Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Aina za Laana na Wepi waliolaaniwa na Allaah?

Swali


NANI HASWA ANASTAHIKI KUAMBIWA LAANA ZA ALLAAH ZIWE JUU YAKO. JE NI MAKAFIR AU MURTADINA AU WANAAFIQ? JE KUNA LAANA YA MTU MMOJA MMOJA UA WENGI WENGI?



JIBU



Shukrani zetu za dhati kwa swali lako kuhusu mas-ala ya laana. Laana si kitu kumpata mtu yeyote yule na hasa akiwa ni Muislamu. Laana kutoka kwa Allaah au Mtume Wake inampata mwenye kuacha amri na yule aliyekengeuka na maagizo yao. Allaah Aliyetukuka na Mtume Muhammad (Swalla Allaahu 'Alayhi wa aalihi wa sallam) wametutajia watu waliteremshiwa laana hizo.


Hebu tutazame baadhi ya mifano:

a)            Allaah Aliyetukuka Anasema: "Hakika Allaah Amewalaani makafiri na Amewaandalia Moto mkali" (33: 64).
b)           Allaah Aliyetukuka Anasema: "Kama wanafiki na wale wenye maradhi nyoyoni mwao na watangazao uovu mjini, hawataacha upotofu, kwa yakini Tutakusalitisha juu yao, kisha hawatakaa humo karibu yako ila muda kidogo tu. Maluuni (wamelaaniwa) hao popote waonekanapo wakamatwe na wauawe kabisa" (33: 60 – 61).
c)           Allaah Aliyetukuka Anasema: "Bila shaka wale wanaomuudhi Allaah na Mtume Wake, Allaah Amewalaani katika dunia na akhera, na Amewaandalia adhabu ifedheheshayo" (33: 57).
d)           Anasema tena Aliyetukuka: "Basi kwa sababu ya kuvunja kwao ahadi yao, Tuliwalaani na Tukazifanya nyoyo zao kuwa ngumu …" (5: 13).
e)          Anasema tena: "Jua kuwa laana ya Allaah iko juu ya madhalimu" (11: 18).
f)           Anasema tena: "Kishaa tuombe kwa unyenyekevu tutake laana ya Allaah iwashukie waongo" (3: 61).
g)         Anasema tena Aliyetukuka: "Wamelaaniwa waliokufuru miongoni mwa Bani Israili kwa ulimi wa Daawuud na 'Iysaa mwana wa Maryam kwa sababu waliasi na wakapindukia mipaka" (5: 78).

Tukizitazama Aayah hizi utapata ya kwamba waliolaaniwa na Allaah Aliyetukuka ni wengi miongoni mwao ni makafiri, madhalimu, walioasi, waliotupa mipaka, wanaomuudhi Allaah na Mtume Wake, wanafiki, waongo, watangazao uovu, wenye kuficha Aliyoteremsha Allaah, na kadhalika.

Ama hawa watakaopata laana ya Allaah, basi Aliyetukuka Anatueleza: "Hao ndio Allaah Aliowalaani. Na ambaye Allaah Amemlaani basi hutamwona kuwa na mwenye kumnusuru" (4: 52).

Na Allaah Anajua zaidi

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Hukumu ya kupeleka barua ya posa kwenye kitambaa cheupe

                      Hukumu ya kupeleka barua ya posa kwenye kitambaa cheupe  Hakika ni kuwa posa ilivyofanyika katika Uislamu kuanzia wakati wa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) inafahamika vilivyo. Posa inaweza kuja kutoka kwa mume na watu wake kwa jamaa za mke au mzazi wa mke kumtafutia binti yake mume. Ikiwa wazazi watakwenda kwa wazazi wa mke, baada ya kupeleka maneno, na wazazi wa mke watataka kupatiwa muda wa kufikiria, kufanya shuuraa, kuulizia, kutafiti na baadaye kukubali au kukataa. Ikiwa wamekubali baada ya kumshauri binti  yao  ni vyema mume mtarajiwa aende amuone atakaye kuwa mkewe ili apate kutulia na kuridhika kabla siku ya Nikaah. Binti huyo au wazazi wake wataweka kiwango cha mahari ambacho mume anatakiwa kutoa. Hii njia ya kuweka pesa kwenye kitambaa au bahasha haipo katika mafunzo ya Kiislam, na huenda ni njia ya kitamaduni fulani au itikadi f...

Maana ya Uadilifu

                                         MAANA  YA  UADILIFU  KATIKA  UISLAMU Assallaam  Aleykum  WarahmatulLaah  Wabarakatuh Alhamdu Lillaahi Rabil'aalamiyn) Allaahumma Swalli 'alaa Muhammad wa 'alaa aali Muhammad kamaa Swallayta 'alaa Ibraahiym wa 'alaa aali Ibraahiym wa Baarik 'alaa Muhammad wa 'alaa aali Muhammad kamaa Baarakta 'alaa Ibraahiym wa 'alaa aali Ibraahiym fil'aalamyna Innaka Hamiydun Majiyd. Ndugu zangu Waislam Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) Anasema katika Qur-aan. إِنَّ اللَّـهَ يَأْمُرُ بِالْعَدْلِ وَالْإِحْسَانِ وَإِيتَاءِ ذِي الْقُرْبَىٰ وَيَنْهَىٰ عَنِ الْفَحْشَاءِ وَالْمُنكَرِ وَالْبَغْيِ ۚيَعِظُكُمْ لَعَلَّكُمْ تَذَكَّرُونَ Hakika Allaah Anaamrishia uadilifu na ihsaan na kuwapa (mahitajio na msaada) jamaa wa karibu; na Anakataza machafu na munkari na ukandamizaji. Anakuwaidhini huenda mkapata kukumb...

Viungo vya Mwili vitashuhudia Matendo ya Mwanaadamu Siku ya Qiyaamah

Anasema Allaah  سبحانه وتعالى   ((الْيَوْمَ نَخْتِمُ عَلَى أَفْوَاهِهِمْ وَتُكَلِّمُنَا أَيْدِيهِمْ وَتَشْهَدُ أَرْجُلُهُمْ بِمَا كَانُوا يَكْسِبُونَ)) ((Leo Tunaviziba vinywa vyao, na iseme Nasi mikono  yao , na itoe ushahidi miguu  yao kwa waliyokuwa wakiyachuma))  [Yaasiyn :65 ] Siku ya Qiyaamah viungo vya miili vitakuwa ni vyenye kushuhudia matendo ya binaadamu aliyoyatenda hapa duniani: Mfano mikono itasema: "nimeiba".  Miguu itasema, "nimekwenda sehemu ya ma'asi". Macho yatasema, "nimetazama machafu".  Masikio yatasema, "nimesikiliza nyimbo, au umbea" na kadhalika. Na hivi ndivyo itakavyokuwa hali ya makafiri, wanafiki na wenye kumuasi Mola siku ya kufufuliwa,  watakapokanusha madhambi waliyoyatenda duniani na kuapa kwamba hawakuyafanya, Allaah  سبحانه وتعالى  Atawafunga midomo  yao na kuviamrisha viungo vizungumze:   عن أنس بن مالك قال: كنا عند النبي صلى ال...