Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Tafsiyr ya Aayah “Na Arshi Yake Ikawa Katika Maji”

SWALI



Naomba maelezo na mafundisho kutoka katika aya "wakaana arshuhuu ala-lmaai" 



MAJIBU



Shukrani zetu za dhati kwa swali lako kuhusu Arshi ya Allaah Aliyetukuka.

Aayah hiyo inapatikana katika Surah Huud (11). Aayah yenyewe inasema hivi:

وَهُوَ الَّذِي خَلَق السَّمَاوَاتِ وَالأَرْضَ فِي سِتَّةِ أَيَّامٍ وَكَانَ عَرْشُهُ عَلَى الْمَاء لِيَبْلُوَكُمْ أَيُّكُمْ أَحْسَنُ عَمَلاً وَلَئِن قُلْتَ إِنَّكُم مَّبْعُوثُونَ مِن بَعْدِ الْمَوْتِ لَيَقُولَنَّ الَّذِينَ كَفَرُواْ إِنْ هَذَا إِلاَّ سِحْرٌ مُّبِين

Maana ya Aayah hiyo ni:
“Na Yeye Ndiye Aliyeumba mbingu na ardhi katika siku sita; na ikawa ‘Arshi Yake juu ya maji; (kakuumbeni) ili Akujaribuni nani kati yenu mwenye ‘amali nzuri zaidi. Na kama ukisema: “Nyinyi mtafufuliwa baada ya mauti”; bila shaka watasema wale waliokufuru: “Hakika haya si chochote isipokuwa ni sihiri bayana."[11: 7].

Hebu tutazame hii ibara imefasiriwa vipi na Wanachuoni wetu wa tafsiyr.

Ibn Kathiyr naye amesema yafuatayo: “Allaah Aliyetukuka, Anatueleza kuhusu uwezo Wake na nguvu Zake, kuwa Ameumba mbingu na ardhi kwa siku sita. Ametaja kuwa 'Arsh Yake ilikuwa juu ya maji kabla ya hapo kama alivyonukuu Ahmad kutoka kwa ‘Imran Huswayn (Radhiya Allaahu ‘anhu) aliyesema: Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) alisema: ‘Kubalini bishara, enyi Bani Tamiym!’ Wakasema: ‘Hakika umetuletea bishara njema na tayari umetupatia’. Kisha akasema (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam): ‘Kubalini bishara, enyi watu wa Yemen!’ Wakasema: ‘Tumekubali. Hivyo tujulishe kuhusu mwanzo wa mambo na ilivyokuwa’. Akasema (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam): ‘Allaah Alikuwepo kabla ya chochote na kiti Chake cha enzi kilikuwa juu ya maji. Aliandika kwenye ubao uliohifadhiwa kila jambo’ …”

Muslim naye amenukuu kutoka kwa ‘Abdullaah bin ‘Amru bin al-‘Aasw (Radhiya Allaahu ‘anhuma) kuwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Hakika Allaah Alikuduria riziki za viumbe wote kabla ya kuumba mbingu na ardhi kwa miaka elfu khamsini na 'Arsh Yake ilikuwa juu ya maji”.


Na Al-Bukhaariy amemkuu Abu Hurayrah (Radhiya Allaahu ‘anhu) kuwa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Je mumeona kilichotumiwa kuanzia kuumbwa mbingu na ardhi? Hakiko hicho (kilichotumiwa) hakipunguzi kwa kilichomo Mkononi Mwake wa kuume (hata chembe) na 'Arsh Yake ilikuwa juu ya maji. Mkononi Mwake kulikuwa na mizani, Aliyokuwa Akiishusha na kuinyanyua” [juzuu ya pili].


Al-Qurtwubiy amesema: “Allaah Amebainisha kuwa kuumbwa kwa 'Arsh na maji kulikuwa kabla ya kuumbwa kwa mbingu na ardhi” [juzuu 5, uk. 8]

Na Allaah Anajua zaidi

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Hukumu ya kupeleka barua ya posa kwenye kitambaa cheupe

                      Hukumu ya kupeleka barua ya posa kwenye kitambaa cheupe  Hakika ni kuwa posa ilivyofanyika katika Uislamu kuanzia wakati wa Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) inafahamika vilivyo. Posa inaweza kuja kutoka kwa mume na watu wake kwa jamaa za mke au mzazi wa mke kumtafutia binti yake mume. Ikiwa wazazi watakwenda kwa wazazi wa mke, baada ya kupeleka maneno, na wazazi wa mke watataka kupatiwa muda wa kufikiria, kufanya shuuraa, kuulizia, kutafiti na baadaye kukubali au kukataa. Ikiwa wamekubali baada ya kumshauri binti  yao  ni vyema mume mtarajiwa aende amuone atakaye kuwa mkewe ili apate kutulia na kuridhika kabla siku ya Nikaah. Binti huyo au wazazi wake wataweka kiwango cha mahari ambacho mume anatakiwa kutoa. Hii njia ya kuweka pesa kwenye kitambaa au bahasha haipo katika mafunzo ya Kiislam, na huenda ni njia ya kitamaduni fulani au itikadi f...

Maana ya Uadilifu

                                         MAANA  YA  UADILIFU  KATIKA  UISLAMU Assallaam  Aleykum  WarahmatulLaah  Wabarakatuh Alhamdu Lillaahi Rabil'aalamiyn) Allaahumma Swalli 'alaa Muhammad wa 'alaa aali Muhammad kamaa Swallayta 'alaa Ibraahiym wa 'alaa aali Ibraahiym wa Baarik 'alaa Muhammad wa 'alaa aali Muhammad kamaa Baarakta 'alaa Ibraahiym wa 'alaa aali Ibraahiym fil'aalamyna Innaka Hamiydun Majiyd. Ndugu zangu Waislam Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) Anasema katika Qur-aan. إِنَّ اللَّـهَ يَأْمُرُ بِالْعَدْلِ وَالْإِحْسَانِ وَإِيتَاءِ ذِي الْقُرْبَىٰ وَيَنْهَىٰ عَنِ الْفَحْشَاءِ وَالْمُنكَرِ وَالْبَغْيِ ۚيَعِظُكُمْ لَعَلَّكُمْ تَذَكَّرُونَ Hakika Allaah Anaamrishia uadilifu na ihsaan na kuwapa (mahitajio na msaada) jamaa wa karibu; na Anakataza machafu na munkari na ukandamizaji. Anakuwaidhini huenda mkapata kukumb...

Viungo vya Mwili vitashuhudia Matendo ya Mwanaadamu Siku ya Qiyaamah

Anasema Allaah  سبحانه وتعالى   ((الْيَوْمَ نَخْتِمُ عَلَى أَفْوَاهِهِمْ وَتُكَلِّمُنَا أَيْدِيهِمْ وَتَشْهَدُ أَرْجُلُهُمْ بِمَا كَانُوا يَكْسِبُونَ)) ((Leo Tunaviziba vinywa vyao, na iseme Nasi mikono  yao , na itoe ushahidi miguu  yao kwa waliyokuwa wakiyachuma))  [Yaasiyn :65 ] Siku ya Qiyaamah viungo vya miili vitakuwa ni vyenye kushuhudia matendo ya binaadamu aliyoyatenda hapa duniani: Mfano mikono itasema: "nimeiba".  Miguu itasema, "nimekwenda sehemu ya ma'asi". Macho yatasema, "nimetazama machafu".  Masikio yatasema, "nimesikiliza nyimbo, au umbea" na kadhalika. Na hivi ndivyo itakavyokuwa hali ya makafiri, wanafiki na wenye kumuasi Mola siku ya kufufuliwa,  watakapokanusha madhambi waliyoyatenda duniani na kuapa kwamba hawakuyafanya, Allaah  سبحانه وتعالى  Atawafunga midomo  yao na kuviamrisha viungo vizungumze:   عن أنس بن مالك قال: كنا عند النبي صلى ال...