Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Faida ya Taqwa (Uchaji Allaah)

                                                                       FAIDA  YA  TAQWA



 Anasema Allaah  سبحانه وتعالى  

((...  وَمَن يَتَّقِ اللَّهَ يَجْعَل لَّهُ مَخْرَجًا ))   ((  وَيَرْزُقْهُ مِنْ حَيْثُ لاَ يَحْتَسِبُ ..))

((Na atakayekuwa na taqwa (kumcha Allaah)  Humtengezea njia ya kutokea))  ((Na Humruzuku kwa njia asiziotegemea)) [At-Twalaaq: 2-3]


Hizo ni kauli za Allaah سبحانه وتعالى katika Kitabu Chake Qur-aan Tukufu, ambayo Uongofu kamili wa mwanaadamu.  Kitabu kisichokuwa na shaka wala kufikiwa na  ubatilifu  mbele yake wala nyuma yake, kimeteremshwa na Mwenye Hikma  Ahimidawaye. 


Maneno yake Allaah سبحانه وتعالى ni kuli ya  haki (ni kweli) kama Anavyosema


((وَمَنْ أَصْدَقُ مِنَ اللّهِ حَدِيثًا))


((Na ni nani msema kweli kuliko Allaah?)) [An-Nisaa: 87] 


Aayah hiyo ya juu imetanguliza sharti mwanzo kwa kupatikana yale Aliyoyaahidi Allaah سبحانه وتعالى.  Sharti hiyo ni kuwa na taqwa (Kumcha Allaah) ili jazaa yake ni Kujaaliwa njia (upenyo, kivuko) na Kuruzukiwa pale asipotegemea.  Iitakapopatikana sharti hiyo, ndipo yatapatikana hayo yaliyoahidiwa.


Tujiulize swali, vipi kufikia taqwa? Au Nini maana ya taqwa?  Jibu ni katika sentensi fupi iliyokamilisha kila kheri. Nayo ni "Kutekeleza yaliyoamrishwa na Allaah سبحانه وتعالى na Mtume صلى الله عليه وآله وسلم  na kujiepusha makatazoYao na kubakia katika mipaka".  Hapo ndipo itakapopatikana taqwa.  Na kuwa na taqwa ndio sababu ya furaha na kufuzu duniani na akhera,  na pia ni sababu ya kuondoshewa shida na dhiki zote.


Taqwa ni wasiya wa watu wa mwanzo na wa mwisho na Mtume صلى الله عليه وآله وسلم aliwausia Maswahaba wake wapenzi :


 عن أبي ذَرٍّ جُنْدُب بِن جُنَادَة، وأبي عبد الرحمن مُعَاذ بِن جَبَلٍ رضي الله عنهما، عن رسول الله صلى الله عليه وسلم قال: ((اتق الله حيثما كنت، وأَتْبِعِ السَّيئةَ الحسنةَ تَمْحُها، وخالقِ الناسَ بخُلُقٍ حسنٍ)).  رَوَاهُ التِّرْمِذِيُّ   وَقَالَ: حَدِيثٌ حَسَنٌ، وَفِي بَعْضِ النُّسَخِ: حَسَنٌ صَحِيحٌ.


Kutoka kwa Abu Dharr Jundub Ibn Junaada na Abu Abdur Rahmaan Mu'adh Ibn Jabal رضي الله عنهما  ambao wamemnukuu   Mtume صلى الله عليه وسلمakisema: ((Mche Allaah popote pale ulipo, na fuatisha kitendo kibaya kwa kitendo kizuri kitafuta (kitendo kibaya), na ishi na watu kwa uzuri)) [At-Tirmidhiy na kasema kuwa ni Hadiyth Hasan na katika maandiko mengine imesemwa kuwa ni Hasan Swahiyh]



Na Taqwa haihitajii kuhakikishwa kuwa mahali fulani au wakati fulani, bali taqwa ya hakika  ni pale mtu anapokua yuko peke yake, akajiepusha na yaliyo haraam japokuwa hakuna mtu anayemuona. Na ndipo aliposema Mtume صلى الله عليه وآله وسلم kuwa 'Taqwa iko hapa' akiashiria kwenye kifua chake palipo na moyo na kusema mara tatu.

Maoni

badrzaeske alisema…
Best of 2021 - Casino Gaming | GIBC
Top Online 위닉스 먹튀 Casinos 2021 ✓ List of the Top Gambling Casinos 1xbet online ✓ Play 토토 사이트 해킹 now at the world's top casino 토토가입머니 for real mgm바카라작업 cash with GIBC.

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Mume kunyonya maziwa ya mkewe inafaa...?

Swali Mume kunyonya maziwa (matiti) ya mkewe inafaa...? Jibu Hakuna Uharamu wa Mume  kunyonya matiti ya mke wake.  Allaah(Subhaana wa Taala) Anasema kwamba:  ((نِسَآؤُكُمْ حَرْثٌ لَّكُمْ فَأْتُواْ حَرْثَكُمْ أَنَّى شِئْتُمْ وَقَدِّمُواْ لأَنفُسِكُمْ وَاتَّقُواْ اللّهَ وَاعْلَمُواْ أَنَّكُم مُّلاَقُوهُ وَبَشِّرِ الْمُؤْمِنِينَ)) ((Wake zenu ni kama konde zenu. Basi ziendeeni konde zenu mpendavyo. Lakini jitangulizieni kheri nafsi zenu, na mcheni Allaah , na jueni kuwa hakika nyinyi mtakutana Naye. Na wape bishara njema Waumini)) [2:223] Kwahiyo mwanamke anayo ruhusa ya kumchezea mkewe sehemu yoyote ya mwili wake pamoja na kunyonya maziwa ya mkewe isipokuwa tu Kufanya naye jimai kwa sehemu ya nyuma (liwati). Aayah hii:  “ Wake zenu ni konde kwenu. Basi ziendeeni konde zenu (panapotoka kizazi) vyovyote mpendavyo. “   imeteremka kuhusu Mayahudi waliokuwa wakisema kuwa mwanaume akimuingilia mke wake kupitia upande wa nyuma basi anazaliwa mtoto akiwa ana makengeza. Ndipo i

Kusikiliza Nasheed na Kaswida zenye Muziki na Vinanda

Swali Inafaa Kusikiliza Nasheed na Kaswida zenye  Muziki na Vinanda Jibu  Shukrani zetu za dhati kwa swali lako kuhusu hukumu ya muziki inayotiwa katika Nashiyd na Qaswiydah. Muziki na utumiaji wa ala za muziki ni haramu katika Dini yetu hii, Uislamu. Zifuatazo ni dalili kuhusu hilo:   Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “ Kutakuwa watu katika Ummah wangu watakao halalisha uzinzi, uvaaji wa Hariri, pombe (unywaji) na ma’aazif (ala za muziki) ” (al-Bukhaariy).   Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “ Mwisho wa zama (dunia) kutakuwa na maporomoko ya ardhi, mawe kutoka mbinguni na kugeuza kwa wanyama, wakati ambapo ala za muziki na waimbaji wanawake watakapoenea na pombe kuruhusiwa ” (atw-Twabaraniy).   Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “ Watu katika ummah wangu watakunywa pombe, kuiita kwa jina jingine. Watatiwa furaha kwa uchezaji wa ala za muziki na uimbaji wa wanawake (watakao

Amana katika Uislamu

                                                   AMANA  KATIKA  UISLAMU Assallaaam Aleykum Sallaam WarahmatulLaah Wabarakatuh Baada ya kumhimidi na kumshukuru Allaah Aliyetukuka Ambaye Ametuneemesha na fursa hii ya kukutana ili kunasihiana na kukumbushana. Swalah na salamu zimfikiye hashimu, Muhammad (Swalla Allaahu ‘Alayhi wa aalihi wa sallam), Maswahaba zake, ahli zake na Waumini wote mpaka Siku ya Qiyaamah. Maudhui yetu ya leo ni muhimu sana katika zama zetu za leo na matatizo mengi tunakumbana nayo kwa sababu ya kukosekana. Hiyo ni maudhui ya amana. Huenda mmoja wetu akauliza: Amana ina maana gani katika Dini yetu ya kweli? Suala hilo limejibiwa na Imaam al-Qurtwubiy (Allaah Amrehemu) pale aliposema: Amana inajumlisha shughuli zote za Kidini. Amana ndio faradhi ambazo kwayo Allaah Aliyetukuka Amewapatia waja Wake. Na wametofautiana katika tafsili, hivyo kukawa na kauli nyingi. Baadhi yake ni: Pakasemwa: Hiyo ni kuweka amana ya mali na nyengineyo.