Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Hali zinazofanana na damu ya ugonjwa

          Hali zinazofanana na damu ya ugonjwa




Mwanamke anaweza kufikwa na mambo yenye kusababisha damu ikatoka ukeni mwake. Mfano wa mambo hayo ni operesheni za kwenye tupu. Ziko aina mbili:
Hali ya kwanza  Anajua kuwa hatopata hedhi tena baada ya operesheni kwa sababu amefanya operesheni ya kuondosha tupu au ovari. 


Mwanamke huyu hana hukumu moja kama mwanamke mwenye damu ya ugonjwa; ana hukumu moja kama mwanamke mtwaharifu anayepata umanjano na maji ya uchafu-uchafu. 


Hivyo atatakiwa kuendelea kuswali, kufunga na kufanya jimaa. Hahitajii kuoga kwa ajili ya damu hii. 


Hata hivyo ni wajibu kwake kujiosha na kusitisha damu kwa kitambaa au kitu mfano wake ili damu isitoke. Kisha atawadhe kwa ajili ya swalah. Asitawadhe isipokuwa baada ya kuingia kwa wakati ikiwa kama swalah hiyo ina wakati maalum kama zile swalah tano. 


Vinginevyo, wakati wa swalah za sunnah zisizokuwa na nyakati maalum, atawadhe pale anapotaka.


Hali ya Pili Hajui kuwa hatopata hedhi baada ya operesheni; kuna uwezekano kabisa akapata hedhi. 


Mwanamke huyu ana hukumu moja kama mwanamke mwenye damu ya ugonjwa. Dalili ya hilo ni maneno ya Mtume Muhammad(Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) kumwambia Faatwimah bint Abiy Hubaysh:
“Wakati hedhi inapokuja acha swalah. Pindi hedhi yako inapoisha jisafishe na uswali.”Al-Bukhaariy (306)


Maneno ya Mtume Muhammad(Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) “Wakati hedhi inapokuja” inafahamisha kuwa hukumu ya damu ya ugonjwa inamhusu yule mwanamke ambaye anaweza kupata hedhi. Ama kuhusu mwanamke ambaye hawezi kupata hedhi, damu yake ni yenye kutoka kwenye mshipa uliyopasuka kwa hali yoyote ile.


Na  Allaah  anajua  zaidi

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Mume kunyonya maziwa ya mkewe inafaa...?

Swali Mume kunyonya maziwa (matiti) ya mkewe inafaa...? Jibu Hakuna Uharamu wa Mume  kunyonya matiti ya mke wake.  Allaah(Subhaana wa Taala) Anasema kwamba:  ((نِسَآؤُكُمْ حَرْثٌ لَّكُمْ فَأْتُواْ حَرْثَكُمْ أَنَّى شِئْتُمْ وَقَدِّمُواْ لأَنفُسِكُمْ وَاتَّقُواْ اللّهَ وَاعْلَمُواْ أَنَّكُم مُّلاَقُوهُ وَبَشِّرِ الْمُؤْمِنِينَ)) ((Wake zenu ni kama konde zenu. Basi ziendeeni konde zenu mpendavyo. Lakini jitangulizieni kheri nafsi zenu, na mcheni Allaah , na jueni kuwa hakika nyinyi mtakutana Naye. Na wape bishara njema Waumini)) [2:223] Kwahiyo mwanamke anayo ruhusa ya kumchezea mkewe sehemu yoyote ya mwili wake pamoja na kunyonya maziwa ya mkewe isipokuwa tu Kufanya naye jimai kwa sehemu ya nyuma (liwati). Aayah hii:  “ Wake zenu ni konde kwenu. Basi ziendeeni konde zenu (panapotoka kizazi) vyovyote mpendavyo. “   imeteremka kuhusu Mayahudi waliokuwa wakisema kuwa mwanaume akimuingilia mke wake kupitia upande wa nyuma basi anazaliwa mtoto akiwa ana makengeza. Ndipo i

Kusikiliza Nasheed na Kaswida zenye Muziki na Vinanda

Swali Inafaa Kusikiliza Nasheed na Kaswida zenye  Muziki na Vinanda Jibu  Shukrani zetu za dhati kwa swali lako kuhusu hukumu ya muziki inayotiwa katika Nashiyd na Qaswiydah. Muziki na utumiaji wa ala za muziki ni haramu katika Dini yetu hii, Uislamu. Zifuatazo ni dalili kuhusu hilo:   Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “ Kutakuwa watu katika Ummah wangu watakao halalisha uzinzi, uvaaji wa Hariri, pombe (unywaji) na ma’aazif (ala za muziki) ” (al-Bukhaariy).   Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “ Mwisho wa zama (dunia) kutakuwa na maporomoko ya ardhi, mawe kutoka mbinguni na kugeuza kwa wanyama, wakati ambapo ala za muziki na waimbaji wanawake watakapoenea na pombe kuruhusiwa ” (atw-Twabaraniy).   Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “ Watu katika ummah wangu watakunywa pombe, kuiita kwa jina jingine. Watatiwa furaha kwa uchezaji wa ala za muziki na uimbaji wa wanawake (watakao

Hukumu ya Mke kutoka nyumbani bila Ruksa ya mumewe

Naam shukrani kwa swali lako kuhusu mkeo kutoka bila ya ruhusa yako kwenda katika mishuari zake. Matatizo haya hutokea mara nyingi kwa mke kutokuwa na ufahamu na ujuzi wa Dini ya Kiislamu. Au mara nyingine huwa kweli ana elimu lakini hushindwa kufuata kimatendo kwa sababu moja au nyingine. Au huenda akawa na elimu, lakini akakosa Dini. Kwa ajili hiyo Imaam al-Bukhaariy, ana mlango katika  Swahiyh  yake wenye kichwa cha habari, “ Elimu Kabla Ya ‘Amali ”. Hata hivyo, huenda mtu akawa na elimu lakini akawa hana ‘amali kwa sababu ya kutokuwa na ikhlaasw.   Ni juu ya mke kumtii mumewe katika mambo yasiyo ya maasi, kwani hakuna utiifu katika maasiya. Ikiwa mume hakutoa ruhusa mbali na kuwa yu mbali na mkewe ni wajibu wa mke kutii amri hiyo. Hata hivyo, haifai kwa mume kuweka vikwazo vya kupita kiasi,  kama kumzuia kwenda kwa wazazi wake na mahali ambapo anaweza kupata elimu ya Kidini. Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala) Anasema: “ Wakikutiini, basi msiwatafutie njia ” (an-Nisaa’ [4]: 34). Hii