Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Talaka za Bid´ah

Swali


Tumejua kupitia barnamiji hii ya kwamba haipiti Talaka kwa mwenye hedhi na mwenye mimba. Je, ni kuwa haipiti kabisa au inapita baada ya Twahara?



Jibu



Talaka ya mwenye hedhi haipiti kutokana na kauli sahihi (yenye nguvu) ya wanachuoni, tofauti na kauli ya jamhuri. Jamhuri ya wanachuoni wanaona kuwa inapita. Hali kadhalika kwa mwenye nifasi. 


Lakini kauli ya sahihi katika kauli za wanachuoni, na ndio waliokuwa wakifutu baadhi ya Taabi´iyn na Ibn ´Umar (Radhiya Allaahu ´anhumaa) na akaichagua Shayk-ul-Islaam bin Taymiyyah, mwanafunzi wake Ibn al-Qayyim na kundi katika wanachuoni, kuwa Talaka hii haipiti. Kwa kuwa inakwenda kinyume na Shari´ah ya Allaah, kwa kuwa Allaah Kawekea Shari´ah kumtaliki mwanamke katika hali ya Twahara ya nifasi, hedhi na katika Twahara ambayo mume wake hakumjamii. 


Hii ndio Talaka ya Kishari´ah. Akimtaliki katika hedhi, nifasi au Twahara ambayo amemjamii, Talaka hii ni Bid´ah na wala haipiti kutokana na kauli ya sahihi ya wanachuoni. Kwa Kauli ya Allaah (Jalla wa ´Alaa):
يَا أَيُّهَا النَّبِيُّ إِذَا طَلَّقْتُمُ النِّسَاءَ فَطَلِّقُوهُنَّ لِعِدَّتِهِنَّ
“Ee Nabii! Mtakapowataliki wanawake, basi watalikini katika wakati wa eda (twahara na si katika hedhi) zao.” (65:01)
Bi maana katika Twahara ya jimaa. Namna hii ndivyo walivyosema wanachuoni kuhusu (maana ya) “watalikini katika wakati wa eda.” Wawe Twahara hawakuingiliwa au wawe na ujauzito. 



Hii ndio Talaka ya katika eda. Ama Talaka ya mjamzito wanachuoni wanaona kuwa inapita, na mwenye kusema kuwa haipiti kakosea. Talaka ya mjamzito inapita kwa wanachuoni, Talaka isiyopita ni ya mwenye hedhi na nifasi na Twahara ambayo mwanamke kaingiliwa na hakujadhihiri mimba yake. 



Talaka hizi (sampuli tatu) hazipiti kutokana na kauli ya sahihi ya wanachuoni, kwa kuwa zinakhalifu na Shari´ah ya Allaah na vile vile ni katika hali ambayo haikuwekwa Talaka kama tulivyotangulia kusema. Na baadhi ya ´Awwaam wanastaajabu na kusema Talaka ya mjamzito haipiti, hili ni kosa. Hii ni katika kauli za ´Awwaam zisizokuwa na asli katika Shari´ah wala maneno ya wanachuoni. Mjamzito Talaka inapita. Ni wajibu kujua hilo.

Rejea Nuur ´alaad-Darb

Na  Allaah anajua  zaidi

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Mume kunyonya maziwa ya mkewe inafaa...?

Swali Mume kunyonya maziwa (matiti) ya mkewe inafaa...? Jibu Hakuna Uharamu wa Mume  kunyonya matiti ya mke wake.  Allaah(Subhaana wa Taala) Anasema kwamba:  ((نِسَآؤُكُمْ حَرْثٌ لَّكُمْ فَأْتُواْ حَرْثَكُمْ أَنَّى شِئْتُمْ وَقَدِّمُواْ لأَنفُسِكُمْ وَاتَّقُواْ اللّهَ وَاعْلَمُواْ أَنَّكُم مُّلاَقُوهُ وَبَشِّرِ الْمُؤْمِنِينَ)) ((Wake zenu ni kama konde zenu. Basi ziendeeni konde zenu mpendavyo. Lakini jitangulizieni kheri nafsi zenu, na mcheni Allaah , na jueni kuwa hakika nyinyi mtakutana Naye. Na wape bishara njema Waumini)) [2:223] Kwahiyo mwanamke anayo ruhusa ya kumchezea mkewe sehemu yoyote ya mwili wake pamoja na kunyonya maziwa ya mkewe isipokuwa tu Kufanya naye jimai kwa sehemu ya nyuma (liwati). Aayah hii:  “ Wake zenu ni konde kwenu. Basi ziendeeni konde zenu (panapotoka kizazi) vyovyote mpendavyo. “   imeteremka kuhusu Mayahudi waliokuwa wakisema kuwa mwanaume akimuingilia mke wake kupitia upande wa nyuma basi anazaliwa mtoto akiwa ana makengeza. Ndipo i

Kusikiliza Nasheed na Kaswida zenye Muziki na Vinanda

Swali Inafaa Kusikiliza Nasheed na Kaswida zenye  Muziki na Vinanda Jibu  Shukrani zetu za dhati kwa swali lako kuhusu hukumu ya muziki inayotiwa katika Nashiyd na Qaswiydah. Muziki na utumiaji wa ala za muziki ni haramu katika Dini yetu hii, Uislamu. Zifuatazo ni dalili kuhusu hilo:   Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “ Kutakuwa watu katika Ummah wangu watakao halalisha uzinzi, uvaaji wa Hariri, pombe (unywaji) na ma’aazif (ala za muziki) ” (al-Bukhaariy).   Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “ Mwisho wa zama (dunia) kutakuwa na maporomoko ya ardhi, mawe kutoka mbinguni na kugeuza kwa wanyama, wakati ambapo ala za muziki na waimbaji wanawake watakapoenea na pombe kuruhusiwa ” (atw-Twabaraniy).   Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “ Watu katika ummah wangu watakunywa pombe, kuiita kwa jina jingine. Watatiwa furaha kwa uchezaji wa ala za muziki na uimbaji wa wanawake (watakao

Hukumu ya Mke kutoka nyumbani bila Ruksa ya mumewe

Naam shukrani kwa swali lako kuhusu mkeo kutoka bila ya ruhusa yako kwenda katika mishuari zake. Matatizo haya hutokea mara nyingi kwa mke kutokuwa na ufahamu na ujuzi wa Dini ya Kiislamu. Au mara nyingine huwa kweli ana elimu lakini hushindwa kufuata kimatendo kwa sababu moja au nyingine. Au huenda akawa na elimu, lakini akakosa Dini. Kwa ajili hiyo Imaam al-Bukhaariy, ana mlango katika  Swahiyh  yake wenye kichwa cha habari, “ Elimu Kabla Ya ‘Amali ”. Hata hivyo, huenda mtu akawa na elimu lakini akawa hana ‘amali kwa sababu ya kutokuwa na ikhlaasw.   Ni juu ya mke kumtii mumewe katika mambo yasiyo ya maasi, kwani hakuna utiifu katika maasiya. Ikiwa mume hakutoa ruhusa mbali na kuwa yu mbali na mkewe ni wajibu wa mke kutii amri hiyo. Hata hivyo, haifai kwa mume kuweka vikwazo vya kupita kiasi,  kama kumzuia kwenda kwa wazazi wake na mahali ambapo anaweza kupata elimu ya Kidini. Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala) Anasema: “ Wakikutiini, basi msiwatafutie njia ” (an-Nisaa’ [4]: 34). Hii