Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Maana ya Aya ya 103 katika Surat Al-An’aam yanayosema “Macho Hayamzunguki”

Maana ya Aya ya 103 katika Surat Al-An’aam yanayosema  “Macho Hayamzunguki”


Shaykh Fawzaan (Hafidhwahu Allaah) amesema:

“Na maana “Bila kuzunguka wala kayfiyah (kuzunguka vipi”, wao hawamzunguki Allaah (‘Azza wa Jalla), na kwamba wao wanamuona (Allaah) Subhaanahu bila ya kumzunguka. Na Allaah Mtukufu haiwezekani Yeye  kuzungukwa.

Anasema Subhaanahu:
وَلَا يُحِيطُونَ بِهِ عِلْمًا ﴿١١٠﴾
na wala hawawezi kufikia kuelewa chochote cha ujuzi Wake. [Twaahaa: 110]


Na Anasema Jalla Wa ‘Alaa:

لَّا تُدْرِكُهُ الْأَبْصَارُ وَهُوَ يُدْرِكُ الْأَبْصَارَ  
Macho hayamzunguki bali Yeye Anayazunguka macho yote. [Al-An’aam: 103]

“Macho hayamzunguki”
Maana yake (katika Aayah hiyo) ni kuwa, “Hayamzunguki Yeye (macho ya mtu)”, na wala maana yake si “Hayamuoni.” Kwa sababu Allaah (Subhaanahu wa Ta’alaa) Hakusema, “Hayamuoni Yeye macho.” bali Kasema, “Macho hayamzunguki.” Kudiriki ni kitu na kuona ni kitu kingine.

Hayo (macho) yanamuona Subhaanahu bila kumzunguka (pande zote kwa uoni), na kwa hili kuna radd (majibu) kwa yule mwenye kustadili (kutolea dalili) kwa Aayah hii kupinga kuonekana Allaah Qiyaamah. Akidai (mpotevu huyo) kuwa haiwezekani kuonekana Allaah, kwa sababu Allaah Kasema, “Macho hayamzunguki bali Yeye Anayazunguka macho yote;” [Al-An’aam: 103]

Tunawajibu (wenye itikadi hizo potofu), kuwa nyinyi hamfahamu maana ya “Macho hayamzunguki bali Yeye Anayazunguka macho yote”, bali maana yake ni “Hayamzunguki Yeye macho” na si maana yake “Hayamuoni Yeye”, na Hakusema Allaah, “Hayamuoni Yeye macho.”


[At-Ta’liyqaat Al-Mukhtaswarah ‘Alaa Al-‘Aqiydati Atw-Twahaawiyyah, mj. 1, uk. 78]


Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Hukumu ya kupeleka barua ya posa kwenye kitambaa cheupe

                      Hukumu ya kupeleka barua ya posa kwenye kitambaa cheupe  Hakika ni kuwa posa ilivyofanyika katika Uislamu kuanzia wakati wa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) inafahamika vilivyo. Posa inaweza kuja kutoka kwa mume na watu wake kwa jamaa za mke au mzazi wa mke kumtafutia binti yake mume. Ikiwa wazazi watakwenda kwa wazazi wa mke, baada ya kupeleka maneno, na wazazi wa mke watataka kupatiwa muda wa kufikiria, kufanya shuuraa, kuulizia, kutafiti na baadaye kukubali au kukataa. Ikiwa wamekubali baada ya kumshauri binti  yao  ni vyema mume mtarajiwa aende amuone atakaye kuwa mkewe ili apate kutulia na kuridhika kabla siku ya Nikaah. Binti huyo au wazazi wake wataweka kiwango cha mahari ambacho mume anatakiwa kutoa. Hii njia ya kuweka pesa kwenye kitambaa au bahasha haipo katika mafunzo ya Kiislam, na huenda ni njia ya kitamaduni fulani au itikadi f...

Maana ya Uadilifu

                                         MAANA  YA  UADILIFU  KATIKA  UISLAMU Assallaam  Aleykum  WarahmatulLaah  Wabarakatuh Alhamdu Lillaahi Rabil'aalamiyn) Allaahumma Swalli 'alaa Muhammad wa 'alaa aali Muhammad kamaa Swallayta 'alaa Ibraahiym wa 'alaa aali Ibraahiym wa Baarik 'alaa Muhammad wa 'alaa aali Muhammad kamaa Baarakta 'alaa Ibraahiym wa 'alaa aali Ibraahiym fil'aalamyna Innaka Hamiydun Majiyd. Ndugu zangu Waislam Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) Anasema katika Qur-aan. إِنَّ اللَّـهَ يَأْمُرُ بِالْعَدْلِ وَالْإِحْسَانِ وَإِيتَاءِ ذِي الْقُرْبَىٰ وَيَنْهَىٰ عَنِ الْفَحْشَاءِ وَالْمُنكَرِ وَالْبَغْيِ ۚيَعِظُكُمْ لَعَلَّكُمْ تَذَكَّرُونَ Hakika Allaah Anaamrishia uadilifu na ihsaan na kuwapa (mahitajio na msaada) jamaa wa karibu; na Anakataza machafu na munkari na ukandamizaji. Anakuwaidhini huenda mkapata kukumb...

Viungo vya Mwili vitashuhudia Matendo ya Mwanaadamu Siku ya Qiyaamah

Anasema Allaah  سبحانه وتعالى   ((الْيَوْمَ نَخْتِمُ عَلَى أَفْوَاهِهِمْ وَتُكَلِّمُنَا أَيْدِيهِمْ وَتَشْهَدُ أَرْجُلُهُمْ بِمَا كَانُوا يَكْسِبُونَ)) ((Leo Tunaviziba vinywa vyao, na iseme Nasi mikono  yao , na itoe ushahidi miguu  yao kwa waliyokuwa wakiyachuma))  [Yaasiyn :65 ] Siku ya Qiyaamah viungo vya miili vitakuwa ni vyenye kushuhudia matendo ya binaadamu aliyoyatenda hapa duniani: Mfano mikono itasema: "nimeiba".  Miguu itasema, "nimekwenda sehemu ya ma'asi". Macho yatasema, "nimetazama machafu".  Masikio yatasema, "nimesikiliza nyimbo, au umbea" na kadhalika. Na hivi ndivyo itakavyokuwa hali ya makafiri, wanafiki na wenye kumuasi Mola siku ya kufufuliwa,  watakapokanusha madhambi waliyoyatenda duniani na kuapa kwamba hawakuyafanya, Allaah  سبحانه وتعالى  Atawafunga midomo  yao na kuviamrisha viungo vizungumze:   عن أنس بن مالك قال: كنا عند النبي صلى ال...