Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Mashahidi katika talaka

                      Mashahidi katika talaka




Allaah (Subhaana wa Ta´ala) amesema kwamba:
فَإِذَا بَلَغْنَ أَجَلَهُنَّ فَأَمْسِكُوهُنَّ بِمَعْرُوفٍ أَوْ فَارِقُوهُنَّ بِمَعْرُوفٍ وَأَشْهِدُوا ذَوَيْ عَدْلٍ مِّنكُمْ وَأَقِيمُوا الشَّهَادَةَ لِلَّـهِ
“atakapokaribia kufikia muda wao, basi wazuieni kwa wema au farikianeni nao kwa wema na mshuhudishe mashahidi wawili wenye uadilifu katika nyinyi na simamisheni ushahidi kwa ajili ya Allaah. “65:02


Ameamrisha kuwepo mashahidi wakati mume atapomrejea mke. Ummah umeafikiana juu ya kwamba mashahidi wanatakiwa kuwepo. Wako waliosema kwamba maamrisho ni kwa njia ya uwajibu na wengine wamesema maamrisho ni kwa njia ya mapendekezo tu.
Baadhi ya watu wamedhani kuwa ushahidi ni kwa ajili ya talaka na kwamba talaka haipiti isipokuwa mpaka kuwepo mashahidi. Haya yanakwenda kinyume na maafikiano, Qur-aan na Sunnah. Hakuna yeyote katika wanachuoni wanaotambulika aliyesema hivo. Mara ya kwanza talaka iliruhusiwa kwa kuwepo mashahidi. Kuliamrishwa kuwepo kwa mashahidi wakati aliposema:
فَإِذَا بَلَغْنَ أَجَلَهُنَّ فَأَمْسِكُوهُنَّ بِمَعْرُوفٍ
“atakapokaribia kufikia muda wao, basi wazuieni kwa wema.”
Makusudio ya mtengamano katika Aayah ni kumwacha pindi eda yake itakapokwisha. Hii sio talaka, kumrejea wala kumuoa. Ni lazima wawepo mashahidi juu ya mambo haya matatu kwa maafikiano ya waislamu.
Hekima ya hilo ni kwamba shaytwaan anaweza kumshawishi mwanaume ambapo akamtaliki mwanamke kwa mara ya tatu na akalificha hilo pasi na yeyote kujua. Matokeo yake mwanamke huyo akabaki kuishi pamoja naye ilihali amekwishaharamika kwake. Ndipo Allaah akaamrisha pindi atapomrejea awashuhudishe mashahidi ili watu wajue ni mara ngapi amemwacha.
Hilo ni tofauti na talaka. Pindi mwanaume atapomtaliki mke wake itawadhihirikia watu ya kwamba sio mwanamke wake tena.


Rejea Kitab Majmuu´-ul-Fataawaa (33/33-34)

Na Allaah  anajua  zaidi

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Hukumu ya kupeleka barua ya posa kwenye kitambaa cheupe

                      Hukumu ya kupeleka barua ya posa kwenye kitambaa cheupe  Hakika ni kuwa posa ilivyofanyika katika Uislamu kuanzia wakati wa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) inafahamika vilivyo. Posa inaweza kuja kutoka kwa mume na watu wake kwa jamaa za mke au mzazi wa mke kumtafutia binti yake mume. Ikiwa wazazi watakwenda kwa wazazi wa mke, baada ya kupeleka maneno, na wazazi wa mke watataka kupatiwa muda wa kufikiria, kufanya shuuraa, kuulizia, kutafiti na baadaye kukubali au kukataa. Ikiwa wamekubali baada ya kumshauri binti  yao  ni vyema mume mtarajiwa aende amuone atakaye kuwa mkewe ili apate kutulia na kuridhika kabla siku ya Nikaah. Binti huyo au wazazi wake wataweka kiwango cha mahari ambacho mume anatakiwa kutoa. Hii njia ya kuweka pesa kwenye kitambaa au bahasha haipo katika mafunzo ya Kiislam, na huenda ni njia ya kitamaduni fulani au itikadi f...

Maana ya Uadilifu

                                         MAANA  YA  UADILIFU  KATIKA  UISLAMU Assallaam  Aleykum  WarahmatulLaah  Wabarakatuh Alhamdu Lillaahi Rabil'aalamiyn) Allaahumma Swalli 'alaa Muhammad wa 'alaa aali Muhammad kamaa Swallayta 'alaa Ibraahiym wa 'alaa aali Ibraahiym wa Baarik 'alaa Muhammad wa 'alaa aali Muhammad kamaa Baarakta 'alaa Ibraahiym wa 'alaa aali Ibraahiym fil'aalamyna Innaka Hamiydun Majiyd. Ndugu zangu Waislam Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) Anasema katika Qur-aan. إِنَّ اللَّـهَ يَأْمُرُ بِالْعَدْلِ وَالْإِحْسَانِ وَإِيتَاءِ ذِي الْقُرْبَىٰ وَيَنْهَىٰ عَنِ الْفَحْشَاءِ وَالْمُنكَرِ وَالْبَغْيِ ۚيَعِظُكُمْ لَعَلَّكُمْ تَذَكَّرُونَ Hakika Allaah Anaamrishia uadilifu na ihsaan na kuwapa (mahitajio na msaada) jamaa wa karibu; na Anakataza machafu na munkari na ukandamizaji. Anakuwaidhini huenda mkapata kukumb...

Viungo vya Mwili vitashuhudia Matendo ya Mwanaadamu Siku ya Qiyaamah

Anasema Allaah  سبحانه وتعالى   ((الْيَوْمَ نَخْتِمُ عَلَى أَفْوَاهِهِمْ وَتُكَلِّمُنَا أَيْدِيهِمْ وَتَشْهَدُ أَرْجُلُهُمْ بِمَا كَانُوا يَكْسِبُونَ)) ((Leo Tunaviziba vinywa vyao, na iseme Nasi mikono  yao , na itoe ushahidi miguu  yao kwa waliyokuwa wakiyachuma))  [Yaasiyn :65 ] Siku ya Qiyaamah viungo vya miili vitakuwa ni vyenye kushuhudia matendo ya binaadamu aliyoyatenda hapa duniani: Mfano mikono itasema: "nimeiba".  Miguu itasema, "nimekwenda sehemu ya ma'asi". Macho yatasema, "nimetazama machafu".  Masikio yatasema, "nimesikiliza nyimbo, au umbea" na kadhalika. Na hivi ndivyo itakavyokuwa hali ya makafiri, wanafiki na wenye kumuasi Mola siku ya kufufuliwa,  watakapokanusha madhambi waliyoyatenda duniani na kuapa kwamba hawakuyafanya, Allaah  سبحانه وتعالى  Atawafunga midomo  yao na kuviamrisha viungo vizungumze:   عن أنس بن مالك قال: كنا عند النبي صلى ال...