Ruka hadi kwenye maudhui makuu

Swalaatul-ghayb (Kumswalia Swalah Maiti Aliyefia Mbali)

                       Swalaatul-ghayb (Kumswalia Swalah Maiti Aliyefia Mbali)



SWALI

Je inafaa kwa waisilam kumsalia maiti ikiwa hayupo mbele yao?  Ama kuwa nchi nyengine au sehemu nyengine mji ulele.

   
JIBU

Wametofautiana Maulamaa kuhusu Swalaatul-Ghayb (Swalaah ya Jeneza ya Asiyekuwepo. 


Imaam Ash-Shaafi’iy na Imaam Ahmad wamekwenda kwa mtazamo wa kuwa jambo hili lafaa kishari’ah kwa kutolea dalili hoja zao kwa Hadityh hii: 


Kutoka kwa Abuu Hurayrah  (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)    alitangaza kifo cha Mfalme An-Najjaashiy siku aliyokufa akatoka nao katika Mswalla akapanga safu nao akapiga Takbira nne.   [Al-Bukhaariy na Muslim].

Alimuombolezea An-Najaashiy katika siku ailiyofariki, na akatoka na Maswahaba zake kwenda kumswalia katika kiwanja, kisha akawatangulia kwenye safu na akapiga takbira nne. 

Inajulikana kuwa huyu An-Najaashiy alikuwa ni Mfalme kule Uhabashi (Ethiopia) alikuwa Mkiristo mwanzo na kisha alisilimu kwa siri na alipofariki Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)  alijulishwa kifo chake na akamswalia.

Ama Imaam Abuu Haniyfah na Imaam Maalik wamekwenda katika msimamo kuwa Swalaatul-ghayb haifai ki-shariy’ah. Na hoja yao ni jawabu lao kuhusiana na kisa cha An Najaashiy kuswaliwa na Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) ni jambo lenye kumhusu (Khususiyaat) Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) pekee. Na inawezekana kuwa kitanda cha An-Najaashiy kilinyanyuliwa hadi kwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)   na akamswalia mbele ya hadhara.

Na wakasema (upande wa Mahanafi na Maalik) kuwa, Haikupokelewa kuwa wakati wa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)  alikuwa akiwaswalia wale wanaokufa ambao wako mbali naye. Na wakasema kuiacha (huko kumswalia aliyefariki mbali) ni Sunnah. Na hata kuifanya kwake ni Sunnah, na hakuna njia yoyote inayowezekana ya wale baada ya Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kubebewa na kuletewa kitanda cha Maiti aliyefia mbali ili waiswalie! Kwa hiyo kufanya Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)  hivyo kulikuwa ni Makhsusi tu kwake yeye.

Na Imaam Ahmad katika moja ya riwaya zake mbili, ameonelea ikiwa ni mtu muhimu katika Uislam, au mwenye mchango mkubwa katika Diyn, anaweza kuswaliwa. Kasema, “Atakapokufa mtu mwema, aswaliwe.” Na muono huu pia baadhi ya ‘Ulamaa wa karibuni wameufuata.

Ama kilicho bora zaidi kwa muono wa ‘Ulamaa  wakubwa, ni kuwa, Swalaatul-Ghayb inamstahikia kishariy’ah yule ambaye amefariki katika nchi au eneo ambalo hakuna wa kumswalia (Hakuswaliwa huko alipofia). Ama yule aliyefariki na akaswaliwa huko alipofariki, basi hakuna haja ya kumswalia Swalaatul-ghayb. Na hili ndilo walilolikubali na kulipitisha ‘Ulamaa  na Ma-Imaam wakubwa wa zamani na wa sasa. Ndio msimamo wa   Al-Khatwaabiy, Ar-Rawayaaniy na amelieleza hilo Imaam Abuu Daawuwd katika Sunnan, mlango wa ‘Swalaah kwa Muislam aliye katika ardhi nyingine palipo na Washirikina.’

Na huu ndio msimamo wa Shaykhul-Islaam Ibn Taymiyyah na mwanafunzi wake hodari Ibnul Qayyim, Kasema Imaam Ibnul Qayyim katika kitabu chake maarufu cha Zaadul Ma’ad: “…Na amesema Shaykhul-Islaam Ibn Taymiyyah: Kilicho sahihi ni kuwa, ikiwa Aliyeghibu (maiti) aliyefia katika nchi au sehemu ambayo hakuswaliwa, basi ataswaliwa Swalaatul-ghayb. Kama alivyoswali Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kumswalia An-Najaashiy kwani yeye alikufa akiwa miongoni Makafiri na hakuswaliwa. Na kama angekuwa ameswaliwa huko alipokuwa, basi asingeswaliwa tena kwani ile faradhi ya kumswalia maiti ingekuwa ishatekelezwa.”

Na kauli hiyo ya Shaykhul-Islaam kutoka kwa mwanafunzi wake, ndio pia katika riwaayah nyingine ya Imaam Ahmad.

Na muono huu unatiliwa nguvu sana na matukio wakati wa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na Makhalifa wake waongofu kwani walikufa wengi miongoni mwa Maswahaba katika sehemu na maeneo mbalimbali nje ya pale alipokuwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)  na hata Makhalifa wake baadaye, na hakuna ushahidi unaoonyesha kuwa hao waliokufa maeneo ya mbali, waliswaliwa Swalaatul-ghayb. Na asili katika masuala ya ‘Ibaadah ni ‘Tawqiyfiyah’ kukifu hadi papatikane dalili ya kishariy’ah kuhusu kufanyika au kutofanyika kwa jambo.

Na Allaah Anajua zaidi

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

Mume kunyonya maziwa ya mkewe inafaa...?

Swali Mume kunyonya maziwa (matiti) ya mkewe inafaa...? Jibu Hakuna Uharamu wa Mume  kunyonya matiti ya mke wake.  Allaah(Subhaana wa Taala) Anasema kwamba:  ((نِسَآؤُكُمْ حَرْثٌ لَّكُمْ فَأْتُواْ حَرْثَكُمْ أَنَّى شِئْتُمْ وَقَدِّمُواْ لأَنفُسِكُمْ وَاتَّقُواْ اللّهَ وَاعْلَمُواْ أَنَّكُم مُّلاَقُوهُ وَبَشِّرِ الْمُؤْمِنِينَ)) ((Wake zenu ni kama konde zenu. Basi ziendeeni konde zenu mpendavyo. Lakini jitangulizieni kheri nafsi zenu, na mcheni Allaah , na jueni kuwa hakika nyinyi mtakutana Naye. Na wape bishara njema Waumini)) [2:223] Kwahiyo mwanamke anayo ruhusa ya kumchezea mkewe sehemu yoyote ya mwili wake pamoja na kunyonya maziwa ya mkewe isipokuwa tu Kufanya naye jimai kwa sehemu ya nyuma (liwati). Aayah hii:  “ Wake zenu ni konde kwenu. Basi ziendeeni konde zenu (panapotoka kizazi) vyovyote mpendavyo. “   imeteremka kuhusu Mayahudi waliokuwa wakisema kuwa mwanaume akimuingilia mke wake kupitia upande wa nyuma basi anazaliwa mtoto akiwa ana makengeza. Ndipo i

Kusikiliza Nasheed na Kaswida zenye Muziki na Vinanda

Swali Inafaa Kusikiliza Nasheed na Kaswida zenye  Muziki na Vinanda Jibu  Shukrani zetu za dhati kwa swali lako kuhusu hukumu ya muziki inayotiwa katika Nashiyd na Qaswiydah. Muziki na utumiaji wa ala za muziki ni haramu katika Dini yetu hii, Uislamu. Zifuatazo ni dalili kuhusu hilo:   Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “ Kutakuwa watu katika Ummah wangu watakao halalisha uzinzi, uvaaji wa Hariri, pombe (unywaji) na ma’aazif (ala za muziki) ” (al-Bukhaariy).   Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “ Mwisho wa zama (dunia) kutakuwa na maporomoko ya ardhi, mawe kutoka mbinguni na kugeuza kwa wanyama, wakati ambapo ala za muziki na waimbaji wanawake watakapoenea na pombe kuruhusiwa ” (atw-Twabaraniy).   Mtume wa Allaah (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “ Watu katika ummah wangu watakunywa pombe, kuiita kwa jina jingine. Watatiwa furaha kwa uchezaji wa ala za muziki na uimbaji wa wanawake (watakao

Hukumu ya Mke kutoka nyumbani bila Ruksa ya mumewe

Naam shukrani kwa swali lako kuhusu mkeo kutoka bila ya ruhusa yako kwenda katika mishuari zake. Matatizo haya hutokea mara nyingi kwa mke kutokuwa na ufahamu na ujuzi wa Dini ya Kiislamu. Au mara nyingine huwa kweli ana elimu lakini hushindwa kufuata kimatendo kwa sababu moja au nyingine. Au huenda akawa na elimu, lakini akakosa Dini. Kwa ajili hiyo Imaam al-Bukhaariy, ana mlango katika  Swahiyh  yake wenye kichwa cha habari, “ Elimu Kabla Ya ‘Amali ”. Hata hivyo, huenda mtu akawa na elimu lakini akawa hana ‘amali kwa sababu ya kutokuwa na ikhlaasw.   Ni juu ya mke kumtii mumewe katika mambo yasiyo ya maasi, kwani hakuna utiifu katika maasiya. Ikiwa mume hakutoa ruhusa mbali na kuwa yu mbali na mkewe ni wajibu wa mke kutii amri hiyo. Hata hivyo, haifai kwa mume kuweka vikwazo vya kupita kiasi,  kama kumzuia kwenda kwa wazazi wake na mahali ambapo anaweza kupata elimu ya Kidini. Allaah (Subhaanahu wa Ta’ala) Anasema: “ Wakikutiini, basi msiwatafutie njia ” (an-Nisaa’ [4]: 34). Hii