Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Damu ya nifasi na hukumu yake

               Damu ya nifasi na hukumu yake




Nifasi ni damu inayotoka ukeni kwa sababu ya kuzaa. Inakuja kwa kuzaa, baada ya kuzaa au siku mbili mpaka tatu kabla ya kuzaa sambamba na machungu. Shaykh-ul-Islaam Ibn Taymiyyah (Rahimahu Allaah) amesema:
“Damu inayotoka wakati machungu yanaanza ni nifasi na haikukomeka kwa siku mbili wala tatu. Katika hali hii machungu ya uzazi ni yale yanayofuatiwa na uzazi. Vinginevyo sio nifasi.”
Wanachuoni wametofautiana juu ya uchache na wingi wake. Shaykh-ul-Islaam Ibn Taymiyyah amesema:
“Nifasi haina muda maalum kwa uchache na wingi wake. Lau tutakadiria kuwa mwanamke atapata damu zaidi ya siku arubaini, sitini au sabini kisha ikakatika, hiyo ni nifasi. Lakini lau itakuja kwa kuendelea itazingatiwa kuwa ni damu isiyokuwa na maana na katika hali hiyo nifasi itakuwa ni yenye kukomeka kwa siku arubaini. Kikomo hichi ndicho kwa jumla kilichokuja katika mapokezi.”Majmuu´-ul-Fataawaa (19/37).



Damu yake ikizidi zaidi ya siku arubaini na amezowea kuwa inakata au akaona alama kuwa inakata karibuni, atasubiri mpaka ikatike. Vinginevyo ataoga baada ya siku arubaini kwa sababu ndivyo ilivyo kwa jumla. Nifasi ikigongana na hedhi atamili upande wa hedhi mpaka ikatike. Baada ya hapo namna hii ndivyo inatakiwa kuwa ada yake anayoitendea kazi katika mustaqbal. Na ikiwa damu itaendelea kutoka, itahesabika kuwa ni damu ya ugonjwa ambayo atatakiwa kutendea kazi hukumu zake baada ya hapo.
Damu ikikatika kabla ya siku arubaini atazingatiwa kuwa ni mtwaharifu. Hivyo atatakiwa kuoga, kuswali, kufunga na kufanya jimaa na mume wake. Lakini hili linahitajia kusitoke damu chini chini kwa muda wa siku moja. Vinginevyo ile damu yenye kukatika haina hukumu yoyote, hivyo ndivyo alivosema Ibn Qudaamah katika “al-Mughniy”.
Nifasi inaanza kuthibiti pale mwanamke anapozaa kitu kinachoashiria mwanaadamu. Lau mimba yake itaharibika na kusiwe na uashiriaji kuwa ni mwanaadamu basi damu yake sio nifasi. Katika hali hiyo ni mshipa uliyopasuka na hivyo anakuwa na hukumu moja kama mwanamke ambaye yuko na damu ya ugonjwa. Muda mdogo kabisa ambapo kipomoko [mtoto tumboni] anaweza kupata umbo la mwanaadamu ni siku thamanini kuanzia siku ujauzito ulipoanza. Muda wake mrefu kabisa ni siku tisini. al-Majd bin Taymiyyah amesema:
“Akipata damu na maumivu kabla ya muda huo, aipuuze. Na ikiwa atapata damu baada ya muda huo, aache kuswali na kufunga. Ikiwa baada ya kuzaa itamdhihirikia kuwa haikuwa kama alivyodhania, atafanya yale aliyoacha kuyafanya. Na itapomdhihirikia alivofanya ndivyo, atachukulia hivo na hatolipa chochote.”Sharh-ul-Iqnaa´.


Na  Allaah  anajua  zaidi

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Mume kunyonya maziwa ya mkewe inafaa...?

Swali Mume kunyonya maziwa (matiti) ya mkewe inafaa...? Jibu Hakuna Uharamu wa Mume  kunyonya matiti ya mke wake.  Allaah(Subhaana wa Taala) Anasema kwamba:  ((نِسَآؤُكُمْ حَرْثٌ لَّكُمْ فَأْتُواْ حَرْثَكُمْ أَنَّى شِئْتُمْ وَقَدِّمُواْ لأَنفُسِكُمْ وَاتَّقُواْ اللّهَ وَاعْلَمُواْ أَنَّكُم مُّلاَقُوهُ وَبَشِّرِ الْمُؤْمِنِينَ)) ((Wake zenu ni kama konde zenu. Basi ziendeeni konde zenu mpendavyo. Lakini jitangulizieni kheri nafsi zenu, na mcheni Allaah , na jueni kuwa hakika nyinyi mtakutana Naye. Na wape bishara njema Waumini)) [2:223] Kwahiyo mwanamke anayo ruhusa ya kumchezea mkewe sehemu yoyote ya mwili wake pamoja na kunyonya maziwa ya mkewe isipokuwa tu Kufanya naye jimai kwa sehemu ya nyuma (liwati). Aayah hii:  “ Wake zenu ni konde kwenu. Basi ziendeeni konde zenu (panapotoka kizazi) vyovyote mpendavyo. “   imeteremka kuhusu Mayahudi waliokuwa wakisema kuwa mwanaume akimuingilia mke wake kupitia upande wa nyuma basi anazaliwa mtoto akiwa ana makengeza. Ndipo i

Kusikiliza Nasheed na Kaswida zenye Muziki na Vinanda

Swali Inafaa Kusikiliza Nasheed na Kaswida zenye  Muziki na Vinanda Jibu  Shukrani zetu za dhati kwa swali lako kuhusu hukumu ya muziki inayotiwa katika Nashiyd na Qaswiydah. Muziki na utumiaji wa ala za muziki ni haramu katika Dini yetu hii, Uislamu. Zifuatazo ni dalili kuhusu hilo:   Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “ Kutakuwa watu katika Ummah wangu watakao halalisha uzinzi, uvaaji wa Hariri, pombe (unywaji) na ma’aazif (ala za muziki) ” (al-Bukhaariy).   Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “ Mwisho wa zama (dunia) kutakuwa na maporomoko ya ardhi, mawe kutoka mbinguni na kugeuza kwa wanyama, wakati ambapo ala za muziki na waimbaji wanawake watakapoenea na pombe kuruhusiwa ” (atw-Twabaraniy).   Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “ Watu katika ummah wangu watakunywa pombe, kuiita kwa jina jingine. Watatiwa furaha kwa uchezaji wa ala za muziki na uimbaji wa wanawake (watakao

Hukumu ya Mke kutoka nyumbani bila Ruksa ya mumewe

Naam shukrani kwa swali lako kuhusu mkeo kutoka bila ya ruhusa yako kwenda katika mishuari zake. Matatizo haya hutokea mara nyingi kwa mke kutokuwa na ufahamu na ujuzi wa Dini ya Kiislamu. Au mara nyingine huwa kweli ana elimu lakini hushindwa kufuata kimatendo kwa sababu moja au nyingine. Au huenda akawa na elimu, lakini akakosa Dini. Kwa ajili hiyo Imaam al-Bukhaariy, ana mlango katika  Swahiyh  yake wenye kichwa cha habari, “ Elimu Kabla Ya ‘Amali ”. Hata hivyo, huenda mtu akawa na elimu lakini akawa hana ‘amali kwa sababu ya kutokuwa na ikhlaasw.   Ni juu ya mke kumtii mumewe katika mambo yasiyo ya maasi, kwani hakuna utiifu katika maasiya. Ikiwa mume hakutoa ruhusa mbali na kuwa yu mbali na mkewe ni wajibu wa mke kutii amri hiyo. Hata hivyo, haifai kwa mume kuweka vikwazo vya kupita kiasi,  kama kumzuia kwenda kwa wazazi wake na mahali ambapo anaweza kupata elimu ya Kidini. Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala) Anasema: “ Wakikutiini, basi msiwatafutie njia ” (an-Nisaa’ [4]: 34). Hii