, "nimetazama machafu".  Masikio yatasema, "nimesikiliza nyimbo, au umbea" na kadhalika. Na hivi ndivyo itakavyokuwa hali ya makafiri, wanafiki na wenye kumuasi Mola siku ya kufufuliwa,  watakapokanusha madhambi waliyoyatenda duniani na kuapa kwamba hawakuyafanya, Allaah  سبحانه وتعالى  Atawafunga midomo  yao na kuviamrisha viungo vizungumze:   عن أنس بن مالك قال: كنا عند النبي صلى ال...