Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Je, inafaa kwenda kwa mganga kwa lengo la kumrudisha Mume?

*Swali*

Mume wangu amenikimbia yuko Mkoa mwingine na sipati huduma yeyote

jee si dhambi kwenda kwa mganga ili apate kurudi? kama dhambi munanishauri nifanye nini na nasikia mtu akidai Talaka pepo ya Mola haisikii hata harufu?  Mtihani mkubwa kwangu umekuwa naomba msaada wenu.

*Majibu*

✅Tambua na tahadhari kwamba kwenda kumkabili mganga ni kumshirikisha Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) katika Majina Yake na Sifa Zake tukufu kwani unamkabili mganga kwa kuamini kwamba yeye atakuwa na uwezo wa kumrudisha mume wako na hali yeye ni kiumbe kama wewe dhaifu kabisa.

⏩Waganga hawana ila kutumia uchawi na kulaghai watu kwa kutaka mapato au chumo kutoka kwa watu wanaomwendea.

➡Mtu Mwenye kumwendea mganga ikiwa kwa ajili ya kumtegemea amtatulie matatizo yake au amtabirie jambo, hutoka nje ya Uislamu kutokana na kauli ya Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)⤵

((من أتى كاهناً فصدقه بما يقول فقد كفر بما أنزل على محمد صلى الله عليه وسلم))  رواه أبو داود  

((Atakayemwendea mchawi na kuamini aliyoambiwa, basi amekufuru yale aliyoteremshiwa Muhammad [Swalla Allaahu ‘alayhi wa sallam]))
↪Imepokelewa na Imaam Abu Daawud

✅Hivyo pia ni kumshirkisha Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) na ni dhambi ambayo Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) Hamsamehe mja⤵

((إِنَّ اللّهَ لاَ يَغْفِرُ أَن يُشْرَكَ بِهِ وَيَغْفِرُ مَا دُونَ ذَلِكَ لِمَن يَشَاء وَمَن يُشْرِكْ بِاللّهِ فَقَدِ افْتَرَى إِثْمًا عَظِيمًا))

((Hakika Allaah Hasamehe kushirikishwa, na Husamehe yaliyo duni ya hilo kwa Amtakaye. Na anayemshirikisha Allaah basi hakika amezua dhambi kubwa))
↪Surat An-Nisaa Aya ya 48.

➡Hatari nyingine ni kwamba mwenye kumshirkisha Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) Hataingia Peponi⤵

((إِنَّهُ مَن يُشْرِكْ بِاللّهِ فَقَدْ حَرَّمَ اللّهُ عَلَيهِ الْجَنَّةَ وَمَأْوَاهُ النَّارُ وَمَا لِلظَّالِمِينَ مِنْ أَنصَار))

((Kwani anayemshirikisha Allaah hakika Allaah Atamharimishia Pepo, na mahala pake ni Motoni. Na waliodhulumu hawatakuwa na wa kuwanusuru))
↪Surat Al-Maaidah Aya ya 72

✅Zingatia na fuata yafuatayo na InshaAllaah mumeo ikiwa ana kheri na wewe atarudi kwako, na ikiwa hakuna kheri, basi muombe Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) Akupe mwenye kheri zaidi yake.

1⃣Unatakiwa ujiulize mwenyewe kwanini mumeo amekukimbia? Bila ya shaka kuna sababu fulani.

➡Ikiwa ulikuwa na udhaifu fulani kwake, basi jambo la kwanza ni kujirekebisha huo udhaifu au tabia ambayo huenda ikawa ni sababu ya kukukimbia.

2⃣Unatakiwa uwatafute watu katika jamaa zako au jamaa zake wakusaidie kuwasiliana naye na waseme naye wapate kujua tatizo lenu ili mpate kusuluhishwa.

➡Ikiwa ni makosa kutoka kwako nawe unamtaka mumeo arudi, basi ujirekebishe na ukiri makosa yako na uombe radhi kwake na kumuahidi kwamba hutorudia tena na uko tayari kumridhisha. Salamu hizi hakikisha zinamfikia kwanza.

✅Kisha tambua kwamba Muislamu anapokutwa na mitihani ya aina yoyote anapaswa kuwa na subira na kumshukuru Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) kwa kuamini Qadhwaa na Qadar.

✅Kumbuka kwamba kupewa mitihani kuna maana ya kupandishwa daraja la mja anaposubiri.

✅Zidisha Taqwa na kumkabili Mola wako Aliyekuumba na Mwenye uwezo wa kukuondolea kila mitihani, shida, dhiki na matatizo.

(( وَمَن يَتَّقِ اللَّهَ يَجْعَل لَّهُ مَخْرَجًا)) 

((Na anayemcha Mwenyezi Mungu Humtengezea njia ya kutokea))
↪Surat At-Twalaaq Aya ya 2

(( وَمَن يَتَّقِ اللَّهَ يَجْعَل لَّهُ مِنْ أَمْرِهِ يُسْرًا ))

((Na anayemcha Allaah, Humfanyia mambo yake kuwa mepesi))
↪Surat At-Twalaaq Aya ya 4.

⏩Amka usiku katika thuluthi ya mwisho ya usiku uswali Tahajjud na umuombe Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala).

✅Jishughulishe na kumkumbuka Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) kila mara asubuhi na jioni, kwa kusoma Qur-aan, kusikiliza mawaidha, kutafuta elimu ya dini yako, yote haya yatakupa faida ya dunia na Akhera na yatakuridhisha nafsi yako, na pia yatakupunguzia mawazo.

➡Anasema Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala)⤵

((الَّذِينَ آمَنُواْ وَتَطْمَئِنُّ قُلُوبُهُم بِذِكْرِ اللّهِ أَلاَ بِذِكْرِ اللّهِ تَطْمَئِنُّ الْقُلُوبُ))

((Wale walioamini na zikatua nyoyo zao kwa kumkumbuka Allaah   Hakika kwa kumkumbuka Allaah ndio nyoyo hutua!))
↪Surat Ar-Ra'ad Aya ya 28.

✅Kuwa na tawakkul (kumtegemea Allah) na Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) kwa mambo yako yote Naye Atakufungulia kila njia za kheri⤵

(( وَمَن يَتَوَكَّلْ عَلَى اللَّهِ فَهُوَ حَسْبُهُ إِنَّ اللَّهَ بَالِغُ أَمْرِهِ قَدْ جَعَلَ اللَّهُ  لِكُلِّ شَيْءٍ قَدْرًا))

((Na anayemtegemea Allaah Yeye Humtosha. Hakika Allaah Anatimiza amri yake. Allaah Kajaalia kila kitu na kipimo chake))
↪Surat At-Twalaaq Aya ya 3

✅Baada ya kufafanua yote hayo, tunamuomba Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) Akufanyie wepesi mtihani wako na Akufungulie lililo na kheri nawe.

Na Allaah Anajua zaidi

Imeandaliwa na *Imaam Masjid Tawbah*

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Hukumu ya kupeleka barua ya posa kwenye kitambaa cheupe

                      Hukumu ya kupeleka barua ya posa kwenye kitambaa cheupe  Hakika ni kuwa posa ilivyofanyika katika Uislamu kuanzia wakati wa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) inafahamika vilivyo. Posa inaweza kuja kutoka kwa mume na watu wake kwa jamaa za mke au mzazi wa mke kumtafutia binti yake mume. Ikiwa wazazi watakwenda kwa wazazi wa mke, baada ya kupeleka maneno, na wazazi wa mke watataka kupatiwa muda wa kufikiria, kufanya shuuraa, kuulizia, kutafiti na baadaye kukubali au kukataa. Ikiwa wamekubali baada ya kumshauri binti  yao  ni vyema mume mtarajiwa aende amuone atakaye kuwa mkewe ili apate kutulia na kuridhika kabla siku ya Nikaah. Binti huyo au wazazi wake wataweka kiwango cha mahari ambacho mume anatakiwa kutoa. Hii njia ya kuweka pesa kwenye kitambaa au bahasha haipo katika mafunzo ya Kiislam, na huenda ni njia ya kitamaduni fulani au itikadi f...

Maana ya Uadilifu

                                         MAANA  YA  UADILIFU  KATIKA  UISLAMU Assallaam  Aleykum  WarahmatulLaah  Wabarakatuh Alhamdu Lillaahi Rabil'aalamiyn) Allaahumma Swalli 'alaa Muhammad wa 'alaa aali Muhammad kamaa Swallayta 'alaa Ibraahiym wa 'alaa aali Ibraahiym wa Baarik 'alaa Muhammad wa 'alaa aali Muhammad kamaa Baarakta 'alaa Ibraahiym wa 'alaa aali Ibraahiym fil'aalamyna Innaka Hamiydun Majiyd. Ndugu zangu Waislam Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) Anasema katika Qur-aan. إِنَّ اللَّـهَ يَأْمُرُ بِالْعَدْلِ وَالْإِحْسَانِ وَإِيتَاءِ ذِي الْقُرْبَىٰ وَيَنْهَىٰ عَنِ الْفَحْشَاءِ وَالْمُنكَرِ وَالْبَغْيِ ۚيَعِظُكُمْ لَعَلَّكُمْ تَذَكَّرُونَ Hakika Allaah Anaamrishia uadilifu na ihsaan na kuwapa (mahitajio na msaada) jamaa wa karibu; na Anakataza machafu na munkari na ukandamizaji. Anakuwaidhini huenda mkapata kukumb...

Viungo vya Mwili vitashuhudia Matendo ya Mwanaadamu Siku ya Qiyaamah

Anasema Allaah  سبحانه وتعالى   ((الْيَوْمَ نَخْتِمُ عَلَى أَفْوَاهِهِمْ وَتُكَلِّمُنَا أَيْدِيهِمْ وَتَشْهَدُ أَرْجُلُهُمْ بِمَا كَانُوا يَكْسِبُونَ)) ((Leo Tunaviziba vinywa vyao, na iseme Nasi mikono  yao , na itoe ushahidi miguu  yao kwa waliyokuwa wakiyachuma))  [Yaasiyn :65 ] Siku ya Qiyaamah viungo vya miili vitakuwa ni vyenye kushuhudia matendo ya binaadamu aliyoyatenda hapa duniani: Mfano mikono itasema: "nimeiba".  Miguu itasema, "nimekwenda sehemu ya ma'asi". Macho yatasema, "nimetazama machafu".  Masikio yatasema, "nimesikiliza nyimbo, au umbea" na kadhalika. Na hivi ndivyo itakavyokuwa hali ya makafiri, wanafiki na wenye kumuasi Mola siku ya kufufuliwa,  watakapokanusha madhambi waliyoyatenda duniani na kuapa kwamba hawakuyafanya, Allaah  سبحانه وتعالى  Atawafunga midomo  yao na kuviamrisha viungo vizungumze:   عن أنس بن مالك قال: كنا عند النبي صلى ال...