Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Kumtaliki mke ambaye mmekataa kufunika uso

Swali


Ipi hukumu kwa mwanamke kuonesha uso wake? Mwanamke ambaye hasikii maneno ya mume wake na anafunua uso wake, je inajuzu kumtaliki?



Jibu


Ndio. Kufuniko uso ni wajibu. 


Ni wajibu kwa mwanamke kufuniko uso wake kwa kuwandio ´Awrah kubwa kwenye mwili wake. Maono hutazama usoni mwa wanawake. Na wala hajulikani mwanamke mzuri kutokana na mbaya isipokuwa ni kwa (kutazama) uso wake. Uso ni fitina kubwa. 


Ni wajibu kwa dada wa Kiislamu kufunika uso wake kutokana na wanaume ambao sio Mahaarim zake. Na wala asijali ushawishi wa washawishi leo hii ambao wanatatiza suala la mwanamke kufuniko uso wake. Hakika Dini yake ndio imemlazimisha hilo. Na kumcha Allaah na kumtii Allaah na Mtume Wake ndio ambao wamemlazimisha.

Asijali upuuzi ambao unaenezwa hivi leo. Kufuniko uso kuna tofauti, kuna kadhaa na kadhaa. Wanachotaka ni mwanamke kuonesha uzuri wake au akae na wanaume naye ni mwenye kuonesha uzuri wa uso wake, wanja wake na vipodozi vya usoni mwake na kukaa nao kama jinsi anavyokaa na Mahaarim zake au mume wake. Haya zimepotea. Na hii ni njia ya kupotea kwa heshima yake na kuchukulia sahali heshima na karama ya mwanamke.
Mwanamke akiasi na akakataa kushikamana na Hijaab, mume wake amtaliki. Kwa kuwa haya ni maasi. Na wala haijuzu kwake kubaki nae hali ya kuwa anaendelea na maasi haya. Isitoshe jambo lingine ni kuwa, atawalea wasichana wake katika kufunua Hijaab. Kwa kuwa wasichana humuiga mama yao.


Mhusika : Imaam Swaalih bin Fawzaan al-Fawzaan

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Mume kunyonya maziwa ya mkewe inafaa...?

Swali Mume kunyonya maziwa (matiti) ya mkewe inafaa...? Jibu Hakuna Uharamu wa Mume  kunyonya matiti ya mke wake.  Allaah(Subhaana wa Taala) Anasema kwamba:  ((نِسَآؤُكُمْ حَرْثٌ لَّكُمْ فَأْتُواْ حَرْثَكُمْ أَنَّى شِئْتُمْ وَقَدِّمُواْ لأَنفُسِكُمْ وَاتَّقُواْ اللّهَ وَاعْلَمُواْ أَنَّكُم مُّلاَقُوهُ وَبَشِّرِ الْمُؤْمِنِينَ)) ((Wake zenu ni kama konde zenu. Basi ziendeeni konde zenu mpendavyo. Lakini jitangulizieni kheri nafsi zenu, na mcheni Allaah , na jueni kuwa hakika nyinyi mtakutana Naye. Na wape bishara njema Waumini)) [2:223] Kwahiyo mwanamke anayo ruhusa ya kumchezea mkewe sehemu yoyote ya mwili wake pamoja na kunyonya maziwa ya mkewe isipokuwa tu Kufanya naye jimai kwa sehemu ya nyuma (liwati). Aayah hii:  “ Wake zenu ni konde kwenu. Basi ziendeeni konde zenu (panapotoka kizazi) vyovyote mpendavyo. “   imeteremka kuhusu Mayahudi waliokuwa wakisema kuwa mwanaume akimuingilia mke wake kupitia upande wa nyuma basi anazaliwa mtoto akiwa ana makengeza. Ndipo i

Kusikiliza Nasheed na Kaswida zenye Muziki na Vinanda

Swali Inafaa Kusikiliza Nasheed na Kaswida zenye  Muziki na Vinanda Jibu  Shukrani zetu za dhati kwa swali lako kuhusu hukumu ya muziki inayotiwa katika Nashiyd na Qaswiydah. Muziki na utumiaji wa ala za muziki ni haramu katika Dini yetu hii, Uislamu. Zifuatazo ni dalili kuhusu hilo:   Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “ Kutakuwa watu katika Ummah wangu watakao halalisha uzinzi, uvaaji wa Hariri, pombe (unywaji) na ma’aazif (ala za muziki) ” (al-Bukhaariy).   Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “ Mwisho wa zama (dunia) kutakuwa na maporomoko ya ardhi, mawe kutoka mbinguni na kugeuza kwa wanyama, wakati ambapo ala za muziki na waimbaji wanawake watakapoenea na pombe kuruhusiwa ” (atw-Twabaraniy).   Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “ Watu katika ummah wangu watakunywa pombe, kuiita kwa jina jingine. Watatiwa furaha kwa uchezaji wa ala za muziki na uimbaji wa wanawake (watakao

Hukumu ya Mke kutoka nyumbani bila Ruksa ya mumewe

Naam shukrani kwa swali lako kuhusu mkeo kutoka bila ya ruhusa yako kwenda katika mishuari zake. Matatizo haya hutokea mara nyingi kwa mke kutokuwa na ufahamu na ujuzi wa Dini ya Kiislamu. Au mara nyingine huwa kweli ana elimu lakini hushindwa kufuata kimatendo kwa sababu moja au nyingine. Au huenda akawa na elimu, lakini akakosa Dini. Kwa ajili hiyo Imaam al-Bukhaariy, ana mlango katika  Swahiyh  yake wenye kichwa cha habari, “ Elimu Kabla Ya ‘Amali ”. Hata hivyo, huenda mtu akawa na elimu lakini akawa hana ‘amali kwa sababu ya kutokuwa na ikhlaasw.   Ni juu ya mke kumtii mumewe katika mambo yasiyo ya maasi, kwani hakuna utiifu katika maasiya. Ikiwa mume hakutoa ruhusa mbali na kuwa yu mbali na mkewe ni wajibu wa mke kutii amri hiyo. Hata hivyo, haifai kwa mume kuweka vikwazo vya kupita kiasi,  kama kumzuia kwenda kwa wazazi wake na mahali ambapo anaweza kupata elimu ya Kidini. Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala) Anasema: “ Wakikutiini, basi msiwatafutie njia ” (an-Nisaa’ [4]: 34). Hii