Ruka hadi kwenye maudhui makuu

kuvumilia maudhi ya wanawake wanapokuwa wajawazito

Swali: Mimi nilioa na tahamaki mke wangu akaniomba talaka kwa hoja kwamba hakuishi maisha ya starehe vile alivyotarajia. Mimi ni kijana na mwanafunzi vilevile ambaye hali yangu ni ya kawaida. Kuniomba kwake talaka kulikuwa ni pasi na haki na mimi sikuwa na nia ya kumtaliki kwa kuwa alikuwa ni mjamzito. Je, akiniomba talaka ni haki kwangu kurudishiwa mahari? Isitoshe mahari yenyewe ilikuwa ni misaada kutoka kwa watu. Je, ikiwa atanipa mahari hayo nina haki ya kuzitumia au nitatakiwa kuzirudisha kule nilikozichukua pamoja na kuwa mimi ni mwenye madeni tele yasiyojua yeyote isipokuwa Allaah pekee.



Jibu: Katika hali hii mwanaume akiweza kuwa na subira na asimjibu ndio bora zaidi. Hili ni kwa sababu mbili:


Ya kwanza: Baadhi ya wanawake wanapokuwa na mimba wanawachukia waume zao. Wanawachukia waume zao hata kama ameishi naye miaka mingi. Kwa hivyo awe na subira juu yake mpaka yataisha. Huenda akarudi katika hali yake ya kawaida na yakamuondoka yaliyomkereta moyoni mwake.

Ya pili: Huenda baada ya kujifungua akaelewa kuwa anatakiwa kubaki kwa mume wake na hatimaye yakamwondoka yaliyomo moyoni mwake.
Mimi naona kwamba ikiwa amemridhia tabia na dini yake basi awe na subira juu yake na amfanyie wepesi mpaka migogoro iishe. Baada ya yeye kujifungua ataangaliwa kama kweli anaona hawezi kubaki basi ni sawa akaomba haki yake. Mwanamke wa Thaabit bin Qays (Radhiya Allaahu ´anhaa) alikuja kwa Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) na kumwambia:
“Ee Mtume wa Allaah! Sina cha kumtia dosari Thaabit bin Qays si katika tabia wala dini. Lakini mimi nachelea kufuru katika Uislamu.”
Kumesemwa tabia na dini. Isitoshe huyu ni miongoni mwa wale ambao Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) amemshuhudilia Pepo.
Aliposema kuwa anachelea kufuru katika Uislamu bi maana kwamba hawezi. Hapo ndipo alipomwambia (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam):
“Je, utaweza kumrudishia bustani yake?” Akajibu: “Ndio.” Mtume (Swalla Allaahu ´alayhi wa sallam) akamwita na kumwambia: “Chukua bustani yako na umtaliki.”
Akachukua bustani yake na kumtaliki. Kwa hivyo tunamshauri mwanaume huyu asubiri mpaka pale mwanamke huyu atapojifungua. Huenda vilevile akabadilika baada tu ya kujifungua midhali ameridhika na dini na tabia yake. Vinginevyo mambo yasipobadilika basi hakuna ubaya kwake akamuomba haki yake yote aliyompa kuanzia mahari, zawadi na vinginevyo. 


Ikiwa baadaye atarudi kwake basi hivyo vitu ni vya mwanaume kwa kuwa alivichukua kwa haki. Ikiwa alivichukua kwa haki yake basi yeye ndiye mwenye kuvimiliki. Wakati mwanaume alipovichukua kwa ajili ya ndoa amekuwa ni mwenye kuvimiliki. Vikirudi kwake basi ni miliki yake. Katika hali hii sio wajibu kwake kuvirudisha kwa yule aliyevichukua kutoka kwake.



Rejea al-Liqaa' ash-Shahriy (31)

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Mume kunyonya maziwa ya mkewe inafaa...?

Swali Mume kunyonya maziwa (matiti) ya mkewe inafaa...? Jibu Hakuna Uharamu wa Mume  kunyonya matiti ya mke wake.  Allaah(Subhaana wa Taala) Anasema kwamba:  ((نِسَآؤُكُمْ حَرْثٌ لَّكُمْ فَأْتُواْ حَرْثَكُمْ أَنَّى شِئْتُمْ وَقَدِّمُواْ لأَنفُسِكُمْ وَاتَّقُواْ اللّهَ وَاعْلَمُواْ أَنَّكُم مُّلاَقُوهُ وَبَشِّرِ الْمُؤْمِنِينَ)) ((Wake zenu ni kama konde zenu. Basi ziendeeni konde zenu mpendavyo. Lakini jitangulizieni kheri nafsi zenu, na mcheni Allaah , na jueni kuwa hakika nyinyi mtakutana Naye. Na wape bishara njema Waumini)) [2:223] Kwahiyo mwanamke anayo ruhusa ya kumchezea mkewe sehemu yoyote ya mwili wake pamoja na kunyonya maziwa ya mkewe isipokuwa tu Kufanya naye jimai kwa sehemu ya nyuma (liwati). Aayah hii:  “ Wake zenu ni konde kwenu. Basi ziendeeni konde zenu (panapotoka kizazi) vyovyote mpendavyo. “   imeteremka kuhusu Mayahudi waliokuwa wakisema kuwa mwanaume akimuingilia mke wake kupitia upande wa nyuma basi anazaliwa mtoto akiwa ana makengeza. Ndipo i

Kusikiliza Nasheed na Kaswida zenye Muziki na Vinanda

Swali Inafaa Kusikiliza Nasheed na Kaswida zenye  Muziki na Vinanda Jibu  Shukrani zetu za dhati kwa swali lako kuhusu hukumu ya muziki inayotiwa katika Nashiyd na Qaswiydah. Muziki na utumiaji wa ala za muziki ni haramu katika Dini yetu hii, Uislamu. Zifuatazo ni dalili kuhusu hilo:   Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “ Kutakuwa watu katika Ummah wangu watakao halalisha uzinzi, uvaaji wa Hariri, pombe (unywaji) na ma’aazif (ala za muziki) ” (al-Bukhaariy).   Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “ Mwisho wa zama (dunia) kutakuwa na maporomoko ya ardhi, mawe kutoka mbinguni na kugeuza kwa wanyama, wakati ambapo ala za muziki na waimbaji wanawake watakapoenea na pombe kuruhusiwa ” (atw-Twabaraniy).   Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “ Watu katika ummah wangu watakunywa pombe, kuiita kwa jina jingine. Watatiwa furaha kwa uchezaji wa ala za muziki na uimbaji wa wanawake (watakao

Hukumu ya Mke kutoka nyumbani bila Ruksa ya mumewe

Naam shukrani kwa swali lako kuhusu mkeo kutoka bila ya ruhusa yako kwenda katika mishuari zake. Matatizo haya hutokea mara nyingi kwa mke kutokuwa na ufahamu na ujuzi wa Dini ya Kiislamu. Au mara nyingine huwa kweli ana elimu lakini hushindwa kufuata kimatendo kwa sababu moja au nyingine. Au huenda akawa na elimu, lakini akakosa Dini. Kwa ajili hiyo Imaam al-Bukhaariy, ana mlango katika  Swahiyh  yake wenye kichwa cha habari, “ Elimu Kabla Ya ‘Amali ”. Hata hivyo, huenda mtu akawa na elimu lakini akawa hana ‘amali kwa sababu ya kutokuwa na ikhlaasw.   Ni juu ya mke kumtii mumewe katika mambo yasiyo ya maasi, kwani hakuna utiifu katika maasiya. Ikiwa mume hakutoa ruhusa mbali na kuwa yu mbali na mkewe ni wajibu wa mke kutii amri hiyo. Hata hivyo, haifai kwa mume kuweka vikwazo vya kupita kiasi,  kama kumzuia kwenda kwa wazazi wake na mahali ambapo anaweza kupata elimu ya Kidini. Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala) Anasema: “ Wakikutiini, basi msiwatafutie njia ” (an-Nisaa’ [4]: 34). Hii