Swali
NANI HASWA ANASTAHIKI KUAMBIWA LAANA ZA ALLAAH ZIWE JUU YAKO. JE NI MAKAFIR AU MURTADINA AU WANAAFIQ? JE KUNA LAANA YA MTU MMOJA MMOJA UA WENGI WENGI?
JIBU
NANI HASWA ANASTAHIKI KUAMBIWA LAANA ZA ALLAAH ZIWE JUU YAKO. JE NI MAKAFIR AU MURTADINA AU WANAAFIQ? JE KUNA LAANA YA MTU MMOJA MMOJA UA WENGI WENGI?
JIBU
Shukrani zetu za dhati kwa swali lako kuhusu mas-ala ya laana. Laana si kitu kumpata mtu yeyote yule na hasa akiwa ni Muislamu. Laana kutoka kwa Allaah au Mtume Wake inampata mwenye kuacha amri na yule aliyekengeuka na maagizo yao . Allaah Aliyetukuka na Mtume Muhammad (Swalla Allaahu 'Alayhi wa aalihi wa sallam) wametutajia watu waliteremshiwa laana hizo.
Hebu tutazame baadhi ya mifano:
a) Allaah Aliyetukuka Anasema: "Hakika Allaah Amewalaani makafiri na Amewaandalia Moto mkali" (33: 64).
b) Allaah Aliyetukuka Anasema: "Kama wanafiki na wale wenye maradhi nyoyoni mwao na watangazao uovu mjini, hawataacha upotofu, kwa yakini Tutakusalitisha juu yao , kisha hawatakaa humo karibu yako ila muda kidogo tu. Maluuni (wamelaaniwa) hao popote waonekanapo wakamatwe na wauawe kabisa" (33: 60 – 61).
c) Allaah Aliyetukuka Anasema: "Bila shaka wale wanaomuudhi Allaah na Mtume Wake, Allaah Amewalaani katika dunia na akhera, na Amewaandalia adhabu ifedheheshayo" (33: 57).
d) Anasema tena Aliyetukuka: "Basi kwa sababu ya kuvunja kwao ahadi yao , Tuliwalaani na Tukazifanya nyoyo zao kuwa ngumu …" (5: 13).
e) Anasema tena: "Jua kuwa laana ya Allaah iko juu ya madhalimu" (11: 18).
f) Anasema tena: "Kishaa tuombe kwa unyenyekevu tutake laana ya Allaah iwashukie waongo" (3: 61).
g) Anasema tena Aliyetukuka: "Wamelaaniwa waliokufuru miongoni mwa Bani Israili kwa ulimi wa Daawuud na 'Iysaa mwana wa Maryam kwa sababu waliasi na wakapindukia mipaka" (5: 78).
Tukizitazama Aayah hizi utapata ya kwamba waliolaaniwa na Allaah Aliyetukuka ni wengi miongoni mwao ni makafiri, madhalimu, walioasi, waliotupa mipaka, wanaomuudhi Allaah na Mtume Wake, wanafiki, waongo, watangazao uovu, wenye kuficha Aliyoteremsha Allaah, na kadhalika.
Ama hawa watakaopata laana ya Allaah, basi Aliyetukuka Anatueleza: "Hao ndio Allaah Aliowalaani. Na ambaye Allaah Amemlaani basi hutamwona kuwa na mwenye kumnusuru" (4: 52).
Na Allaah Anajua zaidi
Maoni