Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Kumtaliki mke ambaye mmekataa kufunika uso

Swali


Ipi hukumu kwa mwanamke kuonesha uso wake? Mwanamke ambaye hasikii maneno ya mume wake na anafunua uso wake, je inajuzu kumtaliki?



Jibu


Ndio. Kufuniko uso ni wajibu. 


Ni wajibu kwa mwanamke kufuniko uso wake kwa kuwandio ´Awrah kubwa kwenye mwili wake. Maono hutazama usoni mwa wanawake. Na wala hajulikani mwanamke mzuri kutokana na mbaya isipokuwa ni kwa (kutazama) uso wake. Uso ni fitina kubwa. 


Ni wajibu kwa dada wa Kiislamu kufunika uso wake kutokana na wanaume ambao sio Mahaarim zake. Na wala asijali ushawishi wa washawishi leo hii ambao wanatatiza suala la mwanamke kufuniko uso wake. Hakika Dini yake ndio imemlazimisha hilo. Na kumcha Allaah na kumtii Allaah na Mtume Wake ndio ambao wamemlazimisha.

Asijali upuuzi ambao unaenezwa hivi leo. Kufuniko uso kuna tofauti, kuna kadhaa na kadhaa. Wanachotaka ni mwanamke kuonesha uzuri wake au akae na wanaume naye ni mwenye kuonesha uzuri wa uso wake, wanja wake na vipodozi vya usoni mwake na kukaa nao kama jinsi anavyokaa na Mahaarim zake au mume wake. Haya zimepotea. Na hii ni njia ya kupotea kwa heshima yake na kuchukulia sahali heshima na karama ya mwanamke.
Mwanamke akiasi na akakataa kushikamana na Hijaab, mume wake amtaliki. Kwa kuwa haya ni maasi. Na wala haijuzu kwake kubaki nae hali ya kuwa anaendelea na maasi haya. Isitoshe jambo lingine ni kuwa, atawalea wasichana wake katika kufunua Hijaab. Kwa kuwa wasichana humuiga mama yao.


Mhusika : Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Hukumu ya kupeleka barua ya posa kwenye kitambaa cheupe

                      Hukumu ya kupeleka barua ya posa kwenye kitambaa cheupe  Hakika ni kuwa posa ilivyofanyika katika Uislamu kuanzia wakati wa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) inafahamika vilivyo. Posa inaweza kuja kutoka kwa mume na watu wake kwa jamaa za mke au mzazi wa mke kumtafutia binti yake mume. Ikiwa wazazi watakwenda kwa wazazi wa mke, baada ya kupeleka maneno, na wazazi wa mke watataka kupatiwa muda wa kufikiria, kufanya shuuraa, kuulizia, kutafiti na baadaye kukubali au kukataa. Ikiwa wamekubali baada ya kumshauri binti  yao  ni vyema mume mtarajiwa aende amuone atakaye kuwa mkewe ili apate kutulia na kuridhika kabla siku ya Nikaah. Binti huyo au wazazi wake wataweka kiwango cha mahari ambacho mume anatakiwa kutoa. Hii njia ya kuweka pesa kwenye kitambaa au bahasha haipo katika mafunzo ya Kiislam, na huenda ni njia ya kitamaduni fulani au itikadi f...

Maana ya Uadilifu

                                         MAANA  YA  UADILIFU  KATIKA  UISLAMU Assallaam  Aleykum  WarahmatulLaah  Wabarakatuh Alhamdu Lillaahi Rabil'aalamiyn) Allaahumma Swalli 'alaa Muhammad wa 'alaa aali Muhammad kamaa Swallayta 'alaa Ibraahiym wa 'alaa aali Ibraahiym wa Baarik 'alaa Muhammad wa 'alaa aali Muhammad kamaa Baarakta 'alaa Ibraahiym wa 'alaa aali Ibraahiym fil'aalamyna Innaka Hamiydun Majiyd. Ndugu zangu Waislam Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) Anasema katika Qur-aan. إِنَّ اللَّـهَ يَأْمُرُ بِالْعَدْلِ وَالْإِحْسَانِ وَإِيتَاءِ ذِي الْقُرْبَىٰ وَيَنْهَىٰ عَنِ الْفَحْشَاءِ وَالْمُنكَرِ وَالْبَغْيِ ۚيَعِظُكُمْ لَعَلَّكُمْ تَذَكَّرُونَ Hakika Allaah Anaamrishia uadilifu na ihsaan na kuwapa (mahitajio na msaada) jamaa wa karibu; na Anakataza machafu na munkari na ukandamizaji. Anakuwaidhini huenda mkapata kukumb...

Viungo vya Mwili vitashuhudia Matendo ya Mwanaadamu Siku ya Qiyaamah

Anasema Allaah  سبحانه وتعالى   ((الْيَوْمَ نَخْتِمُ عَلَى أَفْوَاهِهِمْ وَتُكَلِّمُنَا أَيْدِيهِمْ وَتَشْهَدُ أَرْجُلُهُمْ بِمَا كَانُوا يَكْسِبُونَ)) ((Leo Tunaviziba vinywa vyao, na iseme Nasi mikono  yao , na itoe ushahidi miguu  yao kwa waliyokuwa wakiyachuma))  [Yaasiyn :65 ] Siku ya Qiyaamah viungo vya miili vitakuwa ni vyenye kushuhudia matendo ya binaadamu aliyoyatenda hapa duniani: Mfano mikono itasema: "nimeiba".  Miguu itasema, "nimekwenda sehemu ya ma'asi". Macho yatasema, "nimetazama machafu".  Masikio yatasema, "nimesikiliza nyimbo, au umbea" na kadhalika. Na hivi ndivyo itakavyokuwa hali ya makafiri, wanafiki na wenye kumuasi Mola siku ya kufufuliwa,  watakapokanusha madhambi waliyoyatenda duniani na kuapa kwamba hawakuyafanya, Allaah  سبحانه وتعالى  Atawafunga midomo  yao na kuviamrisha viungo vizungumze:   عن أنس بن مالك قال: كنا عند النبي صلى ال...