Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Hukmu ya Muislamu Anayejiua

                                                     Hukmu ya Muislamu Anayejiua





Uislamu umetukataza kujiua na yeyote mwenye kujiua atakuwa ametenda madhambi makubwa na yatakayomsababishia kuingia motoni na kuharamishiwa pepo. Isitoshe, ataadhibiwa kwa chombo kilekile alichotumia kujiulia. Allaah Aliyetukuka Atuepushe kabisa na balaa hilo la kujinyonga au kujiua kwa njia yoyote ile.

Anasema Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kutoka katika Hadiyth iliyosimuliwa na Abu Hurayrah,
"Yeyote atakayejitupa kutoka mlimani na kujiua, atatupwa ndani ya moto milele. Atakayekunywa sumu na kujiua, basi atatupwa motoni na huko atakuwa akiinywa hiyo sumu milele. Atakayejiua kwa kipande cha chuma, atatiwamotoni akiwa na kipande hicho cha chuma akijitwanga nacho tumboni kwake humo motoni milele." Al-Bukhaariy na Muslim

Kadhaalika, mtu anayejiua, au jambazi, au aliyefariki kwa kutumia madawa ya kulevya au kuuza, mlevi n.k. wote hao watatengwa kuswaliwa na Viongozi wa Dini ili iwe funzo kwa wale wenye tabia hizo waweze kujiepusha na maovu hayo. Lakini, hata hivyo, wanaweza kuswaliwa na watu wa kawaida.


HUKUMU  YA  KUJIUA KWA SABABU YA MATESO NA MITIHANI YA KIDUNIA


Tufahamu kuwa mitihani katika hii dunia na haswa kwa Muumini ni lazima. Na kila mmoja anapimwa na Allaah Aliyetukuka kwa kiasi cha Imani yake. Allaah Aliyetukuka Anasema:
Je! Wanadhani watu wataachwa kwa kuwa wanasema: Tumeamini. Nao wasijaribiwe? Hakika Tuliwajaribu waliokuwa kabla yao, na kwa yakini Allaah Atawatambulisha walio wa kweli na Atawatambulisha walio waongo” [Al-Ankabut [29]: 2 – 3].
Na tena:
Mnadhani kuwa mtaingia Peponi, bila ya kukujieni kama yaliyo wajia wale waliopita kabla yenu? Iliwapata shida na madhara na wakatikiswa hata Mtume na walio amini pamoja naye wakasema: Lini nusura ya Allaah itakuja? Jueni kuwa nusura ya Allaah ipo karibu” [Al-Baqarah [2]: 214].

Mtume (Swalla Allaahu ‘Alayhi wa aalihi wa sallam) anatuelezea kuwaMuislamu mzuri ni yule anaponeemeshwa hushukuru na hiyo ikawa ni kheri kwake na anapopata mitihani husubiri, na hiyo pia ikawa ni kheri kwake. [Muslim].

Kujiua kwa sababu ya mateso ni miongoni mwa madhambi makubwa inayompeleka mwenye kufanya kitendo hicho motoni. Kwa hivyo, mwenye kujiua makaazi yake siku ya Kiyama ni Motoni.  Dalili kutoka Hadiyth zifuatazo:

Kutoka kwa Jundab kwamba Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Mtu alifikwa na maafa ya majeraha akajiua, hivyo Allaah Amesema: Mja wangu amejisababisha kufa mwenyewe kwa kuharakiza, hivyo Nimemharamisha Pepo.” [Al-Bukhaary]

Kutoka kwa Abu Hurayrah (Radhiya Allaahu ‘anhu) kwamba Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema:  “Yeyote atakayejitupa kutoka mlimani na kujiua ataingia motoni akiuangukia ambako ataishi humo milele. Na yeyote atakayekunywa sumu na kujiua nafsi yake, atabeba sumu yake mkononi mwake huku anainywa motoni ambako ataishi milele. Na yeyote atakayejiua kwa silaha ya chuma, atabeba silaha yake mkononi mwake na huku anajichinja tumbo lake motoni ambako ataishi milele.” [Al-Bukhaariy]


Anas bin Maalik ameripoti kuwaMtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Asiombe mmoja wenu kufa kwa sababu ya shida iliyomfika, bali ikiwa hakupata msaada aombe (du’aa) “Ee Allaah, nijaalie niishi ikiwa uhai kwangu ni kheri na nipe mauti ikiwa mauti kwangu ni kheri kwangu” [Muslim]

Kadhaalika, mtu anayejiua, au jambazi, au aliyefariki kwa kutumia madawa ya kulevya au kuuza, mlevi n.k. wote hao watatengwa kuswaliwa na Viongozi wa Dini ili iwe funzo kwa wale wenye tabia hizo waweze kujiepusha na maovu hayo. Lakini, hata hivyo, wanaweza kuswaliwa na watu wa kawaida.


Allaah Aliyetukuka Atuepushe na balaa la kujiua na mabalaa mengine kama hayo.


Na Allaah Anajua zaidi.

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Mume kunyonya maziwa ya mkewe inafaa...?

Swali Mume kunyonya maziwa (matiti) ya mkewe inafaa...? Jibu Hakuna Uharamu wa Mume  kunyonya matiti ya mke wake.  Allaah(Subhaana wa Taala) Anasema kwamba:  ((نِسَآؤُكُمْ حَرْثٌ لَّكُمْ فَأْتُواْ حَرْثَكُمْ أَنَّى شِئْتُمْ وَقَدِّمُواْ لأَنفُسِكُمْ وَاتَّقُواْ اللّهَ وَاعْلَمُواْ أَنَّكُم مُّلاَقُوهُ وَبَشِّرِ الْمُؤْمِنِينَ)) ((Wake zenu ni kama konde zenu. Basi ziendeeni konde zenu mpendavyo. Lakini jitangulizieni kheri nafsi zenu, na mcheni Allaah , na jueni kuwa hakika nyinyi mtakutana Naye. Na wape bishara njema Waumini)) [2:223] Kwahiyo mwanamke anayo ruhusa ya kumchezea mkewe sehemu yoyote ya mwili wake pamoja na kunyonya maziwa ya mkewe isipokuwa tu Kufanya naye jimai kwa sehemu ya nyuma (liwati). Aayah hii:  “ Wake zenu ni konde kwenu. Basi ziendeeni konde zenu (panapotoka kizazi) vyovyote mpendavyo. “   imeteremka kuhusu Mayahudi waliokuwa wakisema kuwa mwanaume akimuingilia mke wake kupitia upande wa nyuma basi anazaliwa mtoto akiwa ana makengeza. Ndipo i

Kusikiliza Nasheed na Kaswida zenye Muziki na Vinanda

Swali Inafaa Kusikiliza Nasheed na Kaswida zenye  Muziki na Vinanda Jibu  Shukrani zetu za dhati kwa swali lako kuhusu hukumu ya muziki inayotiwa katika Nashiyd na Qaswiydah. Muziki na utumiaji wa ala za muziki ni haramu katika Dini yetu hii, Uislamu. Zifuatazo ni dalili kuhusu hilo:   Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “ Kutakuwa watu katika Ummah wangu watakao halalisha uzinzi, uvaaji wa Hariri, pombe (unywaji) na ma’aazif (ala za muziki) ” (al-Bukhaariy).   Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “ Mwisho wa zama (dunia) kutakuwa na maporomoko ya ardhi, mawe kutoka mbinguni na kugeuza kwa wanyama, wakati ambapo ala za muziki na waimbaji wanawake watakapoenea na pombe kuruhusiwa ” (atw-Twabaraniy).   Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “ Watu katika ummah wangu watakunywa pombe, kuiita kwa jina jingine. Watatiwa furaha kwa uchezaji wa ala za muziki na uimbaji wa wanawake (watakao

Hukumu ya Mke kutoka nyumbani bila Ruksa ya mumewe

Naam shukrani kwa swali lako kuhusu mkeo kutoka bila ya ruhusa yako kwenda katika mishuari zake. Matatizo haya hutokea mara nyingi kwa mke kutokuwa na ufahamu na ujuzi wa Dini ya Kiislamu. Au mara nyingine huwa kweli ana elimu lakini hushindwa kufuata kimatendo kwa sababu moja au nyingine. Au huenda akawa na elimu, lakini akakosa Dini. Kwa ajili hiyo Imaam al-Bukhaariy, ana mlango katika  Swahiyh  yake wenye kichwa cha habari, “ Elimu Kabla Ya ‘Amali ”. Hata hivyo, huenda mtu akawa na elimu lakini akawa hana ‘amali kwa sababu ya kutokuwa na ikhlaasw.   Ni juu ya mke kumtii mumewe katika mambo yasiyo ya maasi, kwani hakuna utiifu katika maasiya. Ikiwa mume hakutoa ruhusa mbali na kuwa yu mbali na mkewe ni wajibu wa mke kutii amri hiyo. Hata hivyo, haifai kwa mume kuweka vikwazo vya kupita kiasi,  kama kumzuia kwenda kwa wazazi wake na mahali ambapo anaweza kupata elimu ya Kidini. Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala) Anasema: “ Wakikutiini, basi msiwatafutie njia ” (an-Nisaa’ [4]: 34). Hii