Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Kuoga Hedhi kwa Mwanamke

                                                KUOGA  HEDHI  KWA  MWANAMKE



Assallaam Aleykum WarahmatulLaah Wabarakatuh

BismiLLaah wa AlhamduliLLaah was-Swalaatu wa Salaamu ‘alaa Muhammad wa ‘alaa  aalihi wa Aswhaabihil Kiraam, wa ba’ad.

Naam Siku ya Leo tutakumbushana kuhusiana na Kuoga josho la Hedhi kwa Wanawake, Kwasababu Baadhi ya Wanawake wanafanya Makosa mengi katika Kuoga kwao baada ya kukata kwa Hedhi na KOSA kubwa baadhi wa wanawake HAWAOGI  KICHWANI hiyo wengi wanaswali hali ya kuwa bado hawapo TWAHARA (Yaani bado wapo na Hedhi na wengine wanakuwa na JANABA kwa sababu hawaogi KICHWANI).

Ni wajibu kwa mwanamke mwenye hedhi pale anapotwaharika kuosha mwili wake wote. Mtume Muhammad(Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amesema kumwambia Faatwimah bint Abiy Hubaysh:
“Wakati hedhi inapokuja acha swalah. Pindi hedhi yako inapoisha jisafishe na uswali.”Al-Bukhaariy (306)


Uwajibu wa chini kabisa katika kuoga ni kulowa mwili mzima ikiwa ni pamoja na mashina ya kichwa. 

Hata hivyo bora zaidi ni iwe kwa mujibu wa Hadiyth ya Mtume Muhammad(Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) wakati Asmaa´ bint Shakl alipomuuliza namna gani mwanamke ataoga baada ya kutwaharika na hedhi:
“Mmoja wenu atachukua maji na mkunazi wake ajitwaharishe vizuri. Kisha ajimiminie maji kichwani mwake na akisugue kichwa msuguo wa nguvu mpaka afikilie mashina ya kichwa chake. Halafu atamwagia juu yake maji. Baada ya hapo atachukua kitambaa kilichotiwa miski ajitwaharishe nacho.” Asmaa´ akasema: “Atajitwaharisha nacho vipi?” Akasema (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam): “Ametakasika Allaah!” ´Aaishah akamwambia: “Utapitisha mahali palipokuwa damu.”Muslim (332).



Sio wajibu kufumua nywele ikiwa hazikukazwa sana kiasi cha kwamba kunachelea juu yake maji yasifike kwenye mashina ya nywele. Muslim amepokea kupitia kwa Umm Salamah (Radhiya Allaahu ´anhaa) ya kwamba alimwambia Mtume Muhammad(Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
Mimi ni mwanamke mwenye misuko. Je, nizifumue kwa ajili ya kuoga janaba?” Katika upokezi mwingine imekuja “kwa ajili ya kuoga hedhi na janaba? Akasema: “Hapana. Hakika yakutosha kumwagia kichwa chako mateko matatu ya maji kisha utajimiminia maji mwilini na hapo unakuwa umetwaharika.”Muslim (330).


Mwanamke akitwaharika hedhi yake katikati ya wakati wa swalah basi ni wajibu kwake kuharakisha kuoga ili aweze kuwahi kutekeleza swalah kwa wakati wake.
Na akiwa katika safari na hana maji au ana maji lakini anaogopa madhara endapo atayatumia au ana maradhi na maji yanaweza kumdhuru, basi badala yake atafanya Tayammum mpaka pale kizuizi kitapoondoka. Baada ya hapo ni wajibu kwake kuoga.
Kuna wanawake ambao wanatwaharika na hedhi katikati ya wakati wa swalah na wanachelewesha kuoga mpaka wakati wa swalah nyingine. Hoja yao ni kwamba hawawezi kujitwaharisha vizuri katika wakati huu. Hii sio hoja wala udhuru. Anaweza kuoga kwa wajibu wa chini kabisa na kuswali kwa wakati. Kisha pale atapopata wakati wa kutosha anaweza kujitwaharisha vizuri.



Rejea Kitaab Ad-Dimaa' at-Twabiy´iyyah lin-Nisaa' 



Ukiwa na Maoni/Ushauri au Swali Tafadhali wasiliana na Imaam Masjid Tawbah kwa simu +255714974397



Na  Allaah  anajua  zaidi

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Mume kunyonya maziwa ya mkewe inafaa...?

Swali Mume kunyonya maziwa (matiti) ya mkewe inafaa...? Jibu Hakuna Uharamu wa Mume  kunyonya matiti ya mke wake.  Allaah(Subhaana wa Taala) Anasema kwamba:  ((نِسَآؤُكُمْ حَرْثٌ لَّكُمْ فَأْتُواْ حَرْثَكُمْ أَنَّى شِئْتُمْ وَقَدِّمُواْ لأَنفُسِكُمْ وَاتَّقُواْ اللّهَ وَاعْلَمُواْ أَنَّكُم مُّلاَقُوهُ وَبَشِّرِ الْمُؤْمِنِينَ)) ((Wake zenu ni kama konde zenu. Basi ziendeeni konde zenu mpendavyo. Lakini jitangulizieni kheri nafsi zenu, na mcheni Allaah , na jueni kuwa hakika nyinyi mtakutana Naye. Na wape bishara njema Waumini)) [2:223] Kwahiyo mwanamke anayo ruhusa ya kumchezea mkewe sehemu yoyote ya mwili wake pamoja na kunyonya maziwa ya mkewe isipokuwa tu Kufanya naye jimai kwa sehemu ya nyuma (liwati). Aayah hii:  “ Wake zenu ni konde kwenu. Basi ziendeeni konde zenu (panapotoka kizazi) vyovyote mpendavyo. “   imeteremka kuhusu Mayahudi waliokuwa wakisema kuwa mwanaume akimuingilia mke wake kupitia upande wa nyuma basi anazaliwa mtoto akiwa ana makengeza. Ndipo i

Kusikiliza Nasheed na Kaswida zenye Muziki na Vinanda

Swali Inafaa Kusikiliza Nasheed na Kaswida zenye  Muziki na Vinanda Jibu  Shukrani zetu za dhati kwa swali lako kuhusu hukumu ya muziki inayotiwa katika Nashiyd na Qaswiydah. Muziki na utumiaji wa ala za muziki ni haramu katika Dini yetu hii, Uislamu. Zifuatazo ni dalili kuhusu hilo:   Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “ Kutakuwa watu katika Ummah wangu watakao halalisha uzinzi, uvaaji wa Hariri, pombe (unywaji) na ma’aazif (ala za muziki) ” (al-Bukhaariy).   Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “ Mwisho wa zama (dunia) kutakuwa na maporomoko ya ardhi, mawe kutoka mbinguni na kugeuza kwa wanyama, wakati ambapo ala za muziki na waimbaji wanawake watakapoenea na pombe kuruhusiwa ” (atw-Twabaraniy).   Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “ Watu katika ummah wangu watakunywa pombe, kuiita kwa jina jingine. Watatiwa furaha kwa uchezaji wa ala za muziki na uimbaji wa wanawake (watakao

Hukumu ya Mke kutoka nyumbani bila Ruksa ya mumewe

Naam shukrani kwa swali lako kuhusu mkeo kutoka bila ya ruhusa yako kwenda katika mishuari zake. Matatizo haya hutokea mara nyingi kwa mke kutokuwa na ufahamu na ujuzi wa Dini ya Kiislamu. Au mara nyingine huwa kweli ana elimu lakini hushindwa kufuata kimatendo kwa sababu moja au nyingine. Au huenda akawa na elimu, lakini akakosa Dini. Kwa ajili hiyo Imaam al-Bukhaariy, ana mlango katika  Swahiyh  yake wenye kichwa cha habari, “ Elimu Kabla Ya ‘Amali ”. Hata hivyo, huenda mtu akawa na elimu lakini akawa hana ‘amali kwa sababu ya kutokuwa na ikhlaasw.   Ni juu ya mke kumtii mumewe katika mambo yasiyo ya maasi, kwani hakuna utiifu katika maasiya. Ikiwa mume hakutoa ruhusa mbali na kuwa yu mbali na mkewe ni wajibu wa mke kutii amri hiyo. Hata hivyo, haifai kwa mume kuweka vikwazo vya kupita kiasi,  kama kumzuia kwenda kwa wazazi wake na mahali ambapo anaweza kupata elimu ya Kidini. Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala) Anasema: “ Wakikutiini, basi msiwatafutie njia ” (an-Nisaa’ [4]: 34). Hii