Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Tafsiyr ya Aayah “Na Arshi Yake Ikawa Katika Maji”

SWALI



Naomba maelezo na mafundisho kutoka katika aya "wakaana arshuhuu ala-lmaai" 



MAJIBU



Shukrani zetu za dhati kwa swali lako kuhusu Arshi ya Allaah Aliyetukuka.

Aayah hiyo inapatikana katika Surah Huud (11). Aayah yenyewe inasema hivi:

وَهُوَ الَّذِي خَلَق السَّمَاوَاتِ وَالأَرْضَ فِي سِتَّةِ أَيَّامٍ وَكَانَ عَرْشُهُ عَلَى الْمَاء لِيَبْلُوَكُمْ أَيُّكُمْ أَحْسَنُ عَمَلاً وَلَئِن قُلْتَ إِنَّكُم مَّبْعُوثُونَ مِن بَعْدِ الْمَوْتِ لَيَقُولَنَّ الَّذِينَ كَفَرُواْ إِنْ هَذَا إِلاَّ سِحْرٌ مُّبِين

Maana ya Aayah hiyo ni:
“Na Yeye Ndiye Aliyeumba mbingu na ardhi katika siku sita; na ikawa ‘Arshi Yake juu ya maji; (kakuumbeni) ili Akujaribuni nani kati yenu mwenye ‘amali nzuri zaidi. Na kama ukisema: “Nyinyi mtafufuliwa baada ya mauti”; bila shaka watasema wale waliokufuru: “Hakika haya si chochote isipokuwa ni sihiri bayana."[11: 7].

Hebu tutazame hii ibara imefasiriwa vipi na Wanachuoni wetu wa tafsiyr.

Ibn Kathiyr naye amesema yafuatayo: “Allaah Aliyetukuka, Anatueleza kuhusu uwezo Wake na nguvu Zake, kuwa Ameumba mbingu na ardhi kwa siku sita. Ametaja kuwa 'Arsh Yake ilikuwa juu ya maji kabla ya hapo kama alivyonukuu Ahmad kutoka kwa ‘Imran Huswayn (Radhiya Allaahu ‘anhu) aliyesema: Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alisema: ‘Kubalini bishara, enyi Bani Tamiym!’ Wakasema: ‘Hakika umetuletea bishara njema na tayari umetupatia’. Kisha akasema (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam): ‘Kubalini bishara, enyi watu wa Yemen!’ Wakasema: ‘Tumekubali. Hivyo tujulishe kuhusu mwanzo wa mambo na ilivyokuwa’. Akasema (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam): ‘Allaah Alikuwepo kabla ya chochote na kiti Chake cha enzi kilikuwa juu ya maji. Aliandika kwenye ubao uliohifadhiwa kila jambo’ …”

Muslim naye amenukuu kutoka kwa ‘Abdullaah bin ‘Amru bin al-‘Aasw (Radhiya Allaahu ‘anhuma) kuwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Hakika Allaah Alikuduria riziki za viumbe wote kabla ya kuumba mbingu na ardhi kwa miaka elfu khamsini na 'Arsh Yake ilikuwa juu ya maji”.


Na Al-Bukhaariy amemkuu Abu Hurayrah (Radhiya Allaahu ‘anhu) kuwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Je mumeona kilichotumiwa kuanzia kuumbwa mbingu na ardhi? Hakiko hicho (kilichotumiwa) hakipunguzi kwa kilichomo Mkononi Mwake wa kuume (hata chembe) na 'Arsh Yake ilikuwa juu ya maji. Mkononi Mwake kulikuwa na mizani, Aliyokuwa Akiishusha na kuinyanyua” [juzuu ya pili].


Al-Qurtwubiy amesema: “Allaah Amebainisha kuwa kuumbwa kwa 'Arsh na maji kulikuwa kabla ya kuumbwa kwa mbingu na ardhi” [juzuu 5, uk. 8]

Na Allaah Anajua zaidi

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Mume kunyonya maziwa ya mkewe inafaa...?

Swali Mume kunyonya maziwa (matiti) ya mkewe inafaa...? Jibu Hakuna Uharamu wa Mume  kunyonya matiti ya mke wake.  Allaah(Subhaana wa Taala) Anasema kwamba:  ((نِسَآؤُكُمْ حَرْثٌ لَّكُمْ فَأْتُواْ حَرْثَكُمْ أَنَّى شِئْتُمْ وَقَدِّمُواْ لأَنفُسِكُمْ وَاتَّقُواْ اللّهَ وَاعْلَمُواْ أَنَّكُم مُّلاَقُوهُ وَبَشِّرِ الْمُؤْمِنِينَ)) ((Wake zenu ni kama konde zenu. Basi ziendeeni konde zenu mpendavyo. Lakini jitangulizieni kheri nafsi zenu, na mcheni Allaah , na jueni kuwa hakika nyinyi mtakutana Naye. Na wape bishara njema Waumini)) [2:223] Kwahiyo mwanamke anayo ruhusa ya kumchezea mkewe sehemu yoyote ya mwili wake pamoja na kunyonya maziwa ya mkewe isipokuwa tu Kufanya naye jimai kwa sehemu ya nyuma (liwati). Aayah hii:  “ Wake zenu ni konde kwenu. Basi ziendeeni konde zenu (panapotoka kizazi) vyovyote mpendavyo. “   imeteremka kuhusu Mayahudi waliokuwa wakisema kuwa mwanaume akimuingilia mke wake kupitia upande wa nyuma basi anazaliwa mtoto akiwa ana makengeza. Ndipo i

Kusikiliza Nasheed na Kaswida zenye Muziki na Vinanda

Swali Inafaa Kusikiliza Nasheed na Kaswida zenye  Muziki na Vinanda Jibu  Shukrani zetu za dhati kwa swali lako kuhusu hukumu ya muziki inayotiwa katika Nashiyd na Qaswiydah. Muziki na utumiaji wa ala za muziki ni haramu katika Dini yetu hii, Uislamu. Zifuatazo ni dalili kuhusu hilo:   Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “ Kutakuwa watu katika Ummah wangu watakao halalisha uzinzi, uvaaji wa Hariri, pombe (unywaji) na ma’aazif (ala za muziki) ” (al-Bukhaariy).   Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “ Mwisho wa zama (dunia) kutakuwa na maporomoko ya ardhi, mawe kutoka mbinguni na kugeuza kwa wanyama, wakati ambapo ala za muziki na waimbaji wanawake watakapoenea na pombe kuruhusiwa ” (atw-Twabaraniy).   Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “ Watu katika ummah wangu watakunywa pombe, kuiita kwa jina jingine. Watatiwa furaha kwa uchezaji wa ala za muziki na uimbaji wa wanawake (watakao

Hukumu ya Mke kutoka nyumbani bila Ruksa ya mumewe

Naam shukrani kwa swali lako kuhusu mkeo kutoka bila ya ruhusa yako kwenda katika mishuari zake. Matatizo haya hutokea mara nyingi kwa mke kutokuwa na ufahamu na ujuzi wa Dini ya Kiislamu. Au mara nyingine huwa kweli ana elimu lakini hushindwa kufuata kimatendo kwa sababu moja au nyingine. Au huenda akawa na elimu, lakini akakosa Dini. Kwa ajili hiyo Imaam al-Bukhaariy, ana mlango katika  Swahiyh  yake wenye kichwa cha habari, “ Elimu Kabla Ya ‘Amali ”. Hata hivyo, huenda mtu akawa na elimu lakini akawa hana ‘amali kwa sababu ya kutokuwa na ikhlaasw.   Ni juu ya mke kumtii mumewe katika mambo yasiyo ya maasi, kwani hakuna utiifu katika maasiya. Ikiwa mume hakutoa ruhusa mbali na kuwa yu mbali na mkewe ni wajibu wa mke kutii amri hiyo. Hata hivyo, haifai kwa mume kuweka vikwazo vya kupita kiasi,  kama kumzuia kwenda kwa wazazi wake na mahali ambapo anaweza kupata elimu ya Kidini. Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala) Anasema: “ Wakikutiini, basi msiwatafutie njia ” (an-Nisaa’ [4]: 34). Hii